Akina dada, kwanini mnakubali kutoa namba kisha mkipigiwa simu hampokei?

Kijana sijakuelewa una omba no ya simu, unatongoza au unaomba mzigo at the first time which in which maana hivi ni vitu tofauti kabisa
 

Mtu humjui unajisikiaje vibaya… nyie hamjui tu kuna mazingira huwezi mnyima mtu namba
 
ndo maana mimi huwa siombi namba, natongoza kwanza nikikubaliwa ndo naomba namba au naweza nikapewa mzigo kabla sijaomba namba.

[emoji23] mtu unapokea simu yake mara anaanza kukupa sifa za uongo ams sms za kipuuzi hata mimi sijibuu
 
Mtu humjui unajisikiaje vibaya… nyie hamjui tu kuna mazingira huwezi mnyima mtu namba
Kwani ukimpokea na ukamsikiliza anataka nn alafu ukachukua uamuzi wa kukataa au kukubali utapungukiwa na nn kwenye maisha yako ?
Kitendo cha kukuomba namba ina maana anahitaji uwe mwanzo wenu wa kujuana hivyo unapo kataa kupokea simu yake inamfanya aone kama umemdharau na kumuona hana hadhi ya kujuana na ww.

Kama akipiga msikilize anacho taka then mwambie kuwa anacho kitaka hakiwezekaniki mpe na sababu ya kwann hakiwezekaniki nadhani hata yeye ataridhika huna haja ya kutdarau simu yake.
Kama ambavyo mlikutana mpaka akakuomba namba basi tambua kuwa mnaweza kukutana tena katika mazingira mengine ambayo ww utakuwa unahitaji msaada wake.
 

Ukiona tunafanya hivyo ujue yeye ni sababu sio wote ni waelewa Kama wewe
 
Kwaiyo nikipokea simu ndio yeye atanioa [emoji38]
Mungu anakupa unachostahili...kama ndo huyo kaletwa na ukaona hakufai ndo Ivo utaangaika sanaa kumpata mwsho wa siku ni kwenda kwa waganga na kuwasumbua wahubiri..
 
Endeleeni kuzibana,na Sisi hela hatutoi
 
Wewe unataka apokee simu na kujibu sms ili umfabyeje? Kwanini unalazimisha kumdinya mke wa watu?
 
Ukiona tunafanya hivyo ujue yeye ni sababu sio wote ni waelewa Kama wewe
Ukiona umemkatalia hitaji lake na akashindwa kuwa muelewa na akawa msumbufu kwako basi hapo una uhalali wa kumpiga brock lakini siyo kukataa kumpokea hata kabla ya kumsikiliza.
Tatizo sisi linapo kuja mawasiliano kati ya me na ke kinacho tangulia vichwani mwetu ni ngono na uzinzi tu,mtu anaweza kukuomba namba yako kwa dhamira ya kukutongoza lakini akabadilisha dhamira yake baada ya kujua ww ni mtu wa aina gani na mkawa na urafiki wenye tija katika maisha yenu.
Mtu anaweza asikufae kwenye mapenzi lakini akakufaa kwenye mambo mengine.
 
Bro mapenzi hayatafutwi hivyo huyo hata akipokea simu utakula za uso mpaka ushangae, mpenzi huwa anakuja tu automatically maishani mwako
Hii ni kweli,wewe ni love therapist bro😐😐😐
 
Basi kwa kufanya hivyo unajiona uko so special as if mwanamke ni wewe mwenyewe tu hapa duniani.

Lakini sikulaumu wewe, Nina ilaumu jamii na wanaume kwa ujumla maana shobo zao ndio zimewafanya muwe na hii overbloated ego
 
Kaka unautumia akili nyingi sana kwa watu ambao hawajozea kuangaisha ubongo.

Unatumia akili nyingi kutoa ufafanuzi kwa watu ambao wanaishi kimazoea tangu udogoni mpaka wanakuwa watu wazima.

Jamii yetu hii ina social settings ambazo ndio watu wanaishi kwa kuzifuata na huwezi ukawabadilisha hata iwe vipi

Kikawaida mwanamke wa kitanzania hasa binti akiombwa namba ya simu na mwanaume asiyejua, tayari akilini mwake anajua kinachofuata hapo ni mtongozo tu basi hakuna kingine...

...Na ndio maana mara nyingi wanaaza kujihami mapema kama vile kukuandalia aina ya majibu atakayokupa hata kabla hujamtafuta.

Mimi wiki iliyopita nilimuomba mmoja wao namba alikuja eneo ninalofanyia kazi, yaani ile amemaliza tu kunitajia tarakinu ya mwisho akaniambie eti "ila Mimi sitembeagi na waume za watu" ilibidi nitabasamu tu huku nikishangaa sana.

Kwa hiyo hii ndio aina ya wanawake waliopo kwenye jamii yetu.. ukimuomba namba ya simu tafsiri yake ni umemtaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…