Van brokhost
Member
- Dec 26, 2022
- 21
- 10
Kweli wewe Chizi. Mzalendo wa Uganda atakua na uzalendo na Zanzibar pia!!Sultan alipinduliwa na Wazalendo wakiongozwa na John Okello. Kisha akamaliza kazi yake kwa kumuita Karume atoke mafichon aje ongoza nchi.
Mohamed Said hawezi kukuletea story za John Okello kuwa Ni shujaa kwasababu sio mwislamu
Kama Okello hakuhusika hapo kwenye mahojiano muhimu anafanya nini? Wala urojo wakubali tu Okello ndo alifanya mambo, Karume alilaza
Msikilize hapo akiongea akiwa na Karume.
Kijana mdogo sana miaka 29 akapindua nchi. Bila Okello Zanzibar ingekua bado chini ya Sultani.
Okello tutakukumbuka Daima, haijalishi umekufa ila kumbukumbu yako haitafutika.
Last...Mohamed Said hawezi kukuletea story za John Okello kuwa Ni shujaa kwasababu sio mwislamu
Nadhani Okello angekuwa mwislamu mpaka leo mchango wake ungekuwa unaimbwa Zanzibar. Hata kama ni kidogoLast...
Hapana historia ya Okello naifahamu vyema.
Na sijui kwa nini wengi wenu hapa mnashikilia kuwa alikuwa mtu muhimu sana kiasi mnasema ni baba taifa la Zanzibar.
Nimejitahidi kueleza historia ya mapinduzi na mipango yake na pia kukuelezeni wahusika wakuu lakini inaelekea hamtaki kusikia.
Mnataka kuifanya historia ya Okello kuwa historia ya Mkristo aliyekuja kuwaokoa Waislam Waafrika waliokuwa wanakandamizwa na Waarabu.
Hii siyo historia ya mapinduzi.
Mleta mada ficha ujinga wako, Okello kamuondoa mkoloni gani?
Nadhani Shida kubwa ipo Hapa. Na wanajaribu sana kumzika kwenye hili Tukio. But watu hatudanganyiki. John Okello baba wa Taifa la Zanzibar.Mohamed Said hawezi kukuletea story za John Okello kuwa Ni shujaa kwasababu sio mwislamu
See... Nlisema mimi shida ni DINI YA OKELLO. UKRISTO WAKE NDO UMEMPONZA WATU WA ZANZIBAR HAWATAKI IONEKANE ALIKUWA MWAFRIKA ALIYEKUJA OKOA WAAFRIKA WENZIE. WANAFIKIRIA KWANZA JINA LAKE. MAANA UNAWEZA KUTA HATA HAKUWA MKRISTO ILA ANA JINA LA KIKRISTO.Last...
Hapana historia ya Okello naifahamu vyema.
Na sijui kwa nini wengi wenu hapa mnashikilia kuwa alikuwa mtu muhimu sana kiasi mnasema ni baba wa taifa la Zanzibar.
Nimejitahidi kueleza historia ya mapinduzi na mipango yake na pia kukuelezeni wahusika wakuu lakini inaelekea hamtaki kusikia.
Mnataka kuifanya historia ya Okello kuwa historia ya Mkristo aliyekuja kuwaokoa Waislam Waafrika waliokuwa wanakandamizwa na Waarabu.
Hii siyo historia ya mapinduzi.
Kwani lafudhi ya sauti ni issue si unaigiza tu.Mouse...
Lafidhi yake radioni ilotumika kuwatisha watu.
Ukiona hivyo, ujue LOGIC inagoma.Baba...
Tufanye mjadala wa kiuugwana sote hapa tunufaike.
Tukiingiza kejeli tutavuruga.
Ndiye aliyeongoza Mapinduzi Matukufu.Kweli wewe Chizi. Mzalendo wa Uganda atakua na uzalendo na Zanzibar pia!!
Una miaka mingapi?, Maana wewe pengine hukuwepo wakati wa NYERERE na umesimuliwa tu.Museme kwa nyerere pia mpikaji na mpotoshaji wa histori! Nyerere alikuwa wa mchongo na aliipika historia ya Tanzania shem on her
Una uhakika gani hiyo picha ya mwanzo ndio ya 1964 na siyo hiyo ya chini ya Okelo Kwamba Ni ya siku za mbele baada ya Uhuru huo?Sela...
Nakuwekea picha hiyo hapo chini itazame na linganisha:
View attachment 2479862
Hii picha hawa Makomredi wamesimama wapigwe picha na picha hii imepigwa mapinduzi yameshatokea siku chache zilizopita.
Picha hii imepigwa Okello anawekewa silaha na yeye mwenyewe ameshika silaha apigwe picha.
Katika hiyo picha ya Makomredi wawili nimepata kuzungumza nao Amour Dughesh na Hashil Seif.
Dughesh alinionyesha picha nyingine ya yeye na comrade mwingine ambae ni rafiki yangu wakiwa kwenye combat wameshika bunduki wako lindoni.
Picha hii ni tofauti na picha hiyo ya kwanza hapo juu.
Nakuwekea na picha nyingine hapo chini lakini huyu kwa mjuonekano wake ni ''askari'' tofauti sana na waliomzunguka Okello.
''Eti utafiti.''
''No research no right to speak.''
Chairman Mao.
Utafiti ndiyo msingi wa elimu.
Si kitu cha kubeza au kukejeli.
Nimemjua vipi Comrade Hashili Seif:
Comrade Hashil Seif Hashil, UMMA Party na mapinduzi ya Zanzibar
Kwa wale walionisoma siku tatu zilizopita nilipokieleza kitabu, ''Mimi, Umma Party na Mapinduzi ya Zanzibar,'' kilichoandikwa na Comrade Hashil Seif Hashili niliweka miadi ya kurejea mara nitakapokimaliza kitabu. Nimekimaliza kitabu leo asubuhi. Kitabu hiki ni kitabu kizuri sana na ukikianza...www.jamiiforums.com
View attachment 2479876
Nyerere kwangu ni wa mchongo! Nasisitiza hiloUna miaka mingapi?, Maana wewe pengine hukuwepo wakati wa NYERERE na umesimuliwa tu.
NB
Kuna mitazamo miwili ya uandishi wa historia.
"Bourgeoisie perceptions" na " Marxist perceptions".
Inategemea unatumia mtazamo gani kuandika historia yako.
By the way, sijaona kitabu cha historia alichoandika NYERERE.
Nimesoma vitabu vya historia ya Tanzania vilivyoandikwa na I .KIMAMBO, John Illife, Ogot,nk. Sijamwona NYERERE ( tutajie kitabu cha historia alichroandika Nyerere, na kama siyo chuki binafsi dhidi ya Nyerere).
Tuache kuwasingizia watu vitu ambavyo hawakutenda kwa maslahi yetu.
Nyerere kwangu ni wa mchongo! Nasisitiza hilo
Alikuwa na jina la kizungu ila hakuwa Mkristo.See... Nlisema mimi shida ni DINI YA OKELLO. UKRISTO WAKE NDO UMEMPONZA WATU WA ZANZIBAR HAWATAKI IONEKANE ALIKUWA MWAFRIKA ALIYEKUJA OKOA WAAFRIKA WENZIE. WANAFIKIRIA KWANZA JINA LAKE. MAANA UNAWEZA KUTA HATA HAKUWA MKRISTO ILA ANA JINA LA KIKRISTO.
Sela...Una uhakika gani hiyo picha ya mwanzo ndio ya 1964 na siyo hiyo ya chini ya Okelo Kwamba Ni ya siku za mbele baada ya Uhuru huo?
NB kwa wazoefu wa harakati za kivita, asiye kamanda kabisa Hana Uhuru wa kuwasogelea makamanda Kama vile, huwa hajiamini na kwa namna flani hujitofautisha hats kwa muonekano wa uso wake uliojaa uoga mkuu.
Mzee lazima ukubaliane hata moyoni John O Ni moja ya makamanda waliojitolea maisha yao bila malipo kuhakikisha wanaondoka wadhalimu. Na kwa moyo wangu naamini John hata baada ya kuondoka visiwani alikosekana tu mtu wa kushirikiana nae kuikomboa Afrika iliyokuwa ikipigana kuwaondoa wadhalim wa ulaya huko Angola, Kongo, Mozambique.
Na pengine leo John angekuwa shujaa wa kuimbwa Kama Che,Mandela nk.
Sasa uzalendo wapi kwa wazanzibari upo wapi? Unadhani alikua na uzalendo kwa wazanzibari au uadui tuu? Unafahamu nini unaposema neno "Uzalendo" ?Ndiye aliyeongoza Mapinduzi Matukufu.
Mzee hujui kuwa sio kila utafiti ni sahihi? Ni mara ngapi tulisikia dawa fulani iligundulika baada ya utafiti kuwa haifai tena kwa matumizi baada ya kubainika mapungufu yake?Frank...
Sijapatapo kuhangaika na Nyerere ila nimeandika historia yake kwa kadri ya uwezo wangu.
Kuhusu Okello historia yake naifahamu vizuri kwa utafiti kwani nilikuwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany wakati anaandika, "Kwaheri Uhuru Kwaheri Ukoloni.''
Siwezi kumlazimisha mtu kuniamini anaweza kuamini atakacho.
Tatizo lako wewe unajifanya mjuaji sana angalia hapo unapojisifu eti unajua vingi kuliko mimi...ulisema waliokifanya kazi kwenye mashamba ya mkonge ni wamakonde nikakuuliza mbona mimi nawajua wazee wengi wa kimwera na kiyao waliokaenda kufanya kazi kwenye mashamba ya mkonge? Kwanini uwataje wamakonde tu?Mnachi...
Sababu ni kuwa mimi nimetafiti na nimefika hadi Kipumbwi na nimezungumza na Victor Mkello na msaidizi wake Maulid Sheni.
Nimefika hadi Sakura walipokuwa wanaishi Wamakonde kwa ufupi nayafahamu haya mambo kupita wewe.
Ndiyo unapokataa kusikiliza utafiti naamua iwe basi amini upendacho hapana haja ya ubishi.
Mimi niko hapa kuisomesha historia ambayo kabla haikuwa inajulikana.
Tatizo lako wewe unajifanya mjuaji sana angalia hapo unapojisifu eti unajua vingi kuliko mimi...ulisema waliokifanya kazi kwenye mashamba ya mkonge ni wamakonde nikakuuliza mbona mimi nawajua wazee wengi wa kimwera na kiyao waliokaenda kufanya kazi kwenye mashamba ya mkonge? Kwanini uwataje wamakonde tu?