Akumbukwe John Okello, Baba wa Taifa la Zanzibar. Bila huyu leo Zanzibar wangekuwa bado Utumwani

Akumbukwe John Okello, Baba wa Taifa la Zanzibar. Bila huyu leo Zanzibar wangekuwa bado Utumwani

Ohh nahisi.
Je mzee Karume alikuwepo kisiwani wakati wa mapinduzi akishiriki bega kwa bega?
Pengine hakuwepo! Ndio maana anaskika okelo akimwita, je alikuwa wapi?
Na kwanini amekimbia?
Na Ni kwanini aitwe yeye badala ya wengine ?
Akichaguliwa na Nyerere tu kushika madaraka
 
Akichaguliwa na Nyerere tu kushika madaraka
Kichakaa...
Karume, Babu, na Hanga hawakuwapo Zanzibar lakini si kama walikimbia.

ASP waliweka mkakati huu ikiwa mapinduzi hayatafanikiwa harakati zitaendelea Karume akiongoza akiwa nje ya Zanzibar.
 
Tad...
Ikiwa huwezi kusoma basi si tatizo.

Mimi katika maisha yangu nimekuwa sichagui katika kutafuta elimu nasoma kila kitu isipokuwa matusi.

Ndiyo sababu nimekuwa hivi.

Ikiwa utakuwa unasoma vile unavyopenda ndiyo hivyo leo unaamini hadithi ya Okello.

Ungemsoma na Ghassany ungemsoma Abeid Mmasai na wengine hawajatajwa katika historia ya mapinduzi.

Mwisho ungejiuliza mbona Kassim Hanga hatajwi katika historia ya mapinduzi ilhali yeye ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa mapinduzi?

Kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika ungejiuliza mbona Ally Sykes TANU Card No. 2 na kaka yake Abdul Sykes TANU Card No. 3 hawatajwi kwenye historia ya TANU?

Ikutoshe baba yao Kleist Sykes ndiyo aliyeasisi African Association 1929 na ndiye aliyejenga ofisi ya TAA ilipozaliwa TANU 1954.

Vipi historia nzima inamtaja Nyerere peke yake?
Mzee wangu naona umerukia kwenye mada nyingine unakwepa lengo la hoja yangu..

Hizo history za TANU kupindishwa ni sababu ya mimi sipendi maandiko ya histori ya Tanzania hata hivyo sio lengo la uzi huu na swali langu kwa ujumla...

Swali langu kwako ni hili... umeangalia hiyo video kuona kile ambacho nimekwambia ya kwamba kwenye mahojiano Okello anatambulika kuwa ni kiongozi wa jeshi la mapinduzi kutokana na statement ya swali la pili la mwandishi ambalo lilimlenga okello!?
 
Mzee wangu naona umerukia kwenye mada nyingine unakwepa lengo la hoja yangu..

Hizo history za TANU kupindishwa ni sababu ya mimi sipendi maandiko ya histori ya Tanzania hata hivyo sio lengo la uzi huu na swali langu kwa ujumla...

Swali langu kwako ni hili... umeangalia hiyo video kuona kile ambacho nimekwambia ya kwamba kwenye mahojiano Okello anatambulika kuwa ni kiongozi wa jeshi la mapinduzi kutokana na statement ya swali la pili la mwandishi ambalo lilimlenga okello!?
Tadpole,
Sina sababu ya kukwepa.

Nimeandika kama ilivyo kawaida yangu.

Uko huru kuamini utakacho.
Hakuna tatizo.
 
Kipekee kabisa tunapoenda kuaga mwezi wa 4 mwezi wa historia kwa kamanda wa ukombozi alieuwawa na utawala wa Idd Amini Dada, kwa wapenzi wa makala na rejea za historia Gazet la the monitor limekuwa na makala mfululizo zenye kumbukumbu za shujaa wa Mapinduzi ya Zanzibar.

Tembelea www.monitor.co.ug kwa habari zaidi.

Field Marshall John Okello alikuwa mjeuri sana achilia mbali ushujaa wake hakuwa mtu wa vidogo alipenda vikubwa tu.

R.I.P Kamanda

In memory of a gallant officer

Salute

Wadiz
 
Okello alifanya kazi kubwa sana ya kufanikisha Mapinduzi ya Zanzibar.
Tatizo lake alitaka cheo kikubwa hali ya kuwa hakuwa mtanzania.

Okello ni raia wa Uganda. Ilifikia mahali kwa huo mchango wake hakutaka hata kumheshimu Karume na Nyerere, ndio maana alifukuzwa Tanzania na akarudi Uganda.

Okello alikuwa na kiburi, hakuwa mnyenyekevu, alijiona m'babe mwenye akili nyingi na mtaalam.

Hata mimi ningemfukuza Okello na kusahau kabisa.
Nyerere alimfukuza 24 hours Ban.
 
Kipekee kabisa tunapoenda kuaga mwezi wa 4 mwezi wa historia kwa kamanda wa ukombozi alieuwawa na utawala wa Idd Amini Dada, kwa wapenzi wa makala na rejea za historia Gazet la the monitor limekuwa na makala mfululizo zenye kumbukumbu za shujaa wa Mapinduzi ya Zanzibar...

Kwetu tunaambiwa viongozi hawana wajibu wananchi tuhamasishane na tuongozane wenyewe kupambana na ma CCM. Tukishamaliza tuwaite wao sasa waje kulamba asali Kwa starehe zao.
 
Okello baba wa Taifa la Zanzibar. Na Mzee Karume alikuja force Wabantu sisi tuoe Waarabu ndo kisa cha kupatikana mashombeshombe hasa Pemba. Hawa mashujaa wetu wakumbukwe.

Mumeelewa waafrika wakiuza waafrika wenzao

 
Nimeelewa jinsi ambavyo mwafrika Okello alivyoona wenzie wanateswa na weupe akaja waokoa.
 
Basi nayo inahitaji akina Okello wengi waje kufanya mapinduzi kwayo. Tunahitaji akina Okello wengi sana kumbe

Hujasikiliza bado Miafrika mengine ikijipeleka yenyewe kuuzwa kirahisi Kama Ile inayojipeleka kwa wachungaji kuuliwa kule Kenya

 
Hujasikiliza bado Miafrika mengine ikijipeleka yenyewe kuuzwa kirahisi Kama Ile inayojipeleka kwa wachungaji kuuliwa kule Kenya


Kuuana miafrika haishangazi sana. Nenda hapo tu Somalia au Sudan... Utakimbia.... Somalia ndo usiseme. Kote huko wanahitaji Okello angekuwepo.
 
Dah... Hadi kupewa Radio kutoa tamko KUBWA kama hilo, hata kwa akili ya kawaida lazima huyu alikuwa mtu muhimu sana kwenye "operation" aka Mapinnduzia

Kwahiyo walimkuta mtaani amekaa wakampa radio kutoa tamko hilo?
Aliwekwa mstari mbele kama liability ili mapinduz yakifeli,ye ndo abebe msalaba,wenyeji walikuwa Wana hofu,na WA bara walihofu ingeleta ingemletea sura mbaya Mwalimu Jk
 
Back
Top Bottom