Ali Kiba anadai kila mtu kazaliwa Muislamu na kwamba Wakristo wote ni watu waliobadili dini

Anaelewa kwani mkuu, mimi niliangalia nikampuuza Tu. kuna vitu vingine ni sensitive sana kuviongelea kwa kuegemea upande flani hasa ukiwa public figure.

Mambo ya dini, kabila au siasa ambazo huusisha hisia kali si sawa maana reactions au athari sake huwa hazitabiriki
 
W Wewe unathibitisha vipi babu yako ni Ibrahim zaidi ya kuambiwa tu na watu toka nje ya nchi yetu.
Mimi sina dini, labda wewe ndiyo mwenye chuki kwasababu una upande unaoutetea.
 
Huo ni msimamo wa waislamu karibia wote

Ila ukweli ambao hausemwi ni kuwa watu wote tulizaliwa tukiwa atheist

Wengine tumekulia familia zina waislamu na wakristu na tunapendana sana sababu tunaheshimiana mipaka yetu.
Kuku tunawapelekea watuchinjie ili tukila nao wasijiskie tofauti na hata akikukuta maeneo unakula kitimoto wala hamaindi tena anakuacha unakila in peace
 
Uislam na ukristo huo ni mgawanyo wa majukumu tu uliopangwa na ngozi nyeupe kuitawala Dunia hasa africa, nyie bakieni mkipiga kelele tu na kusujudia ujinga wao wanabakia kuwazoom tu miridi yao waliyo ipandikiza kwenu inavyo fanya kazi, hata mkichinjana tu wao hawana hasara
 
ibrahim yule baba wa isaka aliye baba wa yakobo aliye baba wa yuda
 
Analingania dini yake jambo ambalo ni jema, naona wengine wanaona kuwa anakosea sijui public figure sijui brand aah hapana maana naye bado ni muumini ana wajibu wa kuutimiza kwa anayemuabudu wa kueneza ukweli kwa wasioujua ili waufahamu hana woga na ni jambo zuri

Ila kwa aliyosema ndiyo siyo sahihi uislamu japo unanasibishwa sijui na Ibrahimu kupitia Ishmael lakini ni dini iliyoibuka miaka ya 610 hivi wakati huo tayari ukristo ulishakuwepo zamani sana uislamu ni dini ya juzi tu kupitia kwa Muhammad ndiyo maana hata katika hoja mbalimbali zinapowatatiza allah kupitia wahyi wake kwa Muhammad aliwaambia wawaulize watu waliokuwa na kitabu kabla yao ambao ni wakristo


( فَإِن كُنتَ فِي شَكٍّ مِّمَّا أَنزَلْنَا إِلَيْكَ فَاسْأَلِ الَّذِينَ يَقْرَءُونَ الْكِتَابَ مِن قَبْلِكَ ۚ لَقَدْ جَاءَكَ الْحَقُّ مِن رَّبِّكَ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْمُمْتَرِينَ )

يونس (94) Yunus

Na ikiwa unayo shaka katika tuliyo kuteremshia, basi waulize wasomao Kitabu kabla yako. Kwa yakini imekwisha kujia Haki kutoka kwa Mola wako Mlezi. Basi usiwe miongoni mwa wenye shaka.

Kwa hiyo quran yake inawtambua watu waumini walikuwepo kabla ya uislamu tena wenye kitabu ambao wanapaswa wawafundishe waislamu wakipata utata juu ya hoja. Kwa hiyo nadharia ni uongo
 
Tatizo ni kwamba watu waliotuletea hivi vitabu na hizi hadithi hawana njia ya kuthibitisha chochote zaidi kuleta madai ya hadithi.
Hivyo, sidhani kama ni sawa kuchagua upande kwenye hizo hadithi na kusema kila mtu kazaliwa katika upande flani kama alivyofanya Kiba.
 
Huo ni msimamo wa waislamu karibia wote
Haswaa huo ndio msingi,lakini hatukatazi watu wangine wasipinge,kama kuna wanaopinga sawa ila uislamu umeshaweka huo utaratibu tayari.
Ila ukweli ambao hausemwi
Hausemwi na nani wakati wewe unasema na tumeshasikia watu kadhaa wakisema huu unaosema ukweli.

Hivyo huu unaosema ni ukweli ambao hausemwi sio kweli mkuu,huu ni ukweli(kwa mujibu wako) ambao unasemwa.
kuwa watu wote tulizaliwa tukiwa atheist
Na huu ni msimamo wa atheist pia kama ambavyo ulivyokuwa msimamo wa uislamu.

Hivyo kila mtu anavutia ngoma upande wake.
 
Kiba kakaririshwa. Binadamu tunazaliwa bila dini yoyote. Katika Makuzi/malezi ndo tunakutana na dini za wazazi na walezi wetu mfano ukikuta mzazi wako mlokole,mkatoliki,msabato,muislam,mpagan,muabudu mizimu,budha etc nawe unafata huko kisha mbeleni ukiwa mkubwa unaweza kuasi na kufata upendapo
 
nonsense.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…