Alichokisema Ismail Jussa baada ya Tume kutoa Rasimu ya Katiba...

Alichokisema Ismail Jussa baada ya Tume kutoa Rasimu ya Katiba...

Zanzibar tutasimama kwenye hoja hadi tufike pale tutakapo . Mungu ibariki Zanzibar
nchi kadogo tunalisumbua bonge la nchi .
Tembo lazima atamtapika chura alie mmeza

Wazanzibari mna haki ya kudai mnachodai. Muungano sio msahafu toka mbinguni. Hata Mungu mahali pengine na wakati mwingine amesema usifungamane na wao usionia nao pamoja. Miaka hamsini tumevumiliana na inaonekana umoja wetu unazidi kuwa karaha zaidi. Katika Biblia takatifu, Ndugu wawili, Ibrahimu na Lutu walikuwa wakikaa pamoja na kuchunga mifugo yao pamoja, lakini wakati ukafika watumishi wao wakaanza kugombana. Abrahamu akamwambia Lutu, sii vyema sisi tugombane, tazama ardhi ni kubwa wewe nenda upande huu na mimi nitaenda upande ule na hii itakuwa suluhisho la ugomvi kati ya watumishi wangu na wa kwako. Wakati umefika kwa dhati kabisa, turuhusu Zanzibar iwe nchi kamili na Tanganyika vivyo hivyo. Ila tubaki na shirikisho la masuala tutakayokubaliana kwa uwazi wa pande zote.
 
LET TANGANYIKA COME TO FREE ZANZIBAR.

WaTanganyika mnakhofia nini kuundwa kwa Serikali yenu. Na cha aibu na kufedhehesha katika Rasimu wamesema Serikali 3 yaani ya Shirikisho, Zanzibar na Tanzania Bara (hawajasema Tanganyika) kwanini?

na vile vile Muungano laazima uwe wa Mkataba.

Hongera sana Mwakilishi. Hakuna marefu yasio na ncha.
sasa ncha ileeee.. tudime tu tutafika Insh'Allah

Allah akubarik sana
.
 
Haaa tutegemee kuzaliwa kwa shirikisho la zanzibar, lenye serikali za pemba na unguja. Zanzibar haitakuwa moja tena!

na vile vile tutegemee kuzaliwa kwa Shirikisho la wakristo na shirikisho la waislam. Tanganyika haitakuwa moja tena. Itagawika kama Sudan.
 
waliberali wana mambo!! Tuwaache watu wafanye mambo yao
 
Njia mmeshaonyeshwa kilichobaki ni kuwatakia safari njema.
Mlisha kuwa kero kubwa ndani ya muungano.

Ninapoona watu kama ninyi mnatoa comment safi namna hii nafarijika sana....Nakumbukia kale kawimbo nikapendako ka sikinde kanakoimba....Bubu hutaka kusemaeee...mambooo,....mambo yanapomzidiaaaaax2.
 
Mkuu, hoja za kuwa na mamlaka kamili haziwezi kutetewa na majina ya zamani na sasa.
Hayo ni majina tu, hayana maana.

Jusa anajisifu kwa kurudishiwa mambo yanayokula zaidi kuliko yanayozalisha.
Elimu ya Juu - viwavi jeshi.
Jeshi la polisi - viwavi jeshi

hiyo ni expenditure mkuu, hakuna revenue hapo.

C.C Barubaru
 
Last edited by a moderator:
Sasa kwa msururu huo, kuna muungano hapo? Mambo mengine haya ni vichekesho, kwani huu muungano wa nini hasa? Mi naona unatujazia Wapemba Buguruni, bora uvunjike warudi kwao wakakazane kwenye mikarafuu

neno huweza kuwa na maana zaid ya moja
 
Mimi ni mtanganyika. Nimefuatilia mjadala huu kwa makini. Nimebaini kuwa watanganyika hawakujiandaa kuwa na serikali yao. Inashangaza sana kuona kuwa hata baada ya serikali ya tanganyika kuruhusiwa, bado watanganyika wengi wanaiwaza zanzibar. Huo ni udhaifu mkubwa. Kinachotakiwa kwa sasa watanganyika tuangalie namna ya serikali yetu itakavyoundwa kwa ufanisi. Zanzibar hawana shida sana kwa kuwa wana pa kuanzia. Sisi tunaanza sifuri. Tukiendeleza malumbano itadhihilika kuwa sisi watanganyika ndio tunaohitaji zaidi muungano huu. Ushahidi wa jambo hili ni katika jina lililopendekezwa. Tume imependekeza tanzania bara, kwa nini isiitwe tanganyika? Mbona zanzibar ipo?. Tunalichukia jina la nchi yetu?. Tupo kamili kweli?. Kwa nini tunaelekeza shutuma kwa wazanzibar badala ya kujikita katika kujenga tanganyika yetu. Tujirekebishe.
 
Liberal-supporting, belonging to, or associated with the Liberal Party in Canada, the United Kingdom, or Australia
 
SAFARI YA KUELEKEA MAMLAKA KAMILI IMEPIGA HATUA KUBWA:

Na Ismail Jussa

Mamlaka ambayo tayari Zanzibar itakuwa imeyarejesha kwa kuondolewa kwenye Muungano kupitia Rasimu ilotangazwa leo ni:

1. Polisi.

2. Mikopo na Biashara ya Nchi za Nje.

3. Kodi ya Mapato.

4. Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.

5. Mabenki ya Kibiashara na Fedha za Kigeni.

6. Leseni ya viwanda na takwimu.

7. Elimu ya Juu.

8. Maliasili ya mafuta na gesi asilia.

9. Baraza la Taifa la Mitihani.

10. Usafiri na usafirishaji wa anga.

11. Utafiti.

12. Utabiri wa Hali ya Hewa.

13. Takwimu.

14. Mahkama ya Rufani.

15. Ushirikiano wa Kimataifa.

KAZI ILIYOBAKI KWA WAZANZIBARI ILI KUTIMIZA MAMLAKA KAMILI

Ni kutumia hatua zilizobakia kuyarejesha pia mamlaka katika mambo muhimu yafuatayo:

1. Mambo ya Nje.

2. Uraia na Uhamiaji.

3. Sarafu na Benki Kuu.

4. Ushuru wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa.

5. Usajili wa Vyama vya Siasa.

TANBIHI:
Wananchi na hasa Vijana wa Zanzibar tumefikia hatua ya kurejesha mamlaka katika mambo hayo 15 kutokana na umoja wetu na kutumia njia za amani huku tukiwa na msimamo usiyoyumba. Tuendelee kuwa pamoja, tukitumia njia za amani kabisa kukamilisha mamlaka kamili tunayoyataka.

Naiona ileeeee.........

Hajui kuwa zanzibar ni kisiwa? Ipo siku population pressure itakuwa kubwa,na kama tunachojua asilimia kubwa ya watu wa zanzibar ni waislam ambao wanaweza kuoa hadi wake wanne.
Kwa haraka haraka ina wastani wa wanawake 672892(sensa ya 2012), sasa je iwapo hao watu watazaa kila mmoja azae watoto wawili,nini hatima ya zanzibar baada ya miaka 50 ijayo?
Watu wakiwa zaidi ya eneo lililopo watawapeleka wapi,kama zanzibar itasimama kama nchi?
 
zanzibar mmesahau upemba na uunguja? je, mtaendelea kwa jeuri gani. serikali itaweza kuhudumia gharama hizi zilizoongezeka? kwa pato gani, pato la zanzibar not more than bilioni mia tano kwa mwaka. then compere na gharama za uendeshaji zilizo ogezekae(polisi, elimu ya juu, takwimu, n.k).Kumbuka mnategemea sector ya huduma tu hasa mahoteli na watalii wengi walio kuwa wanaingia zanzibar sio wa direct to znzr ni wale waliokuwa wanakuja mbuga za wanyama na kutazama mlima kilimanjaro ndo walikuwa wanamalizia zanzibar then wanakwea pipa. zingatia pia, kwa dizaini hii ukivunjika huu muungano ujue wakija means wanakuja kwenye nchi mbili, so gharama zitaongezeka kwao na kuathiri soko la utarii zanz ambalo ndo linachangia kwenye pato la taifa kwa kiasi kikubwa. Ila kubwa zaidi kwani nyie wazanzibari hamjui yanayo endelea huku zanji, kunakampeni za kuwafukuza wapemba unguja? na ambazo zinashamili sana kila iitwapo leo. u wil spend a lot of time kupambana nyie wenyewe kuliko kujenga nchi.......binafsi siwalaani., bt zanzibar endapo muungano ukivunjika mtatikisika sana na kurecover itawachukuwa mda na msipo angalia you 're going to die. Mnafurahia mauti yenu, sio mbaya lakini
 
RWANDA na BURUNDI wenyewe wantegemea Tanzania itakuwa ZNZ.
Kwa hili la utabiri wa hali ya hewa Jussa anataka rada ambayo watafanyia uleberal wao bila Tanganyika kuwa soma. Huyu jamaa ni zaidi ya gaidi, pia kachemka hakumuelewa WARIOBA, uraia maana yake ni jeshi la polisi, pole sana mleberali
 
Ninapoona watu kama ninyi mnatoa comment safi namna hii nafarijika sana....Nakumbukia kale kawimbo nikapendako ka sikinde kanakoimba....Bubu hutaka kusemaeee...mambooo,....mambo yanapomzidiaaaaax2.

Mkuu CHADEMA ni watani zetu wa jadi lakini hao Uamsho wana laana.
Walipoanza kuua watu wa Mungu nikajua hatuna kitu nao in common.
 
Kifuatacho…
PEMBA nayo iachwe IPUMUWE!
Ndani ya Zanzibar kuwe na NCHI MBILI, kila moja iwe na MAMLAKA KAMILI,
Serikali hizo ni ya UNGUJA nay a PEMBA.
Safi sana.
 
Jusa ni mwehu flani tu, anajidanganya na kuwadanganya waznz, hana uzalendo wwte, anadhani kuvunja muungano ndio cuf kuingia madarakani??? Znz ina uchumi gani wa kujiendesha

Mkuu kuvunjika muungano sio CUF kuingia madarakani wala sio CCM kun'gan'gania madaraka ni jambo ambalo wazanzibar wanalitaka na wamelisubiri kwa muda mrefu.

Usikasirike kwa hili jambo la kuvunjwa mungano,Ujue kuwa kuvunjwa mungano ni kuvunja makubaliano ya kisiasa baina ya Zanzibar na Tanganyika lakini makubaliano na maelewano ya wazanzibari na watanganyika yatabakia pale pale kwani watu wa nchi mbili hivi wameungana kabla ya kuwepo kwa mungano wa kisiasa ulioletwa na karume pamoja na Nyerere 😉
 
SAFARI YA KUELEKEA MAMLAKA KAMILI IMEPIGA HATUA KUBWA:

Na Ismail Jussa

Mamlaka ambayo tayari Zanzibar itakuwa imeyarejesha kwa kuondolewa kwenye Muungano kupitia Rasimu ilotangazwa leo ni:

1. Polisi.

2. Mikopo na Biashara ya Nchi za Nje.

3. Kodi ya Mapato.

4. Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.

5. Mabenki ya Kibiashara na Fedha za Kigeni.

6. Leseni ya viwanda na takwimu.

7. Elimu ya Juu.

8. Maliasili ya mafuta na gesi asilia.

9. Baraza la Taifa la Mitihani.

10. Usafiri na usafirishaji wa anga.

11. Utafiti.

12. Utabiri wa Hali ya Hewa.

13. Takwimu.

14. Mahkama ya Rufani.

15. Ushirikiano wa Kimataifa.

KAZI ILIYOBAKI KWA WAZANZIBARI ILI KUTIMIZA MAMLAKA KAMILI

Ni kutumia hatua zilizobakia kuyarejesha pia mamlaka katika mambo muhimu yafuatayo:

1. Mambo ya Nje.

2. Uraia na Uhamiaji.

3. Sarafu na Benki Kuu.

4. Ushuru wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa.

5. Usajili wa Vyama vya Siasa.

TANBIHI:
Wananchi na hasa Vijana wa Zanzibar tumefikia hatua ya kurejesha mamlaka katika mambo hayo 15 kutokana na umoja wetu na kutumia njia za amani huku tukiwa na msimamo usiyoyumba. Tuendelee kuwa pamoja, tukitumia njia za amani kabisa kukamilisha mamlaka kamili tunayoyataka.

Naiona ileeeee.........

Red.....naona wanataka kuleta ujanja wa Nyerere wa chama kuchika hatamu.... kwanini vyama viwe chini ya serikali ya mungano wakati wameshaona kuwa mungano unaofaaa ni mungano wa shirikisho?

Mfano Nchi za scandinavia kuna chama kinachointwa "social democratic" hichi chama kiko nchi zote za scandinavia Norway,sweden,Denamrk,Finland, hivi nchi za scandinavia zimeungana kishirikisho lakini kila nchi ina mamlaka kamili ya chama chake,hapa kinachofatwa ni "Ideology" ya chama si kingine kwa hiyo haina maana ya yoyote kuwa vyama vya siasa viwe kwenye serikali ya mungano
 
Mimi nadhani ingekuwa bora tuondokane na huu muungano maana chokochoko hazitaisha, tumetumia mabilioni ya pesa kuja na hii rasimu, pesa ambazo zingeweza kabisa kuinua elimu yetu.

Ipo harufu huko mbeleni tutakuja tumia matrilioni mengine kwa ajili ya hayo saba yaliyobaki kwenye muungano.

These people will never rest mpaka wahakikishe wameuvunja.
Naunga mkono mawazo ya hapo juu, ndio njia pekee ya kumaliza malalamiko wasiyokwisha.
 
Zanzibar tutasimama kwenye hoja hadi tufike pale tutakapo . Mungu ibariki Zanzibar
nchi kadogo tunalisumbua bonge la nchi .
Tembo lazima atamtapika chura alie mmeza

mlikubali kuolewa wenyewe mwaka 1964, mkitusumbua tutawapiga kibuti vile vile.
 
Ndugu yangu Ismail Juha... Mengi kati ya hayo hapo chini ni matumizi zaidi na sio uchumi zaidi... naomba ni highligth mzigo kwetu waZanzibar in red.
1. Polisi.

2. Mikopo na Biashara ya Nchi za Nje.

3. Kodi ya Mapato.

4. Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.

5. Mabenki ya Kibiashara na Fedha za Kigeni.

6. Leseni ya viwanda na takwimu.

7. Elimu ya Juu.

8. Maliasili ya mafuta na gesi asilia.

9. Baraza la Taifa la Mitihani.

10. Usafiri na usafirishaji wa anga.

11. Utafiti.

12. Utabiri wa Hali ya Hewa.

13. Takwimu.

14. Mahkama ya Rufani.

15. Ushirikiano wa Kimataifa

Ni Muhimu wakati unashangilia useme pia yako wapi mafuta na bandari ziko wapi za kuendesha huo uchumi wa kuendesha hizo huduma?
Bora umuelimishe huyu mmanga anayelilia kurejeshwa sultani Zanzibar. Hivi kusherehekea utengano ndio fahari? Tuombe mungu hili la serikali tatu watu wafumbuke macho kwamba sio mwelekeo mwema kwa Tanzania kama taifa.
 
Back
Top Bottom