Alichokisema Rais Magufuli Tabora ni kweli; majungu watu hawafanyi kazi. Kanisa lajengwa katikati ya barabara, lapiga muziki masaa 24

Alichokisema Rais Magufuli Tabora ni kweli; majungu watu hawafanyi kazi. Kanisa lajengwa katikati ya barabara, lapiga muziki masaa 24

Kwa kweli imani zingine ni kero wengine sijui ni ulimbukenii,naamini ibada ina mda wake,sio unafungulia mziki Kwa sauti Kwa ajili ya kuwasikilizisha wengine, bila kujali kuna wagonjwa n.k
Kuna chombo kinakula fedha za serikali kwa kutotimiza wajibu wake, huwa sielewi kwanini hakiwajibishwi "NEMC"
 
Nikiwa Tabora ambapo nilikwenda kwenye msiba wa rafiki yangu aliyefiwa na mama yake mwezi huu. Nilikutana na kituko cha mwaka ambapo tukiwa hapo msibani ulisikika muziki mkubwa sana kiasi ambacho huwezi kuongea na mtu jirani yako, huwezi kupokea simu au kusikiliza simu. Nilipouliza nikaambiwa hilo ni kanisa la walokole Bethel, ambao walifukuzwa kutoka kata ya cheyo ndio wamehamia Kariakoo Tabora kata ya Kitete, ambapo toka wahamie Muziki ni masaa 24 kwa sauti ya juu sana.

Wakazi wa eneo hilo licha ya kulalamika kwa mkuu wa wilaya kwa maandishi DC Komanya, mkurugenzi, mtendaji kata, mwenyekiti wa mtaa, polisi mkuu wa kituo Mmassy, OCD, bado kanisa hilo linaendelea na fujo, vurugu huku mchungaji wa kanisa hilo Mch Jackson akiwambia wakazi hao kuwa serikali yote ya mkoa ameiweka mfukoni.

Mbaya zaidi huyo kaamua kujenga katikati ya barabara na kuziba barabara mtaa hivyo hapapitiki kwa gari, huwezi kupitisha mgonjwa, maiti hata kwa matumizi ya kawaida.

Jirani na kariakoo Ni eneo la Tukutuku ambapo nyumba zaidi ya Mia zilivunjwa kwa kujengwa maeneo yasiyoruhusiwa na bila kibali cha manispaa. Kanisa hilo linajengwa katikati ya barabara bila kibali? Au ndio afisa mipango miji katoa kibali Cha kujenga katikati ya barabara be? Haya yanafanyika huku Mkuu wa Mkoa yupo, Mkuu wa Wilaya yupo, Mkurugenzi yupo, Afisa Mipango Miji yupo na taarifa za malalamiko wanazo au ndiyo ukweli wa maneno ya rais Magufuri kuwa Tabora wamekalia majungu hawafanyi kazi?

NB: Kanisa na nyumba ya mchungaji vimejengwa kuziba barabara. Muziki mkubwa kanisani waliomo ndani sasa hata kumi hawafikiriki.

View attachment 1701280
Hilo kanisa mbona lipo miaka mingi sana au nimekosea location ?
 
Hilo kanisa mbona lipo miaka mingi sana au nimekosea location ?
Hapana , hilo kanisa lilikuwa Mwanga Shop kata ya Cheyo wakafukuzwa kwa wehu wao. Ndio wakamia hapo . Mleta mada Ni mkweli kabisa happy Kuna makanisa mbali kidogo la Efata , Moravian na lingine jirani na Westland school yote haya hayana tatizo ni wastaarabu wana muziki wanafungulia taratibu bila shida isipokuwa hawa vichaa ni vichaa kabisaaa , maajabu serikali kuruhusu vichaa kuongeza mambo ya ndoa , kumuandaa mwanamke kabla ya tendo huku spika zikiwa wazi kwa sauti kubwa .
 
Hapana , hilo kanisa lilikuwa Mwanga Shop kata ya Cheyo wakafukuzwa kwa wehu wao. Ndio wakamia hapo . Mleta mada Ni mkweli kabisa happy Kuna makanisa mbali kidogo la Efata , Moravian na lingine jirani na Westland school yote haya hayana tatizo ni wastaarabu wana muziki wanafungulia taratibu bila shida isipokuwa hawa vichaa ni vichaa kabisaaa , maajabu serikali kuruhusu vichaa kuongeza mambo ya ndoa , kumuandaa mwanamke kabla ya tendo huku spika zikiwa wazi kwa sauti kubwa .
Yeah nafikir la EFATA ndiyo lina muda mrefu kuliko hayo mengine.
Wayback 2010 hilo la karibu na Westland ndiyo walikuwa anajenga
 
Nikiwa Tabora ambapo nilikwenda kwenye msiba wa rafiki yangu aliyefiwa na mama yake mwezi huu. Nilikutana na kituko cha mwaka ambapo tukiwa hapo msibani ulisikika muziki mkubwa sana kiasi ambacho huwezi kuongea na mtu jirani yako, huwezi kupokea simu au kusikiliza simu. Nilipouliza nikaambiwa hilo ni kanisa la walokole Bethel, ambao walifukuzwa kutoka kata ya cheyo ndio wamehamia Kariakoo Tabora kata ya Kitete, ambapo toka wahamie Muziki ni masaa 24 kwa sauti ya juu sana.

Wakazi wa eneo hilo licha ya kulalamika kwa mkuu wa wilaya kwa maandishi DC Komanya, mkurugenzi, mtendaji kata, mwenyekiti wa mtaa, polisi mkuu wa kituo Mmassy, OCD, bado kanisa hilo linaendelea na fujo, vurugu huku mchungaji wa kanisa hilo Mch Jackson akiwambia wakazi hao kuwa serikali yote ya mkoa ameiweka mfukoni.

Mbaya zaidi huyo kaamua kujenga katikati ya barabara na kuziba barabara mtaa hivyo hapapitiki kwa gari, huwezi kupitisha mgonjwa, maiti hata kwa matumizi ya kawaida.

Jirani na kariakoo Ni eneo la Tukutuku ambapo nyumba zaidi ya Mia zilivunjwa kwa kujengwa maeneo yasiyoruhusiwa na bila kibali cha manispaa. Kanisa hilo linajengwa katikati ya barabara bila kibali? Au ndio afisa mipango miji katoa kibali Cha kujenga katikati ya barabara be? Haya yanafanyika huku Mkuu wa Mkoa yupo, Mkuu wa Wilaya yupo, Mkurugenzi yupo, Afisa Mipango Miji yupo na taarifa za malalamiko wanazo au ndiyo ukweli wa maneno ya rais Magufuri kuwa Tabora wamekalia majungu hawafanyi kazi?

NB: Kanisa na nyumba ya mchungaji vimejengwa kuziba barabara. Muziki mkubwa kanisani waliomo ndani sasa hata kumi hawafikiriki.

View attachment 1701280
watu wamesogezewa huduma ya injili hapo
 
watu wamesogezewa huduma ya injili hapo
Hapo hakuna injili , Kuna vichaa na wajasilia dini tupu tena wehu kasoro kuvua nguo .Injili ndio unasema ufundishe jinsi ya kumuandaa mwanamke kabla ya tendo spika zikiwa wazi , watoto chini ya miaka kumi na nane 18 wakiwa wanasikia wa ndani na n'nje hilo wanaloita kanisa lao . Kupiga muziki kama wehu kwa sauti ya juu ndio injili ? Kuathiri majirani , wagonjwa , wazee, watoto ndio injili ? Injiliya wapi ? Ya nani ? Maana maandiko yako wazi soma 6:5 Mathayo Tena msalipo msiwe Kama wale wanafiki wanaotaka kuonekana na watu .
 
Nikuambie kitu?

Tatizo linaanzia kwa Mwenyekiti wa Mtaa. Wananchi mpaka wanaandika barua kwa Mkurugenzi ambapo shughuli hiyo ni ndogo sana kwa Mwenyekiti wa Mtaa ni wazi kuna tatizo kubwa kwenye ngazi hiyo
Mwenyekiti wa mtaa Ni empty set na njaa kali .
 
Majirani hapo pia wanaweza kuwasha moto juu ya moto.Mikesha ya vigodolo na miziki ya kutosha kwa mwezi mfululizo.
Huo mtaa unageuka pahala pa burudani za kidunia na Heaven.

Ukitaka kujua ubaya wa maeneo kama hayo uwe na Mtoto au mgonjwa utelewa hayo mahubiri na huo mziki jinsi unavyoumiza.

Nina ushahidi mdogo sana miaka ya 2014 Mahala flani Moro..kuna jirani alisumbua sana wenzake na Midundo mizito zaidi ya hiyo.

Basi miaka ile kila mtu aliiweka Serikali mfukoni.
Nyumba moja ilijichanga ukaletwa mzigo wenye watts za kutosha.Ukapigwa masaa 24.Ukipata joto huu unawashwa huu.
Mpaka leo mtaa ule huwezi washa mziki wa aina yoyote ile kwa sauti mana pana Historia hiyo.Kuwa wewe washa utakodishwa ambao utakaa karibu yako bila kuchoka.
Tena kuna ngoma kali sana za Kibongo..mkito mkito..Unapigwa mziki mpaka viumbe vya ardhini vinakuja juu.
Kuabudu na kusifu bila kujali mazingira yanayozunguka.Ni unafiki wa hali ya juu kabisa na ni roho mbaya mno sio Upendo huo.
 
Kuna matatizo mengi sana mengine ukifuata taratibu za kiubinadamu basi utachelewa.
Niliwahi kuumwa sana nikatoka Hospital kuugulia nyumbani , jirani yangu hakuwa anajali.Ni kelel na mziki mkali.Ikanilazimu kumdadisi jirani anatumia chombo ipi.
Huku tunachekeana nilikuja kuleta chombo mara 3 ya alicho nacho..sasa kuna amani na utulivu pia.
Mana napenda mziki..kuna mida flani unajua huu watu wamechoka unawasha sasa kutuma salamu kuwa your not alone.
Tutavunja hizi kuta😀😀😀
Maisha sasa yapo poa kabisa..unyonge unyonge wa kwenye Serikali za mitaa haupo tena.
Tunavyo visa vingi sana..vya namna hiyo..
 
Majirani wa hapo kwa kuwa wanajua tatizo.Wanaweza anzisha nao kanisa lao la Praise and Worship..Hapo mnatafuta Pastor wenu analipwa unapigwa mziki na kuomba mpaka Malaika mbinguni wanasema naaam.

Maana si watu wameamua fujo...ya nini kulia lia.
Vijana wapo na hzi kazi wanaziweza hapa mjini.
Unyonge upungue...
 
Usiwaite vichaa watumishi wa Mungu aliye hai. Utapigwa na Mungu. Usitafute sifa humu JF. shauri yako.
Hapana , hilo kanisa lilikuwa Mwanga Shop kata ya Cheyo wakafukuzwa kwa wehu wao. Ndio wakamia hapo . Mleta mada Ni mkweli kabisa happy Kuna makanisa mbali kidogo la Efata , Moravian na lingine jirani na Westland school yote haya hayana tatizo ni wastaarabu wana muziki wanafungulia taratibu bila shida isipokuwa hawa vichaa ni vichaa kabisaaa , maajabu serikali kuruhusu vichaa kuongeza mambo ya ndoa , kumuandaa mwanamke kabla ya tendo huku spika zikiwa wazi kwa sauti kubwa .
 
Majirani hapo pia wanaweza kuwasha moto juu ya moto.Mikesha ya vigodolo na miziki ya kutosha kwa mwezi mfululizo.
Huo mtaa unageuka pahala pa burudani za kidunia na Heaven.

Ukitaka kujua ubaya wa maeneo kama hayo uwe na Mtoto au mgonjwa utelewa hayo mahubiri na huo mziki jinsi unavyoumiza.

Nina ushahidi mdogo sana miaka ya 2014 Mahala flani Moro..kuna jirani alisumbua sana wenzake na Midundo mizito zaidi ya hiyo.

Basi miaka ile kila mtu aliiweka Serikali mfukoni.
Nyumba moja ilijichanga ukaletwa mzigo wenye watts za kutosha.Ukapigwa masaa 24.Ukipata joto huu unawashwa huu.
Mpaka leo mtaa ule huwezi washa mziki wa aina yoyote ile kwa sauti mana pana Historia hiyo.Kuwa wewe washa utakodishwa ambao utakaa karibu yako bila kuchoka.
Tena kuna ngoma kali sana za Kibongo..mkito mkito..Unapigwa mziki mpaka viumbe vya ardhini vinakuja juu.
Kuabudu na kusifu bila kujali mazingira yanayozunguka.Ni unafiki wa hali ya juu kabisa na ni roho mbaya mno sio Upendo huo.
Kuna watu kadhaa hapo wanapaswa kuwajibishwa
1.
Mtendaji wa mtaa (yeye ni mlinzi wa amani wa mtaa)

2.
Mwenyekiti wa Mtaa (mwenyekiti wa ulinzi na usalama mtaa)

3.
Mtendaji wa Kata (mwenyekiti wa ulinzi na usalama Kata)

4.
OCS (katibu ulinzi na usalama Kata)

5.
DAS (Katibu wa kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya)

Wakibanwa hao utaona matokeo kabla hakujapambazuka
 
Usiwaite vichaa watumishi wa Mungu aliye hai. Utapigwa na Mungu. Usitafute sifa humu JF. shauri yako.
Mkuu hao ni vichaa kabisaaa na ni watumishi wa ibilisi sio Mungu . Mungu hawezi kutuma watu waende kuwa kero kwa wengine , waende kutesa wagonjwa , wazee , watoto ambao ni majirani kwa upumbafu wao wa kupiga muziki kiendawazimu. Ukiona mambo yamefika humu ujue moto umekolea umebakiza kulipuka tu . Wehu wao huu hapa 1. Kupiga muziki kwa sauti kubwa sana ? Kutoa mahubiri ya ndoa kuandaa mwanamke mbele ya watoto na spika zikiwa wazi .3. Walipohamia kutoka cheyo walikofukuzwa , hawakuwa na choo hapo walikuwa wanavamia vyoo vya majirani bila kuomba 4. Walikuwa wanavamia visima vya majirani kuteka maji . 5. Walipojenga choo wakawa wanachukua ndoo zao za chooni wanadumbukiza kwenye visima vya majirani kuteka maji . Hawa wehu ndio wamuombe Mungu anidhulu ? Masihara .
 
Kuna matatizo mengi sana mengine ukifuata taratibu za kiubinadamu basi utachelewa.
Niliwahi kuumwa sana nikatoka Hospital kuugulia nyumbani , jirani yangu hakuwa anajali.Ni kelel na mziki mkali.Ikanilazimu kumdadisi jirani anatumia chombo ipi.
Huku tunachekeana nilikuja kuleta chombo mara 3 ya alicho nacho..sasa kuna amani na utulivu pia.
Mana napenda mziki..kuna mida flani unajua huu watu wamechoka unawasha sasa kutuma salamu kuwa your not alone.
Tutavunja hizi kuta😀😀😀
Maisha sasa yapo poa kabisa..unyonge unyonge wa kwenye Serikali za mitaa haupo tena.
Tunavyo visa vingi sana..vya namna hiyo..
Mkuu na sisi tunataka tununue vyombo vyenye uwezo mara kumi yake ili wakianza tu muziki wao na sisi tunafungulia mpaka mwisho ndio serikali itaelewa ?
 
Kuna watu kadhaa hapo wanapaswa kuwajibishwa
1.
Mtendaji wa mtaa (yeye ni mlinzi wa amani wa mtaa)

2.
Mwenyekiti wa Mtaa (mwenyekiti wa ulinzi na usalama mtaa)

3.
Mtendaji wa Kata (mwenyekiti wa ulinzi na usalama Kata)

4.
OCS (katibu ulinzi na usalama Kata)

5.
DAS (Katibu wa kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya)

Wakibanwa hao utaona matokeo kabla hakujapambazuka
Hao wote taarifa wanazo ila hawataki kuchukua hatua .
 
Back
Top Bottom