#COVID19 Alichonihadithia jamaa yangu anayesoma China kuhusu chanjo ya COVID-19, kimenistua

#COVID19 Alichonihadithia jamaa yangu anayesoma China kuhusu chanjo ya COVID-19, kimenistua

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Ninaye rafiki yangu anayesoma China ambaye yupo huko takribani miaka 3 sasa. Nilipojaribu kumuuliza kuhusu namna serikali ya China inavyofanya kuhamasisha raia wake kuchanja chanjo ya Covid, au kuhakikisha kila raia wake amechanja ili kujikinga na corona.

Yule rafiki yangu ameniambia serikali ya China imetengeneza chanjo na kuiweka kwenye vituo vya Kutolea huduma alafu raia yeyote anayetaka kuchanja aende mwenyewe kwa hiyari yake.

Wala huwezi kukuta afisa au kiongozi wa serikali akisisitizia watu kuchanja. Alichoniambia ni kwamba mkazo mkubwa wamewekeza kwenye kinga. Inavyoonekana wamepuuza kwa kiasi mambo ya chanjo.

Sasa najiuliza huku ndiko corona ilikoanzia, wao wameendelea sana kiteknolojia kuliko sisi, iweje sisi tusisitize suala la chanjo kiwango cha kutaka kulazimishana wakati wazalisha chanjo hawajafikia huko?

Ni kwa nini tunajilazimisha kuchukua chanjo zao hali ya kuwa hata wenye chanjo wenyewe hawaziamini kiwango hiki?

Ni kwa nini serikali yetu inatumia nguvu kubwa sana, ukizingatia alinidokeza nesi mmoja kwamba wamepewa kila mtu kuchanja watu hamsini kwa siku?
 
Ukweli ni kwamba, waliochanja wanawaonea wivu wasiochanja, kwamba kama kuna madhara kwny chanjo basi mnataka tuyaipate wote

Ukichanja unapata covid, usipochanja unaipata pia..

Watueleimishe tu athari za kuchanja na kutokuchanja tujipime
 
Mkuu kwanini uhangaike? Wewe kama hujisikii kuchanja acha tu endelea na mambo mengine, waache wanaotaka kuchanja. Huna haja kuhangaisha nafsi yako

We si unamuamini rafiki yako allyeko China? Inatosha mkuu, achana na mambo ya chanjo we endelea na mengine tu
 
Siku nyingine baada ya kumsikiza rafiki yako, nawe ufanye research japo kwa uchache kabla ya kufanya hitimisho...

Kitakwimu, China ni nchi ya 6 ulimwenguni kwa kuwa na watu wengi waliochanjwa (sasa imagine ilivyo na watu wengi na bado wapo nambari 6)

Screenshot_20220202-153629-2.png


 
Hivi hapa kwetu ni lazima!!??!!, mi sijawahi kufuatwa na mgambo au yeyote akanilazimisha kwenda kuchanjwa. lakini tujue tu kwamba wenzetu wameshaendelea sana hasa kwenye sector ya afya hivyo hutilia mkazo sana kwenye kinga za kawaida ili kuuepusha mwili na kemikali za tiba. hapa kwetu ni tofauti imagine ije lockdown au tulazimishwe kuvaa barakoa popote kwenye mkusanyiko nayo tutaona ni mateso tu
 
kwani Tz tumelazimishwa kuchanja? mbona ni hiari tu? ila ukiwa unaenda nchi zao ndio lazima uchanje, muulize huyo aliyepo china, tunaingia huko?
 
Pata chanjo wewe...utajuta siku ukiunasa huo ugonjwa...milioni tatu hadi none lazima zikuishe
 
Mkuu kwanini uhangaike? Wewe kama hujisikii kuchanja acha tu endelea na mambo mengine, waache wanaotaka kuchanja. Huna haja kuhangaisha nafsi yako

We si unamuamini rafiki yako allyeko China? Inatosha mkuu, achana na mambo ya chanjo we endelea na mengine tu
Mkuu, huko vijini sasa hivi Serikali ya Tanzania inachanja watu kwa nguvu, mama akipeleka mtoto kliniki hapati huduma hadi mama achanjwe chanjo ya Corona.
 
Mkuu, huko vijini sasa hivi Serikali ya Tanzania inachanja watu kwa nguvu, mama akipeleka mtoto kliniki hapati huduma hadi mama achanjwe chanjo ya Corona.
Kijiji gani?
 
Mkuu, huko vijini sasa hivi Serikali ya Tanzania inachanja watu kwa nguvu, mama akipeleka mtoto kliniki hapati huduma hadi mama achanjwe chanjo ya Corona.
Una uhakika na hizi tuhuma ?
Ungeujua mchakato wa kupata chanjo usingeongea hivi, kwa kifupi ni kwamba una taarifa finyu sana juu ya zoezi zima la utoaji wa chanjo ya Covid hapa nchini.
 
kwani Tz tumelazimishwa kuchanja? mbona ni hiari tu? ila ukiwa unaenda nchi zao ndio lazima uchanje, muulize huyo aliyepo china, tunaingia huko?
Kaniambia kule ukiingia huulizwi chanjo ila unapimwa kama umeambukizwa hiyo tu inatosha na sio raia toka nje tuu bali hata wao ukitoka jimbo moja kwenda kingine sharti muhimu sio chanjo ila ni kupimwa ikiwa una maambukizi
 
Pata chanjo wewe...utajuta siku ukiunasa huo ugonjwa...milioni tatu hadi none lazima zikuishe
Suala la kuugua halina kinga ni ninachojiuliza ni kwa nini taifa la china wenye kuaminika kuwa na sheria ngumu hawalazimishi wananchi wao kuchanja?
 
Back
Top Bottom