Alikufa tar 24/7 na alizaliwa tar 24/7 na zote zikiwa ni Ijumaa

Alikufa tar 24/7 na alizaliwa tar 24/7 na zote zikiwa ni Ijumaa

Duu poleni 24/7 tarehe yangu ya kuzaliwa kuna Uzi mmoja nlikua namtafuta pacha wangu kumbe kashatangulia mbele ya haki
 
Weee bidada lile jukwaa uloniad cjaiona mpk leo nifah

Sasa hivi upepo upo siasani mwaya, subiri uchaguzi ukishaisha ndio tutatafutana kwenye yale 'mambo' yetu na nitakuelewesha vizuri hilo swali lako.
 
Last edited by a moderator:
pole sana...

ila kuna "unproven theory" about days za kuzaliwa na days za kufa...miezi na siku zinakuwa na tabia za kushabihiana...
 
Manaake hatorudi tena.na wewe jiandae ife mikononi.mwa Yesu
 
Wakuu habari zenu,

Kuna swala limenishangaza kidogo! Kuna mdogo wangu amefariki juzi Ijumaa ya tar 24/7/2015 kwa ugonjwa wa kansa ya utumbo mpana. Siku mbili nyuma kabla hajafa alikuwa anaongea vitu vya ajabu ajabu na akili inakuwa sawa, ila siku ile ambayo alikuwa anakata roho alikuwa anaongea kiarabu si kiarabu yaani alikuwa anaongea lugha isiyoeleweka na kabla ya kukata roho aliniambia nipige magoti na akanishika kichwani huku akitaja jina langu. Na pia alifanya hivyo kwa watu wote tuliokuwa tunamuhudumia kwa ukaribu sana.

Ila kilichonishangaza zaidi ni kitendo cha kufa tarehe aliyozaliwa na zote zikiwa ni siku ya ijumaa! Alizaliwa 24/7/92 na amekufa 24/7/2015 zote zikiwa ni ijumaa.

Swali langu ni kwamba hii inaweza kuwa na maana yoyote?

Marehemu alikuwa anakupa unabii ! Fungua Kanisa upige hela !
 
Back
Top Bottom