mrangi
JF-Expert Member
- Feb 19, 2014
- 88,759
- 123,368
Kuna mambo mengine humu huwezi zungumza!ila nashangaa sjui zombe amekwepaje kwepaje mpk akachomoka kwenye kesi hiyo.....Enzi za Zombe
Ova
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna mambo mengine humu huwezi zungumza!ila nashangaa sjui zombe amekwepaje kwepaje mpk akachomoka kwenye kesi hiyo.....Enzi za Zombe
Ila wanaomfahamu nasikia ukimuona hayuko vizuri sana kiakili japo sio kichaa paseeeKuna mambo mengine humu huwezi zungumza!ila nashangaa sjui zombe amekwepaje kwepaje mpk akachomoka kwenye kesi hiyo.....
Ova
Yeah ila waliouliwa watarudishia uhai?huoni hapo mahakama nayo imetenda kosa la kusabibisha uhai mwingine upoteeAfe na yeye aone uchungu kama ni muhusika
Yaani mijitu imetenda kosa la mauaji 2006,hukumu ikatoka 2016,miaka 10 baadae!Hii mijitu bado inapumua!View attachment 1111303
Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Mrakibu wa Polisi (SP), Christopher Bageni, aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kuwaua wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro, amepinga adhabu hiyo katika Mahakama Rufaa jijini Dar es Salaam.
SP Bageni amewasilisha maombi ya mapitio Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambayo yamepangwa kusikikizwa Juni 16, mwaka huu mbele ya jopo la majaji watatu, Stellah Mugasha, Ferdinand Wambali na Rehema Kerefu.
Katika maombi yake ya mapitio, Bageni amewasilisha sababu mbalimbali za kupinga adhabu hiyo ikiwamo kwamba jopo la majaji lilifanya makosa ya dhahiri katika muonekano na hivyo kusababisha haki kutozingatiwa katika kutoa hukumu hiyo.
SP Bageni alihukumiwa adhabu hiyo Septemba 16 mwaka 2016 na Mahakama ya Rufaa ya Tanzania mbele ya jopo la majaji watatu, Jaji Benard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage.
Mahakama ya Rufaa ilitoa hukumu hiyo baada ya kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) akipinga aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO) Kamishna Msaidizi wa Polisi, Abdallah Zombe na maofisa wenzake watatu akiwemo Bageni kuachiwa huru na Mahakama Kuu mwaka 2009.
Hukumu hiyo ilisomwa na aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufaa wakati huo, Jaji John Kahyoza. Aliwataja wajibu rufani kuwa ni Zombe, SP Bageni, aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.
Katika kesi hiyo, wafanyabiashara wa madini waliouwawa ni Sabinus Chigumbi, maarufu Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva taksi, mkazi wa Manzese Dar es Salaam, Juma Ndugu.
Walidaiwa kutenda makosa hayo Januari 14, mwaka 2006, katika Msitu wa Pande, uliopo wilayani Kinondoni baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao Sinza, walipokuja Dar es Salaam kuuza madini.
Mtanzania
Ataishi kwa shida sanaIla wanaomfahamu nasikia ukimuona hayuko vizuri sana kiakili japo sio kichaa paseee
Fair enough mkuu,nimefurahishwa na ujibuji wa hoja hii,umetumia facts kujibu hoja ahsante na haya ndio majadiliano ya JF,tuna haki ya kutofautiana,ninashukuru kwa wewe binafsi kujua kuwa Mr.Bageni alihusika na ninategemea ulitoa ushahidi wako,ILA swali langu hapa je kunyongwa hadi kufa kwa Mr.Bageni (au mtu yeyote )ndio kutatufanya watanzania tuogope makosa yanayakuja na death penalty?utafiti mwingi tu hapa duniani imethibitisha kuwa death sentence sio kinga kwa watu kutotenda makosa ya aina hii,states nyingi za USA zinafuta adhabu hii(kwangu bado ni ya kinyama)na hapa Africa kuna nchi ambazo hazina death sentence na still haki inatendeka,na ulipogusia kuwa serikali yetu itaonekana inatenda HAKI ,hii sio kweli and its a debate of another day.Kumuua BAGENI hakutarudisha uhai wa kina Chigumbi ila itakua fundisho kwa polisi wengine wanao ua watu wasio na hatia na kuwaibia. Vile vile kutaonyeaha kwamba institutions za serikali hii ziko hai na serikali inasimamia haki sio serikali ya wacha wapigwe tu kama untouchable mmoja alivyosemaga. Binafsi najua Bageni alihusika kuwaua wale watu huku akijua ni kosa mbele ya binadamu na dhambi mbele za Mungu.
Otherwise atuambie walikufaje au nani aliwau?
ninatanguliza pole zangu kwa ndugu na familia za wafanya biashara hao waliopoteza maisha yao kinyama mno ,familia hizi zinaishi bila wapendwa wao na bread winners wao its tough life;ILA kwa upande wa pili wa adhabu hii ya KIFO,hivi ikitekelezwa itaifanya familia za waliouawa kuwa happy?,je utarudisha uhai wa ndugu zao?,je na familia za waliohukumiwa kifo zitakuwa ni familia bora zaidi?je kunyongwa hadi kufa kwa mtuhumiwa kutaleta better closure kwa wanandugu waliopoteza ndugu zao?,binafsi ninachukia adhabu hii ya kifo,ni adhabu inayoonyesha kuwa bado tunaishi maisha very primitive,na adhabu hii sio kuwa unafanya watu waogope kutenda kosa la kuuwa eti na wao watauliwa.ni wakati sasa Tanzania ifute hii adhabu ya kifo maana haina faida yeyote kwa jamii.
sawa mkuu ila fanya kautafiti kadogo ndani ya nchi yetu,je adhabu hii imepunguza hayo makosa uliyoyaorodhesha hapo juu?na elewa hizi adhabu mara nyingi zinakuja na makosa mengi ya kunyonga watu wasio na hatiaHii adhabu haitekelezwi ili kurudisha waliouawa au kuboresha maisha ya ndugu walioachwa au watakaoachwa, inatekelezwa ili mimi na wewe tuogope kufanya uhalifu wa aina hiyo, kama hakuna adhabu ya kifo, mimi naweza kuja nyumbani kwako, nikakulawiti wewe, mke wako na binti yako, kisha nikawaua kwa kuwachinja mkeo na binti yako, Je, wewe uliyebaki, utajisikia vizuri kuniona mimi niko hai ili mradi tu niko gerezani? Gerezani ni maisha tu kama maisha mengine, kuna watu kule wanakula vizuri tu na kuishi vizuri..
Je, ni haki kwa aliyekatisha maisha ya wengine kikatili, kuendelea kula bata tu huko gerezani?
Ahsante sana Deceiver................ umeniongezea elimu mkuu. BarikiwaMrakimu ni superintendent of polisi. Hii ni ngazi ya tano kwa maafisa wa polisi.
1. Assistant inspector of police
2. Inspector of police
3. Senior inspector of police
4. Assistant superintendent of police
5. SUPERINTENDENT OF POLICE
Ni ngazi kubwa. Hua anasimamia wilaya au kituo kama Urafiki. Mabatini. Oysterbay na police post za sehemu sugu kama Kigogo na Kwa aziz ally
Marejeo ndiyo review au revisionView attachment 1111303
Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Mrakibu wa Polisi (SP), Christopher Bageni, aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kuwaua wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro, amepinga adhabu hiyo katika Mahakama Rufaa jijini Dar es Salaam.
SP Bageni amewasilisha maombi ya mapitio Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambayo yamepangwa kusikikizwa Juni 16, mwaka huu mbele ya jopo la majaji watatu, Stellah Mugasha, Ferdinand Wambali na Rehema Kerefu.
Katika maombi yake ya mapitio, Bageni amewasilisha sababu mbalimbali za kupinga adhabu hiyo ikiwamo kwamba jopo la majaji lilifanya makosa ya dhahiri katika muonekano na hivyo kusababisha haki kutozingatiwa katika kutoa hukumu hiyo.
SP Bageni alihukumiwa adhabu hiyo Septemba 16 mwaka 2016 na Mahakama ya Rufaa ya Tanzania mbele ya jopo la majaji watatu, Jaji Benard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage.
Mahakama ya Rufaa ilitoa hukumu hiyo baada ya kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) akipinga aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO) Kamishna Msaidizi wa Polisi, Abdallah Zombe na maofisa wenzake watatu akiwemo Bageni kuachiwa huru na Mahakama Kuu mwaka 2009.
Hukumu hiyo ilisomwa na aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufaa wakati huo, Jaji John Kahyoza. Aliwataja wajibu rufani kuwa ni Zombe, SP Bageni, aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.
Katika kesi hiyo, wafanyabiashara wa madini waliouwawa ni Sabinus Chigumbi, maarufu Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva taksi, mkazi wa Manzese Dar es Salaam, Juma Ndugu.
Walidaiwa kutenda makosa hayo Januari 14, mwaka 2006, katika Msitu wa Pande, uliopo wilayani Kinondoni baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao Sinza, walipokuja Dar es Salaam kuuza madini.
Mtanzania
Jane A Chipofya wa Isanga,kafa na uzuri wake binti wa kimalawi yule...Mh hiyo kesi ilisikitisha sana kwanza mashahidi walikua wengi mpaka wakapunguzwa kwa sababu ushahidi wengine ulikua unafanana cha ajabu Zombe hakupatikana na hatia...ila police wengine walioachiwa kwa kesi hiyo nao walitangulia mbele ya haki hata yule Mwanamke pekee pia alishafariki...
Kumbuka tu maafisa wa polisi ni wanaovaa nyota mabegani. Hawa wanaovaa V kama matrafiki wengi sio maafisa wa polisi.Ahsante sana Deceiver................ umeniongezea elimu mkuu. Barikiwa
Mrakimu ni superintendent of polisi. Hii ni ngazi ya tano kwa maafisa wa polisi.
1. Assistant inspector of police
2. Inspector of police
3. Senior inspector of police
4. Assistant superintendent of police
5. SUPERINTENDENT OF POLICE
Ni ngazi kubwa. Hua anasimamia wilaya au kituo kama Urafiki. Mabatini. Oysterbay na police post za sehemu sugu kama Kigogo na Kwa aziz ally
Umeacha SIPA/Insp.; Insp.; ASP; SP; SSP; ACP; SACP;...
I don't think so!Ndg za marehem nao wazembe..huyu mm nisingemwacha salama
Alifia hotelini,chezea damu ya mtu!Huu ni ukweli
I don't think so!