Aliyekuwa Mrakibu wa Polisi, Kinondoni akata rufaa dhidi ya hukumu yake ya kunyongwa hadi kufa

Aliyekuwa Mrakibu wa Polisi, Kinondoni akata rufaa dhidi ya hukumu yake ya kunyongwa hadi kufa

Yaani mijitu imetenda kosa la mauaji 2006,hukumu ikatoka 2016,miaka 10 baadae!Hii mijitu bado inapumua!
MTU atakae pinga kwamba haya majambazi hayakutena kosa la mauaji,inabidi aperekwe milembe apimwe akili.
Ingekuwa USA,hawa watu hawakutakiwa kushitkiwa na jeshi la polisi,ambalo wao walikuwa miongoni mwake,hapa haki haiwezi kutendeka,upelelezi wa hii kesi ilibidi ufanywe na kikosi maalum kutoka Takukuru.
Tume maalum iliundwa chini ya Jaji....
 
Mrakimu ni superintendent of polisi. Hii ni ngazi ya tano kwa maafisa wa polisi.
1. Assistant inspector of police
2. Inspector of police
3. Senior inspector of police
4. Assistant superintendent of police
5. SUPERINTENDENT OF POLICE
Ni ngazi kubwa. Hua anasimamia wilaya au kituo kama Urafiki. Mabatini. Oysterbay na police post za sehemu sugu kama Kigogo na Kwa aziz ally
Namba 3 hakuna cheo kama hicho
 
Eti mimi nilifanya kazi ya police aliefyatua risasi hajakamatwa ila waliohusika kufanya mpango mpaka wa mauaji hawana hatia wakati hela na Madini waliondoka nayo hukumu ya kesi ile ilikua haipo sawa kwa wengine kuachiwa ni vile walikua police na hukumu ilikua inawabeba ilitaliwa wachukuliwe kama majambazi tuu asingetoka mtu pale....majambazi yameteka na kuua mambo ya huyu alirudisha risasi sawa wapi na wapi wakati wote walitenda njama ya kuteka,kuua na kuondoka na Mali... hakuna hukumu nyepesi ya vile kwa wengine kuachiwa uraiani...
Nikurekebishe kidogo ni kwamba baada ya zombe and Co kutekeleza hilo tukio mwanzo kabisa ilijulikana wale wafanya biashara walikuwa majambazi hvyo askar wote waliokuwa zamu hyo siku walirudisha silaha zao salama bila tatzo ila sekeseke likaanza siku tatu au nne baada ya tukio baada ya baadhi ya wananchi Ku rise hoja kwamba wale hawakuwa majambazi Bali wafanyabiashara, na ndipo wakaamuliwa askar wote waliokuwa zamu wakamatwe na kuwekwa mahabusu huku tume ya uchunguzi ya Kipenka ikienderea .. Hapo ndipo yule askar aliyefyatua risas akapata mwanya Wa kutokomea mpaka Leo hii
 
sawa mkuu ila fanya kautafiti kadogo ndani ya nchi yetu,je adhabu hii imepunguza hayo makosa uliyoyaorodhesha hapo juu?na elewa hizi adhabu mara nyingi zinakuja na makosa mengi ya kunyonga watu wasio na hatia
Hiyo ya kunyonga watu wasio na hatia haihusiani..

Ukisema kufanya utafiti, sio kuangalia kama adhabu imesaidia kupunguza uhalifu, unatakiwa uchukua kipindi ambacho hakukuwa na hiyo adhabu kisha ulinganishe na kipindi ambacho kuna adhabu hiyo.. Wewe umefanya utafiti gani?

Kwa saikolojia ya kawaida tu, kama nikiua watu kwa kukusudia halafu mimi siuwawi, siwezi kuogopa kuua, maana najua mimi nitaendelea kuishi, nitaendelea kuonana na familia yangu na ndugu zangu na washkaji watakuwa wananilitea fegi naendelea kupuliza, wewe na familia yako mmezikwa.

Labda nirudi kwenye hoja ya kunyonga watu wasio na hatia; kwa namna yeyote ile, suluhisho sio kuondoa adhabu, ni sawasawa na kuondoa adhabu ya kifungo gerezani kwa sababu kuna watu wanafungwa bila hatia, nadhani mfano umejitosheleza.

Tuendelee, naona sijachoka kuandika, mkuu wewe una umri gani? Unauelewe mpana wa wahalifu na aina za uhalifu unaofanywa na binadamu?
Kuna binadamu huwa wanafanya uhalifu ambao ukiusikia au kuuona utakubali mtu kama huyo adhabu ya kunyongwa ni sawa, kuna mtu ana historia ya uhalifu na ukatili tangu mdogo, uporaji wa kutumia silaha na kuua, mtu kama huyo, anahukumia kukaa gerezani, lakini mtu huyohuyo, anamuua mfungwa mwenzie, mhalifu kama huyo wamfanyeje? Tayari wameshamfunga kifungo cha maisha lakini anaua wafungwa wenzake..

Wamuongezee kifungi kingine cha maisha ili aendelee kuwaua wenzie au wafanyaje?
 
Naomba ni-declare interest kwamba niliwahi kufanya kazi Jeshi la Polisi tena Kikosi hicho hicho cha kupambana na majambazi na mpaka naacha kazi nilikuwa hapo hapo Oysterbay,na askari wote waliokumbwa na kesi ninawafahamu maana nilifanya nao kazi,hukumu ya Jaji Kipenka ya kuwaachia huru watuhumiwa wote ilikuwa sahihi maana askari aliyewafyatulia wale marehemu hakuwahi kukamatwa mpaka leo!! wengine wote walirudisha silaha zao Armory zikiwa na risasi kamili kama walivyochukua isipokuwa huyo mmoja,ndio maana Jaji Kipenka wakati anawaachia huru watuhumiwa alisema kabisa "MLETENI MTUHUMIWA ALIYEUA MAANA YEYE NDIE ALIRUDISHA SILAHA IKIWA HAINA RISASI"kwa hiyo naamini hili Jopo la Majaji wa Mahakamani ya Rufaa nitamuachia huru Christopher Bageni maana hakufyatua risasi hata moja kuua marehemu
Hivi askari kurudisha silaha jioni ikiwa na idadi ile ile ya risasi alizokabidhiwa asubuhi inaweza kuwa utetezi tosha kwamba askari huyo hakutumia silaha yake kuua? Maana kama askari mwenyewe kama ana tabia ya kushiriki kwenye matukio machafu ya mauaji ili kujinufaisha si kazi ngumu kwake yeye kuwa na risasi zake za pembeni za kufanyia kazi na unapofika muda wa kurudisha silaha ofisini anarudisha na risasi kwa idadi ile ile aliyokabidhiwa.
 
ninatanguliza pole zangu kwa ndugu na familia za wafanya biashara hao waliopoteza maisha yao kinyama mno ,familia hizi zinaishi bila wapendwa wao na bread winners wao its tough life;ILA kwa upande wa pili wa adhabu hii ya KIFO,hivi ikitekelezwa itaifanya familia za waliouawa kuwa happy?,je utarudisha uhai wa ndugu zao?,je na familia za waliohukumiwa kifo zitakuwa ni familia bora zaidi?je kunyongwa hadi kufa kwa mtuhumiwa kutaleta better closure kwa wanandugu waliopoteza ndugu zao?,binafsi ninachukia adhabu hii ya kifo,ni adhabu inayoonyesha kuwa bado tunaishi maisha very primitive,na adhabu hii sio kuwa unafanya watu waogope kutenda kosa la kuuwa eti na wao watauliwa.ni wakati sasa Tanzania ifute hii adhabu ya kifo maana haina faida yeyote kwa jamii.
Ngoja ndugu yako auwawe!
 
Hii adhabu haitekelezwi ili kurudisha waliouawa au kuboresha maisha ya ndugu walioachwa au watakaoachwa, inatekelezwa ili mimi na wewe tuogope kufanya uhalifu wa aina hiyo, kama hakuna adhabu ya kifo, mimi naweza kuja nyumbani kwako, nikakulawiti wewe, mke wako na binti yako, kisha nikawaua kwa kuwachinja mkeo na binti yako, Je, wewe uliyebaki, utajisikia vizuri kuniona mimi niko hai ili mradi tu niko gerezani? Gerezani ni maisha tu kama maisha mengine, kuna watu kule wanakula vizuri tu na kuishi vizuri..

Je, ni haki kwa aliyekatisha maisha ya wengine kikatili, kuendelea kula bata tu huko gerezani?
The world is not Fair.

Anayeua auawe tu
 
Sasa kwanini wasimpeleke??

Bdw Kwanini askari polis mnaua ua watu km njiwa unavyompiga manati??akili zenu wap zina shida nyie watu nyie??

mara mtulipue mibomu..shukuruni mtaa naoishi hakuna askari walah ningelala na m1 mbele...ningemtega akategeka..angekunywa sumu bila kupenda shenzy typ
Tuliza munkari dada

Kuna uzi kule uliletwa juu ya wanao kamatwa kwa kwenda Pm ,ukasema mtu wa Jf ukamatwe kwa lipi

Ukisoma katikati ya mistari hii comment yako ni sababu ya wewe kukamatwa

Ndio uzuri tu wa kuwa na ID feki
 
Hii adhabu haitekelezwi ili kurudisha waliouawa au kuboresha maisha ya ndugu walioachwa au watakaoachwa, inatekelezwa ili mimi na wewe tuogope kufanya uhalifu wa aina hiyo, kama hakuna adhabu ya kifo, mimi naweza kuja nyumbani kwako, nikakulawiti wewe, mke wako na binti yako, kisha nikawaua kwa kuwachinja mkeo na binti yako, Je, wewe uliyebaki, utajisikia vizuri kuniona mimi niko hai ili mradi tu niko gerezani? Gerezani ni maisha tu kama maisha mengine, kuna watu kule wanakula vizuri tu na kuishi vizuri..

Je, ni haki kwa aliyekatisha maisha ya wengine kikatili, kuendelea kula bata tu huko gerezani?

Tafiti za adhabu ya kifo zinasemaje?

Studies zinaonesha kwamba leading criminologists (crime experts) overwhelmingly do not believe the death penalty is an effective deterrent to crime. Huu ni ukweli; murder rates katika nchi zilizo na capital punishment aren’t necessarily lower than zile za nchi zisizo na capital punishment!
 
Huyu Bageni ni mfano wa Polisi wengi tu wanaofanya matukio kwa kutumia kivuli cha upolisi.
Mwisho wa siku haya ndiyo uwa yanawakuta.
 
kuna wadau kuelewa ni wagumu,aliyerudisha silaha ikiwa haina risasi ndie aliyewafyatulia wale marehemu wote risasi,namaanisha wote waliokuwa Doria walikuwa na silaha,but silaha iliyotumika ni moja tu ya huyo aliyekimbia
Ingekuwa vizuri ungemtaja kwa majina huyo mfyatua risasi ili akionekana popote pale akamatwe.
 
ninatanguliza pole zangu kwa ndugu na familia za wafanya biashara hao waliopoteza maisha yao kinyama mno ,familia hizi zinaishi bila wapendwa wao na bread winners wao its tough life;ILA kwa upande wa pili wa adhabu hii ya KIFO,hivi ikitekelezwa itaifanya familia za waliouawa kuwa happy?,je utarudisha uhai wa ndugu zao?,je na familia za waliohukumiwa kifo zitakuwa ni familia bora zaidi?je kunyongwa hadi kufa kwa mtuhumiwa kutaleta better closure kwa wanandugu waliopoteza ndugu zao?,binafsi ninachukia adhabu hii ya kifo,ni adhabu inayoonyesha kuwa bado tunaishi maisha very primitive,na adhabu hii sio kuwa unafanya watu waogope kutenda kosa la kuuwa eti na wao watauliwa.ni wakati sasa Tanzania ifute hii adhabu ya kifo maana haina faida yeyote kwa jamii.

Adhabu ya kifo ipo tu lakini sidhani na sina hakika kama wahukumiwa huwa wananyongwa.
 
Back
Top Bottom