Aliyemuelewa Mo Dewji kuhusu uwekezaji Simba atujuze

We utakuwa mzaramo ukishapata mihogo unaridhika...
Hizi hoja kuntu na huyu ndiye mwana simba wa ukweli
Tengua kauli ndugu kabila ya mtu na hayo mahaba yake ya kihayawani kwa Mo yanaingilianaje?
 

Tatizo la watu wanataka watafutwe mmoja mmoja wajibiwe kile walichonacho vichwani mwao, yaani kila alichokiuliza kilishatolewa maelezo tena siku nyingi sana uvivu wake wa kufatilia mambo na ile tu kuonekana nae kachangia ndio kinamfanya aandike aandikayo
 
Nadhani tutumie neno KUPANGA NI KUCHAGUA.
Kinachoweza kuwa sumu kwako, ni chakula kwa mwingine.

Hakuna haja ya kushikana mashati kwa sababu tumeamua kufanya machaguo tofauti.

Kimfaacho mtu, ndicho chake.
Spirit ya kunyamazisha, kuziba masikio na kupofua watu wasihoji, wasisikie wala kuona mwenendo wa timu na uwekezaji kwa njia ya timu kushinda mechi, kuleta makombe na kulalamikia ngarama kubwa za uwendeshaji sio sawa. Hii Ina attract upangaji wa matokeo kwenye ligi na mashindano. Yaani unaogopa timu ikifungwa wadau wataibua madhambi yako.
 
Malofa uwa mna wenge,unamuita MO tapeli,wakati mtoto wako anasoma elimu bure ya serikali baada ya kulalimika school fees ya elf ishirini kwa mwaka imekuwa kubwa kwako!!!mjinga sana wewe kiumbe
 
Sasa kuna tofauti ya nyumba yako na nyumba ya urithi. Watu wameitunza Simba tangu mwaka 1936 hata babu yako hajazaliwa, hivyo hawawezi kutokea wajanja wachache wakaipiga mnada kwa njia za kiujanjaujanja kwa bei ya kutupa ili watu wachache wanufaike.

Kaka Simba na Yanga sio timu za makombe ya CAF champions league, hizi ni timu za watani wa jadi vijiwe ambavyo jioni watu wanakwenda kupiga bao, kunywa kahawa na kutazama mazoezi. Kama mo anataka timu ya makombe kwanini asianzishe timu yake kama zile za Azam, Mamelod, TP Mazembe na nyingine za hivyo? Kama fedha anazo kwanini asianzishe timu yake badala ya kulalamikia 24.3b za kuitunza Simba? Kwanini wanakuja Yanga/Simba kama hakuna pesa ni hasara tupu? Mo atuombe radhi wanasimba kwa kutudanganya lakini kwa kusema yeye anaingia hasara tuuuuuuu. Hasemi ameuza jezi za shilingi ngapi, yeye ni hasarahasara TU kwenye conference zake zote. Kaamzishe timu yako bhana usitusimange.
 
Malofa uwa mna wenge,unamuita MO tapeli,wakati mtoto wako anasoma elimu bure ya serikali baada ya kulalimika school fees ya elf ishirini kwa mwaka imekuwa kubwa kwako!!!mjinga sana wewe kiumbe
Kwani mo si wale waliopewa mashamba ya mkonge na kwenda kuyakopea fedha, au? Kama JPM asingekuwa shabiki wa Simba huenda mo nae angekuwa kama Manji.
 
Kwani mo si wale waliopewa mashamba ya mkonge na kwenda kuyakopea fedha, au? Kama JPM asingekuwa shabiki wa Simba huenda mo nae angekuwa kama Manji.
Wakati wanapewa mashamba wewe kwanini ukupewa na wewe ukakope bank uwe bilionea?! Mmegeuza jukwaa la sport kama kijiwe cha kahawa kwa kuandika mambo ya abunuasi
 
Mkuu watu woooote labda wewe tulielewa kuwa gharama yooooote ya kuitunza Simba kwa mwaka ni sh. 5.1b, na mo alisema anazitoa yeye mfukoni mwake. Hakusema kwamba 5.1b ni top up.

Lakini ukimsikiliza vizuri ni kama vile anatamani kuzidai hizo 24.3b alizotumia kwa Simba ila anaogopa akizidai ataliamsha dude. Anatamani hizo 24.3b ziwe ni sehemu ya 20b anazodaiwa lakini anahofia kufanya hivyo kuepusha kimbembe kutoka kwa wadau.
 
Acha kujadili matukio tafuta fact, neda Tume ya ushindani watakupa majibu yote ya maswali yako.
 
Wachezaji wazuri hawawezi kuja Simba na Yanga tuseme ukweli. Tunaowasajili kutoka nje hawana thamani hiyo tunayowapa. Kuna watanzania ambao wanawazidi akina kagere, kahata, shikalo, sarpong, Wawa, Yacouba na wengine lakini hawapewi nafasi TU na makocba. Hata makocha wengine hawana uwezo wa kuwazidi akina Mkwasa lakini hawapewi nafasi.

Hivyo, tuwe makini na sajili zinazotuongezea gharama za kuendesha timu. Kama Tanzania kuna mchezaji mzuri lazima atapenda kuondoka kwenda timu nzuri kama Al-Ahly, Raja, Masri, Ulaya, nk.
 
Mimi kuwa fair ni baada ya yeye kuwa fair pia, uwekezaji hakuna anaeupinga na msema kweli ni mpenzi wa Mungu, wafanyabiashara lazima wapate faida ili wapate moyo wa kuwekeza lakini wasiuache ukweli na kukumbatia faida za kificho. Transparency ililipa jana, inalipa leo na itakulipa hata kesho.

Baadhi ya mambo yasisubiri wakati wa press conference, wekeni mengine kwenye majukwaa ya wadau wa timu kama official website ya timu, Instagram, na magazine au News letter ya club ili kupunguza gap kati ya wadau na uongozi.
 
Nani amekatazwa kwenda kuwekeza simba? hao unaozani wanaweza kuwekeza simba walikuwa wapi kabla mo hajawekeza? ligi kuu bara haina mdhamini nenda kaizamini wewe basi
Simba ilimkubali mo bila kuhoji wala kushindanishwa kutokana na Yanga kuchukua ubingwa back to back kwa miaka 3 mfululizo wakati wa Manji. Hii ni kama GSM pia ilivyoingia yanga baada ya Simba kushinda misimu mitatu chini ya mo. Tofauti ni kwamba Yanga na GSM wanapita njia nyoofu na wazi labda kutokana na umakini wa msolla na wenzake.
 
Sawa wanasimba tumekubali janja janja ya Mo,tuje kwenu nyinyi vyura ambao muwekezaji wenu sio janjajanja mnamafanikio gani tangia gsm achukue umiliki wa jezi za Yanga?
Bado tunajitafuta
 
Mleta thread msamehe Boss Mo, ni Mswahili mwenzetu tena zaidi ya Mzaramo
 
Wewe ni miongoni mwa wajinga ambao hata hiyo Yanga yako huna msaada nayo zaidi ya kelele tu
 
Nusu kaputi ya mo imekukolea. Mo hawezi kuweka mchanganuo wa haki ya Lilah kuhusu matumizi hizo 24.3b. Huenda humo zimo pia za kununua mechi, waamuzi, wazee wa Simba, wajumbe wa tume ya Fair competition, nk. Ataziandikaje in public?
Wewe umeweka shilingi ngapi hata hiyo kwenye Yanga yako??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…