ππjambazi huyo alikamatwa julai 27 mwaka huu Mkoani Morogoro alikokuwa amejificha kukwepa polisi na walipofika eneo la Kisongo jijini Arusha akiwa kwenye gari amefungwa pingu mkononi alijaribu kuruka kuwakimbia polisi.
Waseme tu kuwa amepigwa mpaka akafariki.
Siku ilipotoka habari ya huyo askari kuuawa mimi nilisema hapa ni bora ajiue kabla hajakamatwa kwani akikamatwa atakufa kifo cha mateso sana. Inaonekana jamaa aliteswa polepole mpaka akafa.Huyo jamaa atakua amekufa kifo kibaya sana.
Jiongeze.Yani askari wanazidiwa nguvu na mtuhumiwa aliyefungwa pingu mpaka anapata chance ya kuruka kwenye gari???
Karma.Hamna kuundwa kamati wala chchte, tunajua hakuruka kwenye gari wala nn ila amepata anachostahili, Hakika kifo chake kilikua chauchungu mno.
Ni kweli mkuu haiwezekani aruke kwa sababu mikono ndo inaruka,na mikono ilikuwa na pingu.Polisi polisi polisi. Unawezaje kuruka kwenye gari ukiwa umefungwa pingu mikononi? Iundwe kamati ya kuchunguzwa kifo hicho.
KISONGO...... !!!!!!Jambazi aliyemuua kwa kumkata mapanga Askari polisi, H.2407 Constable Damasi Magoti wa kituo Cha polisi Mbughuni wilayani Arumeru, Jacob Kideko au Ramadhani Kichwa(43) Mkazi wa Makiba amefariki dunia katika jaribio la kuwatoroka polisi alipokuwa akimsafirishwa jijini Arusha.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa Arusha,jambazi huyo alikamatwa julai 27 mwaka huu Mkoani Morogoro alikokuwa amejificha kukwepa polisi na walipofika eneo la Kisongo jijini Arusha akiwa kwenye gari amefungwa pingu mkononi alijaribu kuruka kuwakimbia polisi.
Taarifa hiyo inadai kwamba mtuhumiwa alipata majeraha kichwani na michubuko kwenye mwili wake, Hata hivyo polisi walijaribu kuokoa Maisha yake kwa kumpeleke katika hospital ya Mkoa Mount Meru ,lakini alipoteza Maisha akiwa njiani.
Inadaiwa kuwa jambazi huyo alikuwa akisakwa na Askari wa gereza kuu la Arusha baada ya kufungwa miaka 16 ,Septembe 10 ,2008 lakini alitoroka mnamo April 1, 2017 akiwa chini ya ulinzi wa askari wa Magereza.
Marehemu Magoti aliuawa usiku Julai 23 mwaka huu wakati akitekeleza majukumu yake katika Kijiji Cha Makiba akijaribu kumkamata mtuhumiwa wa wizi nyumbani kwake, ndipo jambazi huyo alitokea jirani na eneo la tukio na kumshambulia kwa kumkata mapanga sehemu mbalimbali na kupoteza Maisha.
mkuu unaniangusha.Yani askari wanazidiwa nguvu na mtuhumiwa aliyefungwa pingu mpaka anapata chance ya kuruka kwenye gari???
unajiangusha mwenyewe chief.mkuu unaniangusha.
sawa mkuu.unajiangusha mwenyewe chief.
Mwanamke akishaanza mahusiano ya nje ni bora uachane naye, ona sasa starehe ya muda mfupi inavuruga familia ya marhemu jambazi na marehemu askariAskari alikuwa na mahusiano na mke wa marehemu. Kisa kilianzia hapo. Hakuna ujambazi hapo
hata Mimi mkuu naiamini hii taarifa Kama nilivyoamini Ile ya askari aliyepiga risasi juu ikakata Kona,ikajipinda na kwenda kumpiga Binti Akwilina!Naomba wote tulio iamini hii taarifa kutoka Jeshi letu la polisi tukutane hapa!! Mimi naanza 100% hii taarifa ni ya kweli π
Askari alikuwa na mahusiano na mke wa marehemu. Kisa kilianzia hapo. Hakuna ujambazi hapo
Hakuwa ameoa huyu jamaaaAskari alikuwa na mahusiano na mke wa marehemu. Kisa kilianzia hapo. Hakuna ujambazi hapo
Hadi uone Cheti Cha ndoa ndipo usema alikuwa hajaoa?Hakuwa ameoa huyu jamaaa