Aliyemuua askari Arusha adaiwa kufa akijaribu kuwatoroka polisi

Aliyemuua askari Arusha adaiwa kufa akijaribu kuwatoroka polisi

Jambazi aliyemuua kwa kumkata mapanga Askari polisi, H.2407 Constable Damasi Magoti wa kituo Cha polisi Mbughuni wilayani Arumeru, Jacob Kideko au Ramadhani Kichwa(43) Mkazi wa Makiba amefariki dunia katika jaribio la kuwatoroka polisi alipokuwa akisafirishwa jijini Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda was polisi mkoa wa Arusha, Justine Masejo,jambazi huyo alikamatwa julai 27 mwaka huu Mkoani Morogoro alikokuwa amejificha kukwepa polisi na walipofika eneo la Kisongo jijini Arusha akiwa kwenye gari amefungwa pingu mkononi alijaribu kuruka kuwakimbia polisi.

Taarifa hiyo inadai kwamba mtuhumiwa alipata majeraha kichwani na michubuko kwenye mwili wake, Hata hivyo polisi walijaribu kuokoa Maisha yake kwa kumpeleke katika hospital ya Mkoa Mount Meru ,lakini alipoteza Maisha akiwa njiani.

Inadaiwa kuwa jambazi huyo alikuwa akisakwa na Askari wa gereza kuu la Arusha baada ya kufungwa miaka 16 ,Septembe 10 ,2008 lakini alitoroka mnamo April 1, 2017 akiwa chini ya ulinzi wa askari wa Magereza.

Marehemu Magoti aliuawa usiku Julai 23 mwaka huu wakati akitekeleza majukumu yake katika Kijiji Cha Makiba akijaribu kumkamata mtuhumiwa wa wizi nyumbani kwake, ndipo jambazi huyo alitokea jirani na eneo la tukio na kumshambulia kwa kumkata mapanga sehemu mbalimbali na kupoteza Maisha.
Jeshi la polisi la tz haliaminiki, linaongoza kwa kutoa kauli na maelezo ya uongo. Sina uhakika kama uongo ni shehemu ya mafunzo yao
 
sasa si bora wangemuulia huko porini aliwe na wanyama......kumpeleka hsptl ni usumbufu kwa wahudumu wa afya.....wengi wako bize na duduMIZI CORONA...........
 
Siku ndugu yako akifa mikononi mwa polisi uje ushangilie hivi hivi
Duh! we mtu wa wapi?
Yaani niwe na ndugu jambazi au gaidi halafu niwe na huruma nae!!

Sasa hao ndugu wa huyo askari wenyewe hawana uchungu na ndugu yao ?
Huyu aliisha wahi fungwa na akatoroka, hapo ujue kuna askari magereza alifukuzwa kazi.

HAKUNA HURUMA YA KINAFIKI KWANGU KWA WATU WA NAMNA YAKE.
 
Huyo hata kama walimsukuma ili adondoke wakati gari ipo kwenye mwendo kasi ni sawa kabisa, hatakiwi kuishi ni hatari kwa jamii.
Unamhukumu huku umemnyima nafasi ya kumsikiliza. Polisi unawaamini?
 
Polisi wanaweza kukutandika rungu za utosi had ukakata roho kama hamuamini hayaa
 
Duh! we mtu wa wapi?
Yaani niwe na ndugu jambazi au gaidi halafu niwe na huruma nae!!

Sasa hao ndugu wa huyo askari wenyewe hawana uchungu na ndugu yao ?
Huyu aliisha wahi fungwa na akatoroka, hapo ujue kuna askari magereza alifukuzwa kazi.

HAKUNA HURUMA YA KINAFIKI KWANGU KWA WATU WA NAMNA YAKE.
Alifungwa akatoroka na akaendelea na maisha bila kutafutwa? Taarifa za polisi wa Tanzania ni za kusikiliza kwa makini waongo waongo sana. Askari wa Arusha wapiga dili vibaya mno mzee huwajui tu. Kesi ya Zombe ilikuwa hivi hivi.
Tena wakati mwingine askari mwanamke anachukua mumewe ambaye si askari wanaenda kupiga dili kitaa.
Huyo askari ilikuwaje akaenda kumkata mhalifu aliyetoroka jela pekeyake? Hili swali halijibiwi sijui kwa nini.
 
Case closed ukiuwa nawe uuwawe Ili kubalance.Ametimiza kanuni ya kuuwa kwa upanga
 
Kwa umri ule bado unafanya ujambazi akili matope kama ukuiba ujanani Acha riziki yako haipo kwenye wizi.
 
Polisi polisi polisi. Unawezaje kuruka kwenye gari ukiwa umefungwa pingu mikononi? Iundwe kamati ya kuchunguzwa kifo hicho.
Kama Mbowe anatuhumiwa gaidi,huyo mwenye pingu kutaka kutoroka unaona ajabu!!!
Polisi wetu Mungu anawaona!
 
Unamhukumu huku umemnyima nafasi ya kumsikiliza. Polisi unawaamini?
Unajua ukiwa askari halafu umepewa jukumu la kumkamata mtu ambae ameisha toa roho ya askari mwenzako, hali inakuwaje ?

Tuache unafiki huyo ni jambazi asie takiwa kuishi na wanadamu. Tena huyu ana roho mbaya sana fikiria kaua kwa upanga alitaka kuondoka na kichwa kabisa cha polisi.
 
Itakuwa HIRIZI za jambazi ziliishiwa nguvu na kushindwa kwepa/zuia risasi za askariii
Ndumba yeyeto huwa inaexpire au kukutana na ndumba kali zaidi, mganga Ili apige pesa yako ni lzm akupe matumaini feki.
 
Polisi polisi polisi. Unawezaje kuruka kwenye gari ukiwa umefungwa pingu mikononi? Iundwe kamati ya kuchunguzwa kifo hicho.
Mkuu Hilo jambazi nasikia limecheza mazoezi ya judo na shotokan karate, kwaiyo kuruka akiwa na pingu Ni simple kwake
 
Back
Top Bottom