Aliyotenda Ole Sabaya ni madogo kuliko ya Paul Makonda. Rais Samia malizia kiporo hiki

Aliyotenda Ole Sabaya ni madogo kuliko ya Paul Makonda. Rais Samia malizia kiporo hiki

Wakuu Kwema!

Kuomba msamaha ni ushujaa, msamaha ni neno la kijeshi katika mapambano.
Unapomkosea mtu akawa na uchungu na wewe basi jua kuwa ipo siku yako, Kama sio wewe basi moja ya kizazi chako.

Upepo unavuma, wenye macho haya tuliyaona miaka mitatu minne iliyopita, tuliandika na kuonya hasa Wale waliojitia Wana nguvu ambazo kimsingi hawana,
Nilishawahi kuandika na Leo narudia, ukipewa Cheo chochote iwe ni Urais,Uwaziri, u-IGP au Cheo chochote kile usije ukadhani wewe ni Mkubwa, huna ukubwa wowote, huna lolote,
Siku zote mkubwa ni yule atendaye haki, apendaye maagizo ya Mungu, mwenye upendo, asiye na fitna na hila, asiyeua wala kumwaga damu za watu wasio na hatia.

Vile unavyotumia nguvu kuonea watu, na kuwatesa watu hasa wasio na hatia ndivyo hivyo hivyo Mungu atatumia nguvu kukuonea na kukutesa.
Vile watoto wa watu ulivyowaua na kuwaangamiza wanavyoteseka, ndivyo hivyo hivyo watoto wako na kizazi chako kitakavyo Tessa na MUNGU.

Kila siku nasema Mungu ni mwaminifu, ana Haki. Huwezi Tesa watu alafu ati uishi Kwa Raha, haijawahi tokea na kamwe haitatokea. Ni suala la muda tuu.

Mungu hajakupa Cheo ili utese watu, Ili uwadhulumu watu, ili uwavuruge watu wake.


Kaka yangu, Kama utanisikia naomba uzingatia haya, tafuta uliowakosea Kama wapo, uwaombe Radhi, Watafute Kwa muda wako,
Usiende kuomba Mungu msamaha, huko unaenda kupoteza muda wako, Mungu haombwagi Msamaha,

Upepo unavuma, bendera uelekeo unaenda mashariki.

Kaka yangu ni Bora Mungu akulipe wewe kwani wewe ndiye uliyekosea kuliko kukuacha wewe na kuhamishia kipigo kwenye kizazi chako.

Baba alichelewa kujihami, alikurupuka kukiwa kumekucha, akakesha akiomba, akataja majina matamu ya Mungu Mkuu lakini hiyo haikumsaidia. Na nadiriki kusema, watoto walioachwa na Baba, mke na wajukuu wanapaswa waombe toba ya kweli kwani vita ya Mungu haimalizwi na kaburi. Vita ya Mungu haimalizwi na mauti, vita vya kibinadamu ndio halimalizwa na kifo.

Kaka yangu.
Bado hujachelewa. Tafuta uliowakosea uwaombe Radhi kuanzia mwakani 2022 mpaka 2025 utakuwa katika vita mbaya na Mungu Mkuu.

Nimekuambia mapema ili ujihami Kwa kuomba Msamaha Kwa uliowakosea ili Mungu aghairi.
Vinginevyo Mungu atakuwa mwaminifu kwako Kwa 100% kukutesa Kama ulivyofanya.

Mimi mdogo wako;

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Morogoro
Sjui kama ben saa nane ataombwa msamaha huko aliko,alfonsi mawazo, na wengineo waliouawa na kaka yako.
Adhabu imkute hapa hapa duniani ili atubu akiwa na mfueni za kutosha
 
Nasikia Bashite na Mama siku hizi haziendi sawa,Nasikia alimpakazia kwa jiwe,hadi jiwe akambadilishia Mama msaidizi wake,Bashite alimtaka msaidiz wa Mama wapige mshindo furani,msaidizi akachomoa,kuona hivyo Bashite akaenda kumpakazia kwa Jiwe,akahamishwa,Msaidizi ikabidi amueleze ukweli Mama,tokea hapo picha limesanuka...Kwa hiyo chochote chaweza tokea.
Comment yako imetawaliwa na neno la "Nasikia" JF huenda kwa fact na sio kutumia neno nasikia,unasikia kutoka wapi? hearsay haiwezi kutumika as an evidence.
 
Laa kazi kweli kweli, jee lini mara ya mwisho umemuona Makonda? Mtumie nauli arudi, yuko University of Uppsala, Sweden anafanya Master in Government and Management. Kamfuate.
Hao ni wapumbavu na wote hao wanaotaka Makonda akamatwe ni watu wenye chuki na Magufuli over!
 
Ww ndio kapilimba mwenyewe nini? Maana mlishirikiana na Magufuli kuendesha uhalifu na ukatili wa hali ya juu ndani ya nchi hii.
Msaidizi wake yuko RAS Tabora ndio muuaji no 1 pia kuna mwingine John Nyaulingo alivunjika mifuu anaweweseka kwa damu za watu hadi sasa........damu za watu hazìtawaacha kamwe....Makonda pia....Henry Kisanduku usimuache.....damu damu damu
 
Msaidizi wake yuko RAS Tabora ndio muuaji no 1 pia kuna mwingine John Nyaulingo alivunjika mifuu anaweweseka kwa damu za watu hadi sasa........damu za watu hazìtawaacha kamwe....Makonda pia....Henry Kisanduku usimuache.....damu damu damu
duuuuh
 
Mambo aliyoyafanya ingekua kama ni Mexico ama Colombia wangekua wamesha mmaliza
Kweli Tanzania ni nchi ya amani!!Yaani kwa maumivu yale ya teka teka watu!Bado Makonda hajapigwa wala kujeruhiwa na kina MO,ROMA MKATOLIKI,WAHANGA WA KUTAJWA KWENYE MADAWA YA KULEVYA!!NA N.K???MI NILIDHANI HADI SASA MAKONDA ANGEKUA KABURINI!!!!
 
Kwanza hebu niambie umeshaenda kumjulia hali Gaidi Mbowe kule Segerea au upo tu JF wakati Mwenyekiti wako ananyea ndoo??
Mbowe kuwa segerea ni matakwa ya Sabaya na lile Jini tulilolizika ila MUNGU atatenda Miujiza
 
Nimepata taarifa kwamba Ndugu Paul Makonda anasumbua sana viongozi huku na kule kutaka kujua hatima yake ndani ya nchi hii.

Nimsihi tu wakati wa kunyolewa inabidi atulie. Acha kusumbua viongozi ili dola ifanye kazi yake. Ungewasumbua kabla ya kuvamia Clouds na silaha za kivita,ili wakushauri.

Amekuwa na wasiwasi wa kutiwa nguvuni muda wowote. Wajinga wachache wanamshauri atoroke. Aende wapi na Interpol ipo,utadakwa tu.
Umezipata wapi hizo taarifa?
Mbona takukuru walishatoa taarifa kwamba hawana mpango nae?
 
Hata kwa sabaya ulisema hivyo hivyo kwamba hawawezi kumfunga....Jinai haifi...Makonda lazima atakamatwa tu ,kumbuka USA washampiga tanchi moja ya makosa yake ni mauaji(Dhuluma ya haki ya kuishi) ,Ben Saanane kabla ya kupotea alikuwa na mbishe na makonda ,kupora mali za wafanyabiashara ,kumiliki genge la unyang'ang'anyi(Organized Crime) ,ujambazi wa kutumia silaha etc
Akili ya kitanzania ndio hii kufurahia kuanguka kwa mwenzake.

Labda upeleke kikosi cha kwako ndio utaweza kumkamata.
 
Back
Top Bottom