Ama kweli kisa hiki cha Nairobi Kenya, cha kijana aliyeachwa hai na gaidi kina mafunzo mengi, be nice to people you never know..!!

Ama kweli kisa hiki cha Nairobi Kenya, cha kijana aliyeachwa hai na gaidi kina mafunzo mengi, be nice to people you never know..!!

Kama uko serious.. Kisa kinaelezea hivI kwa tafsiri isiyo rasmi;

Kijana Reuben alikuwa ni muhudumu wa hoteli ambayo magaidi hao walikuwa wakifika mara kwa mara kujipatia kahawa na mambo mengine mpaka akazoeana nao (hakujua ni magaidi).

Sasa, pamoja na kwamba hao wateja (magaidi) kuwa wakorofi na wababe walipokuwa wakihitaji huduma, mshikaji alikuwa akiwapa huduma kwa upole na unyenyekevu ile kiroho safi.

Siku ya tukio, Reuben akiwa amelala chini na watu wengine, aliinua kichwa chake na kugonganisha macho na gaidi mmoja akamfahamu.. Gaidi akakumbuka ukarimu wa Reuben, akawaua watu wengine wote na kumuacha hai Reuben. Wema wake ulimuokoa na kifo.

Hapo vipi mkuu? Najua nimesaidia wengi.
umejitaidi kujua shida zetu mzee
 
Anaekt hio kiwewe mkuu,
mi nakuambia wampige shot za maana anasema kila kitu

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndio tatizo la interrogator wa Kiafrika, huwa hawakawii kumuumiza mtu kabla ya kuwa na uhakika, unakuta maskini wa watu mumemtoa makucha na meno ndio hatimaye mnagundua hana hatia, ilhali ni mambo ya kutumia akili wakati wa kuhoji, mnacheza na saikolojia yake hadi mnamkamata, mtu anajikuta ameeleza yote bila kuguswa sehemu.
 
Huyo dogo kaweweseka na hiyo hali ya kuachwa nikwamba haamini kilichotokea.

Angekua yuko connected na hao jamaa asingalikuwepo kusubiri majanga yaanze ,kungalifanyika kitu ili asiwepo kusubiri majanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chang'aa tu
FB_IMG_15473432151437689.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
ANAFAA KUHOJIWA KWA KINA ASIJEKUWA NDO ALIYEWAPA RAMANI NA MCHONGO MZIMA HAO MAGAIDI. SIO WA KUMWACHA KIRAHISIRAHISI ATI ALIWAKARIMU NDO WAKAMUACHA SALAMA.
SHETANI HANAGA RAFIKI, KUNA "SMOKING GUN" HAPO NIAMINI MIMI.
Hizi ndo akili za wana usalama bongo. Ukimkuta mtu njiani kazidiwa ukampakia kwenye gari umuwahishe hospitali akikufikia we ndo mtuhumiwa wa kwanza. Hivi hakuna namna nyingine ya kuwaza tofauti na hii?!
 
Kabla hamjawaza huyo jamaa kuhusika ilitakiwa muwaze hivi kama kweli amehusika ana ujasiri gani wa kujianika kwenye camera? Na kwanini ajioneshe hivyo?! Nini lengo lake?
 
Kwa upelelezi wenu wa kijinga mtapigwa sana na watawatoroka hao magaidi wakijifanya ni wahanga ama wamepona pona, kwanini msifikirie huyo jamaa ndiye informer wao na alihusika kupanga njama na kuwapa ramani za jengo hilo kabla hawajaja?
Kwa upelelezi wetu wa hapa bongo wa kijinga jinga ndio maana kila siku tunakamata watu wasio husika kwa fikra zetu ndogo. Soma vizuri hapo. Ramani ya nini wakati unaambiwa jamaa walikuwa wanakuja kwenye jengo kama wateja.

Au umesahau kwamba westgate jamaa walikuwa mpaka na duka lao kwenye mall?
 
Nashukuru mkuu nimekupata.....

Navyo fahamu mm jambazi/gaidi akisha fahamu umemtambua hakuachi salama ili kuondoa ushahidi...

Hatuwezi kumhukumu huyu dogo lakini angetakiwa achunguzwe na kuhojiwa....
Huwa sio majambazi, ni magaidi. Waondoe ushahidi vipi wakati wanajua kabisa kutoka hai pale ni zero.

Dogo kilichomuokoa ni good customer service. Walipokuja kutaka uduma yeye bila kujua kama hao ni magaidi aliwapa uduma nzuri japo walikuwa wakorofi lakini yeye dogo aliendelea kutoa uduma safi kwao kwani mteja ni mfalme kwenye biashara yoyote.
 
Kwaiyo jamaa alimpa gaidi na kahawa kabisa? Au mimi ndo sijaelewa Kimombo?

Sent from my SM-J530F using Tapatalk
hao magaidi walikuwa wakifika hotelini mara kadhaa siku za nyuma karibuni.. na yeye ndiye aliyekuwa akiwahudumia mara kwa mara na kuwa mkarimu kwao. siku hiyo ya tukio wakamwacha huru asepe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru mkuu nimekupata.....

Navyo fahamu mm jambazi/gaidi akisha fahamu umemtambua hakuachi salama ili kuondoa ushahidi...

Hatuwezi kumhukumu huyu dogo lakini angetakiwa achunguzwe na kuhojiwa....
magaidi huwa wanajitambua na hawana cha kupoteza, mara nyingi wana mafunzo ya dini na sababu za kina za wao kufanya mauaji. hata lile tukio la garisa kuna waliokuwa wakiachwa huru na kuondoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa sio majambazi, ni magaidi. Waondoe ushahidi vipi wakati wanajua kabisa kutoka hai pale ni zero.

Dogo kilichomuokoa ni good customer service. Walipokuja kutaka uduma yeye bila kujua kama hao ni magaidi aliwapa uduma nzuri japo walikuwa wakorofi lakini yeye dogo aliendelea kutoa uduma safi kwao kwani mteja ni mfalme kwenye biashara yoyote.
Kwenye upelelezi mkuu huyu dogo anatakiwa akahojiwe.... Hata shetani kuna mda anakuwa malaika
 
Back
Top Bottom