kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Tunahitaji amani sio utulivu, lakini ni heri ya utulivu kuliko demokrasia yenye vurungu, na bila kusahau kuwa demokrasia kwa watu hata wasiokuwa na vyama; ni zaidi ya vyama vya siasa kurahisishiwa kuwa viongozi na kwenda Ikulu.
Amani: Ni kuwa na uhakika wa kuwaona wajukuu zako kutokana na kupatiwa ulinzi na usalama pamoja na kuwa na uhakika wa kupata mahitaji ya msingi (chakula, hewa safi, maji safi, malazi safi, usafiri safi, elimu safi, matibabu safi na haki zako zote).
Utulivu: Ni kwenda kulala hata kama una njaa. Unalazimika au unalazimishwa kwenda kulala hata kama hujala kitu. Unaongozwa na kiongozi ambae hamjamchagua, hamumpendi wala hamumfahamu katokea wapi. unalazika kutii hata kama hutaki au unataka; yaani unapigwa halafu unaamrishwa usilie. Hali kama hiyo au inayofanana na hiyo ndio utulivu.
Demokrasia: Ni uhuru wa kujiamulia kile unachotaka ufanyiwe na kufanyia wengine, au kujifanyia mwenyewe. Kwaasili sisi hatuna asili ya demokrasia, majumbani kwetu hakuna demokrasi na hatukulelewa kidemokrasia; utapigwa na kunyamazishwa hapohapo usipige kele, watoto wetu na wanawake hawana uhuru wa kujichagulia na kuamua majumbani. Shule na vyuoni hakuna demokrasia.
Demokrasia imeletwa kwetu kama furushi la mzigo ambao lazima ulipokee hata kama hutaki. Waliotuletea demokrasia walikuwa na malengo yao yenye maslahi kwao kuliko kwetu. Demokrasia imeletwa kwetu na watu ambao walitutawala bila hiyari yetu, walipora rasilimali zetu bila hiyari yetu, walitupiga na kutuua wapendavyo, walifanya mizengwe kwenye chaguzi tusipate uhuru.
Demokrasia lazima tuwe makini nayo, sio kuchukua kila kitu. Neno "demokrasia" kwetu ni chanzo cha maandamano, uhalifu, vita, wizi wa kura, kutekana, kuharibu mali za wengine, na kutumia muda wa kuzalisha mali kwa kufanya demokrasia; demokrasia inaondoa umoja na mshikamano hivyo divide and rule kwao waletaji. Waliotuletea walijua kuwa italeta "divide" ili wao wa "rule". Tutachapana ili wauze silaha zao, na watapata vibaraka kwa njia rahisi sana na kukomba rasilimali zetu kirahisi
Nikiona mtu katekwa huwa najiuliza kwanza kwanini katekwa yeye sio mimi? nani kamteka? kwanini katekwa? Maana Kutekwa kunaweza kufanywa kwa sababu za usalama, kwa kulipa kisasi, ugomvi wa mapenzi, ardhi na kugombea uongozi au mali. Kutekwa kunaweza kuwa kwa kichawi au fitina TU.
Vyama vya siasa: Vinatumia demokrasia kama njia kujipatia kipato kupitia kupata uongozi, kupata ruzuku na misaada ya wahisani. Kama mazingira hayawawezeshi wanasiasa kuendelea kutawala au kupata uongozi basi hakuna demokrasia.
Demokrasia ni zaidi ya viongozi wa siasa kupata au kuendelea kuwa viongozi, bali demokrasia ni kwa watu watu wote kuanzia majumbani, mashuleni, mitaani na kwenye taasisi zote lazima kuwe na mifumo ya kidemokrasia. Demokrasia haianzii ikulu bali kwenye ngazi ya familia, jamii na vyama vya siasa vyenyewe.
Tukae chini kama taifa tukubaliane tunataka tuelekee wapi na tuelekeeje bila kutegemea vikundi vya vyatu vituamulie. Tusiwe kama dodoki kuzoa kila maelekezo kutoka nje bila kuyachambua kulingana na context na background yetu. Tusiruhusu mtu au watu watuchagulie kutupa kati ya Amani, Utulivu au demokrasia kwa matakwa yake ya kundi lake..
Amani: Ni kuwa na uhakika wa kuwaona wajukuu zako kutokana na kupatiwa ulinzi na usalama pamoja na kuwa na uhakika wa kupata mahitaji ya msingi (chakula, hewa safi, maji safi, malazi safi, usafiri safi, elimu safi, matibabu safi na haki zako zote).
Utulivu: Ni kwenda kulala hata kama una njaa. Unalazimika au unalazimishwa kwenda kulala hata kama hujala kitu. Unaongozwa na kiongozi ambae hamjamchagua, hamumpendi wala hamumfahamu katokea wapi. unalazika kutii hata kama hutaki au unataka; yaani unapigwa halafu unaamrishwa usilie. Hali kama hiyo au inayofanana na hiyo ndio utulivu.
Demokrasia: Ni uhuru wa kujiamulia kile unachotaka ufanyiwe na kufanyia wengine, au kujifanyia mwenyewe. Kwaasili sisi hatuna asili ya demokrasia, majumbani kwetu hakuna demokrasi na hatukulelewa kidemokrasia; utapigwa na kunyamazishwa hapohapo usipige kele, watoto wetu na wanawake hawana uhuru wa kujichagulia na kuamua majumbani. Shule na vyuoni hakuna demokrasia.
Demokrasia imeletwa kwetu kama furushi la mzigo ambao lazima ulipokee hata kama hutaki. Waliotuletea demokrasia walikuwa na malengo yao yenye maslahi kwao kuliko kwetu. Demokrasia imeletwa kwetu na watu ambao walitutawala bila hiyari yetu, walipora rasilimali zetu bila hiyari yetu, walitupiga na kutuua wapendavyo, walifanya mizengwe kwenye chaguzi tusipate uhuru.
Demokrasia lazima tuwe makini nayo, sio kuchukua kila kitu. Neno "demokrasia" kwetu ni chanzo cha maandamano, uhalifu, vita, wizi wa kura, kutekana, kuharibu mali za wengine, na kutumia muda wa kuzalisha mali kwa kufanya demokrasia; demokrasia inaondoa umoja na mshikamano hivyo divide and rule kwao waletaji. Waliotuletea walijua kuwa italeta "divide" ili wao wa "rule". Tutachapana ili wauze silaha zao, na watapata vibaraka kwa njia rahisi sana na kukomba rasilimali zetu kirahisi
Nikiona mtu katekwa huwa najiuliza kwanza kwanini katekwa yeye sio mimi? nani kamteka? kwanini katekwa? Maana Kutekwa kunaweza kufanywa kwa sababu za usalama, kwa kulipa kisasi, ugomvi wa mapenzi, ardhi na kugombea uongozi au mali. Kutekwa kunaweza kuwa kwa kichawi au fitina TU.
Vyama vya siasa: Vinatumia demokrasia kama njia kujipatia kipato kupitia kupata uongozi, kupata ruzuku na misaada ya wahisani. Kama mazingira hayawawezeshi wanasiasa kuendelea kutawala au kupata uongozi basi hakuna demokrasia.
Demokrasia ni zaidi ya viongozi wa siasa kupata au kuendelea kuwa viongozi, bali demokrasia ni kwa watu watu wote kuanzia majumbani, mashuleni, mitaani na kwenye taasisi zote lazima kuwe na mifumo ya kidemokrasia. Demokrasia haianzii ikulu bali kwenye ngazi ya familia, jamii na vyama vya siasa vyenyewe.
Tukae chini kama taifa tukubaliane tunataka tuelekee wapi na tuelekeeje bila kutegemea vikundi vya vyatu vituamulie. Tusiwe kama dodoki kuzoa kila maelekezo kutoka nje bila kuyachambua kulingana na context na background yetu. Tusiruhusu mtu au watu watuchagulie kutupa kati ya Amani, Utulivu au demokrasia kwa matakwa yake ya kundi lake..