Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Kama Jambo Dogo kama hilo linakushinda mpaka uombe ushauri, ni bora usubiri Akili ikomae ndio uingie ndoani, maana Kwa Akili hizi ndoa itakushinda mapema Mno.

Mtu unashindwa kujua kipi kitangulie kipi kifuate,
Kwa sababu ya ubinafsi wako ndio maana ukamkatili huyo mtoto wa Watu Kwa kisingizio cha rafiki yako sijui anamatatizo gani.

Tafsiri yake ni kuwa hata ukioa utatanguliza mambo ya marafiki kuliko Familia yako(Mkeo na watoto),

Hata huyo Mchumba wako ni hamnazo, yaani Bora ungetoa sababu ya mzazi anaumwa lakini kumbe ni matatizo ya rafiki yako.
Mkuu nafikiri bado hujajiandaa kuwa na Familia.
Huu ndio ukweli wenyewe
 
Umemkosea na umempa fedheha kwa familia yake, na Umevunja Ahadi..!!!

Kama ni mimi ningeshakublokilia mbali everywhere kuanzia kwenye Moyo,nafsi,akili etc

Unaonekana hauna msimamo wala clear vision, Mwanaume mwenye Vision habadili plans zake kwa changamoto za ghafla, huyo Dada ningemjua ningemshauri akusahau angaalie maisha yake
Asante sana!
 
Alafu ATI mpaka ashauriwe akaombe Msamaha ni kwamba hajui kuwa amefanya Makosa, hajali, na bila Shaka hampendi huyo Binti WA Watu.

Ashamtia aibu Binti wa Watu Huko kwao, lakini Hilo kwake halioni Kwa vile hajafanyiwa yeye.

Alafu angefanyiwa yeye angekuja hapa kupiga mayowe Wanawake ni wabaya.
Tabia za ubinafsi, kutojali hisia za wengine ni moja ya tabia Mbaya zinazotesa wengi katika jamii.

Kwa Sisi tusioweza kuvumilia huwaga hatuchelewi kujibu mapigo.

Ndio maana nikiwaambia Wanawake watafute Pesa wajitegemee waachane na kuhudumiwa naonekana mchawi na Mchukia Wanawake wakati tayari nimeshasoma Gap na kujua jamii yetu ni yanamna gani.
Madini haya mkuu
 
Jamaa ulichemka Sana

We endekeza tu maneno ya watu kukataa ndoa na kuleta ujana. Kitu unasahau ni kuwa Hao unaowaona marafiki zako leo hutakuja kuwaona kesho ukiwa unaumwa unavaa pampers.

Ujana huwa unawasumbua Sana, stori nyingiiiii ila hamjui ya mbele yenu.

Wewe ulijitolea kuacha kutoa mahali na kujenga familia yako ambayo kimsingi ndio rafiki wako wa kweli na kumsaidia mshkaji, subiri sasa utakuja kuona Nani Atakuwa upande wako katika maisha yako.
Yaani umemwambia ukweli kabisa.
 
Ila huyo mwanamke hana akili pamoja na kumuaibisha bado kajileta mfyuu zake
Labda kamwandalia tukio.
Wanawake tuna style za kulipiza kisasi ambazo hata kwenye biblia ya shetani hazipo.
 
Nafikiri una umri mdogo/ hauna ustaarabu au hujapevuka kiakili.

Kama ulipata dharura kama hiyo ulitakiwa utumie busara ya kutuma wazee au mshenga akaombe ukweni waahirishe hiyo siku....na sababu kuu mmepata dharura inayohitaji pesa.

Jifunze ustaarabu naona kama unajiona spesho sana.
Hujui kesho yako huenda mkeo au nduguze watakuvusha eneo flani.

Unaweza kuwachukulia poa...haya ni maisha tu...unayemchukulia poa kesho kibao kinakugeuka
That's my Glenn.
 
Nimezungumzia CLEAR VISION AS A MAN

Nikimaanisha kua Mwanaume kama Mwanaume lazima usimamie juu ya ulichokipanga na kukiratibu bila kujali kuna changamoto gani imeingia kati

Issue za kusaidiana zipo tu na hazijawahi kuisha

Kwa mwanaume aina yako maendeleo utayasikia kwenye bomba, unaonyesha hauna muelekeo

Mwanaume kamili hayumbishwi na changamoto za ghafla anasimamia mipango yake kama alivyoiratibu

Wewe hutapiga hatua yoyote kubwa ya maendeleo trust me ukijaribu kunyanyuka ikitokea changamoto unapangua mpango wako ghafla

Kwa mwenendo huo utakua ni mtu wa kurudi nyuma daily
Mimi naona hata nikikugongea like tu haitoshi. Darasa zuri wasipoelewa basi tena.
 
Wakuonewa huruma hapo ni wewe 😂😂😂

Sisi wazoefu WA mapenzi tunajua nini kinafuata kwako kwenye ishu za mahusiano.

Kesho kutwa hapa utakuja kuwatukana Wanawake ni Mbwa,
Nipo nimekaa hapa
Nimeweka hapa hili jambo si kwa sababu natafuta huruma. Sina hata chembechembe za kudai huruma. Iko hivi, tushauriane kwa lengo la kujifunza. Uzoefu wa mapenzi na suala la mahusiano ya ndoa ni vitu viwili tofauti. Hata makahaba wana uzoefu katika mapenzi lakini mbona hawapo katika ndoa? suala gumu kabisa hapa JF baadhi yenu mnapenda kuwashusha watu mpaka kwenye level zenu kisha unoangea kutokea kwenye level yako. My conscience is clear Bro,,,changia mada kwa mawazo ya kujenga. Hizo hoja nyepesi sijui wenye akili sijui ukomavu wa akili sijui ubinafsi,,, ni bla bla tu za kupoteza muda. Click to the point objectively!
 
Nakuhakikishia huyo Mwanamke ukimuoa lazima atakuja kulipiza kisasi kwa aibu ulihompa.

Hata ningekuwa mimi lazima ningelipiza.
Kwanza aje aombe msamaha kwetu aniondolee aibu aliyonisababishia halafu sasa ni deal naye kimafia.

Hajui ni aibu kiasi gani kamsababishia huyo binti. Na mabinti tunavyosimangwaga mwanaume akiingia mitini..usipokuwa na roho ngumu unaweza kunywa sumu.
 
Nimeweka hapa hili jambo si kwa sababu natafuta huruma. Sina hata chembechembe za kudai huruma. Iko hivi, tushauriane kwa lengo la kujifunza. Uzoefu wa mapenzi na suala la mahusiano ya ndoa ni vitu viwili tofauti. Hata makahaba wana uzoefu katika mapenzi lakini mbona hawapo katika ndoa? suala gumu kabisa hapa JF baadhi yenu mnapenda kuwashusha watu mpaka kwenye level zenu kisha unoangea kutokea kwenye level yako. My conscience is clear Bro,,,changia mada kwa mawazo ya kujenga. Hizo hoja nyepesi sijui wenye akili sijui ukomavu wa akili sijui ubinafsi,,, ni bla bla tu za kupoteza muda. Click to the point objectively!

Wewe ndio umemshusha huyo Mchumba wako ambaye mnamuda mrefu mnafahamiana miaka nenda Rudi, unategemea humu Nani atakupandisha zaidi ya kukushusha kama ulivyofanya?

Umeweka Watu wachangie na hii ndio michango yenyewe.

Pointi wadau wameshazitoa kuwa umepuyanga,
Unapaswa usubiri ukomae Kiakili ndipo utajua wapi umekwama.

Mapenzi ndio yanaunda Ndoa. Hakuna Ndoa bila mapenzi. Ila mapenzi yanaweza kuwepo bila ya Ndoa.

Ili ndoa uimudu lazima mapenzi uyamudu.
Ndio maana nikakuambia bado haujakomaa Kiakili.

Kuhusu hao makahaba ni maamuzi Yao kuwa hivyo walivyo, ukahaba ni maamuzi sio Tabia, umalaya ndio Tabia
 
Hata ningekuwa mimi lazima ningelipiza.
Kwanza aje aombe msamaha kwetu aniondolee aibu aliyonisababishia halafu sasa ni deal naye kimafia.

Hajui ni aibu kiasi gani kamsababishia huyo binti. Na mabinti tunavyosimangwaga mwanaume akiingia mitini..usipokuwa na roho ngumu unaweza kunywa sumu.
Kabisa mkuu
 
Mkuu
Nisikilize kwa makini.

Uliamua kutoa msaada kwa rafiki kwa ugumu alioupitia na ilipaswa ndiyo ukae nanmwenzako muyajenge lakini kitendo cha yeye kusema bora muachane ni wazi neno ndoa kwake ni STATUS na siyo mahusiano.

Ndugu katika Jf.
Nikiwa kama mwanamke ninayejua ni namna gani jamii inacheka wanawake pale mchumba anapotokomea kusipo julikana au maarufu kama kuingia mitini, kauli ya binti ya TUACHANE ilikuwa ni njia ya kum pressurize huyo mwanaume aachane na hizo plan za rafiki yake na astick kwenye original plan ya kwenda kumtolea hiyo mahari.

Kauli ya tuachane kwa wakati huo haikuwa inamaanisha tuachane ila ilitumika kama silaha ya mwisho ya kujaribu kumrudisha mwanaume kwenye akili zake.
 
Wewe ndio umemshusha huyo Mchumba wako ambaye mnamuda mrefu mnafahamiana miaka nenda Rudi, unategemea humu Nani atakupandisha zaidi ya kukushusha kama ulivyofanya?

Umeweka Watu wachangie na hii ndio michango yenyewe.

Pointi wadau wameshazitoa kuwa umepuyanga,
Unapaswa usubiri ukomae Kiakili ndipo utajua wapi umekwama.

Mapenzi ndio yanaunda Ndoa. Hakuna Ndoa bila mapenzi. Ila mapenzi yanaweza kuwepo bila ya Ndoa.

Ili ndoa uimudu lazima mapenzi uyamudu.
Ndio maana nikakuambia bado haujakomaa Kiakili.

Kuhusu hao makahaba ni maamuzi Yao kuwa hivyo walivyo, ukahaba ni maamuzi sio Tabia, umalaya ndio Tabia
Naheshimu sana michango yenu na napenda kuishia hapa. Kwangu mimi, kuwajali watu wengine walio katika shida ambazo ninazimudu ni ibada kwangu. Ndoa ikishindikana leo, itafanyika kesho. Kama si kwa huyu basi ni kwa mtu mwingine. Sina shaka! huyu mahusiano yetu hayatakuwepo tena. Nimeyavunja rasmi this morning. Nitajipa nafasi, si kwa lengo la kukua maana nimekua na akili imekomaa haswa. Imani yangu ni kwamba nitakutana na mtu mwenye mtazamo ule ninaoutaka, ikitokea hajapatikana wala hakuna shida. Ninaishi na nitaishi kwa kuwajalii wengine.
 
Naheshimu sana michango yenu na napenda kuishia hapa. Kwangu mimi, kuwajali watu wengine walio katika shida ambazo ninazimudu ni ibada kwangu. Ndoa ikishindikana leo, itafanyika kesho. Kama si kwa huyu basi ni kwa mtu mwingine. Sina shaka! huyu mahusiano yetu hayatakuwepo tena. Nimeyavunja rasmi this morning. Nitajipa nafasi, si kwa lengo la kukua maana nimekua na akili imekomaa haswa. Imani yangu ni kwamba nitakutana na mtu mwenye mtazamo ule ninaoutaka, ikitokea hajapatikana wala hakuna shida. Ninaishi na nitaishi kwa kuwajalii wengine.

😂😂😂

Kusaidia Watu bila Akili nako ni upunguani.

Ndio maana Manzoni nikakuambia wewe bado haujakua Kiakili, ndio maana hata hujui maana ya Familia.
Familia ndio kitu cha Kwanza Kwa mwanaume na Mwanamke mwenye utimamu wa Akili.
Huwezi sema unasaidia wengine ATI Kwa kisingizio cha ibada huku ukivunja ahadi na Binti uliyekaa naye kwenye mahusiano muda mrefu.

Unajiangalia wewe pekeako Kwa sababu wewe ni mbinafsi.
Hauangalii ni muda gani umempotezea Binti WA watu tena Bora yeye angekuwa amekukosea Ila wewe ndio umemkosea,
Yeye kakasirika ndio maana akakumaind lakini Kwa vile wewe unakiburi hukutaka kujishusha na kuomba Radhi.

Ninyi ndio wale wanaume wa humu JF ambao mnapenda muonekano Kwa nje ni Wema Kwa kuwajali watu wa nje(marafiki ikiwemo wa JF) Kwa kujifanya mnamichango ya kistaarabu kumbe ndani ni Mbwa mwitu.
Si unaona, huku unajifanya mstaarabu Sana unapotoa comments zako lakini unayoyafanya Huko kwenye Maisha halisi mfano Kwa hiyo Mchumba wako ni ushenzi uliopitiliza.

Hata kama utaamua ku-move on muombe Msamaha hiyo Mrembo wa Watu, ili uendelee na Maisha yako Kwa Amani.
Kumpotezea mtoto wa Watu muda na kupeana ahadi na viapo kisha kuvivunja Kwa sababu za kijinga ni usaliti wa Hali ya juu.
Na Dawa ya wasaliti inafahamika,

Ni hayo tuu.
 
Na kwann mtu ku force ndoa.
Ujue mwanaume ukisham force tu baya mambo ya mahali sijui kwenda ukweni hata kaama huna nia mbaya lazima utamfanya asanuke na kujiuliza !!!
 
Kweli wanaume mmekuwa adimu..na kumdhalilisha kote huko bado karudi[emoji849][emoji849][emoji848]

Tena anaomba na msamaha mammmae
 
Kweli wanaume mmekuwa adimu..na kumdhalilisha kote huko bado karudi[emoji849][emoji849][emoji848]

Tena anaomba na msamaha mammmae
Afanye nini na vijana wengi wanataka kula bure na watunzwe?
 
Back
Top Bottom