Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

1. Nisubiri nikomae 2. Sijui kipi kitangulie 3. Nina ubinafsi 4. mchumba wangu ni hamnazo 5. sijajiandaa kuwa na familia 6. jambo dogo kama hilo linanishinda
Toa ushauri ili nisiendelee kuwa katika haya unayoyafikiria kuwa yapo

1. Nimekupa ushauri kuwa usubiri Kwanza ukomae,

2. Ujue nini maana ya Familia.
Mkeo ndio wewe, Watoto wenu ndio matunda yenu. Ni lazima uwe na upendo na uweze kulinda familia yako Kwa gharama yoyote.

3. Usichopenda kufanyiwa usimfanyie mwenzako. Tafsiri yake Acha Ubinafsi.
Fikiria wewe ndio umetoa taarifa kwenu kuwa kuna Mchumba atakuja umtambulishe, Ndugu wote wanajua na pengine wamejiandaa, alafu mwisho wa siku huyo Binti anakuambia amepata ushuru, unaulizia udhuru gani ukitegemea taarifa ya maana, ATI demu wako anakuambia sijui rafiki yake kapata matatizo, utamuelewa?

4. Kuomba Msamaha ni dalili ya MTU anayejitambua, mwenye upendo, anayejali na MTU mnyenyekevu kuwa amekosea.
Kama huwezi kuomba Msamaha ATI mpaka uambiwe sijui ubembelezwe hiyo ni dalili ya kutojitambua, uchanga na kutokukomaa.

5. Kuwa mwanaume ni kuwa na Akili.
Kuiona Jana na Leo kisha kuikadiria kesho(maono)
Sio kila Jambo uombe ushauri, ni dalili kuwa Bado Akili yako haijaweza kujisimamia na huna uwezo wa kuwa Baba.

Kumbuka ukiwa Baba, Mkeo ataitegemea Akili yako kutatua matatizo yake na familia.
Sasa kama Akili haijakomaa Mkeo atapata wapi wa kumtegemea kimawazo?

Mwisho, usidhani nimekukandia, Ila najaribu kuongea Kwa Lugha Kali ili upate uchungu uweze kunielewa kirahisi
 
Busara ni kujenga hoja zenye mantiki katika mada iliyowekwa. Kufikiria mambo mengine nje ya mada na kujenga mitazamo hasi ambayo haipo ni kupoteza muda na kujitwika mambo yasiyo na tija. Kama elites, tushauriane kwa staha. Mambo unayoyaona madogo na yasiyohitaji kujadiliwa, kwa wengine ni inshu kubwa. Tuendelee kushauriana!

Mada yako Ipo kwenye mrengo Hasi, na chanzo cha uhasi huo ni mhusika wewe ndani ya hicho kisa.

Wewe ndiye umemkatili huyo Binti.

Sasa ukiambiwa ukweli unaona kama tunamitazamo hasi.
Wewe kama huna Mtazamo Hasi, nini kinakushinda kwenda kuomba Msamaha mpaka uite Jambo hilo ni masharti ya huyo Mchumba wako?
Jambo ambalo Kwa MTU mwenye Akili wala asingesubiri kuambiwa akaombe Msamaha kwani angeenda mwenyewe.

Acha Ubinafsi
 
1. Nimekupa ushauri kuwa usubiri Kwanza ukomae,

2. Ujue nini maana ya Familia.
Mkeo ndio wewe, Watoto wenu ndio matunda yenu. Ni lazima uwe na upendo na uweze kulinda familia yako Kwa gharama yoyote.

3. Usichopenda kufanyiwa usimfanyie mwenzako. Tafsiri yake Acha Ubinafsi.
Fikiria wewe ndio umetoa taarifa kwenu kuwa kuna Mchumba atakuja umtambulishe, Ndugu wote wanajua na pengine wamejiandaa, alafu mwisho wa siku huyo Binti anakuambia amepata ushuru, unaulizia udhuru gani ukitegemea taarifa ya maana, ATI demu wako anakuambia sijui rafiki yake kapata matatizo, utamuelewa?

4. Kuomba Msamaha ni dalili ya MTU anayejitambua, mwenye upendo, anayejali na MTU mnyenyekevu kuwa amekosea.
Kama huwezi kuomba Msamaha ATI mpaka uambiwe sijui ubembelezwe hiyo ni dalili ya kutojitambua, uchanga na kutokukomaa.

5. Kuwa mwanaume ni kuwa na Akili.
Kuiona Jana na Leo kisha kuikadiria kesho(maono)
Sio kila Jambo uombe ushauri, ni dalili kuwa Bado Akili yako haijaweza kujisimamia na huna uwezo wa kuwa Baba.

Kumbuka ukiwa Baba, Mkeo ataitegemea Akili yako kutatua matatizo yake na familia.
Sasa kama Akili haijakomaa Mkeo atapata wapi wa kumtegemea kimawazo?

Mwisho, usidhani nimekukandia, Ila najaribu kuongea Kwa Lugha Kali ili upate uchungu uweze kunielewa kirahisi
Hujanikandia, unaeleza mtazamo wako, ambao, kwa namna yoyote si sheria kwangu wala jinsi nilivyo. Utabaki kuwa mtazamo wako. Uhalisia uko hivi, akili yangu nii komavu sana. Leo yangu na kesho yangu imeshabarikiwa sana kiasi nisichoweza kueleza. Siombi msamaha kwa jambo mtu analolisababisha mwenyewe. Ninawajibiika kuomba msamaha kwa kile nilichokisababisha mimi. Ukinielewa vibaya ukafanya maamzi mabaya na ukategemea mimi nikuombe msamaha, haitaweza kutokea. I have to close this case. Sitaomba msamaha na yeye asubuhi hii namjulisha kwamba sitaweza kuendelea na hayo mahusiano. Tuendelee kushauriana kwa manufaa ya wengine pia.
 
Mada yako Ipo kwenye mrengo Hasi, na chanzo cha uhasi huo ni mhusika wewe ndani ya hicho kisa.

Wewe ndiye umemkatili huyo Binti.

Sasa ukiambiwa ukweli unaona kama tunamitazamo hasi.
Wewe kama huna Mtazamo Hasi, nini kinakushinda kwenda kuomba Msamaha mpaka uite Jambo hilo ni masharti ya huyo Mchumba wako?
Jambo ambalo Kwa MTU mwenye Akili wala asingesubiri kuambiwa akaombe Msamaha kwani angeenda mwenyewe.

Acha Ubinafsi
"Mtu mwenye akili",,,labda useme mtu mwenye huruma. Wenye akili hawapo hivyo!
 
Wote mnaomponda mshkaji kwa kumsaidia jamaa yake hamna akili, kuna baadhi ya marafiki ni bora kuliko ndugu hata mimi ingetokea situation kama hiyo kwa jamaa flani ningefanya ivo ivo, mnaosema mke atakusaidia siku unamatatizo inamaana hamjui kuwa kuna wanawqke hukimbia familia kipindi cha shida?
Hatujamponda kwa kuwa amemsaidia rafikiye,tumemsema kwa sababu ya kutotoa taarifa ya kuahirisha jambo aliloahidi hata pale baada ya mchumba wake kususa angetakiwa atume wazee watoe taarifa kule ukweni,but unfortunately hakufanya hivyo
 
Hii duuu kwenye
Ni kweli ulikosea. Ushatoa ahadi unaenda kutoa mahari, alaf unapotelea mitini, lazima uwatake ladhi, lakini ujielezee.
Jibu zuri kama hilo

Inaonesha upo kwenye makundi ya watu wasiopenda kujishusha😅
Kama unamtaka ni vyema na busara kugusia kwa nini ulikwama na una malengo na binti yao, endapo walifikiri vingine ikawaudhi, unawaomba radhi
 
Kuna binadam wengine wana historia ndefu sana katika maisha yetu. Niliamua kumusaidia na sikuona sababu ya huyu mpenzi wangu kupaniki na kuomba tuachane. Leo anaporudi na masharti ya kwamba niombe msamaha nyumbani kwao, naona kama ananikoroga kichwa tu.
Kuna jambo nature ilitaka kukuokoa lakini huelewi somo
 
Hujanikandia, unaeleza mtazamo wako, ambao, kwa namna yoyote si sheria kwangu wala jinsi nilivyo. Utabaki kuwa mtazamo wako. Uhalisia uko hivi, akili yangu nii komavu sana. Leo yangu na kesho yangu imeshabarikiwa sana kiasi nisichoweza kueleza. Siombi msamaha kwa jambo mtu analolisababisha mwenyewe. Ninawajibiika kuomba msamaha kwa kile nilichokisababisha mimi. Ukinielewa vibaya ukafanya maamzi mabaya na ukategemea mimi nikuombe msamaha, haitaweza kutokea. I have to close this case. Sitaomba msamaha na yeye asubuhi hii namjulisha kwamba sitaweza kuendelea na hayo mahusiano. Tuendelee kushauriana kwa manufaa ya wengine pia.

"Miezi michache iliyopita, nilitengana na mwenzi wangu wa muda mrefu baada ya kusitisha kuota mahari nyumbani kwao na kuamua kumsaidia rafiki yangu ambae alikuwa kwenye changamoto fulani za kimaisha"

Embu soma hayo maelezo yako, afu uone Nani kakosea baina yako na huyo Mchumba wako.

Hujui kuvunja ahadi ni moja ya Usaliti?
Ushamuahidi mtoto wa Watu alafu unakuja na visababu uchwara visivyo na kichwa na miguu.

Ungekuwa na Akili ungefanya moja ya mambo haya;
1. Ungetakiwa kuomba Radhi
2. Ungetuma Wawakilishi kule ukweni.

Afu ushasema ni Mchumba wako WA muda mrefu, kumaanisha kama MTU mwenye Akili unayejua thamani ya muda na mahusiano, usingeweza fanya kitu kama hicho.

Ni Sawa na MTU mjinga ambaye amekaa kwenye mahusiano Kwa miaka 10 alafu ndoa au mahusiano yake yavunjike ati Kwa kushindwa kusema neno "Samahani" lenye silabi nne.
Ni MTU mjinga tuu asiyejua anataka nini kwenye Maisha..
 
namjulisha kwamba sitaweza kuendelea na hayo mahusiano.
Wewe ndo ulimuambia unamkaribisha akijiona anakuhitaji. Anyways, mpige chini—ni Sawa kwa sababu hakusikiliza na kuchukua 50 zake,
Ila pia unaweza kuwa romantic na kumwambia “mpenzi, you should have listened, anyways, wazazi wamekasirika, nakupenda sana, nitajua la kufanya”

Unaenda siku ya kutoa mahari, unaelezea situation na kutoa samahani kama angalizo tu la endapo walichukia
 
"Mtu mwenye akili",,,labda useme mtu mwenye huruma. Wenye akili hawapo hivyo!

Wakuonewa huruma hapo ni wewe 😂😂😂

Sisi wazoefu WA mapenzi tunajua nini kinafuata kwako kwenye ishu za mahusiano.

Kesho kutwa hapa utakuja kuwatukana Wanawake ni Mbwa,
Nipo nimekaa hapa
 
Omba msamaha kwa kutoka nje ya muda,peleka hela za watu. Usichelewe ukikutana na jamaa wanaopinga hili jambo unaweza ukashawishiwa ukaghairi kabisa
 
Umemkosea na umempa fedheha kwa familia yake, na Umevunja Ahadi..!!!

Kama ni mimi ningeshakublokilia mbali everywhere kuanzia kwenye Moyo,nafsi,akili etc

Unaonekana hauna msimamo wala clear vision, Mwanaume mwenye Vision habadili plans zake kwa changamoto za ghafla, huyo Dada ningemjua ningemshauri akusahau angaalie maisha yake



Nimemuambia naona anakaza Fuvu.
Ni mbinafsi Sana.

Mimi ningemshauri huyo Bibie amuombe Msamaha mshikaji kisha ampige tukio litakalomfurahisha.
Huwaga wengine hatumalizagi mambo yetu ubao ukionyesha tumepigwa
 
Kuna binadam wengine wana historia ndefu sana katika maisha yetu. Niliamua kumusaidia na sikuona sababu ya huyu mpenzi wangu kupaniki na kuomba tuachane. Leo anaporudi na masharti ya kwamba niombe msamaha nyumbani kwao, naona kama ananikoroga kichwa tu.

Kama umekosea Kwa nini usiombe Msamaha?😂😂😂

Au haujiamini?😀😀
Kuomba Msamaha sio kujidhalilisha Mkuu. Acha mawazo potofu ya Watu wajinga na wenye ushetani
 
Ila huyo mwanamke hana akili pamoja na kumuaibisha bado kajileta mfyuu zake
Mapenzi mkuu. Husababisha upofu. Majuto ni mjukuu. Ila upo sahihi kabisa. Kuna mwingine namjua aliamua kujilipia mahari mwenyewe. Yaani bwana alikuwa anasuasua (ila walikuwa wanaishi na demu) basi demu akatoa fedha akandaa ndugu wa kule kwa bwana wakapeleka mahari. Mwanaume alikuwa ni mtu wa kujirusha hivi, handsome fulani hivi, demu akakolea mno. ndoa ilifungwa lakini ugomvi ukawa hauishi. Na kila walipokuwa wanagombana jamaa anawaambia marafiki zake, ''kwanza alijioa mwenyewe huyu''.
 
Kuna binadam wengine wana historia ndefu sana katika maisha yetu. Niliamua kumusaidia na sikuona sababu ya huyu mpenzi wangu kupaniki na kuomba tuachane. Leo anaporudi na masharti ya kwamba niombe msamaha nyumbani kwao, naona kama ananikoroga kichwa tu.
Yaani unapanga kupeleka mahari halafu unahairisha na unapoambiwa uombe msamaha unasema unakorogwa kichwa? Dada wa watu kapewa ishara muhimu sana kuwa wewe hufai lakini maskini ameshindwa kuitambua. Wewe huna tofauti na Magufuli kitabia na ndoa yako itakuwa kama ilivyokuwa yake.
 
Kama ulitoa taarifa, hakuna haja ya kuomba msamaha...
 
Ila wewe mbona ishu yako ndogo ..mimi kuna mwana yeye sio tu aliahirisha ila hata manzi ake hakumwambia..Kikeni huko wamejiandaaa kishenzi mavyakula na vilaji kama unavyojua wachaga!.. e bwana eeh!!. Mshkaji hakutokea kabisaaaaaa wala manzi ake hakumwambia kitu yan ilikua bonge la soo na aibu kwa dem..ndugu jamaa walishajaa kupokea mahali na kumwona jamaa ila ikawa tee!!.

Wanawake sas wasivyo na akil wakat mwingine, manzi aliporud dar wakaendelea kuishi na mshkaji..sijui waliyamaliza vp? 😂😂😂
Ukiona mapicha picha mwanzoni inafaa ujiweke kando na huyo mtu.
Kuna ndg yetu alilazimisha kitu kama hiki hadi leo anajutia
 
Kuna binadam wengine wana historia ndefu sana katika maisha yetu. Niliamua kumusaidia na sikuona sababu ya huyu mpenzi wangu kupaniki na kuomba tuachane. Leo anaporudi na masharti ya kwamba niombe msamaha nyumbani kwao, naona kama ananikoroga kichwa tu.
Huenda habari hii ni changamsha genge
 
Back
Top Bottom