Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Mkuu kuna tabia wanaume tumeanza kuchukulia kuwa kuoa ni kama vile kutoa msaada kwa binti au wazazi wake.

Kama humtaki binti mpe ukweli kuwa hauko tayari kumuoa awe huru.

Hii danadana na sababu uchwara ni dharau.
Kila mwanaume ni mkwe mtarajiwa.

Hakuna mwanaume atapenda kuona binti anachukuliwa poa...jitu linamtumia binti yako kwa ulaghai wa kuoa mwishowe unaanza ooh silipi mahari nampa msaada rafiki.

Katika mahusiano ya ndoa hakuna wazazi wenye msaada kimaisha kama wazazi wa binti hasa wazazi waelewa.
Hawatapenda kuona binti amekwama bila kutoa msaada.
Tubadilishe mitazamo ya kikoloni
Umeongea ukweli mkuu,kuna wanaume wanajiona wao ndo wao,yani hawataki kusikiliza mtu yyte Wala ushauri,ni wajuaji,viburi na dharau wanafanya wanayoyataka,ni wababe wajeuri na hawajali,ila mbio za sakafuni huishia ukingoni
 
Kueleza hapo sasa hivi kwamba allimshirikisha mwenziwe kabla ndo akakimbilia kusitisha mahusiano. So angeenda kwa in-laws kama ex ama kama nani?
Mkuu...mwanaume ni simba, kiongozi na mshawishi.

Inategemea na aprochi yake.
Angemwita amwambie....my love plz naomba tuahirishe kwani nilitegemea kupata pesa lakini nimeahirishiwa nami aitaki nikuaibishe kwa wazazi wako.
Naomba tusogeze mbele kidogo...binti asingekataa lakini kutamka wazi unamsaidia rafiki na aio ndg ilikuwa dharau mkuu
 
Sasa MKUU unatak ushaur gani hapo , Hata bila kuambiw na binti inabd ufany hvyo kwakuw jambo lilishapangwa na wew ukabadl gia angani

Tena inabd upgw faini
 
Hatma ya mwanadam ipo mikononi mwa muumba. Maombi mabaya na mengine ya namna hiyo hayana nafasi provided yanatoka kwenye kinywa cha mdhambi kama mimi. Tuendelee kushauriana.
Wala sikuombei uumwe but but unafanya jambo au maamuzi tanguliza utu usiwe na kiburi.

Ona hata kichwa habari kinaonyesha jeuri uliyo nayo
 
Wala sikuombei uumwe but but unafanya jambo au maamuzi tanguliza utu usiwe na kiburi.

Ona hata kichwa habari kinaonyesha jeuri uliyo nayo
Sina jeuri hata kidogo. I'm down to earth, humble. Ndio maana hata binti wa watu anaomba kurudi. Kuna historia zinazoumiza sana katika maisha. Msaada ni muhimu sana kwa watu wengine. Huu ni utamaduni wangu. Ninatamani kila mtu atambue kwamba sikufanya kwa lengo la kumdhalilisha mwenzangu ila alitoa maamzi ya ghafla sana.
 
Mkuu, nipo vema sana upstairs. Haya mambo tushauriane kwa staha tu. Hakuna alie mkamilifu.
.....very sorry mkuu, smahani sana Kwa namna nilivyowasilisha nadhani nimekukwaza kiasi fulani.....samahani sana mkuu...
 
Sina jeuri hata kidogo. I'm down to earth, humble. Ndio maana hata binti wa watu anaomba kurudi. Kuna historia zinazoumiza sana katika maisha. Msaada ni muhimu sana kwa watu wengine. Huu ni utamaduni wangu. Ninatamani kila mtu atambue kwamba sikufanya kwa lengo la kumdhalilisha mwenzangu ila alitoa maamzi ya ghafla sana.
Mkuu ukubali usikubali huna vipaumbele.

Mimi nina huruma sana, naweza kuacha kula mimi nimpe mhitaji. Lakini linapokuja suala muhimu nina vipaumbele visivyobadilika.

Mtu wangu au watu wangu ni kipaumbele changu cha kwanza.

Endapo nitabadili maamuzi nisaidie mwingine.....nitatumia convincing power yangu yote nihakikishe wananiunga mkono nimtangulize mwingine badala yao.

Mwanaume hakikisha una NGUVU YA ushawishi.
Ushawishi
Ushawishi
Ushawiahi wanaume tujitahidi katika hili hatutajuta.
Wanawake ni waelewa mno ukionyesha kuwajali
 
Back
Top Bottom