Amini, Usiamini. Nimepona Magonjwa 100+ Kwa Jina la Yesu!

Amini, Usiamini. Nimepona Magonjwa 100+ Kwa Jina la Yesu!

Thank you for pointing that out; I understand the distinction between symptoms and a disease. However, when I shared my testimony, I wasn’t focusing on medical terminology but on how I experienced healing in my life. Whether it was the symptoms or the underlying condition, I truly believe that through prayer and faith, I found relief and restoration. My intent is not to debate definitions but to testify about what God has done for me

I see!
Ukienda swahili kwa Swahili itapendeza

Kwakuwa umeelewa badilisha kauli yako toa hilo neno Magonjwa mia
 
Hichi ndo kitu kimepelekea unaona Africa Ilipofikia sa hivi.

Tunasafari ndefu sana..

Yaan hata walotuletea hizi dini kuna muda wanatushangaaa
Issue zengine mkuu wala haziitaji dini, kwa wenzetu huko waliyoendelea na kutuletea dini wana mambo kama hayo ila wala hawahusishi dini,uchawi wala Mungu.
 
Huyo Mungu ana nguvu gani?

Huyo Mungu mwenye nguvu mbona ameshindwa na anashindwa kuwasaidia maelfu ya wanawake na watoto wanaoteseka na kufa kwa njaa, vita, magonjwa, majanga ya asili na shida mbalimbali duniani?

Huyo Mungu kama yupo, Ni Mungu mdhaifu, mjinga, mchovu, katili na bandidu na wala HANA msaada wala nguvu yeyote.

Mungu huyo hafai kabisa anastahili kufurushwa.
View attachment 3195668
Hujui usemalo. Mungu akuhurumie tu
 
Thank you for pointing that out; I understand the distinction between symptoms and a disease. However, when I shared my testimony, I wasn’t focusing on medical terminology but on how I experienced healing in my life. Whether it was the symptoms or the underlying condition, I truly believe that through prayer and faith, I found relief and restoration. My intent is not to debate definitions but to testify about what God has done for me

I see!
Go and testify to your gullibles.

This is a public forum.
Jamii forum zone of Thinkers.

Not gullibles.
 
Huu ni ushuhuda wa kweli kabisa. Katika maisha yangu nimekuwa nikiugua magonjwa mengi ya aina mbalimbali. Kifuani, tumboni, miguuni, katika vidole, machoni, masikioni, puani, kichwani, nk, nk. Muda hautoshi kuyaeleza kwa kina. Kwa haraka haraka naweza kusema tangu ujana wangu nimeugua zaidi ya magonjwa 100. Namshukuru Mungu kwakuwa amekuwa akiniponya magonjwa kila yanaponiijia. Ninachokifanya, kila nikiumwa, namuomba Mungu aniponye kwa Jina la Yesu, kisha naweka mkono wangu juu ya sehemu inayoumwa na kuuamuru ugonjwa utoke kwa Jina la Yesu; kisha naamini kwamba imekuwa hivyo. Wakati mwingine inachukua muda kuona matokeo lakini wakati mwingine ugonjwa unatoweka saa hiyo hiyo. Maneno aliyosema Yesu ni kweli kabisa. Katika Mk 16:17-18 anasema: “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu(Yesu) watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.”

Huu ni uthibitisho kuwa Mungu yupo na anatenda miujiza hata leo kwa watu wanaomuamini. Kwa ushuhuda huu sikuambii usiende hospitali. La, hasha! Ukiwa na pesa, nenda. Nenda hata hospitali za nje ya nchi. Hata mimi kuna wakati huwa naenda hospitali kwa kuwa najua kwamba Mungu anaweza pia kuponya kwa kuwatumia madaktari. Hata hivyo ninapoenda hospitali bado naweka matumaini yangu kwa Mungu kwakuwa najua madaktari nao kuna magonjwa yako juu ya uwezo wao au elimu yao; na wakati mwingine nadhani huwa wanajisahau, badala ya kutia moyo wanakatisha tamaa. Kuna siku nilipungukiwa damu, nikaenda kumuona Daktari. Aliponipima na kuhakikisha damu imepungua, akaniuliza: “Damu umepeleka wapi wewe?” Usipokuwa na matumaini kwa Mungu ukiulizwa swali hilo la kuvunja moyo unaweza ukaugua mara mbili zaidi. Na kwa magonjwa niliyougua, kama kila ugonjwa ningekuwa nakimbilia hospitali, ningehitajika kuwa milionea maana ningepaswa kulipa pesa nyingi za matibabu. Namshukuru Yesu anaponya bila kulipa hata senti. Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka hizi za uzima.

Hata hivyo kuna vigezo na masharti ya kuzingatia ili mtu aone kikamilifu uponyaji wa Mungu kwa Jina la Yesu. Baadhi ya vigezo vimeelezwa katika Andiko hili: Kutoka 15:26. “Mungu akasema, ‘Kama mtaisikiliza kwa bidii sauti yangu mimi BWANA Mungu wenu na kuyafanya yaliyo sawa mbele yangu, kama mtayatii maagizo yangu na kuzishika amri zangu zote, sitaleta juu yenu ugonjwa wowote niliowaletea Wamisri, kwa kuwa Mimi ndimi BWANA, niwaponyaye.’” Uponyaji wa Mungu ni wa bure kwa wote wanaozingatia maneno hayo. Ukisikia Mtumishi anakuambia ulipe pesa kwanza ndio akuombee, jihadhari naye. Yesu alipowapa mamlaka wanafunzi wake ya kukemea pepo na kuweka mikono juu ya wagonjwa ili wapone, aliwaambia amewapa bure, hivyo wanapaswa kutoa huduma hiyo bure(Mathayo 10:8).

Yamkini unaumwa, umetibiwa kila mahali hujapona. Usikate tamaa. Ushuhuda huu ukutie moyo kuwa unaweza kupona kwa uwezo wa Jina la Yesu Kristo. Yote yawezekana kwake aaminiye(Mk 9:23). Amen.
Kama unachosema ni kweli, orodhesha hayo magonjwa 100.
 
Soma Biblia kwa utulivu; majibu ya maswali yako yote utayapata humo!
Hizo ni hekaya kama za Abunuwasi tu.

Biblia nimeisoma kuliko hata wewe.

Kwa hivyo huwezi kunidanganya kitu.

Sana sana utashindwa kujibu maswali yangu uanze kufanya ad hominem fallacy kusema kwamba I'm lacking holy spirit to understand the scriptures. While the scriptures are illogical.
 
Back
Top Bottom