Amos Makalla ametudhalilisha na kututukanisha wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla

Amos Makalla ametudhalilisha na kututukanisha wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla

Duh usafi mpaka mfundishwe

Usafi ni utamaduni wa watu,jamii iliyopo pale hapo nje tu kwa mkuu wa mkoa ofisi pachafuuu sana

Ova
Ndio hapo sasa. Mbona Rwanda yenyewe miaka 25 nyuma ilikuwa chafu kama zilivyo nchi nyingi za Afrika. Wakajifunza wenyewe usafi kwa kuelimishana na kusimamiana hadi leo nchi yao ndo imefika hapo ilipofika.
 
Huyu kadhalilisha taifa zima, Akamatwe awekwe ndani lwa udhalilishaji huu
 
Nimeshangazwa na kitendo cha mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam mheshimiwa Amos Makalla kutumia kodi za walalahoi kukodi ndege ya kuwapeleka wamachinga na wadau wengine nchini Rwanda eti kujifunza usafi.

Inamaana Watanzania wenyewe ni wachafu na hawawezi kujifunza usafi mpaka waende kufunzwa na wanyarwanda. Hii si aibu ya mwaka huu mpya wa 2023? Je lile somo lililokuwa linatufunza usafi shuleni halifundishwi tena madarasani?

Ina maana watanzania tumekuwa watu wa kuiga kila kitu kutoka kwa wenzetu hata vile ambavyo tunaweza kuvifanya wenyewe tunashindwa kuvifanya kwa kusubiri kwanza tujifunze kupitia kwa wengine.

Katika hili Makalla amechemsha sana na kuleta aibu kubwa kwa wana Dar es salaam. Hii ni sawa na kumwambia jirani yako amfunze mkeo namna ya kuoga na wakati wewe mumewe unao uwezo huo na dhamana ya kumsimamia mkeo katika hilo.

Mambo ya aibu namna hii ndo yanayosababisha wengi tushindwe kurudi nyumban sasa hivi.
Hauna kiambatishi?? Tunaaminije hii taarifa?
 
Ndio hapo sasa. Mbona Rwanda yenyewe miaka 25 nyuma ilikuwa chafu kama zilivyo nchi nyingi za Afrika. Wakajifunza wenyewe usafi kwa kuelimishana na kusimamiana hadi leo nchi yao ndo imefika hapo ilipofika.
Usafi sisi ni wa Kiki na sifa

Sijuwi kiongozi gani naye atakuwepo

Basi watajaa watu lundo na masista duh wanafanya usafi wa zima moto

Dar ni chafu,watu wake wachafu

Na huko wameenda ni kupoteza muda tu na fedha

Ova
 
Ushawahi kuona wapi nchi moja inatuma raia wake nchi nyingine wakajifunze usafi. Ingekuwa ni swala la kwenda kujifunza mbinu za biashara, intelejensia nk hapo ningeelewa. Lakini swala la usafi kweli ni la kukodi ndege kwenda kuwafunza watu nje ya nchi? Yuko serious kweli!
Acha upotoshaji hakuna ndege iliyokodiwa,Kwa wakazi wa dar uchavu umekuwa ni sehemu ya maisha yenu/yao .Japo hata hao waliokwenda huko hawawezi kubadirisha chochote.Kwa uchafu tu mijitu ya dar imezidi.Kutoa 1000 tu kwa mwezi kama ada ya uzoaji taka hadi mjumbe aingilie kati.Tatizo ni siasa tu huyo RC na mabaraza ya madiwani wakiamua kuweka sheria kali watu watabadirika tu.Tatizo siasa ohoo hawq ndio wapiga kura wetu tutawaudhi.
 
Tatizo la uchafu linaanzia kwa hawa viongozi wetu ambao ni wanasiasa,wao ni wachafu ndio maana wanashindwa ata kuweka majiji yao safi...mbona Kilimanjaro na Iringa ni miji iliyo safi....vp Dar es salaam kipindi cha Keenja ilivyokuwa safi?...usafi unatakiwa kuwa kwenye damu
 
Pima kuona nia ilompelekea kufanya hivyo ni njema au hila ?

Kama ni kwa nia njema basi wala usihusudu.

“At the end of the day the intention is important “
 
Hiyo hela bora ingeongeza nguvu kwenye kuzibua mitaro,kununulia gari la takataka au kupiga sakafu baadhi ya masoko ambayo kipindi cha mvua uwa yanajaa matope ukiyaangalia uwa kama mabwawa ya kinyesi
 
Nimeshangazwa na kitendo cha mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam mheshimiwa Amos Makalla kutumia kodi za walalahoi kukodi ndege ya kuwapeleka wamachinga na wadau wengine nchini Rwanda eti kujifunza usafi.

Inamaana Watanzania wenyewe ni wachafu na hawawezi kujifunza usafi mpaka waende kufunzwa na wanyarwanda. Hii si aibu ya mwaka huu mpya wa 2023? Je lile somo lililokuwa linatufunza usafi shuleni halifundishwi tena madarasani?

Ina maana watanzania tumekuwa watu wa kuiga kila kitu kutoka kwa wenzetu hata vile ambavyo tunaweza kuvifanya wenyewe tunashindwa kuvifanya kwa kusubiri kwanza tujifunze kupitia kwa wengine.

Katika hili Makalla amechemsha sana na kuleta aibu kubwa kwa wana Dar es salaam. Hii ni sawa na kumwambia jirani yako amfunze mkeo namna ya kuoga na wakati wewe mumewe unao uwezo huo na dhamana ya kumsimamia mkeo katika hilo.

Mambo ya aibu namna hii ndo yanayosababisha wengi tushindwe kurudi nyumban sasa hivi.
Kwani Dudumizi kile kijiwe chako cha kuuza vipande vya muwa pale na Mbagala rangi tatu,unajua kusafisha mazingira baada ya kuuza miwa yako,au kwakuwa umekosa nafasi ya kupasishwa hadi Rwanda,😂
 
Usafi sisi ni wa Kiki na sifa

Sijuwi kiongozi gani naye atakuwepo

Basi watajaa watu lundo na masista duh wanafanya usafi wa zima moto

Dar ni chafu,watu wake wachafu

Na huko wameenda ni kupoteza muda tu na fedha

Ova
Kweli kabisa. Jamaa kaenda kuangamiza kodi zetu maana waliopelekwa huko wakirudi watazuga zuga siku za mwanzoni, afu baada ya mwezi au miezi watarudia maisha yao yale yale waliyozoea.
 
Acha upotoshaji hakuna ndege iliyokodiwa,Kwa wakazi wa dar uchavu umekuwa ni sehemu ya maisha yenu/yao .Japo hata hao waliokwenda huko hawawezi kubadirisha chochote.Kwa uchafu tu mijitu ya dar imezidi.Kutoa 1000 tu kwa mwezi kama ada ya uzoaji taka hadi mjumbe aingilie kati.Tatizo ni siasa tu huyo RC na mabaraza ya madiwani wakiamua kuweka sheria kali watu watabadirika tu.Tatizo siasa ohoo hawq ndio wapiga kura wetu tutawaudhi.
Watu wamekwea pipa mkuu. Wewe uko nchi gani mpaka usiyajue haya yanayoendelea nchini?
 
Kwani Dudumizi kile kijiwe chako cha kuuza vipande vya muwa pale na Mbagala rangi tatu,unajua kusafisha mazingira baada ya kuuza miwa yako,au kwakuwa umekosa nafasi ya kupasishwa hadi Rwanda,😂
Mkuu mimi hakuna kitu ninachochukia kama uchafu. Laiti wana Dar es salaam wangekuwa wanauchukia uchafu kama niuchukiavyo basi mji wetu ungekuwa ni zaidi ya Brussels achilia mbali Kigali nk.
 
Back
Top Bottom