Pre GE2025 Amos Makalla Mwenezi mpya CCM Taifa, Ally Hapi Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi

Pre GE2025 Amos Makalla Mwenezi mpya CCM Taifa, Ally Hapi Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Teuzi ziendane na hadhi basi jamani, Alli Happi na umoja wa wazazi wapi na wapi jamani?
 
Ally Hapi ni mfano mzuri kwa kufanya kilimo baada ya kutenguliwa ukuu wa mkoa. Ameonesha kwa vitendo kwamba siyo lazima apate cheo cha kisiasa ili aishi.
Kwa uzoefu aliopata kwenye kilimo, atakuwa kiongozi anayejua shida za wakulima.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Duuuuuh upande wa mwenezi sijaona mtu mwenye kujipamba ccm na kuwafanya watanzania waiamini na kuweza kuipa kura tena
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] si ni huyo papaa makalla, mtoto wa mjini.
 
Wataalamu wa serikali na siasa hii ya kupata appointment za chama na serikali inaingilianaje? Inaruhusiwa kisheria hiyo?
 
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo tarehe 03 April, 2024 jijini Dar Es Salaam, katika kikao chake maalum, chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na masuala mengine, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, imefanya mabadiliko madogo ya Sekreteriet ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuwachagua wajumbe kama ifuatavyo:
  • Ndugu John Mongella kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, akichukua nafasi ya Anamringi Macha ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga,
  • Ndugu Amos Gabriel Makalla kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, akichukua nafasi ya Ndugu Paul Makonda ambaye ameteulia kuwa Mkuu wa Mkoa Arusha.
  • Ndugu Ally Salum Hapi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania, akichukua nafasi ya Ndugu Gilbert Kalima ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga,
  • Ndugu Jokate Urban Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM akichukua nafasi ya Ndugu Fakii Raphael Lulandala ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.
Aidha katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi, ambaye pia ni Mwenye kiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kazi kubwa na nzuri ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 – 2025.

IMETOLEWA NA IDARA YA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO 03 APRIL, 2024
Lucas Mwaashambwa na Mayalla naona wanaendelea kukosa mvuto.
 
Happi amerudi kwenye cake ya taifa?? Km namuona kidampaa akifurahi kututambia wenzie, basha wake kapata teuzi.

Tutakomaaaa mwaka huu, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Basha wa nani jamani fungua code jamani mamy ake
 
Back
Top Bottom