Amri Kuu Kuliko Zote ni Upendo! Mpende Mungu, Ipende Nchi, Wapende Viongozi, Mpende Jirani Yako Kama Nafsi Yako!. Jirani yako ni Nani?, Unampenda?

Mkuu KANYIMBI , asante sana kwa hii, huu ndio ukweli wa jirani ni nani, na sasa mtashangaa jinsi Taifa litakavyo barikiwa.
P
 
Nimekuelewa Mkuu[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Wanabodi,
Hili ni bandiko la salaams zangu za Krismasi ya mwaka jana ambayo nilisisitiza upendo. Kwenye medani za siasa za vyama, nilisema "CCM kama chama tawala, jirani zake ni Chadema, ACT Wazalendo, CUF, NCCR etc, wana CCM wanawajibu wa kuwapenda vyama vingine kama wanavyojipenda wenyewe!, haiwezekani wao wawe huru kufanya mikutano, lakini wanawazuia wengine!".

Hoja hii ilijibiwa kwa vitendo kwa mikutano ya siasa kuruhusiwa, hivyo haya tunayoandika, sio tunajiandikia kupoteza muda, tunayo yaandika yanafanyiwa kazi.

Ukiandika kuomba kitu fulani, siku ukipewa hicho ulichokiomba, una wajibu wa kumrejelea yule uliyemuomba na kumshukuru kupokea ombi lako na kulitekeleza, hivyo nami baada ya mikutano ya siasa kuruhusiwa, kwanza niliandika makala ya kushukuru, Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa kisha nikaomba ile haki nyingine iliyoporwa irudishwe.

Kikao cha Bunge lijalo, kitapitisha mabadiliko ya sheria ya uchaguzi, vyama vya siasa na Tume ya Uchaguzi, mabadiliko yote hayo ni superficial tuu kama hakuna mabadiliko ya katiba, hivyo mwaka huu ujao wa 2024, let's press for mabadiliko ya katiba ili tufanye uchaguzi mkuu wa 2025 uwe uchaguzi huru na wa haki.
Mungu Ibariki Tanzania
I wish you a erry Christmas and Prosperous New Year!.
P
 
Pasco

"Kuna watu hawapendani huko"!?

Amulia ugomvi Ndugu!
Mkuu NAMBA MOJA AJAYE NCHINI , kuna watu walikuwa hawapendani, wenyewe walikuwa wanajifanyia mikutano ya chama chao, tena mingine wanaifanyia hadi pale patakatifu petu, huku wamepiga marufuku wenzao kufanya mikutano ya hadhara na sometimes kuzuia hata mikutano ya ndani, lakini baada ya wito huu wa upendo, moyo wa upendo ukamwingia mtu, akaumwaga upendo kwa kuruhusu mikutano ya siasa kwa wote. Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa

Mwaka huu ujao wa 2024 tunapigania upendo wa mabadiliko ya katiba ili kutoa haki kwa wote, tufanye mabadiliko ya katiba ili kufanya chaguzi huru na za haki.
P
 
AMRI NGUMU sana HIYO Mwendazake alishindwa kabisa kuwapenda KABISA CHADEMA[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mkuu Sir robby, kumbe wewe ndio ulikuwa hujui, JPM alikuwa anawazimia kichizi Makamanda, ndio maana akawasomba Makamanda kibao wakahamia Chadema. Huo ni Upendo mkubwa.

Maza alipoingia ndio kabisa, amewaita hadi kukaa nao meza kuu, na kukubaliana kugawana mkate pasu kwa pasu, kila mtu apate nusu mkate. Huu ni Upendo mkubwa, Mahali ni pazuri ndugu wanapokaa, wakipata vema na kupendana. Tulikotoka ni kugumu, tunakokwenda ni kurahisi, kuzuri! Heri ya Mwaka Mpya wahusika wote
P
 
Hivi Mungu anampenda shetani!!!?
Mungu anampenda sana tuu shetani ndio maana yupo mpaka kesho!. Ndiye aliyemuumba, na kabla shetani hajafanya lolote, huomba kibali kwa Mungu, akikubaliwa ndipo anafanya ushetani wake!. Sisi Wakristu hili tumelisoma kwa Ayubu, pia Bwana wetu Yesu Kristo alijaribiwa na shetani.
P
 
Tuwapende wapinzani pia, tusiwachukie.
Naunga mkono hoja, No. 1 kaonyesha mfano kwa kukaa nao mezani na wakakubaliana kugawana mkate, pasu kwa pasu, kila mtu kupata nusu mkate.
P
 
Kwa mafundisho ya dini ya Kikristu, tuliyopewa na huyu Masiya aliyezaliwa leo, Bwana wetu Yesu Kristu, aliulizwa amri kuu kuliko zote ni amri gani?,
Pascal Mayalla nimekuelewa vizuri nakubaliana nawe 80% ila kamwe sitakubaliana nawe juu ya kuwapenda viongozi hawa wanatuibia, na kutufanya wajinga miaka nenda rudi mpaka wanafikia kutaka kuitumbukiza nchi kwenye tawala za kigeni kwa kutumia rasilimali zetu.
 
Mkuu Faana , kuna wengi hawajui, love will conquer all!, ukiwapenda hao viongozi wanaotuibia, na kutufanya wajinga miaka nenda, miaka rudi mpaka wanafikia kutaka kuitumbukiza nchi kwenye tawala za kigeni kwa kutumia rasilimali zetu, wanayafanya hayo kwa ukosefu wa upendo, hivyo ukiwapenda, watapata upendo na kuacha hivyo vitendo vyao!.
Merry Christmas and Prosperous New Year.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…