Ana kwa ana na Mwigulu Nchemba: Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Ana kwa ana na Mwigulu Nchemba: Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Huna taarifa hata kidogo, fuatilia upate ukweli ndio uje uandike. Kama kawaida nadhani unatamani niishi kama mbwa koko. nikuhaikikishie watafute wenye taarifa wakwambie nani aliwasaidia walipokuwa na matatizo
Mwigulu ulikuwa unaongeza genge la wahuni wasiojulikana kufanya mauaji na utekaji, ni vema ukatafuta muda ukatubu na uwaombe radhi watanzania, Nape aweza kukushauri
 
Waulize wanajua vzr

Haya majibu ndio yalinifanya nikushauri kukaa kimya, huko mbele ya safari utajutia maamuzi ya kuanzisha huu uzi. Vinginevyo umejipanga na uko radhi kwa yatakayoendelea.

Kwa nchi inayojitanabaisha kuwa na utawala bora, haya ni majibu ya mbunge aliyewahi kuwa naibu waziri na waziri kamili kweli?

Isitoshe mchumi na mwenye PhD? Sasa kama watu hawawezi kuuona huo uwezo wa PhD yako katika kujieleza au kuelimisha watu kuhusu jambo unajipambanuaje na wengine?
 
Mheshimiwa usiache kupita kwenye uzi wetu pendwa "kula tunda kimasihara" utupe na wewe japo ushuhuda kidogo [emoji124][emoji124]

mweshimiwa pengine huwa anapita na kuperuzi tu..hawezi kucomment though pengine naye anatamani lakin...utumishi wa uma unamiiko yake...
 
Iramba bado ina kiu ya maji si ndio?

Huduma za afya hasa hospitali wananchi wa jimbo la iramba magharibi wanategemea Puma mission, Makiungu na Itigi.

Mwigulu Nchemba usivyo na aibu utabisha na hili.

Wanategemea Kiomboi Hospital ya Iramba, Pia wanaweza kwenda Kwa Majirani zao Mkalama
 
Kuna mtu ametupia uzi kuwa siku hizi sivai skafu, huu ni mkutano mkuu wa juzi tarehe 19/2/2020 wakati wa ziara ya mzee Mangula. Skafu nilikuwa navaa hata kabla ya kwenda Ilboru Sekondari haikuwa sare ya Uwaziri.

View attachment 1365715

Kama kuna maswali kunihusu, nitayajibu hapahapa
Kwanini viongozi wengi walikuzwa na mh.freeman mbowe ndio wanapewa vyeo kuliko viongozi walikuzwa na umoja wa vijana wa ccm?
Mkiendelea hivyo hamuoni Kama baada ya miaka 10 bavicha itakuwa imetowa viongozi wengi serekalini kuliko uvccm?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mweshemiwa hili sakata la viongozi kutoka upinzani kurudi nyumbani, wakihama wote si huko nyumbani kutakuwa hakukaliki sasa???
 
INIHUSU KWA KUWA UMESEMA AU KWA KUWA UNATAKA INIHUSU? YAAN RAFIKI YANGU UNAISHI GIZANI KWELIKWELI. ULILISHWA MATANGO PORI YA KISIASA, WALIKULISHA WALISHAHAMIA CCM WEWW BADO UNASHIKILIA. MAISHANI MWANGU SIJAWAHI KUHUSIKA NA HATA JASHO TU LINALOTOKANA NA MATESO KWA MTU. ACHILIA MBALI DAMU


Hii ni zaidi ya utovu wa nidham, kwa haya maelezo inaelekea unalijua hili jambo vizuri sana kiasi cha kuwafahamu wahusika na unakiri kwamba kwa sasa wamehamia CCM, mbaya zaidi hazikuchukiliwa hatua zozote.

Hauoni kwamba unazidi kuleta shaka juu ya aidha uwezo wako wa kufikiri au kuna vitu unaficha kwa makusudi.
 
Huna TAARIFA SAHIHI, HATA SASA NIKO NA TIMU MWANZA. KILA SIKU NATOA 1M KWA AJILI YA TIMU
Kila siku au kila wakati timu inacheza, Mhe tuweke sawa hapo na kama utaambatanisha na ushahidi itapendeza maana timu inalia njaa...
 
Kwaiyo ndo unaicha singida ishuke daraja?

Ushawahi kuwaza kuja kuwa mwenyekiti wa utopolo sport club (yanga)
 
Back
Top Bottom