Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

Na Mwamba wa Kaskazini

Nimefuatilia akaunti za wasiotaka maendeleo ya Tanzania wote na kundi lao linaloumia kuona maendeleo yanayopigwa.

Wote hawa wamekuwa wakiushangilia wimbo mpya wa Msanii Roma ambaye kaimbaimba vitu vingi ambavyo hata yeye binafsi naamini ukimuuliza vingi hawezi kukwambia kwa nini kaimba. Hoja za kushikiwa.

Na waliopenyezewa fedha za ufadhili ndio walikuwa wa kwanza kuibuka kujifanya kama ndiyo wameuona kumbe wanaujua na walikuwa hata studio kuratibu mashairi. Ujinga sana huu.

Roma anaonekana kuingia katika propaganda iliyofeli-analalamikia demokrasia katika nchi ambayo hivi sasa yeye mwenyewe anazunguka nchi nzima kwa amani katika Tamasha la Fiesta akiwa na amani na kufanya muziki wake pamoja na kutukana sana viongozi majukwaani. Anataka nini zaidi?

Ni Msanii anayeimbishwa kasumba na propaganda asizozijua akiagizwa, kwa kujua au bila kujua, alilie demokrasia na uhuru wa kujieleza katika nchi ambayo yeye mwenyewe hivi karibuni kazunguka redio zaidi ya 20 kwenda kuutangaza wimbo wake alioimba na Stamina "Kijiwe Nongwa." Kote kaongea ya uongo na kweli na sasa anaendelea na bata la Fiesta. Ghafla mtu huyo huyo ataibuka kukwambia hakuna uhuru wa kujieleza!!

Namuona Roma aliyeshikiwa akili kabisa eti analilia demokrasia katika nchi ambayo hata yeye ameruhusiwa kuwa na akaunti ya Insta anaweka nyimbo zenye matusi lukuki kwa viongozi. Naona bado anaweweseka na walimteka. Asitumie hii kisiasa, aseme nani walimteka.

Haya ndiyo madhara ya vijana wanaojiona wasomi lakini wasiojielewa- wanajiita wanafalsafa kumbe ni mazuzu tu yanayotumika. Hajui siku wanaomtumia hapa yeye ni kwao, siku pakiwaka, wale watarudi kwao yeye atakwenda ukimbizini!

Unamsanii Roma anayelilia demokrasia kutoka upande mmoja, halili kubanwa demokrasia ndani ya CHADEMA ambako kuna kiongozi kawa Mfalme wa Wafalme, kuna wabunge wa upinzani wanaoburuzwa na kuchukiwa hata wanaposhukuru tu kwa majimbo yao kupata maji.

Shida yake kubwa anaumia kuona Serikali imefufua shirika la ndege sasa watanzania wanasafiri kwa bei nzuri na uhakika.

Roma na wanaomtuma wanaumia kuona tunaongeza mapato, tunazidi kuelekea kujitegemea, tunatoa elimu bure, vituo vya afya vimejengwa, hospitali za wilaya na mikoa zimemalizika na anaumia zaidi kuona ujenzi wa reli ya kisasa na mradi wa umeme Rufiji vyote kwa fedha za ndani.

Roma hana raha kuona mabarabara, flyovers, kuona walimu zaidi ya laki 1.24 wamepandishwa madaraja mwaka huu, shule zinaboreshwa. Hataki na inamuuma.

Roma anaona demokrasia ni watu kuachwa wafanye ghasia- waandamane bila mpango, wapore vitu vya watu, wazuie watu kufanyakazi n.k.

Ni ajabu sana kwamba Roma haoni chochote katika nchi yake-haoni, haoni, haoni. Ila si bure, macho anayo vizuri.

Siku mtakayojua nguvu inayowapotosha hawa vijana mtashangaa na mtabaki mnasaga meno. Lakini wajue Tanzania ni imara sana kuliko wanavyodhani.

Pole yako Roma, endelea kuimbishwa tu. Kitaeleweka.
 
Juzi Lipumba alikua sawa kusema ukishakua kule hata akili zinakua na mushkeli..
 
Kama umesikiliza na kuona kuwa Roma anaigusa serikali bila ya kugusa vyama, basi hiyo ni nafasi ya wewe kwenda kuvigusa hivyo vyama.

Yaani umekarisha mata.ko chini ukisubiri Roma akufanyie kila kitu?
Na naona unajaribu kujitahidi kubisha kuwa hakutekwa, zaidi unaonekana kuumizwa sana na kazi zake.
 
Actually madaraja, flyovers, umeme na mradi wa Rufiji siyo kielelezo cha demokrasia.

Uchaguzi peke yake nao siyo demokrasia. Kipindi cha Hitler unadhani hakukua na wasanii wanaozunguka kufanya show?

Surprisingly unachokishangaa kua ni kuandamana, fujo, ghasia na kutukana hiyo sasa ndiyo demokrasia.
 
maramla,
Katika jamii ya watu wenye utashi huwezi kutegemea wote wawe na mawazo sawa ikitokea hivyo ujue hao siyo watu ni robot ambao wako programmed

Kwa hiyo usione maajabu mtu kuwa na mawazo kinzani maana hata wewe ulichokiandika hapa kuna wengine wanaona na wewe umeshikwa akili na unatumika. Wewe unaona kila kitu kipo sawa kuna wengine wanaona kinyume chake

Kwa hiyo usimuone Roma msaliti ila amejaribu kuonyesha mapungufu ambayo wewe huwezi kuona kwa kuwa unaona kila kitu kipo sawa. Huenda hata alivyotekwa wewe hukujali uliona sawa na hiyo ndiyo demokrasia
 
Kwa hiyo Nandy, Diamond na Harmonize ni wazalendo kwa kusifu na kuabudu? tunatofautiana interest na liheshimiwe hili,hajatukana wala kukashfu mtu kosa lake lipo wapi?? mlitaka na yeye asifie?? Niliyokuwa nikiyaona kwenye Drama za Kifalme za kikorea leo hii nayaona wazii[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sinajua una miaka mingapi lakini Duh! Inasikitisha mimi na wewe wote kuwa Watu wa Taifa moja.Naona Mungu kakupendelea sana kuwa Mtanzania lakin wewe unaonekana ni uzao wa majini( moto).Hauna utu wowote unajifanza mzalendo wakati unaushetani tu.Umejaa chuki dada/kaka.Hizo nyimbo zitakusaidia nini kama zote zikifungiwa au zote zikiwa zinasifu?maisha yenyewe mafupi uchawi wa nini?Ndugu achana na uchawi utakuwa huru.
Mdada roho mbaya kama ya paka wewe.Acha hizo
 
Wewe ni mmojwapo wa wale mchelemchele ndugu Masaburi alisema Kmnawaza kwa kutumia maeneo ya uani! Kwanini mtu yeyote mwenye mawazo huru mnadhani yupo against maendeleo ya CCM? Kwanza yapi? Haya ya kupeleka watu mbugila mbugila simply kwa kumfurahisha mfalme? Bandiko lako na lidumu ipo siku mjukuu wako atakuona hazimo
 
Back
Top Bottom