Ananiambia nijipange kwao Mahari huwa ni kubwa. Nimempa assignment

Ananiambia nijipange kwao Mahari huwa ni kubwa. Nimempa assignment

Kwa hiyo anajiuza?
Halafu hizi habari za mahali ni ushenzi tu. Wote waaliokua wanamfukunyua hawakuwahi kulipa mahali, halafu mtu anayekuja kwa good will ndiye analipishwa mahali, kwamba mahali ni adhabu kwa muoaji.
Wanapokua na mabint zao wanashindwa kuwasimamia katika maadili ili wajiheshimu, akitokea muoaji wanakua viimbelembele, wa kutaja mahali utadhani bint yao alijitunza.
Unakuta hadi wazazi wa single maza eti nao wanadai mahali.

Jamii inatakiwa ku review huu utaratibu, haupo sawa kabisa.
Acha ujinga , unataka kujilinganisha na mwanamke ?? Unapotengeneza himaya lazima kila kitu kiwe chini yako , ndo mana mnazalishiwa wake zenu na wanaume wengine , mana mwanamke anakuona mdebwedo na unakwepa majukumu , ..akikutana na jamaa huko linamhudumia mpak wazazi wake , lazima ulee watoto ambao sio wako..uanaume unapambaniwa jombaa
 
Acha ujinga , unataka kujilinganisha na mwanamke ?? Unapotengeneza himaya lazima kila kitu kiwe chini yako , ndo mana mnazalishiwa wake zenu na wanaume wengine , mana mwanamke anakuona mdebwedo na unakwepa majukumu , ..akikutana na jamaa huko linamhudumia mpak wazazi wake , lazima ulee watoto ambao sio wako..uanaume unapambaniwa jombaa
Hata maana ya mahali unaonekana haujui. Kwa hiyo mahali yako unaenda kumuweka nani chini ya himaya yako? Au mnajipiga vifua na kujiona vidume kwa masimulizibya kale ambayo mazingira ya sasa wala haya support mfumo ule?
Kingine usudhani kuzalishiwa mke wako ni uzembe wako, hiyo mara nyingi ni umalaya wa mwanamke mwenyewe na tabia zake za hovyo ulizozitolea mahali
 
Ungejua nafasi yako kama mwanaume unayetegemea kuanzisha familia itakayokutegema kama mkuu wa kaya kuna vitu ungevitazama kwa jicho la tofauti sana.

Yaani umemchambua binti watu kiasi hicho!? Hapo kisa sio mahari tuu! Hayo maneno yameonyesha ulivyo na roho chungu na mbinafsi.

Kama hakufai si umwache? Au ukiambiwa umwoe bila mahari ndio unamwona mwanamke bora??

Tafuta wakubwa wakueleze maana ya mahari watakuambia Mahari ni kipimo cha kujua kama mwanaume yuko tayari kubeba jukumu la ndoa na familia.

Halafu ukiwa mwanaume ukapangiwa mahari kitendo cha kuikubali tuu ni alama tosha kwamba wewe ni mwanaume mwenye kujielewa, mpambanaji na mpiganaji. Mahari unaweza kulipa yote mahari unaweza lipa kwa awamu.

Halafu, Kama mahari imekushinda utaweza kulea mke na watoto?
usitufokeee waoaji ni sisi watoa mahali ni sisi tushasema hatutoi mahari kubwa bora nikanunue IST itanifariji kuliko kununua redio ndani kila wakat mikelele tuuh
 
Lipa mahari uchukue mke
Hiyo unayotaka wewe itakuja kukutesa
Kama hujalipa mahari kimira na desturi watoto ni Mali ya kikeni na huna sauti.
Je, utakubali?
Huu ni ujinga mkuu ukisema hivi ntauliza swali moja..... kama huna sauti inamaana 'usihusishwe' na malezi ya hao watoto
 
Huyu binti inawezekana kabisa nikaachana naye so soon kama hatokuja na majibu sahihi.

Tume date muda kiasi na nlimwambia misimamo yangu toka mwanzo. Anafanya kazi nami nafanya kazi. Hakuna issue ya kupeana pesa. We share. Mimi sihongi hata siku moja. Tunapendana, basi tunakubaliana kupeana mapenzi. Siuzi, Sinunui.

Sasa kwenye mahari ndio ananiambia baba yake alimuoza dada yake kwa Tsh. Mil 4.5 yeye alisema bila mil 6 hamwachii. Nikamwambia itakuwa baba yake alikuwa anatania, mzazi mwenye akili timamu hawezi hata waza hilo neno. Akakasirika kuwa namwambia baba yake hana akili timamu.

Ilileta shida. Mimi nilisisitiza kuwa, baba yake hawezi dai mahari hiyo sababu nahisi atakuwa mzee mwenye akili. Wapumbavu ndio huwa wana hizo tabia. Akakomaa sana kuwa huo ndio ukweli na baba yake ana akili sana tu.

Muda ukaenda imefika seriously kwenda jitambulisha. Now in a serious tone anasema niandae kama Mil. 6, hivi ili hata akishusha basi iwe 5.4

Nlimuuliza hiyo Mil 5 nalipia nini kwake? Je, nimemkuta bikra? Akainamisha kichwa chini. Je, mashine yake ina regulate joto au ni adjustable? Yaani ana nini ambacho ni special kwangu. Akaanza ugomvi nimemdharau, sababu nimeshakaa naye sana kuna ambao wanamuona dhahabu.

Basi nikamwambia it's ok, akaolewe na hao wanaomuona dhahabu. Akanichunia siku 3, nikapanga nguo zake akija azichukue, aondoke. Siku hiyo kaja amefura sana. Nikajua kaja kubeba mizigo yake. Wala. Anataka tuzungumze nilimwambia mimi kiukweli siendi kutoa mahari kwao. Sioni sababu. Kama yupo tayari kuwa nami nitaenda jitambulisha na zawadi nitabeba ila mahari siendi toa. Kama hakubaliani na hilo abebe mizigo yake tu aende.

Sitoi mahari, hilo nimekataa. Mtu nimemkuta ameshachakatwa sana tu. Namtolea mahari iweje? Halafu acha hilo jambo, yaani why nikalipe pesa kwao? Wanawake ambao wapo tayari niwalete home tuishi wengi tu? Yeye ana nini maalum? Nampenda ni kweli, ila siendi mimi mlipia pesa ili kuendelea kulana naye.

Nitatoa zawadi kwa wazazi na ndugu zake. Zawadi si lazima na haina kiwango. But mahari No. Si yeye tu hata mwingine akija. Akitaka tukubaliane kuishi hataki akatafute mwingine.
KAMA UNAONA HUWEZI SI UTAFUTE MASIKINI MWENZAKO

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Hajamtukana baba mkwe,
sijaona sehemu amemtukana baba mkwe.

Ameongea ukweli..Wewe unafikiri kudai M6 kama mahari ili kumuoza binti ni wazo linaloweza kutoka kwenye kichwa cha mzazi mwenye akili timamu???

Mtoa mada yupo sahihi tu sijaona kosa lake hapo.

Juzi kijana mmoja wa kisukuma hapa singida vijijini ameniambia ameoa mke kwa kutoa ng'ombe 25 wakubwa siyo ndama. Na makabila mengi bado mahari iko kwa mtindo huo.
Hivi ukiwauza hao ngombe 25 hawafiki hiyo 6mil au kosa ni kutamka hiyo 6mil cash?
 
Kila kitu katika maisha ni mapambano,

You need to negotiate (sometimes with yourself) and make appropriate decisions, even crossing a road needs good decision making otherwise tutakupoteza
Bro,hakuna tofauti na human trafficking km unanegotiate afu kuna binadamu katikati ya hayo marumbano ya bei ili aweze kuhama kwao
 
Juzi kijana mmoja wa kisukuma hapa singida vijijini ameniambia ameoa mke kwa kutoa ng'ombe 25 wakubwa siyo ndama. Na makabila mengi bado mahari iko kwa mtindo huo.
Hivi ukiwauza hao ngombe 25 hawafiki hiyo 6mil au kosa ni kutamka hiyo 6mil cash?
Iwe ng'ombe au iwe cash...kosa ni kwann mwanamke auzwe?
Mimi hata nkiwa bakhresa sitoi hata 100 ya mahari
 
Kwa hiyo anajiuza?
Halafu hizi habari za mahali ni ushenzi tu. Wote waaliokua wanamfukunyua hawakuwahi kulipa mahali, halafu mtu anayekuja kwa good will ndiye analipishwa mahali, kwamba mahali ni adhabu kwa muoaji.
Wanapokua na mabint zao wanashindwa kuwasimamia katika maadili ili wajiheshimu, akitokea muoaji wanakua viimbelembele, wa kutaja mahali utadhani bint yao alijitunza.
Unakuta hadi wazazi wa single maza eti nao wanadai mahali.

Jamii inatakiwa ku review huu utaratibu, haupo sawa kabisa.
Hivi kwamfano ukimkuta binti kashazalishwa ni single maza....na penyewe huwa wanaomba mahari?
 
Humu ndani kumejaa vijana waliofundishwa na mitandao ya kijamii! Hujui maana ya mahari nyamaza! Hiyo hela unayotoa kwa familia ya binti unayetaka kumuoa ina jina maalumu inaitwa "mahari". Ukilipa mahali unafungulia lidhaa ya wazazi wa binti kumuachilia binti yao kwa baraka zote na muwe na uhakika mtabarikiwa katika ndoa yenu na uzao wenu. Naweza kulinganabisha "mahari" na "sadaka" unayotoa kwa Mungu wako! Kama hujui maana ya sadaka (japo nayo ni hela) huwezi kujua maana ya "mahari". Tafuta kuwa na amani na familia ya binti wakukabidhi binti yao kiroho safi! Tumia busara hata kwa kulipa kidogo kidogo kuliko kushupaa! Ndo nyingi mnazoingia vijana mnaanza kwa laana ndo maana mnashindwa kuishi na wenza wenu! Povu ruksa!
Okay tuseme mahari ni sadaka.
Kama mungu wa mbingu na nchi hakupangii sadaka hata shingi 50 anapokea, kwanini mahari(sadaka) tupangiane?
 
Back
Top Bottom