Anapost wanaume walionunua magari na chattings zao status wakati mimi niko kwenye hali ngumu kiuchumi


Sasa umeshajua kama jamaa ndio anaishi kwa mwanamke au umejua anaelipa kodi ya pango na matumizi ya nyumbani ni nani anatoa?

Jamaa angekuwa anasimamia nafasi yake haya yasingetokea.. Na hapa inaelekea hali hiyo imesha mtafuna na kumdhoofisha.. Hamtoshelezi mwenzie kimwili wala kiuchumi lazima dharau za reja reja kama hizo ziibuke.

Hapo jamaa ndio ajiachie tu.. Aende chimbo kujitafuta.. Akiforce kukaza kumprove wrong huyo mwanamke atazidi kujimaliza kwa depression ambayo inaweza kusababisha mental issues.. Na maafa.
 
.........Hao wanawake huwa mnawaokata wapi?
Hata mi nashangaa pia sio wanawake tu hata wanaume wanaonunua magari na kudharau wengine na kuona gari ni kitu cha maana sana au wanaume wanaoona kuwa mwanaume mwenzake akimiliki gari kama ana maisha mazuri. Mimi nina magari 2 (langu na la wife) ila sijawahi ona uthamani wake hadi ninyanyase au nidharau wengine kwa namna yoyote. Napakiza yoyote mtoto au mkubwa. Mgonjwa au mzima. Kukiwa na ugonjwa au msiba huku Kijijini ninapoishi huwa Natoa gari 1 hususani ninalolitumia mimi kwa ajili ya shughuli za kijamii.

Pole na Mungu akusaidie bro. Usijihukumu wala kujisikia vibaya. Gari sio kitu mkuu. Pambana kaka.
 
Shetani anapiga patrol hapo anataka achukue point 3 Mungu kashampa go ahead nenda kwa mtumishi wangu Ayubu mjaribu unavyoweza Ila tu usimuue, sasa kaanza kucheza na akili yako Mzee ukiileta mihemko utaharibu ndoa kwan shillings ngapi shemu haumgongi au napo pia anakubania?
 
Pesa na magari ni vitu vya kupatikana lkn je tunavipataje tuanzie hapo
 
Naona siku za hivi karibuni nyuzi za Wanaume kulalamika kuhusu ndoa zao zimekuwa nyingi sana, why??? Au ni mbinu maalumu ya kufanya kampeni ya "kataa ndoa" huku ajenda zikiletwa hapa jukwaani kwa kupitia mlango wa nyuma?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…