Kipindi hiki cha awamu ya tano kimepata misukosuko mingi sana hasa kwa watetezi wa rais, Mhe rais anafanya makosa ambayo hualazimu vijana hasa wengi wakiwa wa chama chake kujitoa akili ili tu waweze kumtetea, imefika maana wanaonekana kama watu wasio na akili nzuri kwa vitendo vyao vya kumtetea rais.
Rais ametukana Kagera watetezi wake wakamtetea, mara hakuna njaa wakamtetea, ni juzi tu amevunja katiba ya nchi watetezi wake wakatetea kitendo kwa kusema rais yupo sawa, leo ameteua mbunge kuwa balozi ili zile nafasi 5 za kikatiba ziwepo watetezi wake humu mitandao na huko vijiweni wametetea kitendo hicho.
Kwani Mhe rais ameamua kucheza na akili za watu hawa kwanini anawadhalilisha watu tena wengine wakiwa wasomi, Mhe rais anachofanya ni udhalilishaji.