Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Bado muda wa kuhoji mwelekeo mzima wa taifa mbona huku wabunge tumewapa muda cha kwanza nidhamu ndani ya kazi.
 
Ukiangalia hapa jukwaani wewe ni mmoja wa waanzisha post nyingi ikiwemo na kuchangia post. Ila kwa sehemu kubwa ya michango yako unachangia kipuuzi, kishabiki na kejeli. Sioni shida kwani ndio demokrasia, tatizo langu ni kwamba wewe umewekwa na chama chako kukitetea hapa mitandaoni. Nilitaraji kwenye sehemu kama hizi ndio ungekuwa unamwaga nondo na kutolea ufafanuzi mambo mengi ikiwemo na upotoshaji wowote. Unaposhauri watu wakasome ilani na ahadi kuna tofauti gani na kile unachoponda kila mara kwamba EL aliwaambia wananchi wakasome ilani ya ukawa kwenye mitandao!!?

Ni kwanini unakimbilia kwenye kejeli na upuuzi, kirahisi ni kwamba mengi ya hayo yaliyoahidiwa yameahidiwa tu kwa mazoea kwani huwezi kuingia kwenye kampeni bila ahadi wala ilani. Nchi hii haijawahi kuwa na tatizo kwenye upande wa maandishi wala mipango, ila tatizo la nchi liko kwenye utekelezaji, hivyo hapa ndio ulipaswa kuchanganua kwamba tunafikaje huko kwani katika budget inayoendelea kusomwa haiakisi hilo. Sasa watu wanataka ufafanuzi isije ikawa ni kauli mbiu kama nyingine zilizowahi kutolewa na mpaka leo hata wale waliozitoa wanashangaa watu wameendeleaje kuwa wavumilivu kwa kile kilichotokea.

Tatizo na wewe hutaki kuona wala kuelewa. Kwani kushughulika na watumishi hewa ni nini? Ama kupunguza matumizi yasiyo na tija (mfano; safari, posho, matamasha, n.k..) wewe unaona ni kitu gani kwani?
Msilete hoja/mada za kishabiki humu halafu mkijibiwa kishabiki muone wanaowajibu kuwa ni punguani.
Maendeleo gani unayotaka kuyafikia bila kuchukua hatua za udhibiti, kurekebisha maadili na uwajibikaji?
Wewe mwenyewe ukiulizwa dira yako ni ipi, hata majibu huna halafu unataka serikali ije na dira?!!! Toa boriti jichoni mwako ndipo uone kibanzi kwa mwenzako.
Nakushauri ongeza juhudi kufanya kazi, lipa kodi shauri na familia yako yote ifanye hayo, jirani zako, ukoo wako nao pia kisha rudi hapa kuuliza tena hayo maswali yako.
 
Siasa za vyama tumeacha 2015 Wewe mpu..mbavu. hapa tunajadili mwelekeo wa taifa letu. Hayo mawazo yako ya mgando peleka chumbani kwako
We mbona hujadili mwelekeo wa chadema? Mna Sera ipi kwa sasa, je ya sukari, au kupambana na ufisadi au ipi hasa??
 
Binafsi uchumi naona unakuwa kwa asilimia 7.1 na tuna wazidi hata wa kenya hivyo basi tukianza kufanya export kwa wingi na import kwa uchache itapelekea hata thamani ya hela kupanda, japo hata sasa ivi hela imepanda, inflation imepungua mpaka asilimia 5.3 mm naona tunaelekea kuzuri, .. kwa sera ya hapa kazi tu.
CCM wanapenda sana watu wanaofikiri kama wewe Hongera
 
We ndio hujui unakokwenda sisi tunaona anatupeleka pazuri sana asante mzee magufuri mafisadi wanaanza kulia hawaelewi pa kushika
 
Mbona Enzi za jakaya mlikuwa hamuongei mlikuwa mnajua mnakoenda kwan... Achen unafiki muachen rais afanye yake
 
Hivi Dr. Bana huwa sio member hapa?
Maana wakati wa mzee Mkapa alijitahidi kwenda naye sawa na alivyokuja JK na 'sera' zikabadilika naye wakabadilika naye. Sijamsikia akitoa mwelekeo wa redet siku za karibuni wala kutoa comments za awamu ya tano!
 
Anatupeleka kwenye nchi ya asali na maziwa "bila sukari"
[emoji87][emoji87][emoji87][emoji87][emoji87]
 
Swali ni lamsingi kwelikweli mdau anataka kufahamu cha ajabu Sasa wachangiaji mnaleta ushabiki na kutupiana vijembe. Hakuna anayepinga kwamba raisi hana nia njema ishu ni kwamba strategies (mbinu) za kutimiza hizo nia njema
 
Hatuamki asubuhi tukasema tunaenda kwenye viwanda, lazima tujiulize vilivyokuwepo kwa nini vilikufa. Tuna mioundombinu ya uhakika? tuna umeme? tuna malighafi? Leo tunalizwa na sukari, tumejiuliza kwa nini hatuwezi kuzalisha sukari ya kutosheleza mahitaji?

Sasa madawati yanapoongezwa ili watu wapate elimu we huoni kwamba hiyo ndiyo njia mojawapo ya kutoamka asbh na kwenda kwenye viwanda? Lakini unafikiri uwekezaji wote huo unafanyika kwa gharama zipi? Kama una Taifa la watu mafisadi, wavivu, wakwepa kodi, wazembe, utawezaje kamilisha mambo yote hayo??
Tusing'ang'anie kwenda mbele wakati hatusafishi na kurekebisha mambo ya msingi kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Hicho ni kichekesho!
 
Chief Bahati mbaya sana chadema siyo reference point yangu.Chadema ni reference point ya ccm,wanaccm na watu wenye brain nyingi kama wewe.ila kwangu Mimi mtu mzima kujilinganisha na mtoto naona kama ni aibu kubwa vile
hakuna wanaoamini viongozi wa ccm kama ukawa hasa chadema kwani kwa mabaya yote waliyokuwa wakizungumzia ccm sikutegemea kama wanaweza kuwapokea waliowahi kuwa viongozi wa ccm tena walioshika nyazifa za juu kama lowassa na sumaye ambao siku zote walituaminisha sio wasafi
 
Hatujui kwamba ataanza kuboresha kwanza umeme ndo afwate viwanda..

Au aanze viwanda kwanza ndo afwate umeme...
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] hii ndo Bongoland
juzi waziri mkuu wake kasema kuna makampuni 52 yanakuja kuwekeza kwrnye Umeme, jpm anasema serikali haitaki tena makampuni yatuuzie Umeme, hawajipanda hawa
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida. Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.
Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa? Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi. Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
Ni aibu sana mtu kutoa swali kama hili la msingi na likajibiwa na baadhi ya watu kimzaha au kutoa vijibu vya kipuuz au visivyo na mashiko,hoja hujibiwa kwa hoja,kama huna hoja kaa pemben,swali lako ni la muhimu kwa mtu anayeitakia nchi hii mema,na siyo kupelekwa pelekwa kama Kondoo.Hoja yako haina tofauti na hoja niliyomuambia rafiki yangu mmoja kuwa "NCHI YETU INA TAKRIBANI MIAKA 55 HAINA DIRA YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZEKA",akabisha akasema Dira ipo,nikamuambia Dira ipo kwenye MAKABRASHA TU.
 
juzi waziri mkuu wake kasema kuna makampuni 52 yanakuja kuwekeza kwrnye Umeme, jpm anasema serikali haitaki tena makampuni yatuuzie Umeme, hawajipanda hawa
Wanasafiri vyombo tofauti
 
Hivi ni sehemu gani, jf, au mitandao mingine naweza pata hoja na mada zinazojibiwa Wa hoja. Maana inaonekana kama huwa kuna watu wanatumwa kujaribu kila mjadala sijuini kwa faida ya nani.

Nitarudi bdae
Mkuu mi naamin hoja hujibiwa kwa hoja,inashangaza mtu anapojibu kama yupo FB,hii ni hatari sana
 
Tafsiri ya hiyo ndugu Tindo ni moja tu, mada hii imewaudhi wana CCM kwa kuhoji utendaji na uelekeo wa serikali hii ya CCM!!

Afadhali hata Jakaya Kikwete alipoingia mwanzoni mwa utawala wake, ingalau alikuwa na utaratibu wa kuwa anazungumza na taifa kila mwisho wa mwezi kuelezea uelekeo wa sera zake za kiuchumi pamoja na kutoa ufafanuzi wa some burning issues za wakati husika. Kwa mfano ikitokea watu watu wanajiuliza swali km hili la mleta mada kwamba hivi tunaelekea wapi, alijitokeza na kutoa msimamo na kuwaweka watu ktk mstari hata kama ni kwa kuzuga tu!!

However, utamaduni huu nao ulijifia automatic, kwani pamoja na hayo ukosoaji kwa kila alichokuja nacho ulimfuata nyuma yake!

Huyu yeye hata hayuko huko bali ni purely anaenda enda tu, yupo yupo tu kwa ku create matukio yatakayompa publicity. Ukiona kakaa kimya kwa muda flani watu wanaanza kutojua uwepo wake, basi ujue atatafutiwa tukio na mahali ambapo ataibukia huku akiwa ameambatana na camera za TV ili watu waseme,
".....lol....aisee lima - Magufuli bwana, leo kidogo awatumbue ........".

Yes, hivi ndivyo tunavyopelekwa na tunavyokwenda kama taifa

Mimi na wengine nadhani tunatarajia Rais pamoja na kurejesha nidhamu ktk utumishi wa umma, kusimamia makusanyo ya kodi nk tulitarajia sasa aje na mikakati mahususi ya kuijengea misingi imara kwa kuhakikisha kunakuwa na sheria madhubuti zitakazosimamia na kuyaimarisha haya anayoyaanzisha.

Lakini binafsi sioni chochote kwani anapita mule mule walikopita watangulizi wake, na maana yake iliyo dhahiri ni moja tu, ni kuwa hata yeye atachoka na atashindwa tu na atatahamaki 2020 imebisha hodi mlangoni kwake!!

Well and good. Tunaambiwa kuna ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015 - 2020 na kwa hiyo tuisome hiyo na ndiyo uelekeo wa Magufuli. Swali kwa hawa wanaosema haya.

Kwani kuna awamu CCM haijawahi kuwa na ilani? Zilileta tofauti gani eti? Mbona ndizo hizo hizo ilani tofauti tofauti za CCM zimekuwa msingi wa malalamiko na majipu haya haya yanayotumbuliwa leo?....This is purely confusion!!
Mkuu umenena
 
Pole!endelea kulala ukiamka utakuta uchaguzi wa 2020 umekwisha.
 
Mkuu mi naamin hoja hujibiwa kwa hoja,inashangaza mtu anapojibu kama yupo FB,hii ni hatari sana
Mkuu kauliza nani anayejua Magufuli anatupeleka wapi,kwa hiyo tegemea majibu kama hayo kwa sababu kuna watu wanajua anakotupeleka na wengine hawajui.
 
Hivi wewe mtu anaomba kura kwa wananchi kwa mtindo wa kubinuka binuka ulitegemea angeweza kuwa na dira ya kuongoza nchi basi unandoto za alinacha
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom