Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Tatizo ni ushamba wako tu! Taifa liko pazuri na linaenda vizuri!

Hakuna nchi duniani inayoendelea kwa maendeleo ya kweli bila kodi! Kama hutaki kulipa kodi Tanzania nenda Marekani Au Uingereza Au China alafu rudi hapa useme hali ya kikodi huko ikoje!

Chuki zenu dhidi ya Samia mbaki nazo nyie wenyewe huko sio kutuletea maneno hapa nchi imepoteza muelekeo wakati mapato yanakusanywa vizuri, miradi inaendelea vizuri na kikubwa zaidi sasa tumeanza kufanya vizuri zaidi kiuchumi kuliko ilivyokuwa hapo awali!

Nenda kafuatilie ripoti ya Bank kuu za Uganda na Kenya uone kwa jinsi gani Tanzania sasa inauza zaidi mazao kwenye hizo nchi kuliko wao wanavyouza kwetu
 
πŸ˜πŸ‘‹
 
Tuzidishe dua tufike salama
 
Usitupigie kelele ,wenda tunayoyaona ni kutokana na MAUMIVU ya mwendazake ,yule mzee alikua mwongo Sana akisaidiwa na timu mapambio ,KAZI ikiwa kufilisi WATU pesa zao pitia KESI za kuhujum uchumi
 
Watanzania wazembe na wapumbavu ni wengi sana. Hivi unatumia kipimo gani kusema Rais SSH hamna kitu?

Yule aliyepita alikuwa hata uhuru wa maoni kwa wananchi amekataza, huyu amewapa uhuru ndiyo huo mnautumia kumkejeli?

Yule alikuwa ana kikundi cha WASIOJULIKANA chini ya Makonda kinateka na kuua, bado hujaridhika na utawala wa Mama ambao una uhakika kutembea au kuishi popote bila kuuawa?

Yule alikuwa anapokonya fedha za matajiri kwenye akaunti na kuwatupa jela, huyu anataka Kodi sahihi na ya haki.

Yule alikuwa anachukua Kodi za Watanzania na kujenga miundombinu Kijijini kwao, huyu anajenga miundombinu panapostahili

Watanzania hamna shukrani
 
Walioiletea MAHANGAIKO na SHIDA hizi TANZANIA ni wale wale hivyo Usitarajie MATATIZO ya Watanzania Yatatatuliwa Nao
Huwezi kutatua MATATIZO na Walioyatengeneza

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…