Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

wana CCM wameanza minong'ono kwamba hii 4 aliyoiacha mwendazake kuimalizia inamtosha !!
 
"Hakuna mtu hapo yaani bora liende tu"

Hivi karibuni nikiwa kwenye msiba wa mzazi wa Waziri jina kapuni kwa masikio yangu nilimsikia mmoja wa mawaziri akimponda waziwazi mama yenu akitoa hiyo kauli ya hapo juu.

Kumpuuza kwakwe yule mama ilhali ni Waziri ilinistaajabisha mno na sikuitarajia kauli kama ile kutoka kwa mtu wa nafasi kama yake.

Ukweli ni kwamba kumbe hata wasaidizi wake wanamchora na kumpuuza.

Sijasimuliwa bali ni kwa masikio yangu.
 
Wakati wa Jiwe wote walikua wachumba tu. Unajua hata beki tatu huwa wanadharau sana sehemu au bosi anayewaheshimu na kuwapatia heshima na hadhi kama binadamu.

Baada ya muda kidogo huchoshwa na amani na utulivu kisha wanakimbilia kule wanakonyanyaswa kwa kusimangwa hadi kwenye msosi
 
Ni maoni yake na pengjne nyuma ya pazia kuna mianya kabaniwa.. Hawa wanasiasa hasa wa kiafrika hawaaminiki na ni wa kuogopa kuliko ukoma
Tatizo ni kipenzi chake kabisa na usiyemdhania bora hata angekuwa wale Sukuma gang wenzangu nisingeshangaa lkn huyo ni msoga OG!
 
"Hakuna mtu hapo yaani bora liende tu"

Hivi karibuni nikiwa kwenye msiba wa mzazi wa Waziri jina kapuni kwa masikio yangu nilimsikia mmoja wa mawaziri akimponda waziwazi mama yenu akitoa hiyo kauli ya hapo juu...
Kwani sheria/muongozo wa serikali juu ya uagizaji bidhaa mfano sukari unasemaje?. Na kitu kizito kilichompiga kichwani juu ya sukari huyo waziri unadhani kama ni wewe ungesemaje?

kuendelea kula matapishi yako au kuwa mwamba kama Dr Slaa wa kutokulamba matapishi. Au bora liende watoto wangu waendelee kuingia chooni?
 
"Hakuna mtu hapo yaani bora liende tu"

Hivi karibuni nikiwa kwenye msiba wa mzazi wa Waziri jina kapuni kwa masikio yangu nilimsikia mmoja wa mawaziri akimponda waziwazi mama yenu akitoa hiyo kauli ya hapo juu...
Shida iko wapi Rais kupondwa na Waziri? Watu wanawaponda hata mitume wa Mungu, Yesu Kristu na Mtume Muhammad na bado dini hizi zina wafuasi wengi tu, sembuse ya Rais Samia?

Let us be serious na tunayopost, mengine ni trash tu
 
Hiyo kawaida sana kwa wanasiasa wetu Uchwara wa kibongo bongo bila unafki mambo hayaendi.

Mwingine alimwambia boss wake "Safiri sana ili tupate pesa za kujengea barabara wapinzani waje kuandamana". Alipotwaa Mamlaka akabadili gia hewani akamwambia " wengine wanasafiri kwenda nje kuliko kwenda vijijini kwako" you see now.

Mwingine aliunga mkono wamachinga waachwe wasibughudhiwe wafanye biashara popote hadharani mbele ya Camera, Leo wamachinga wameondolewa sio city centre tu hadi vichochoroni huko mitaani.

Wengine walimsema Lowassa miaka kumi kuwa ni Fisadi papa hadharani wakiutangazia ulimwengu na dunia yote,lakini hao hao ndio wakamfanya mgombea wao wa Urais na kuutangazia Umma kuwa huyu ni MTU safi so usiamini sana kila mwanasiasa anachosema.
Inaweza huyo Waziri alisema hayo kuwa "hamna kitu bora liende" ili kuwafurahisha ninyi Sukuma gang ambao mlimzunguka hapo.
 
Sukuma gang, wanakuja na uchonganishi, wanaupiga mwingi! Wamejaribu kila kitu, mapandikizi yao yanatemwa.😀
Jamani sasa yanajaribu divide & conquer.
Sukuma gang mkachanjwe, Omnicron itaondoka na mtu.

Everyday is Saturday................................😎
 
ulipashwa kumchapa kibao...maana huyo waziri anatumia kodi zako za bure....anafanya nini kwenye nyadhifa ya uwaziri kama hakubaliana na mamlaka iliyompa huo uwaziri....ulipaswa umchape kibao na kumwambia ajiuzuru haraka iwezekanavyo na ikiwezekana ungemuanika hadharani...

Huo ndio Uzalendo unapaswa kuanzia kwako...sio kuleta hizi blah blah halafu kila siku tunalalamika nchi haiendelei..
 
Wafuasi wa Prof Mkenda acheni kutapatapa. Naona sasa mnataka mchonganisha Bashe na Rais. Yani akili yenu ni kuwa Prof atapigwa chini nafasi aichukue Bashe.

Siasa za Tanzania ngumu sana.

Siku nyingine mwambieni Prof aache jeuri na kejeli.
 
Vitu vingine ni kutumia tu akili kidogo, umeshikilia makali ya panga na unamtukana aliyeshikilia mpini, labda uwe na matope kichwani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…