Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

sio uchumi wa tz tu ulioporomoka. nchi nyingi duniani, hata zile zenye uchumi mkubwa kabisa kama vile Uingereza, Ufaransa n.k zibapitia katika kipindi cha mdororo wa uchumi hii in kutokana na athari zilizosababishwa na ugonjwa wa uviko na vita ya urusi na Ukraine. Hapa hauhitaji kuwa profesa kuelewa kuwa, nguvu ya uzalishaji , utoaji huduma , na ununuzi iliathiriwa na vifo Vinci vilivyosababishwa na maradhi ya uviko. Pia Urusi kama mzalishaji Mkuu wa nishati ya gesi na mafuta katika nchi za ulaya ambazo ndizo hasa soko kuu la bidhaa kutoka nchini kwetu , vita yake dhidi ya Ukraine imepelekea nchi hizo kujihami kwa kupunguza uuzaji wa huduma na bidhaa za msingi kwetu na hivyo kupelekea bidhaa hizo kama vile mafuta, utalii, teknolojia kupanda gharama.

SSH Hajadororesha uchumi wa nchi yetu. Uchumi hupanda na kudorora kwa kufuata kanuni zake. Tuache kumbebesha mzigo rais wetu
 
Unataka uongozi Kama wa jpm ambao vyombo vilifungwa visiripoti lolote baya hata Kama yalikuwepo? Mshukuru mungu keamba everything is open and transparent chini ya Samia. Jpm ndo aliharibu Mambo kibao kutokana na ripoti ya cag. Alitufunga kamba kwamba hakopi kumbe anakopa mikopo yenye riba kubwa Sana na akutupiga fix kuwa tumeingia uchumi wa Kati wakati ni fix tu na bahati mbaya vyombo vyote vya habari alikuwa ameviweka mfuko i
 
Mi sipendi DHARAU, kwann Hadi sasa anawakumbatia mwigu na marope??

Kati yangu me mwananchi na ye kiongozi mwakilishi wa wanananchi nani boss!!!
 
Mi sipendi DHARAU, kwann Hadi sasa anawakumbatia mwigu na marope??

Kati yangu me mwananchi na ye kiongozi mwakilishi wa wanananchi nani boss!!!

Kiongozi atabaki kuwa mtumwa kwa wananchi wake. Ameukubali uongozi maana yake amekubali kuwatumikia wananchi.


Huenda mama hana washauri wazuri, kama kuna tatizo upande wa Mui na Mar, mama anapaswa aliangalie na ikiwezekana awape wengine hizo nafasi.


Tunahitaji watu (wenye imani, huruma, waaminifu na wachapakazi)
 
Mnaweza kunambia ni kipi cha maana alichokifanya rais Samia hadi sasa ambacho kimegusa raia wa kawaida au kumsaidia??

Nambieni ni kipi kakifanya ambacho kinaweza kuwa sababu ya yeye kusema amefanya kazi ya kusaidia wananchi wake

Nataka kimoja tu ambacho kakifanya ambacho tunaweza kusema kimemgusa mtu wa chini tokea awe Rais
 
Kama kuna watu 1000 hapa Tz ambao sio wanasiasa wala watumishi wa umma wala wafanyabiashara wanaomkubali rais samia basi nipo tayari kutoa gari yangu

Wanaomkubali Samia kwasasa kati ya watu milioni 60 huku Bara basi hata 1000 hawafiki

Nimetafuta raia wa kawaida anayemuunga mkono huyu bibi hayupo hata 1000 hawafiki nchi nzima

Hakubaliki, hapendwi wala hakuna mwenye hamu ya kumsikia huo ndio ukweli, mtaani ni ngumu sana kumkuta mtu anamkumbali rais Samia ukiachana na watumishi wachache wa umma na wanasiasa, na wafanyabiashara baadhi.

Huo ndio ukweli, mwambieni Rais ukweli kuwa hakubaliki kabisa kwa upande wa Tanzania bara.
 
1. Tozo
2. Mgao wa umeme
3. Kenge road
4. Mabwana na Watwana
5. T..EAA kufika T..EAM ndani ya mwezi
6. Mchele kufika sh 4,000 kwa kilo
7. GSM kumleta Mayele
8. Uturuki
9. Chanjo
10. Uhuru wa reiniboo na elijibitii

Au mwananchi ulikuwa unamaanisha Uto? Mbona hayo yako wazi tu, yametugusa sisi uliotutaja!
 
Lucas mwashambwa unaitwa huku
 
Rais wa kugusa watu wa Chini kwa kupora watu wa juu kwa kulazimisha makosa ya kubambikiana hatotokea tena Tanzania katika miaka ya karibuni

ni bora watu wabaki kuwa maskini kuliko kuwapunguzia umaskini wa kuumiza wengine
 
1. Elimu bure hadi KIDATO CHA SITA

2. UJENZI WA MADARASA

3. KUPANDISHA MADARAJA YA WATUMISHI NA KUONGEZA MISHAHARA YAO.

4. KODI BILA MTUTU WA BUNDUKI NA DHULMA KWA WAFANYABIASHARA.

5. AJIRA SEKTA ZOTE (ELIMU, AFYA, ULINZI NA USALAMA, TAASISI ZOTE NK)

6. BARABARA NYINGI HASA ZINAZOSIMAMIWANA TARURA.

TUNAWEZA KUANDIKA MPAKA KESHO.

NB. CHUKI ZA DINI YAKE USILETE KWENYE MAISHA YA KAWAIDA NA KUTAKA WATU WENGINE WAMCHUKIA. ADUI WAKO SIO ADUI WETU SISI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…