TANZIA Anayesadikiwa kuwa MwanaJF afariki dunia

TANZIA Anayesadikiwa kuwa MwanaJF afariki dunia

Pole kwa wafiwa..

Mi nilikuwa na mazoea hayo ya kulewa na kurudi usiku naruka hizo nondo asubuhi najikuta nimekwaruzika mwili mzima kisa cha kuacha mchezo huo sitasahau.

Nilirudi siku hiyo kilevi kimezidi kuliko kawaida nikapiga simu na kugonga sikufunguliwa nikachukua maamuzi ya kuruka. Niliacha kila kitu juu ya nondo surwali shati hadi boksa. Nikaingia ndani nikalala na viatu tuu. Asubuhi kidogo mama angu afe kwa presha akajua nimeuliwa nikatupwa juu ya nondo kumbe nguo. Akaingia ndani nimelala uchi akanikagua mzima zaidi ya michubuko tuu. Sitasahau
Dah, noma sana 😂😂 sema hili jambo utatuzi wake ni kuwa na funguo yako tu.

Brother angu yeye ana funguo kabisa, tukikutana maeneo anakwambia anakuwa nayo maana kuna siku alilala kwenye gari alishindwa kuruka fensi akaona isiwe tabu..

Wake zetu / wachumba mtuzoee na mtusamehe tu, sio kama tunapenda ila kuna maeneo ikifika w/kend yaani ukiwaza kutokwenda unaumwa kabisa, mwili unakataa

RIP Mwamba, Pumzika Kwa Amani 🙏
 
Wakati mwingine Kuna mambo yanatokea kwaajili ya kuwa Somo ili wengine waweze kujifunza.

Kule kwetu hakuna Mwanamke anakuwa na Sauti kwa Mume wake. Never on Earth, na wao wanajua Hilo.

Yaani kule kabisa Mwanamke amfungie mlango Mume wake, mbona huyo Mwanamke anakuwa anahamu ya kujiuguza kwa kipigo, manake kipigo atakachopigwa sio Cha Nchi hii.

Anyways, huenda ndiyo Kifo alichoandaliwa Member mwenzetu.

Mbele yake, Nyuma yetu.
 
Ushauli wake wa kumiliki funguo, nimeiona sijaubedha Wala sijaupuuza.

Shida inakuja pale ambako mwenza ameamua kumunyosha huyo unae muita mlevi. Mageiti mengi hunguliwa kwa vitasa ukiwa nje.
Alieko ndani akiamua kukomoa anafunga makomeo kwa ndani , au kama Kuna asikali anatia na makufuri kabisa.

Je hapo funguo Yako itasaidia?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haitosaidia kitu, na mpaka mnafanyiana hayo makusudi ni mmechokana au??

Huyo mjane labda hakusikia simu?
 
To yeye ni single mom bado hajapata ndoa🏃🏃
Kumbe bado yupo Single, kwa mchango aliotoa hapa inaonesha Mume atakayempata atainjoi maisha.

Kuna baadhi ya Wanawake wakishajua ameolewa na Mume Mlevi basi atahakikisha anahela za kunywa Kila siku, anamwachia mlango wazi au hata kumfata Bar kwenda kumchukua akiwa amelewa n.k
 
Jaman wale mnaopenda kulewa au kuchelewa kurudi majumbani mwenu kwa sababu za starehe kama hizi muwe mnakuwa na funguo za ziada ili ukirudi unajifungulia mwenyewe kuepusha vifo visivyo vya lazima.

Inachosha sana kuamshwa na mtu aliyetoka kwenye starehe zake ukatishe usingizi wako ili umfungulie
vp akifunga na komeo utaweza kufungua
 
Kumbe bado yupo Single, kwa mchango aliotoa hapa inaonesha Mume atakayempata atainjoi maisha.

Kuna baadhi ya Wanawake wakishajua ameolewa na Mume Mlevi basi atahakikisha anahela za kunywa Kila siku, anamwachia mlango wazi au hata kumfata Bar kwenda kumchukua akiwa amelewa n.k
Nitafanya kila namna akae sawa,kuna sababu ....hawaanzi iviivi mkuu
 
Wakati mwingine Kuna mambo yanatokea kwaajili ya kuwa Somo ili wengine waweze kujifunza.

Kule kwetu hakuna Mwanamke anakuwa na Sauti kwa Mume wake. Never on Earth, na wao wanajua Hilo.

Yaani kule kabisa Mwanamke amfungie mlango Mume wake, mbona huyo Mwanamke anakuwa anahamu ya kujiuguza kwa kipigo, manake kipigo atakachopigwa sio Cha Nchi hii.

Anyways, huenda ndiyo Kifo alichoandaliwa Member mwenzetu.

Mbele yake, Nyuma yetu.
Yeah,tusiwe na mengi ya kuongezea
 
Wakati unakunywa mipombe huku ulimwita mjumuike pamoja wanaume tuache ubabe tembea na funguo zako utadhibiti hayo yote
Kwanza tukubaliane , kifo kipo ila kinatafuta sababu TU

Mwenza mmoja akiamua kumkoa mwenzake, wakati mwingine hajui matokeo yake Nini

Nimeshuhudia vifo vyenye mahusiano na wenza kufungiwa geiti ,× 2. Arusha sehemu inaitwa kwa "Tondi" alifariki mwanafunzi wa chuo Cha uhasibu kwa kuchomwa na mkuki wa geitini.

Hapohapo Arusha Njiro jirani na "kisaka villa"kijana mmoja alikua amehamia kwenye nyumba yake nahuyo mkewe , Tena Mungu kawajalia kipato wamejenga ghorofa . Siku ya tukio, kwamasimlizi ya walio msikiliza mlinzi, na mjane mwenyewe.

Mme alirejea nyumbani mida ya saa 4 , usiku.
Jamaa anafika kapiga honi, mlinzi ,kamueleza kua geiti limefungwa na funguo ziko ndani.
Jamaa kapiga simu na kubembeleza angarau afunguliwe geiti aingize Gali , atalala kwenye gari.
Mke aligoma kupitisha funguo dirishani Ili mlinzi afungue geiti.

Kilicho fuata ,jamaa aliomba ushauli kwa washikaji ,wakamshauli kwenda Masai camp Ili azuge walau kupambazuke bila kuona usiku ummekua mlefu.

Ile anarudi alfajiri kakutana na Hiace kwenye Kona za mlima uitwao Radio, na
Maisha ya kaishia hapo.
Jamaa zake walio simlia walidai kua.walimsihii apumzike kwenye kota za NHC kijenge, akagoma kwamadai anawahi amuone mkewe asije kushindwa kumsamehe.

Visa viko vingi, nimejalibu kusimlia vicache Ili nisiwachoshe.

Wito wangu kwa mashemeji nawake zetu watarajiwa , jitahidi kutokua vya vifo wenzawenu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Memba mwenzetu ametangulia mbele ya haki. Pengine nisingejisumbua kuripoti huu msiba lakini mazingira ya kifo chake ni ya kuhuzunisha na yenye mafunzo. Sijui username yake ya JF kwani tulikutana ''casually'' kwenye kilevi mwezi wa tatu mwaka huu tena siku moja tu. Katika maongezi alinijulisha kuwa yeye ni ''active member'' wa JF na anapenda sana kuchangia. Baada ya kilevi (maeneo ya Boko) tulipokuwa tunaondoka akanionyesha nyumbani kwake na mimi nikaondoka kurudi kwetu Msasani ninakoishi.

Fast forward, wiki kama mbili zilizopita nilirudi tena maeneo tuliyokutana kwenye mishe zangu. Nikaona msiba kwenye boma aliloniambia ni nyumba yake. Kuulizia kulikoni nikaambiwa ni yeye, mwenye nyumba amefariki. ''Eti'' alitoka kwenye kilevi usiku, akagonga geti, mke akagoma katukatu kumfungulia. Akachukua uamuzi wa kuruka ukuta. Kwa bahati mbaya akachomwa na moja ya nondo zilizoko kwenye geti la nyumba (nadhani wengi mnafahamu nondo zinazochongwa kama mkuki na kuwekwa juu ya kuta au geti ili kuzuia vibaka). Kwa bahati mbaya akavuja damu nyingi mpaka akapoteza maisha. RIP member.
Kudaadeki innalilah wainnailaih rajiun. Mimi nadhani huyo mke wa jamaa vyombo vya usalama vile nae sahani moja akisota jela walau miaka 9 kwa kesi ya mauwaji isiyokuwa na ushahidi itakuwa ni funzo kwa wanawake wapumbavu wapumbavu kama huyo ......
 
Jaman wale mnaopenda kulewa au kuchelewa kurudi majumbani mwenu kwa sababu za starehe kama hizi muwe mnakuwa na funguo za ziada ili ukirudi unajifungulia mwenyewe kuepusha vifo visivyo vya lazima.

Inachosha sana kuamshwa na mtu aliyetoka kwenye starehe zake ukatishe usingizi wako ili umfungulie
Hapo ungeshauri wanawake wenzio kuwa waache viburi visivyokuwa na maàna. Sasa aligoma kufungua alitaka akalale wapi wakati hapo ndipo nyumbani kwake!!!!
 
Back
Top Bottom