Anayeshtakiwa kumuua Mkewe adai haogopi Kunyongwa

Anayeshtakiwa kumuua Mkewe adai haogopi Kunyongwa

JAMANI MAPENZI NI KIUMBE KAMA VIUMBE VINGINE...HUZALIWA, HUKUA, HUSTAWI NA HUFA...

MAPENZI YANAPOKUFA YASILAZISHWE...WATENGANISHWE...KILA MTU ACHA ACHAGUE NJIA YAKE...HII KULAZIMISHA SIJUI HAKUNA WA KUTENGANISHA ZAIDI YA MUNGU...MARA OOOH VUMILIA UTAMPENDA MBELE KWA MBELE...HII SIO SAWA...POLISI WANGELIINGILIA HILI WANGEEPUSHA MENGI...WAZAZI NA NDUGU KUJIFANYA HAYAWAHUSU NDIO YANAPELEKEA MAMBO KAMA HAYA...
 
wajina hapo umepuyanga.sababu ya kumsukuma mkeo ndo imesababisha kumuua.ni uongo 100%.sawa tuseme ni bahati mbaya.na kumchoma moto ni bahati mbaya?umeua bila kukusudia ila umemchoma moto MAKUSUDI
 
haya mambo yanatukuta sisi lakini hata wazazi wetu sometimes tunawaambia wavumiliane but bora kukubali watenganeee ndoa ni hatari sana msipofanana
Na wengine hata wakitengana anabaki kumfuatilia hasa wanaume hupenda asiwe na mwingine[emoji3][emoji3][emoji3], Mungu atusaidie jamani kuna mtu unakuta anavumilia mpaka unabakia shingo tu unachungulia kama mtu anayezama kwenye tope.
 
mimi toka mwanzo nilishasema huwezi kumuua mwanamke uliyempenda mwenyewe ukaenda kwao ukamtolea mahari.

ukiona imefikia hapo kuna jambo kubwa nyuma yake.

Mwamba hata wakunyonge sisi bado tunakuelewa sana …
 
Ndiyo hili nilikuwa nalizungumza kwenye post iliyopita. Kwenye ndoa, ligi ya kushindana na kulipizana visasi, eti huyu alikuwa anani-treat hivi basi na mimi nalipiza ni sumu mbaya sana. Mauaji kama hayo kwenye hii kesi hutokana na mambo kama haya.
Na ubaya ni kwamba siku zote asiyetakiwa kulipa visasi ni mwanamke yeye avumilie tu lakini mwanaume yeye ni haki yake kulipa visasi atakavyo
 
Ningekuwa judge kabla ya yote jamaa angekula fimbo tatu safi za kujiingiza ndoani ndipo mengine yafuate.
 
Na ubaya ni kwamba siku zote asiyetakiwa kulipa visasi ni mwanamke yeye avumilie tu lakini mwanaume yeye ni haki yake kulipa visasi atakavyo
Hili unalisema wewe. Ndoa inahitaji pande zote kuvumiliana, ila general rule ni kuwa mwanaume ndiye anatakiwa kuwa kiongozi wa nyumba. Nimeishi nchi zilizoendelea ambazo wanawake wana haki sawa na wanaume lakini hii principle bado ina apply. Tunaposema awe kichwa cha nyumba hatumaanishi awe na kura ya tufuru ya kuamua kila kitu.
 
Pana mtumishi mmoja wa Mungu akiwa mganga zamani alitoa ushuhuda jinsi kwanini wanandoa wanauwana,
Kama wanamuhitaji mmoja wao Huwa wanatuma mapepo mawili moja kwa mme mwingine kwa mke then kinatafutwa chanzo Cha maudhi kupitia kauli mnaanza kujibizana majibizano upambano moto kwa msaada wa Yale majini mawili yatapelekea mtavurugana haswa mtaanza kupigana ugomvi huo ndio upelekea kifo Cha mlengwa either kwa hasira utamshuti risasi,kumchoma kisu,kumbamiza kichwa,kuangukia kwenye meza ya kioo nk then utabeba hospital ndio kwa heri hio then Yale majini mawili yanaondoka ndipo ufahamu wako unarudi unaanza kuhisi hatia maswali kibao kwann nilikosa uvumilivu.
Watu wajifunze sana somo la emotional intelligence yaani jinsi ya kuikabili migogoro ya ndoa.
Inisaidia usiingie jela kisa mapenzi
Yotee ya nn ukiona mambo hayasomeki ni kutimua mbio sio lazima wote tuoe au tuolewe
 
View attachment 2677118

MFANYABIASHARA Khamis Luwonga (38), anayetuhumiwa kumuua mkewe Naomi Marijani na kumchoma moto kwa kutumia magunia mawili ya mkaa, amedai haogopi kunyongwa hadi kufa wala adhabu nyingine yoyote.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo amedai kuwa anataka "anyongwe kwa haki" kwamba aliua bila kukusudia.

Katika kesi hiyo ya mauaji Na. 4 ya mwaka 2019, mshitakiwa Luwonga ambaye ni mkazi wa Kigamboni, Dar es Salaam, anadaiwa kuwa Mei 15, 2019, akiwa Gezaulole, Kigamboni, alimuua Naomi Marijani.

Luwonga alidai hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dares Salaam baada ya kusomewa maelezo ya mashihidi 28 na vielelezo 14 na upande wa mashitaka.

"Kitu ambacho ninakikataa mheshimiwa hakimu, ni kuwa niliua kwa makusudi. Mimi sikuua kwa makusudi. Hata ninyongwe leo hadi kufa kwa kile cha kweli, nitaangamia kimwili lakini siyo kiroho.

"Siogopi kunyongwa wala siogopi adhabu yoyote ile, lakini ninataka kama nikinyongwa, basi ninyongwe kwa haki kwamba niliua bila kukusudia, kwa sababu ni ajali tu ilitokea," alidai Luwonga.

Hapo Hakim Rugemalira akaingilia akisema: "Unaanza kuhubiri sasa, wewe zungumza unachotaka kuzungumza ili nikiandike kwenye rekodi za mahakama."

Luwonga aliendelea kudai kuwa msingi wa kesi hiyo ni maelezo yake, baada ya kuwaambia polisi kwamba yeye ndiye aliyeua na ndiye aliyekuwa anajitumia ujumbe mfupi kutoka simu ya mkewe kwenda katika simu yake.

"Kama shetani angeendelea kunishikilia hadi leo hi, hakuna mtu angejua kitu nimefanya, lakini roho mtakatifu alinishukia na nilikuwa na sukumwa kusema ukweli. Kwa sababu nilikaa miezi miwili na siku moja bila ukweli kujulikana, hadi sasa Naomi asingejulikana yuko wapi.

"Kutokana na hofu ya Mungu, niliamua kusema ukwell sio kwa sababu nilipata mateso kutoka kwa askari polisi, hapana! Ni mimi mwenyewe niliamua," alidai Luwonga.

Mshtakiwa huyo pia aliiomba mahakama kuwa pindi kesi itakapoanza kusikilizwa, Mahakama Kuu ihamie sehemu ya tukio nyumbani kwake, ili wane mashimo sita aliyoyachimba katika nyumba zake sita na nyumba ya kulala wageni kwa ajili ya maji taka. Alidai kuwa lengo la mahakama kwenda eneo hilo ni ili ione mashimo yaliyochimbwa yalikuwa ni ya maji taka na sio kwa ajili ya kumzika mkewe, kwa sababu yeye ndiye alitaka kwa ajili ya maji machafu.

Ni madai yaliyomfanya hakimu aingilie, akisema: "Sasa mshitakiwa huko unapokwenda ni kwenye ushahidi. Hayo utayazungumza huko Mahakama Kuu katika ushahidi wako."

Mshitakiwa Luwonga alidai: "Mheshimiwa ninaomba ufahamu jambo moja; hawa mawakili wangu nimewaomba wanitetee kwa haki na siyo kupindishapindisha mambo kwa sababu mimi ndiye niliamua mwenyewe kuzungumza ukweli," alidai Luwonga.

Alidai hayo baada ya wakili wake, Mohamed Majaliwa kumtaka aache kuzungumza. Wakili huyo alimtaka wazungumze kwanza wao kabla ya yeye kuendelea kuzungumza mbele ya hakimu.

"Ninawaomba mawakili wa serikali, mnipelekee taarifa zangu kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kwamba aharakishe kesi hi lishe haraka kwa sababu hata Rais na jamii kwa ujumla wanataka kujua mwisho wake kwa sababu kesi yangu hii ilitikisa chi.

"Ninataka kesi hii iwe fundisho kwa watu wengi, kwa sababu tulifanya uzembe mkubwa sana sisi wanandoa na jamii pia ilifanya uzembe hadi mauaji yakatokea, alidai Luwonga.

Baada ya mshitakiwa kudai hivyo, Hakimu Rugemalira alimweleza kwamba hakuna kesi kubwa. Zote zinalingana na hakuna kesi inayotikisa chi, hivyo hata kesi inayomkabili "sio konki" kama alivyodai. Mshitakiwa huyo alidai atakuwa na mashahidi 20 na atakuwa na vielelezo wakati shahidi unaendelea. Atavitoa mwenyewe au mashahidi wake watakuja navyo mahakamani.

"Una haki zako za msingi za kupewa wakili na kupewa orodha ya mashahidi, kama utahitaji na mawakili wako hawa wawapo, hilo ni jukumu lako wewe. Kwa hiyo, unahamishiwa kwenda Mahakama Kuu," alisema Hakimu Rugemalira.

Luwonga anadaiwa kumuua mke wake Naomi kisha kumchoma moto kwa kutumia magunia mawili ya mkaa na baadaye alichukua majivu ya mwili wa marehemu na kwenda kuyafukia shambani kwake Mkuranga mkoani Pwani.

===

Kwanza nianze kuwapongeza wanandoa mliopo mkoa wa Da resalaam. Maana Kwa mujibu wa msajili wa taraka kutoka Nida mkoa unao ongoza Kwa taraka nyingi ni mkoa wa dare salaam.

Ndugu zangu GAZETI la nipashe la Tarehe 3/07/2023 limeandika habari ya Mauaji ya Naomi vizur sana Kona ya habari za mahakamani. GAZETI limeripoti yakuwa Mwanaume aliyemuua Naomi Kisha kumchoma moto alimchoma Kwa magunja mawili ya mkaa.

Pili kichwa Cha mkewe kiliwai sana kuungua maana alikuwa anakigeuza. Tatu amedai Tako lilikuwa na mafuta mengi. Nne sehemu za Siri za Naomi zlikuwa na mafuta. Tano matiti pia yalikuwa na mafuta.

Sehemu zote zilizokuwa na mafuta zilichelewa kuungua ila zilisaidia moto kukolea.

Zingatio;
Mshitakiwa anadai alikuwa na mgogoro wa ndoa na mke wake takribani miaka miwili hawakushirki tendo la ndoa,na Kila mmoja alikuwa analala chumba chake.

Ilifikia hatua Kila mmoja akawa anatoka na kulala nje ya ndoa PASIPO kuulizana au kuagana.

Naomi aliwai kumkata mmewe Kwa kisu na mme alishafika polisi mara kadhaa KULALAMIKA lakini polisi walimfukuza Kwa kumwambia atoke hapo huyo ni mkewe wao hawaingilii ndoa za watu.

Naomi aliwai mvuta mmewe sehemu Siri Tena Kwa nguvu mbele ya mama yake na mwanaume.

Naomi aliwai mpiga mmewe na ndoo ya chooni.

Mara ya mwisho jamaa akirudi kwake asubuhi na kukuta Naomi anamwandaa mtoto aende shule, jamaa aliweka simu yake mezani ilipoita Naomi akaishika na kumpelekea mmewe ukubakimwambia pokea simu za Malaya wako.

Mwishowe wakaanza kugombana Naomi akakimbilia kushika uboo na PUMBU zake Kwa nguvu,mume nae kujiami akampushi, puuuuuu! Laalura! Naomi akadondokea ukuta wa bafu na kudodondekea kichwa na kufa pale pale baada ya damu nyingi kuvujia kichwani.

Baada ya kifo mume akawaza akazike apo apo?itakuwa shida,apeleke Mwili shambani akazike, akaogopa Trafiki, mwishowe akaamua kuuchoma Mwili Ili akazike majibu ya Mwili huo shambank kwake.

ujumbe ndoa kama za Naomi na mwenzake ziko ngapi Kwa Sasa?

Je, kama polisi wetu wangeingilia kati haya yote yangetokea?

Ndoa sio msaafu shekhe!.
Namuelewa sana jamaa…. Tunaweza kumuona Katiti sana, lakini hatujui alichopitia hadi kufika hapo

Kwa ujumla, jamii yetu ina jukumu kubwa sana la kusaidia wenye ndoa

Mapito ni magumu sana wajameni
 
Hili tukio nalikumbuka liliwahi kutikisa sana 2019.

Changamoto za ndoa ni kubwa sana na inapotokea ukapata mtu ambaye hamuendani ndio huongezeka maradufu.

Hata hivyo Jamaa kaonesha ujasiri wa hali ya juu ila ndio hivyo mahakama huwa haitoi hukumu kwa huruma.
Cha ajabu hakimu anakomaa kuwa kesi ya jamaa haikutikisa nchi, kuwa ni kesi ya kawaida.
 
Kitendo cha kua tayari kwa hukumu yeyote hata kunyongwa hadi kufa,kinaashiria kua mtuhumiwa amekubali kosa lake,na anaona kabisa kua ni haki kuhukumiwa kwa alichokifanya,

Sometimes majuto huja baada ya kitendo but hua ni too little too late.
Amekubali kosa lake kuwa aliua ila anaongea kisheria kuwa, kama ataamriwa kunyongwa anataka iwe ni kwa haki maana anajua kweli aliua lakini bila kukusudia hivyo hastahili kunyongwa. Hajutii kwa kilichomtokea.
 
Kuna uwoga kuingia kwenye ndoa
Ni bora nitafute mwanamke anizalie
Kuliko kuua mtu
Si mpaka uwe na akili hiyo, jamaa akili yake haiko sawa, atakuwa anavuta bangi hataivyo wanawake ni wavumilivu sana kwa vyvyote vile yapo matukio kadhaa atakuwa alishafanya huko nyuma yakiashilia tukio kubwa kama hilo sema mwanamke hakung'amua mapema au alidharau hiyo hali.Hata kama alinyonga Kuku badala ya kumchinja ni kiashilia tosha kuwa kuna jambo baya linakuja.
 
Back
Top Bottom