Andika neno lolote chungu, zito, lenye maumivu ambalo hautakujaa kusahau mtu alikutamkia

Andika neno lolote chungu, zito, lenye maumivu ambalo hautakujaa kusahau mtu alikutamkia

Ni hatari sana mkuu! Kipindi namaliza form 4 nimechaguliwa kwenda chuo cha mifugo wazazi wote wakawa wamefariki nikawa sina pa kushika mpaka imefikia nakosa hata viatu vya shule. Nikasema wacha niende kwa sister mtoto wa baba mkubwa anipige tafu. Akaniambia nimfuate ofisini kwake (alikuwa dereva wa JWTZ baadaye akaja akahamia UN) ili anipeleke na home kwake nikapaone. Kufika sijui nini kikamjia kichwani akawa ameghairi kunipeleka kwake. Hapo ofisini alikuwa na wadogo zake tumbo moja na binti yake wa nje ya ndoa ambaye alikuwa karibia rika moja na yeye mzazi (alipata mimba akiwa mtoto) na kule kwa mme wake alikuwa anadanganya kwamba huyo binti ni mdogo wake (sasa nikawa nahisi kwamba labda aliogopa nisije nikamtibulia mipango). Basi akaniuliza nina shida gani? Nikamweleza naomba unisaidie hela ya viatu vya shule sina kabisa, likafuata tusi la Kisukuma "ALIYO GHASHI MAKOYE!" Wadogo zake wakacheka sana! sikurudia tena na nikaondoka zangu! Tangu siku hiyo nikakata mawasiliano nikapambana kivyangu mpaka nikamaliza chuo na kupata kazi nzuri tu kipindi hicho, yeye huku nyuma akawa ametengana na mmewe aliyekuwa anamweka mjini, maisha yakampiga mpaka akawa ananitafuta nimpige tafu, anapitishia ujumbe kwa sister wangu! Kwa vile mimi Mgalatia nikawa najibu hivyo hivyo alivyonijibu mimi! Mwisho wa siku anakuja kufariki almanusura azikwe na Halmashauri ya Jiji! Wadogo zake walionicheka kipindi kile wakaja wakafa kwa kujitia kitanzi kutokana na ugumu wa maisha uliowakumba! Karma is a bitch! Binadamu tupendane aisee!

Uliwaroga nini??🤔
 
Siwezi kuolewa na wewe nimeenda kwa mganga nimeambiwa mama yako mchawi anataka kuniuwa au kunipa stroke,endelea kuwaendekeza ndugu zako utazeeka bila kuoa.
 
Habarini wapendwa.

Leo nimekaa nikawa nimepitia. Insta nikaona x kapost picha yake nikakumbuka neno mmoja mabalo nalikumbukka mpka leo liliniuma sana.

Alinisumbua sana ikafika mahali nilipewa mapumziko hospital, sasa kwenye kumpigia kumwambia nimelazwa ,bwana ee alinitext ".

Utajua mwenyewe siumeyataka mwenyewe,wivu tuu, kufatiliana fatiliana".

Asee sitasahau aalikuwa hana utu..sasa naa wewe. Andika Neno lolote CHUNGU ,ZITO,LENYE MAUMIVU AMBALO Hautakujaa kusahau mtu alikutamkia..
Niko nje ya mada kidogo ila naomba niteme nyongo yangu hapa

Niliwai kumuandalia mtu ambaye nilikua nikimpenda sana birthday party ila hakujali na wala hakuja .Nilijinyima sana kumfanikishia ilo jambo ila hakujali niliumia mno mapenz haya baunsa
 
"Hujachangia hata tofali moja wakati najenga nyumba yangu"
" Hamna kazi ambayo utaweza kuifanya wewe ngoja tuone"

Namshukur Mungu niliondoka home leo nipo mkoa mwingine najitegemea na kuilisha familia yangu na mengine mengi🙏🙏
 
Wakati naendesha bolt, mama mmoja anaitwa Evelyn, anakaa ilazo, tulishindwana nikamshusha kwenye gari kabla hata ya kufanya safari. Akaondoka zikapita dk 2 akatuma msg hutakaa ufanikiwe mbwa wewe.

Leo namalizia nyumba ya binti yangu itega, block ambayo kwa plan ya jiji, ni marufuku kujenga flat house.

Ipo siku nitampigia yule mama nimshukuru. Namba yake nilihifadhi mahali pa muda wote
 
Siku nyingine mkianzisha nyuzi kama hizi mnatutag na sisi watumishi tupate points za kusadia watu
 
Back
Top Bottom