Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II --- 80*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Jambo hilo halikuwawia ugumu kwani nyuso za Jona na wenzake zilikusanywa upesi baada ya kufanya utaalamu wao wakizitoa kwenye kamera zilizokuwa zimefungwa kwenye nyumba za wale madereva waliotekwa.


ENDELEA


Na basi sasa kazi inakuwa rahisi na pengine kabla ya jua kuchomoza kila jambo linaweza likawa limekamilika.


Kwakuwa kumi na wawili ni watu wengi sana, kiongozi wao akaona si busara wakiongozana pamoja hivyo wagawane ipate kuwa rahisi kufanya kazi. Endapo taarifa zitakapotoka kuwa walengwa wapo upande fulani, basi waliopo karibu watafanya hiyo kazi wakati msaada zaidi ukiwa njiani waja.


Kila kitu kikawa chema. Ni taarifa tu ndiyo ilikuwa inangojewa hapa na si kinginewe. Muda ukasonga mpaka majira ya saa kumi na mbili hivi ndipo mtandao ukatoa taarifa kuwa walengwa wamepatikana!


Tiiiii! Tiiiii! Tiiiiii! Tarakilishi ya yule jamaa aliyebakizwa makaoni kwa ajili ya kuendesha mitambo ililia. Alikuwa anasinziasinzia. Alikurupushwa na alarm hiyo akarusha macho yake kwenye kioo.


Akaona jina ni Queenland Hotel. Nyuso ambazo zilikuwa zimetunzwa kwenye ghala ya tarakilishi yake zilifanana kwa asilimia tisini na nane na zile ambazo zimeonekana kwenye hoteli ya Queenland!


Akanyanyua simu ya mezani na kumpasha habari mkuu wa kikosi kilichopo huko mtaani pasipo kujali ukubwa wa usiku. Akamweleza bayana kuwa waelekee Queenland na watapata wanachokitaka.


Basi taarifa ikapokelewa na kutumwa tena kwa watu wanne waliokuwa karibu na ilipo hoteli hiyo. Waende huko upesi na wenzao wapo njiani kuwafuata.


Watu hao wanne, wawili majibaba na wawili wakiwa ni wadada, wakaenda mara moja kutekeleza agizo. Walikuwa ndani ya gari aina ya BMW x6 nyeusi ambayo vioo vyake vilikuwa vimefungwa kuwa giza.


Gari likaenda kwa kasi, na lilipofika kwenye uwanja wa hoteli hiyo, kabla ya kushuka watu hawa wakafungia bunduki zao vyuma vya kupunguzia sauti, alafu wakahakikisha mifumo yao ya mawasiliano ipo sawia.



**



“Nimekipenda!” alisema Komandoo Chombo akitazama kuangaza chumba walichotoka kuingia muda si mrefu. Kilikuwa ni chumba kipana kilichokuwa na rangi mbalimbali za kuvutia. Taa kubwa na ya urembo ikining’inia na madirisha mawili ambayo yana mwonekano mzuri wa maghorofa mengine yaanayopakana nayo. Mbali na hapo kuna bafu pana lenye kila aina ya huduma.

Ama kwa hakika vilikuwa vinavutia machoni na viliendana haswa na gharama zake. Wanaume hawa watatu, Komandoo Chombo, Tito na Blanko, wote kwa pamoja walivutiwa nacho.


Wakawa wanaendelea kupekua, isipokuwa Chombo yeye akawa amejitupia kitandani alipopokelewa na godoro laini kubwa lililomhakikishia mapumziko ya furaha.


Muda si mrefu, hodi ikagongwa. Kwakuwa wengine, yaani Tito na Blanko, hawakuwapo mazingira ya karibu, Tito alikuwa bafuni na Blanko akiwa ameenda mpaka kwa nje kuangalia mazingira, Chombo ikampasa kuitikia hodi hiyo.


Akanyanyuka kivivu kujongelea mlango. Alipofika akauliza kabla hajafungua,


“Who’s it?”


Akaitikiwa ni mhudumu. Basi akafungua na kuangaza. Akakutana na mwanadada mrembo aliyekuwa amevalia sare. Mkononi alikuwa amebeba trey ya mvinyo na glasi zake nne.


Akatabasamu akitembea kuzama ndani. Alipofikia mezani akaweka mvinyo ule na kumtazama Komandoo Chombo.


“Are you alone?” akamuuliza akiwa anatazama huku na kule. Chombo akatabasamu kidogo na kusema. “No. I am wrih my friends!”


Mhudumu akatabasamu na kusema, “Oh! It’s sweeter when it’s shared.” kisha akaenda zake kuufuata mlango Chombo akimtazama. Alikuwa anatembea kwa madaha kiasi cha kuvutia kumtazama, achilia mbali urembo wake maridadi.


“Anything else, Mr.?” akauliza mhudumu akiwa ameshikilia mlango.


“No! … Nothing,” akajibu Chombo kwa sauti ya kutokumaanisha.


“Ok, I will be here so soon to take leftovers,” akaaga mhudumu kwa namna hiyo, na Chombo akamsindikiza kwa macho malaini kabla hajaufunga mlangowe kisha akarudi na kuungana na wenzake ambao walikuwa tayari wameshatoka huko walipokuwa.


“Jamani kuna mambo yenu hapo,” akasema akionyeshea ule mvinyo ulioletwa na mhudumu.


“Oooh!” akadakia Tito. “Ila nimekuona ulivyokuwa unamtazama yule mhudumu!” akatania wakacheka. Na basi kwakuwa mhudumu alisema kuwa atakuja kuchukua mabaki muda si mrefu, wanaume hawa hawakukawia wakabwia kinywaji na kuacha chupa i nyeupe ndani ya sekunde kadhaa tu.


Vinywa na makoo yao yalikuwa yamezoea vinywaji vikali. Hii ‘wine’ ilikuwa ni kama sharubati tu. Hata glasi hawakutumia bali waligida kwa mtindo wa tarumbeta.


Ila walipomaliza walijikuta wakihisi vichwa ni vizito sana. Hawakuweza kudumu tena, wakajilaza kana kwamba ng’ombe waliokuwa hoi kwa kulimishwa siku nzima.


Lakini mabwana hawa, mbona si kujiuliza kuletewa kinywaji hicho muda kama huo wa usiku mnene? Pengine imani yao ilikuwa kubwa. Ama tuseme kiu za makoo yao zilizidi uwezo wa wa kufikiria.



**



Akiwa bafuni, anasikia hodi. Miranda anazima bomba lake la maji na kuskiza vema kama kweli akisikiacho ndicho. Ni kweli. Alijiuliza kidogo kabla hajavuta taulo lake akajifuta uso na kulikaza vema kifuani.


“Comiiiing!”


Akatoka kwenda mlangoni. Kabla hajafungua, akachungulia kwanza na kumwona mwanamke aliyevalia sare za wahudumu. Mkononi mwake alikuwa amebebelea trey lenye mvinyo mwekundu pamoja na glasi mbili.


“You’re welcome!”


“Thanks. Sorry for my disturbance.”


“Never mind.”


“Mam, it’s my pleasure to serve you with the finest and royal wine in the country. Hope you are going to enjoy it the same to your stay in our hotel.”


“Thanks,” akasema Miranda akitabasamu kinafki. Mhudumu akazama ndani na kwenda moja kwa moja kwenye meza alipoweka mvinyo aliouleta na kisha akaaga.


“I will be back soon to take leftovers.”


Miranda asijali sana, akarudishia mlango na kurudi bafuni kumalizia zoezi lake. Lakini mhudumu yule, ambaye ndiye yuleyule aliyewapa wale makomandoo mvinyo, hakuwa amekomea kwake.


Sasa akiwa amebebelea mvinyo mmoja wa mwisho akaelekea chumba kilichokuwa kimewahifadhi Jona na Lee. Mvinyo huo mmoja ulikuwa unasindikizwa na glasi mbili pia pembezoni. Kama kawaida akagonga na muda si mrefu akafunguliwa.


“Hey!” alikuwa ni Lee. Kiunoni alikuwa amefungia taulo. Na kabla hajafungua alihakikisha kwanza mhudumu huyo yupo peke yake kwa kuchungulia.


Mhudumu akaomba samahani na kuteta haja yake, amekuja kuwaletea mvinyo bora kabisa. Basi pasi na hiyana, Lee akamkaribisha azame ndani. Mhudumu huo akiwa anatembea kwa maringo, akaingia na kunyookea meza.


Kitandani Jona alikuwa amelala ila si usingizi. Alikuwa anahisi uchovu na pengine isingezidi dakika tano angekuwa ameshapitiwa na usingizi. Hata hivyo kitu pekee kilichomfanya akadumu kwa muda akiwa amcho, ni kumngoja Lee atoke bafuni naye ajimwagie maji.


Basi macho yake yakiwa bado ni mazima, yakamtazama yule mhudumu. Kichwani akajiuliza maswali kadhaa haswa la kuletewa mvinyo wakati ule. Ila akili yake ilikuwa imechoka, zembe kwa muda huo. Hakujali sana. Labda wanataka wateja wao walale unono, akawaza kaupumbavu.


Ila wakati mhudumu anaweka mvinyo mezani, Jona akaona jambo lililompatia shaka. Alidhani pengine ni macho yake ila la hasha, alikuwa sahihi! Kwenye nyonga ya kulia ya mhudumu kulikuwa na bunduki!


Bunduki hiyo ilikuwa imezibwa na sketi ya sare. Ni kuinama kwa mhudumu ndipo kulifanya silaha hiyo ihakisiwe tena endapo kama ungetazama kwa umakini.


Mhudumu akamtazama Jona na kutabasamu, kisha akaanza safari yake ya kimadaha kwenda mlangoni.


Kwa namna alivyokuwa anatembea na namna anavyovutia, mwanaume ungepata wapi wasaa wa kumdhania mwanamke huyu ni hatari? Macho yako yote yangekulevya kufaidi uumbwaji wa Mungu uje kutambua unamalizwa ukiwa unakufa!


Akiwa amebakiza hatua tatu kuufikia mlango, sauti ya kiume ikakoroma, “Please, stop!”


Akasimama.


Akasikia Jona akitoka kitandani na kusimama, basi akaanza kujongesha mkono wake kwenda kwenye silaha. Huenda mambo yamebuma.


Jona akasonga na akasimama hatua mbili nyuma yake. Mwanaume huyo alikuwa amevalia suruali pekee. Macho yake yaliyokuwa na uchovu sasa yalikuwa yanatazama kwa mashaka.


“Who are you?” Jona akauliza.


“I am the waitress!” akajibu mhudumu. Hakuwa amegeuka. Alikuwa anatazama mbele kuangazia mlango. Pale mlangoni alikuwa amesimama Lee, bado hajajua kinachoendelea hapa uzuri.


“Why do you bring wine at this time?” Jona akauliza kwa sauti ya amri.


“It’s our schedule,” akajibu mhudumu, alafu akageuka kumtazama Jona. Bado mkono wake ulikuwa karibu na nyonga yenye silaha.


“Can you please taste it for us?” Jona akaomba. Mhudumu akatabasamu na kuuliza, “Why? You think we want to kill our clients?”


“Maybe!” Jona akajibu akipandisha bega la kulia. “You never know.”


Hapa mhudumu akamtazama Jona machoni, wakatazamana kwa sekunde nne pasipo kufanya jambo.


“Okay!” Mhudumu akabinua mdomo. “I will do what you wish.” kisha akasogelea mvinyo na kumiminia kwenye glasi.



**



ATAKUNYWA? … UTAJUA KESHO …


Simulizi za series


Kwa oda ya simulizi yamwezi wa tano na kuendelea, whatsapp 0685 758 123..
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 80*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


Jambo hilo halikuwawia ugumu kwani nyuso za Jona na wenzake zilikusanywa upesi baada ya kufanya utaalamu wao wakizitoa kwenye kamera zilizokuwa zimefungwa kwenye nyumba za wale madereva waliotekwa.


ENDELEA


Na basi sasa kazi inakuwa rahisi na pengine kabla ya jua kuchomoza kila jambo linaweza likawa limekamilika.


Kwakuwa kumi na wawili ni watu wengi sana, kiongozi wao akaona si busara wakiongozana pamoja hivyo wagawane ipate kuwa rahisi kufanya kazi. Endapo taarifa zitakapotoka kuwa walengwa wapo upande fulani, basi waliopo karibu watafanya hiyo kazi wakati msaada zaidi ukiwa njiani waja.


Kila kitu kikawa chema. Ni taarifa tu ndiyo ilikuwa inangojewa hapa na si kinginewe. Muda ukasonga mpaka majira ya saa kumi na mbili hivi ndipo mtandao ukatoa taarifa kuwa walengwa wamepatikana!


Tiiiii! Tiiiii! Tiiiiii! Tarakilishi ya yule jamaa aliyebakizwa makaoni kwa ajili ya kuendesha mitambo ililia. Alikuwa anasinziasinzia. Alikurupushwa na alarm hiyo akarusha macho yake kwenye kioo.


Akaona jina ni Queenland Hotel. Nyuso ambazo zilikuwa zimetunzwa kwenye ghala ya tarakilishi yake zilifanana kwa asilimia tisini na nane na zile ambazo zimeonekana kwenye hoteli ya Queenland!


Akanyanyua simu ya mezani na kumpasha habari mkuu wa kikosi kilichopo huko mtaani pasipo kujali ukubwa wa usiku. Akamweleza bayana kuwa waelekee Queenland na watapata wanachokitaka.


Basi taarifa ikapokelewa na kutumwa tena kwa watu wanne waliokuwa karibu na ilipo hoteli hiyo. Waende huko upesi na wenzao wapo njiani kuwafuata.


Watu hao wanne, wawili majibaba na wawili wakiwa ni wadada, wakaenda mara moja kutekeleza agizo. Walikuwa ndani ya gari aina ya BMW x6 nyeusi ambayo vioo vyake vilikuwa vimefungwa kuwa giza.


Gari likaenda kwa kasi, na lilipofika kwenye uwanja wa hoteli hiyo, kabla ya kushuka watu hawa wakafungia bunduki zao vyuma vya kupunguzia sauti, alafu wakahakikisha mifumo yao ya mawasiliano ipo sawia.



**



“Nimekipenda!” alisema Komandoo Chombo akitazama kuangaza chumba walichotoka kuingia muda si mrefu. Kilikuwa ni chumba kipana kilichokuwa na rangi mbalimbali za kuvutia. Taa kubwa na ya urembo ikining’inia na madirisha mawili ambayo yana mwonekano mzuri wa maghorofa mengine yaanayopakana nayo. Mbali na hapo kuna bafu pana lenye kila aina ya huduma.

Ama kwa hakika vilikuwa vinavutia machoni na viliendana haswa na gharama zake. Wanaume hawa watatu, Komandoo Chombo, Tito na Blanko, wote kwa pamoja walivutiwa nacho.


Wakawa wanaendelea kupekua, isipokuwa Chombo yeye akawa amejitupia kitandani alipopokelewa na godoro laini kubwa lililomhakikishia mapumziko ya furaha.


Muda si mrefu, hodi ikagongwa. Kwakuwa wengine, yaani Tito na Blanko, hawakuwapo mazingira ya karibu, Tito alikuwa bafuni na Blanko akiwa ameenda mpaka kwa nje kuangalia mazingira, Chombo ikampasa kuitikia hodi hiyo.


Akanyanyuka kivivu kujongelea mlango. Alipofika akauliza kabla hajafungua,


“Who’s it?”


Akaitikiwa ni mhudumu. Basi akafungua na kuangaza. Akakutana na mwanadada mrembo aliyekuwa amevalia sare. Mkononi alikuwa amebeba trey ya mvinyo na glasi zake nne.


Akatabasamu akitembea kuzama ndani. Alipofikia mezani akaweka mvinyo ule na kumtazama Komandoo Chombo.


“Are you alone?” akamuuliza akiwa anatazama huku na kule. Chombo akatabasamu kidogo na kusema. “No. I am wrih my friends!”


Mhudumu akatabasamu na kusema, “Oh! It’s sweeter when it’s shared.” kisha akaenda zake kuufuata mlango Chombo akimtazama. Alikuwa anatembea kwa madaha kiasi cha kuvutia kumtazama, achilia mbali urembo wake maridadi.


“Anything else, Mr.?” akauliza mhudumu akiwa ameshikilia mlango.


“No! … Nothing,” akajibu Chombo kwa sauti ya kutokumaanisha.


“Ok, I will be here so soon to take leftovers,” akaaga mhudumu kwa namna hiyo, na Chombo akamsindikiza kwa macho malaini kabla hajaufunga mlangowe kisha akarudi na kuungana na wenzake ambao walikuwa tayari wameshatoka huko walipokuwa.


“Jamani kuna mambo yenu hapo,” akasema akionyeshea ule mvinyo ulioletwa na mhudumu.


“Oooh!” akadakia Tito. “Ila nimekuona ulivyokuwa unamtazama yule mhudumu!” akatania wakacheka. Na basi kwakuwa mhudumu alisema kuwa atakuja kuchukua mabaki muda si mrefu, wanaume hawa hawakukawia wakabwia kinywaji na kuacha chupa i nyeupe ndani ya sekunde kadhaa tu.


Vinywa na makoo yao yalikuwa yamezoea vinywaji vikali. Hii ‘wine’ ilikuwa ni kama sharubati tu. Hata glasi hawakutumia bali waligida kwa mtindo wa tarumbeta.


Ila walipomaliza walijikuta wakihisi vichwa ni vizito sana. Hawakuweza kudumu tena, wakajilaza kana kwamba ng’ombe waliokuwa hoi kwa kulimishwa siku nzima.


Lakini mabwana hawa, mbona si kujiuliza kuletewa kinywaji hicho muda kama huo wa usiku mnene? Pengine imani yao ilikuwa kubwa. Ama tuseme kiu za makoo yao zilizidi uwezo wa wa kufikiria.



**



Akiwa bafuni, anasikia hodi. Miranda anazima bomba lake la maji na kuskiza vema kama kweli akisikiacho ndicho. Ni kweli. Alijiuliza kidogo kabla hajavuta taulo lake akajifuta uso na kulikaza vema kifuani.


“Comiiiing!”


Akatoka kwenda mlangoni. Kabla hajafungua, akachungulia kwanza na kumwona mwanamke aliyevalia sare za wahudumu. Mkononi mwake alikuwa amebebelea trey lenye mvinyo mwekundu pamoja na glasi mbili.


“You’re welcome!”


“Thanks. Sorry for my disturbance.”


“Never mind.”


“Mam, it’s my pleasure to serve you with the finest and royal wine in the country. Hope you are going to enjoy it the same to your stay in our hotel.”


“Thanks,” akasema Miranda akitabasamu kinafki. Mhudumu akazama ndani na kwenda moja kwa moja kwenye meza alipoweka mvinyo aliouleta na kisha akaaga.


“I will be back soon to take leftovers.”


Miranda asijali sana, akarudishia mlango na kurudi bafuni kumalizia zoezi lake. Lakini mhudumu yule, ambaye ndiye yuleyule aliyewapa wale makomandoo mvinyo, hakuwa amekomea kwake.


Sasa akiwa amebebelea mvinyo mmoja wa mwisho akaelekea chumba kilichokuwa kimewahifadhi Jona na Lee. Mvinyo huo mmoja ulikuwa unasindikizwa na glasi mbili pia pembezoni. Kama kawaida akagonga na muda si mrefu akafunguliwa.


“Hey!” alikuwa ni Lee. Kiunoni alikuwa amefungia taulo. Na kabla hajafungua alihakikisha kwanza mhudumu huyo yupo peke yake kwa kuchungulia.


Mhudumu akaomba samahani na kuteta haja yake, amekuja kuwaletea mvinyo bora kabisa. Basi pasi na hiyana, Lee akamkaribisha azame ndani. Mhudumu huo akiwa anatembea kwa maringo, akaingia na kunyookea meza.


Kitandani Jona alikuwa amelala ila si usingizi. Alikuwa anahisi uchovu na pengine isingezidi dakika tano angekuwa ameshapitiwa na usingizi. Hata hivyo kitu pekee kilichomfanya akadumu kwa muda akiwa amcho, ni kumngoja Lee atoke bafuni naye ajimwagie maji.


Basi macho yake yakiwa bado ni mazima, yakamtazama yule mhudumu. Kichwani akajiuliza maswali kadhaa haswa la kuletewa mvinyo wakati ule. Ila akili yake ilikuwa imechoka, zembe kwa muda huo. Hakujali sana. Labda wanataka wateja wao walale unono, akawaza kaupumbavu.


Ila wakati mhudumu anaweka mvinyo mezani, Jona akaona jambo lililompatia shaka. Alidhani pengine ni macho yake ila la hasha, alikuwa sahihi! Kwenye nyonga ya kulia ya mhudumu kulikuwa na bunduki!


Bunduki hiyo ilikuwa imezibwa na sketi ya sare. Ni kuinama kwa mhudumu ndipo kulifanya silaha hiyo ihakisiwe tena endapo kama ungetazama kwa umakini.


Mhudumu akamtazama Jona na kutabasamu, kisha akaanza safari yake ya kimadaha kwenda mlangoni.


Kwa namna alivyokuwa anatembea na namna anavyovutia, mwanaume ungepata wapi wasaa wa kumdhania mwanamke huyu ni hatari? Macho yako yote yangekulevya kufaidi uumbwaji wa Mungu uje kutambua unamalizwa ukiwa unakufa!


Akiwa amebakiza hatua tatu kuufikia mlango, sauti ya kiume ikakoroma, “Please, stop!”


Akasimama.


Akasikia Jona akitoka kitandani na kusimama, basi akaanza kujongesha mkono wake kwenda kwenye silaha. Huenda mambo yamebuma.


Jona akasonga na akasimama hatua mbili nyuma yake. Mwanaume huyo alikuwa amevalia suruali pekee. Macho yake yaliyokuwa na uchovu sasa yalikuwa yanatazama kwa mashaka.


“Who are you?” Jona akauliza.


“I am the waitress!” akajibu mhudumu. Hakuwa amegeuka. Alikuwa anatazama mbele kuangazia mlango. Pale mlangoni alikuwa amesimama Lee, bado hajajua kinachoendelea hapa uzuri.


“Why do you bring wine at this time?” Jona akauliza kwa sauti ya amri.


“It’s our schedule,” akajibu mhudumu, alafu akageuka kumtazama Jona. Bado mkono wake ulikuwa karibu na nyonga yenye silaha.


“Can you please taste it for us?” Jona akaomba. Mhudumu akatabasamu na kuuliza, “Why? You think we want to kill our clients?”


“Maybe!” Jona akajibu akipandisha bega la kulia. “You never know.”


Hapa mhudumu akamtazama Jona machoni, wakatazamana kwa sekunde nne pasipo kufanya jambo.


“Okay!” Mhudumu akabinua mdomo. “I will do what you wish.” kisha akasogelea mvinyo na kumiminia kwenye glasi.



**



ATAKUNYWA? … UTAJUA KESHO …


Simulizi za series


Kwa oda ya simulizi yamwezi wa tano na kuendelea, whatsapp 0685 758 123..
Unawekaje odaaa bos
 
Back
Top Bottom