SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #4,041
*ANGA LA WASHENZI II --- 81*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Hapa mhudumu akamtazama Jona machoni, wakatazamana kwa sekunde nne pasipo kufanya jambo.
“Okay!” Mhudumu akabinua mdomo. “I will do what you wish.” kisha akasogelea mvinyo na kumiminia kwenye glasi.
ENDELEA
Kabla hajautia kinywani, akasita. Akamtazama kwanza Jona na kisha Lee. Nyuso za wanaume hao tayari zilikuwa zimebeba shaka. Mambo hayakuwa sawa.
Basi mhudumu huyu akapeleka glasi kinywani, ila kabla hajafyonza, akachomoa upesi bunduki yake toka kiunoni. Alifunua sketi yake upesi kiasi kwamba hata nguo ya ndani haikuonekana. Kabla hajawanyooshea wakina Jona na kufyatua, Jona akawa amemfikia! Ila bado akafyatua. Risasi ikaruka na kutoboa mlango.
Kabla tena hajafanya jambo, Jona akawa amempokonya bunduki. Ila naye mhudumu akawa na upesi, hakumruhusu Jona amshambulie, akamng’ang’ania mkono wake, Jona akauvuta kwanguvu na kumtandika kiwiko, akadondoka chini!
Alikuwa anavuja damu puani. Kichwa kilikuwa kinamgonga sana. Hakuweza kunyanyuka tena na kupambana. Jona akamfunga kinywa na mikono kwa kutumia mkanda wake kisha akaenda upesi kwenye chumba cha Miranda kwani alihisi huenda mhudumu yule akawa ameshapitia huko kwani chumba chake kilikuwa cha mwisho kwenye utaratibu wa namba.
“Who’s it?” sauti ya Miranda iliuliza.
“It’s me, Jona!”
“Jona?” Miranda akajiuliza kwa sauti yake ya chini. Alikuwa ameketi kitandani akiwa bado hajatoa taulo mwilini mwake. Kwa ujumla alikuwa amejifunga mataulo mawili, moja kifuani na lingine kichwani, ila kuendea mlango, akajivesha taulo kiunoni kutimiza matatu.
“Umekunywa wine?” lilikuwa swali la kwanza la Jona. Aliuliza akiwa ametoa macho na akizama ndani kwa kuusukuma mlango. Alipotupa macho akaona chupa ya wine mezani. Haikuwa imefunguliwa. Hatimaye akashusha pumzi.
“Kuna nini Jona?” Miranda akauliza kwa uso wa mashaka.
“Tupo under attack,” Jona akamjibu akimtazama kwa macho ya hakika. Ila hakusema sana, akaenda kuufuata mlango atoke, ila kabla akamtazama Miranda na kumwonya, “Usinywe hiyo wine!” kisha haraka akauendea mlango kuelekea kwenye chumba cha wale makomandoo.
“Vipi, amekunywa?” Lee aliuliza. Alikuwa ni punde ametoka kwenye chumba. Ameshavalia suruali na shati jepesi.
“Hajanywa!” Jona akajibu akiwa na haraka. Akauendea mlango wa wale makomandoo akiwa anaongozana na Lee kwa nyuma. Akaukuta mlango ukiwa umefungwa. Akagonga pasipo mafanikio. Akauvamia kuuvunja.
Kutazama ndani akawaona mabwana wale wakiwa wamelala kitandani. Hawakuonekana kujielewa. Na kama wangelikuwa wazima basi wangelikuwa wamedamka punde waliposikia mlago ukigongwa, hata basi ukivunjwa.
Chupa ya wine ilikuwa tupu, haina kitu!
“Wamekunywa!” Lee akaropoka. Walitazamana na Jona, Jona upesi akawafuata wale makomandoo na kuwanusa. Walikuwa wananuka pombe!
Lakini zaidi hawakuwa wanapumua! Mapigo ya moyo yalikuwa yamezima! Kiufupi, walikuwa wamekufa.
“Tunafanyaje, Jona?” Lee akauliza.
“Sijui!” Jona akasema akiketi kwenye kitanda. Alishika kichwa chake kwa mawazo.
Ila upesi akiwa amekumbuka jambo, akamtazama Lee na kumwambia, “Tuondoke hapa upesi! Wauaji wameshajua wapi tulipo.”
“Na vipi kuhusu hii miili?” Lee akauliza.
“Inabidi tuondoke nayo. Hatuwezi kuiacha hapa!” Jona akasema akisimama.
“Hapana, Jona!” akasema Lee akitikisa kichwa. “Ni hatari sana kufanya vivyo. Hatujui maadui wapo wapi, wapo wangapi. Tutawezaje kujiokoa na huku tuna miili mitatu?”
“Sasa tutafanyaje?” akauliza Jona. Alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa. Kwa muda akili yake ilikuwa haifanyi jambo. Alikuwa anawaza mambo mengi kwa wakati mmoja.
“Tutapiga picha na kuzituma mtandaoni,” akasema Lee. “Tutaandika caption, najua picha itasambaa mtandaoni na watapata namna.”
“Seriously?” Jona akatia shaka.
“Ndio. Jona hatuna muda hapa. Lazima tufanye maamuzi ya hekima ama wote tuwe wafu!”
Kabla Jona hajasema jambo, wakasikia sauti za vishindo. Wakahisi si shwari. Haraka Lee akachomoa simu na kupiga picha miili ya wale makomandoo …
Huko nje koridoni kulikuwa na wanaume wawili na mwanamke mmoja. Watu hawa waliokuwa wanatembea sambamba walikuwa wamebebelea bunduki mikononi mwao. Nyuso zao zilikuwa za kazi na macho yao yalikuwa yanaangazia milango mitatu inayofuatana.
Milango mitatu ya vyumba vya Jona na wenziwe.
Basi punde walisimama mbele ya chumba cha wale makomandoo. Chumba hicho kilikuwa wazi tu. Hawakuona mtu. Basi wakausogelea mlango, walipofika, wale wanaume wawili, ghafla mlango ukafungwa kwanguvu na kuwakumba!
Wakaweweseka. Walimparamia mwanamke aliyekuwepo nyuma yao na huo ukawa mwanya mzuri kwa wakina Jona kushambulia. Haraka Jona na Lee wakawarukia, na kwa ustadi wao, wakawapokonya silaha na kuwalalisha chini kwa maumivu.
Haraka wakamshtua Miranda na kumwambia waende upesi kwani mambo yameharibika. Upesi Miranda akatoka na wakaelekea kaskazini mwa hoteli. Muda si mrefu, kwenye eneo la tukio, pale walipokuwa wameachwa wale watu walio hoi kwa kipigo, akawa amewasili mwanamke kamanda, Sword, akiwa ameongozana na watu wanne wengine.
“Where are they?” Mwanamke huyo akauliza. Mwanaume mmoja akanyooshea kidole chake upande wa kaskazini, basi haraka mwanamke huyo kamanda akiwa ameongozana na watu wake wakaelekea huko.
Walisaka, hawakuona mtu! Kabla hawajarudi kwa wale wenzao, wakasikia sauti ya mtu anagugumia. Kwenda kutazama, wakamkuta mlinzi akiwa amefungwa mdomo.
“They’ve escaped!” Mwanamke kamanda akaropoka. Geti la uani lilikuwa wazi. Wakina Jona walikuwa wametoroka, na ni wazi haikuwa muda mrefu. Bado geti lilikuwa linachezacheza!
Basi haraka kamanda Sword na wenzake wakakimbilia huko. Kutazama kushoto na kulia, kwa mbali mkono wao wa kuume, wakaona mtu anaishilia. Wakaanza kukimbia kuelekea huko, kufika hawakuona mtu!
“Shit!” akalaani kamanda Sword akipiga kofi paja lake. Mazingira yalikuwa tulivu mno. Ni usiku huu tena mzito. Magari machache yalikuwa yanaonekana barabarani, watu wanaotembea kwa mguu hawakuwapo.
Basi punde, mawasiliano yakaungana toka kule makaoni. Mwanaume yule aliyekuwepo kwenye mitambo akawaambia wapi alipowaona walengwa wao. Ni mtaa wa pili toka walipo. Wapo barabarani bado hawajapata usafiri!
Lakini pia akawaonya kuwa mmoja wao ameshikilia bunduki.
“Let’s go!” akaamuru kamanda. Moja kwa moja wakaenda huko walipoambiwa.
**
Asubuhi na mapema kila kituo cha habari kikarusha taarifa juu ya watu waliokutwa wakiwa wafu kwenye moja ya mtaa wa London. Watu hao walikuwa ni wale waliokuwa wanawafukuzia wakina Jona, kwa idadi watu wanne! Wawili miongoni mwao wakiwa majeruhi wapo hospitali kupokea huduma.
Mbali na hayo, pia hata ile miili ya wale makomandoo na kile kilichotokea kule hotelini kikarushwa na watu wakajua. Hata watu wa Tanzania nao wakapata habari juu ya wanajeshi wao kwenye nchi ya kigeni. Kuitikia hilo, shughuli za kufuatilia miili hiyo ikaanza mara moja.
Basi, mambo yakazidi kupamba moto. Kwakuwa kikosi nambari ‘wani’ kilikuwa kimeshashindwa kufanya kazi yake ya kuwamaliza wakina Jona, ikabidi sasa kitumwe kikosi cha pili. Cha sasa pia kilikuwa kinaongozwa na watu kumi chini ya kamanda mwanamke mwenye jina la Arrow.
Nao wakadumu kwa siku moja. Wote wakapukutika. Kikatumwa kikosi cha tatu na cha nne, nao hawakuwa wameambulia kitu. Wote wakamalizwa kana kwamba maji. Ilikuwa ni kama utani, lakini watu wakienda hakuna aneyerejea zaidi ya taarifa ya habari ya watu kukutwa kwenye mahoteli, ama barabarani!
Kabla ya kikosi cha tano hakijatumwa, Kamanda mkuu, akaona ni kheri kabla hawajafanya hilo, watulie kwanza kuona wapi wanakosea. Ni wazi sasa wakina Jona watakuwa wanafahamu wanachokifanya.
Wakapanga mipango madhubuti ya kuwa, punde wakina Jona watakapoonekana kwenye kamera basi watoe taarifa polisi kwanza. Wahakikishe watu hao wanahitajika na serikali. Na basi picha zao zitazagaa kutangazwa kwenye vyombo vya habari.
Hapo watakuwa wameihamishia kesi mikononi mwa serikali. Ila,
“Don’t you think it will be risk even for us?” akauliza mmoja. Walikuwa wanafahamu wakina Jona watakuwa ni watu wanaujua nyendo zao, vipi wakikamatwa na polisi, hawatatoa taarifa zao huko kituoni?
“No!” akasema Kamanda mkuu akitikisa kichwa. “Before doing that I will have already killed them!” Basi kikao cha dharura kikawa kimeishia hapo. Na siku hii ikaenda salama mpaka kwenye majira ya saa tano usiku.
Kamanda mkuu akatoka kwenda kwenye tafrija fupi iliyokuwa imeandaliwa na Malkia kwa ajili ya kumpongeza mmoja wa vijana wake, kwa jina Prince Henry, kwa kupata mtoto wao wa kwanza na mwanamke aitwaye Diana Lavik, mwanamke mwenye asili ya kilatini.
Tafrija ilikuwa imehudhuriwa na watu wakubwa na wazito. Ulinzi ulikuwa mkubwa. Watu walikuwa wamependeza kwa suti na magauni ya kumetameta aghali.
Basi bwana Kamanda alipoiingia, haikuchukua muda kupata kinywaji mkononi mwake. Na pia watu wawili watatu wa kupiga naye soga za hapa na pale. Ila akiwa anafanya hivyo, mara akasikia sauti ya mwanamke nyuma yake.
“Hey, gentleman.”
Sauti hii ilikuwa kavu ila tamu masikioni. Haikumchukua muda kamanda akageuka kutazama. Hamaki uso kwa uso akakutana na mwanamke mwenye rangi ya dhahabu. Nywele zilizofundwa vema na macho ya kuvutia. Kiuno kimekabwa na gauni na amepanda kwa viatu virefu nyeusi.
Mwanamke huyu alikuwa ni Glady.
“Do I know you, madam?” Kamanda akauliza.
“Yes, you do!” akajibu Glady akirembua. “Would you mind a dance?”
“Off course!”
Glady akamkwapua Kamanda na kusonga naye kando kucheza wimbo wa taratibu uliokuwa unapiga. Sikioni mwake sauti ya mbali ikamwambia, “Hakikisha unamuua.”
***
LAKINI GLADY ATASEMA YEYE NI NANI? NA ATAMUUAJE KAMANDA KWA WATU WENGI HIVI? WENZAKE WAKO WAPI?
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Hapa mhudumu akamtazama Jona machoni, wakatazamana kwa sekunde nne pasipo kufanya jambo.
“Okay!” Mhudumu akabinua mdomo. “I will do what you wish.” kisha akasogelea mvinyo na kumiminia kwenye glasi.
ENDELEA
Kabla hajautia kinywani, akasita. Akamtazama kwanza Jona na kisha Lee. Nyuso za wanaume hao tayari zilikuwa zimebeba shaka. Mambo hayakuwa sawa.
Basi mhudumu huyu akapeleka glasi kinywani, ila kabla hajafyonza, akachomoa upesi bunduki yake toka kiunoni. Alifunua sketi yake upesi kiasi kwamba hata nguo ya ndani haikuonekana. Kabla hajawanyooshea wakina Jona na kufyatua, Jona akawa amemfikia! Ila bado akafyatua. Risasi ikaruka na kutoboa mlango.
Kabla tena hajafanya jambo, Jona akawa amempokonya bunduki. Ila naye mhudumu akawa na upesi, hakumruhusu Jona amshambulie, akamng’ang’ania mkono wake, Jona akauvuta kwanguvu na kumtandika kiwiko, akadondoka chini!
Alikuwa anavuja damu puani. Kichwa kilikuwa kinamgonga sana. Hakuweza kunyanyuka tena na kupambana. Jona akamfunga kinywa na mikono kwa kutumia mkanda wake kisha akaenda upesi kwenye chumba cha Miranda kwani alihisi huenda mhudumu yule akawa ameshapitia huko kwani chumba chake kilikuwa cha mwisho kwenye utaratibu wa namba.
“Who’s it?” sauti ya Miranda iliuliza.
“It’s me, Jona!”
“Jona?” Miranda akajiuliza kwa sauti yake ya chini. Alikuwa ameketi kitandani akiwa bado hajatoa taulo mwilini mwake. Kwa ujumla alikuwa amejifunga mataulo mawili, moja kifuani na lingine kichwani, ila kuendea mlango, akajivesha taulo kiunoni kutimiza matatu.
“Umekunywa wine?” lilikuwa swali la kwanza la Jona. Aliuliza akiwa ametoa macho na akizama ndani kwa kuusukuma mlango. Alipotupa macho akaona chupa ya wine mezani. Haikuwa imefunguliwa. Hatimaye akashusha pumzi.
“Kuna nini Jona?” Miranda akauliza kwa uso wa mashaka.
“Tupo under attack,” Jona akamjibu akimtazama kwa macho ya hakika. Ila hakusema sana, akaenda kuufuata mlango atoke, ila kabla akamtazama Miranda na kumwonya, “Usinywe hiyo wine!” kisha haraka akauendea mlango kuelekea kwenye chumba cha wale makomandoo.
“Vipi, amekunywa?” Lee aliuliza. Alikuwa ni punde ametoka kwenye chumba. Ameshavalia suruali na shati jepesi.
“Hajanywa!” Jona akajibu akiwa na haraka. Akauendea mlango wa wale makomandoo akiwa anaongozana na Lee kwa nyuma. Akaukuta mlango ukiwa umefungwa. Akagonga pasipo mafanikio. Akauvamia kuuvunja.
Kutazama ndani akawaona mabwana wale wakiwa wamelala kitandani. Hawakuonekana kujielewa. Na kama wangelikuwa wazima basi wangelikuwa wamedamka punde waliposikia mlago ukigongwa, hata basi ukivunjwa.
Chupa ya wine ilikuwa tupu, haina kitu!
“Wamekunywa!” Lee akaropoka. Walitazamana na Jona, Jona upesi akawafuata wale makomandoo na kuwanusa. Walikuwa wananuka pombe!
Lakini zaidi hawakuwa wanapumua! Mapigo ya moyo yalikuwa yamezima! Kiufupi, walikuwa wamekufa.
“Tunafanyaje, Jona?” Lee akauliza.
“Sijui!” Jona akasema akiketi kwenye kitanda. Alishika kichwa chake kwa mawazo.
Ila upesi akiwa amekumbuka jambo, akamtazama Lee na kumwambia, “Tuondoke hapa upesi! Wauaji wameshajua wapi tulipo.”
“Na vipi kuhusu hii miili?” Lee akauliza.
“Inabidi tuondoke nayo. Hatuwezi kuiacha hapa!” Jona akasema akisimama.
“Hapana, Jona!” akasema Lee akitikisa kichwa. “Ni hatari sana kufanya vivyo. Hatujui maadui wapo wapi, wapo wangapi. Tutawezaje kujiokoa na huku tuna miili mitatu?”
“Sasa tutafanyaje?” akauliza Jona. Alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa. Kwa muda akili yake ilikuwa haifanyi jambo. Alikuwa anawaza mambo mengi kwa wakati mmoja.
“Tutapiga picha na kuzituma mtandaoni,” akasema Lee. “Tutaandika caption, najua picha itasambaa mtandaoni na watapata namna.”
“Seriously?” Jona akatia shaka.
“Ndio. Jona hatuna muda hapa. Lazima tufanye maamuzi ya hekima ama wote tuwe wafu!”
Kabla Jona hajasema jambo, wakasikia sauti za vishindo. Wakahisi si shwari. Haraka Lee akachomoa simu na kupiga picha miili ya wale makomandoo …
Huko nje koridoni kulikuwa na wanaume wawili na mwanamke mmoja. Watu hawa waliokuwa wanatembea sambamba walikuwa wamebebelea bunduki mikononi mwao. Nyuso zao zilikuwa za kazi na macho yao yalikuwa yanaangazia milango mitatu inayofuatana.
Milango mitatu ya vyumba vya Jona na wenziwe.
Basi punde walisimama mbele ya chumba cha wale makomandoo. Chumba hicho kilikuwa wazi tu. Hawakuona mtu. Basi wakausogelea mlango, walipofika, wale wanaume wawili, ghafla mlango ukafungwa kwanguvu na kuwakumba!
Wakaweweseka. Walimparamia mwanamke aliyekuwepo nyuma yao na huo ukawa mwanya mzuri kwa wakina Jona kushambulia. Haraka Jona na Lee wakawarukia, na kwa ustadi wao, wakawapokonya silaha na kuwalalisha chini kwa maumivu.
Haraka wakamshtua Miranda na kumwambia waende upesi kwani mambo yameharibika. Upesi Miranda akatoka na wakaelekea kaskazini mwa hoteli. Muda si mrefu, kwenye eneo la tukio, pale walipokuwa wameachwa wale watu walio hoi kwa kipigo, akawa amewasili mwanamke kamanda, Sword, akiwa ameongozana na watu wanne wengine.
“Where are they?” Mwanamke huyo akauliza. Mwanaume mmoja akanyooshea kidole chake upande wa kaskazini, basi haraka mwanamke huyo kamanda akiwa ameongozana na watu wake wakaelekea huko.
Walisaka, hawakuona mtu! Kabla hawajarudi kwa wale wenzao, wakasikia sauti ya mtu anagugumia. Kwenda kutazama, wakamkuta mlinzi akiwa amefungwa mdomo.
“They’ve escaped!” Mwanamke kamanda akaropoka. Geti la uani lilikuwa wazi. Wakina Jona walikuwa wametoroka, na ni wazi haikuwa muda mrefu. Bado geti lilikuwa linachezacheza!
Basi haraka kamanda Sword na wenzake wakakimbilia huko. Kutazama kushoto na kulia, kwa mbali mkono wao wa kuume, wakaona mtu anaishilia. Wakaanza kukimbia kuelekea huko, kufika hawakuona mtu!
“Shit!” akalaani kamanda Sword akipiga kofi paja lake. Mazingira yalikuwa tulivu mno. Ni usiku huu tena mzito. Magari machache yalikuwa yanaonekana barabarani, watu wanaotembea kwa mguu hawakuwapo.
Basi punde, mawasiliano yakaungana toka kule makaoni. Mwanaume yule aliyekuwepo kwenye mitambo akawaambia wapi alipowaona walengwa wao. Ni mtaa wa pili toka walipo. Wapo barabarani bado hawajapata usafiri!
Lakini pia akawaonya kuwa mmoja wao ameshikilia bunduki.
“Let’s go!” akaamuru kamanda. Moja kwa moja wakaenda huko walipoambiwa.
**
Asubuhi na mapema kila kituo cha habari kikarusha taarifa juu ya watu waliokutwa wakiwa wafu kwenye moja ya mtaa wa London. Watu hao walikuwa ni wale waliokuwa wanawafukuzia wakina Jona, kwa idadi watu wanne! Wawili miongoni mwao wakiwa majeruhi wapo hospitali kupokea huduma.
Mbali na hayo, pia hata ile miili ya wale makomandoo na kile kilichotokea kule hotelini kikarushwa na watu wakajua. Hata watu wa Tanzania nao wakapata habari juu ya wanajeshi wao kwenye nchi ya kigeni. Kuitikia hilo, shughuli za kufuatilia miili hiyo ikaanza mara moja.
Basi, mambo yakazidi kupamba moto. Kwakuwa kikosi nambari ‘wani’ kilikuwa kimeshashindwa kufanya kazi yake ya kuwamaliza wakina Jona, ikabidi sasa kitumwe kikosi cha pili. Cha sasa pia kilikuwa kinaongozwa na watu kumi chini ya kamanda mwanamke mwenye jina la Arrow.
Nao wakadumu kwa siku moja. Wote wakapukutika. Kikatumwa kikosi cha tatu na cha nne, nao hawakuwa wameambulia kitu. Wote wakamalizwa kana kwamba maji. Ilikuwa ni kama utani, lakini watu wakienda hakuna aneyerejea zaidi ya taarifa ya habari ya watu kukutwa kwenye mahoteli, ama barabarani!
Kabla ya kikosi cha tano hakijatumwa, Kamanda mkuu, akaona ni kheri kabla hawajafanya hilo, watulie kwanza kuona wapi wanakosea. Ni wazi sasa wakina Jona watakuwa wanafahamu wanachokifanya.
Wakapanga mipango madhubuti ya kuwa, punde wakina Jona watakapoonekana kwenye kamera basi watoe taarifa polisi kwanza. Wahakikishe watu hao wanahitajika na serikali. Na basi picha zao zitazagaa kutangazwa kwenye vyombo vya habari.
Hapo watakuwa wameihamishia kesi mikononi mwa serikali. Ila,
“Don’t you think it will be risk even for us?” akauliza mmoja. Walikuwa wanafahamu wakina Jona watakuwa ni watu wanaujua nyendo zao, vipi wakikamatwa na polisi, hawatatoa taarifa zao huko kituoni?
“No!” akasema Kamanda mkuu akitikisa kichwa. “Before doing that I will have already killed them!” Basi kikao cha dharura kikawa kimeishia hapo. Na siku hii ikaenda salama mpaka kwenye majira ya saa tano usiku.
Kamanda mkuu akatoka kwenda kwenye tafrija fupi iliyokuwa imeandaliwa na Malkia kwa ajili ya kumpongeza mmoja wa vijana wake, kwa jina Prince Henry, kwa kupata mtoto wao wa kwanza na mwanamke aitwaye Diana Lavik, mwanamke mwenye asili ya kilatini.
Tafrija ilikuwa imehudhuriwa na watu wakubwa na wazito. Ulinzi ulikuwa mkubwa. Watu walikuwa wamependeza kwa suti na magauni ya kumetameta aghali.
Basi bwana Kamanda alipoiingia, haikuchukua muda kupata kinywaji mkononi mwake. Na pia watu wawili watatu wa kupiga naye soga za hapa na pale. Ila akiwa anafanya hivyo, mara akasikia sauti ya mwanamke nyuma yake.
“Hey, gentleman.”
Sauti hii ilikuwa kavu ila tamu masikioni. Haikumchukua muda kamanda akageuka kutazama. Hamaki uso kwa uso akakutana na mwanamke mwenye rangi ya dhahabu. Nywele zilizofundwa vema na macho ya kuvutia. Kiuno kimekabwa na gauni na amepanda kwa viatu virefu nyeusi.
Mwanamke huyu alikuwa ni Glady.
“Do I know you, madam?” Kamanda akauliza.
“Yes, you do!” akajibu Glady akirembua. “Would you mind a dance?”
“Off course!”
Glady akamkwapua Kamanda na kusonga naye kando kucheza wimbo wa taratibu uliokuwa unapiga. Sikioni mwake sauti ya mbali ikamwambia, “Hakikisha unamuua.”
***
LAKINI GLADY ATASEMA YEYE NI NANI? NA ATAMUUAJE KAMANDA KWA WATU WENGI HIVI? WENZAKE WAKO WAPI?