Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

SteveMollel, heko sana kaka kwa utunzi wa riwaya kali kabisa. Ni miaka mingi toka nikutane na riwaya ya Kiswahili iliyonivutia na kunipa hamu ya kusoma na kusubiri kwa hamu kama mtoto anayesubiri peremende. Ustadi wako ni mahiri kabisa na umenikumbusha waandishi wa enzi hizo ambao nao walikuwa mahiri sana. Nakufananisha na Eddie Ganzel, unamkumbuka huyu jamaa? Pia staili yako ya kijasusi kama riwaya za mzee Elvis Musiba (RIP) na riwaya zake kama Kufa na Kupona ama Kikosi cha Kisasi na Njama. Nakupa heko na shukurani kwa kutupa burudani hii bure kabisa kaka. Una uwezo wa kuuza kitabu kaka. Nakuahidi siku yoyote nikikutana na riwaya mtunzi akiwa Steve Mollel nitatoa majasho yangu bila kinyongo. Keep it up bro. Na pia asante kutuwakilisha machalii wa Arachuga [emoji3][emoji3]
 
dah. imebidi nizisome story zote 2. kumbe zote tamu.......
 
ANGA LA WASHENZI --- 08

*Simulizi za series inc.*



Macho yake yakaanza kuambaa ambaa huku masikio yake yakifanya kazi ya kusikia sauti ya kila kitu.

Taratibu aliufuata mlango wa sebule kwa tahadhari ya kiwango cha juu.

ENDELEA…

Aliufungua kwa mguu wake wa kushoto akanyooshea bunduki nje, mara mkono wake ukapigwa teke, bunduki ikaponyoka mkono na kurukia mbali.
Alikuwa ni mwanaume mrefu aliyevalia suti na kinyago cheusi cha fuvu la kichwa cha binadamu. Mkono wake wa kushoto alikuwa ameshikilia kamera, ile aliyoweka Miranda mezani, huku akiwa hana silaha yoyote.
Kwa tahadhari aliweka kamera chini kisha akajipanga kwa ajili ya pambano, Miranda pia. Wakakunja ngumi kila mmoja akimvizia mwenzake awe wa kwanza kufungua mchezo.

Miranda aliitazama kamera kiwizi. Alikokotoa na umbali wa silaha yake ilipo. Aliwaza namna gani ya kufanya avipate vyote kwa pamoja. Adui yake alikuwa anawaza namna gani ya kufanya apate mwanya wa kuhepa na kamera.

Hilo ndilo lilikuwa lengo lake, kamera tu! Hakuwa na haja na kingine chochote. Alijua fika kamera ile itakuwa na jambo muhimu, jambo ambalo litakuwa na soko huko anapotaka kuipeleka.

Ila je, mkono wa mwanamke Miranda, utamruhusu?

Akapima zogo kwa kurusha ngumi, Miranda akakwepa na kutupa yake, ikapanguliwa. Akatupa tena nyingine na nyingine, zote zikapanguliwa na mwanaume mvamizi kisha kukawa tena kimya. Wakitegeana.

Mara hii Miranda hakungoja tena kwa muda, akarusha mateke mfululizo. Alijitupa hewani na kufungua nyonga zake. Mvamizi akajituma kukwepa kwa ustadi, kisha akautafuta mwanya na kumpatia Miranda teke la mgongoni lililomtupia chini.
Miranda akanyanyuka upesi. Akakunja ngumi na kumjongea mvamizi. Alishajua sasa anapambana na mtu wa aina gani, mtu mtaalamu mwenye uwezo, hivyo ilibidi awe mwangalifu zaidi.

Hakurusha ngumi wala teke, akangoja. Mvamizi akautuma mwili kwa ngumi mbili, kisha teke, ngumi tatu na teke la kujifungua, vyote Miranda akakwepa kana kwamba alikuwa na miadi navyo.

Mvamizi aliporusha teke la kujikusanya, Miranda akaona sasa fursa ya kushambulia, upesi akainama kukwepa na kuufyeka mguu uliokuwa umemsimamisha mvamizi. Mvamizi akadondoka chini. Ila upesi akajifyatua na mikono yake akasimama.

Akanguruma kwa hasira. Alikuwa amechukia. Pasipo kujua huo ukawa mtaji wa mafanikio kwa Miranda.
Alitupa ngumi na mateke kwa fujo. Miranda akakwepa kwa kasi. Takribani ngumi na mateke ishirini yakavuka yakipita pembeni ya masikio ya mwanamke huyo aliyekuwa mwepesi kuepusha kichwa chake, wakati huo kichwani akitafakari namna ya kushambulia.
Muda ulipowadia, mvamizi akajaa kwenye rada. Alirusha teke la mguu wake wa kushoto, Miranda akalidaka kwa mikono yake miwili. Mvamizi akataka kutuma teke la kulia kwa kutumia balansi ya mguu wa kushoto ulioshikwa na Miranda, akaula wa chuya.

Akiwa hewani amejifyatua, Miranda akamsukuma, alafu kufumba na kufumbua akajituma hewani na kumpa teke kali alilolituma kwa nguvu zake zote, mwanaume akajikuta yupo chini akiugulia maumivu makali.

Haraka Miranda akachumpa samasoti kuifuata bunduki. Akaiokota na kumnyooshea mvamizi, ajabu mvamizi naye alikuwa tayari ameshainyaka kamera na kuitia mkononi. “Ukifyatua tu, naiachia ipasuke! Ni wewe ndiye utakuwa na hasara ikiharibika.” Mvamizi akatishia. Alikuwa amenyoosha mkono wake wa kushoto akiishikilia kamera kwa kidole kimoja.

Miranda akatulia kwanza akifikiria cha kwanza. Hakuharakisha kufyatua risasi, maana aliona anaweza akakosa anachokipigania japokuwa uwezekano ulikuwa mdogo. “Weka bunduki chini!” Mvamizi akaamuru. “Nimesema weka bunduki chini kabla sijaitupa kamera!” akarudia akitishia kwa kuchezesha kamera kidoleni. Miranda akamwomba asifanye hivyo kwani anatii agizo.

Taratibu akainama akijifanya anataka weka silaha chini, ila akilini mwake alikuwa amepanga jambo.
Kabla hajapata mwanya wa kulifanya, honi ikaita huko nje ya uzio! Wote wakatazama getini upesi kana kwamba wataona kitu.
Mvamizi akajua sasa usalama wake unazidi kuwa finyu ya wembamba wa nyufa, na alitakiwa afanye jambo upesi kujing’amua. Hakuwa na budi bali kuituma kamera. Uhai wake ulikuwa muhimu kuliko kanda ya kifaa hicho.

Akairushia mbali ya kulia mwa Miranda. Upande wa mkono ule ule ambao mwanamke huyo alikuwa amebebelea bunduki. Haraka Miranda akaikimbilia na kuinyaka mithili ya kipa mashuhuri. Mpaka chini akadondoka nayo akijigeuzia mgongo.
Kurusha macho kwa mvamizi, akastaajabu kumuona yupo hewani anavuka ukuta! Akarusha risasi tatu haraka. Ila hazikufanikiwa, mvamizi akatua upande wa pili akakimbia.

Punde, loki ya geti dogo ikavunjwa kwa teke kali akaingia Kinoo akiwa amebebelea bunduki ndogo. Aliangaza macho yake huku na huko, akamuona Miranda chini akiwa na kamera na bunduki. Haraka akamfuata. “Vipi, kuna nini?” “Ninyanyue twende ndani,” Miranda akasema akikunja sura kwa hisia za maumivu.

Kinoo akambeba na kwenda naye ndani, akamuweka kwenye kochi. Miranda akamueleza yale yote yaliyotukia. “Miranda, si salama tena kukaa hapa,” alisema Kinoo akitikisa kichwa. “Kama wameshapajua, basi hili halitakuwa tukio la mwisho!” “Kinoo,” Miranda akaita. “Unadhani walikuwa hawajui hapo kabla kama naishi hapa?” “Ndio! Mbona hayakutukia haya?” “Hapana, mimi siamini.” Miranda akabinua mdomo. “Walikuwa wanajua, ila hawakuwa na sababu.” “Umemsahau yule jamaa aliyekuwa anatufuatilia kwenye bodaboda?” Kinoo akakumbushia akinyooshea kidole hewa. “Huoni kama haya matukio yanafuatana? Yule aliyekuwa kwenye boda ndiye huyu ambaye amekuja kutuvamia. Na itakuwa siku ile alijua haya makazi. Yani hatukufanikiwa kumpoteza maboya,” Kinoo akafafanua.

Miranda akakaa kimya kwanza akitafakari. Alimuomba Kinoo amletee kinywaji, Kinoo akatii kwa kumletea chupa moja kubwa ya mvinyo. Mwanamke akaidaka na kuanza kuinywa kama samaki.
Alipopumzika, akasema: “Kinoo, hawa watu wanatupanda kichwani. Kitu kinachonipa presha ni kwamba wanapataje taarifa, ina maanisha wanatufuatilia. Tena kwa ukaribu.

Huyu mvamizi amejuaje kama nina kamera. Kuja kwake hapa ilikuwa ni sababu ya kamera tu, ndiyo maana alipoikwapua, alikuwa anahangaika kuondoka.

Ina maana alituona tukitoka na yule mwanamke kule klabu? Ina maana aliniona nikitoka na kamera kule kwako?

Hivi umeshajiuliza haya maswali?" "Nilikuambia mapema, Miranda. Tunahitaji kumwambia mkuu. Si mpaka maji yakomee shingoni," akasema Kinoo. "Sijakataa kumwambia mkuu, Kinoo. Ila basi tuwe na maelezo ya kueleweka. Anyway, leo nitamwambia yaliyotukia. Bila shaka tunahitaji ulinzi zaidi." "Utamwambia saa ngapi?" "Nikimtumia mrejesho wa zile kemikali." "Inabidi tujiandae." "Na nini?" "Kazi! Unajua tukituma taarifa kama hiyo kazi huja." "Hujazoea tu kazi, Kinoo?" Kinoo akatabasamu. "N'taachaje kuzoea sasa," akasema. Naye akachukua chupa ya mvinyo na kugida. .
.
.
.
*** .
.
.
.
Isingekuwa simu kuita, Jona asingeshtuka na kutoa macho yake kwenye kibao kikavu alichokuwa anapaka rangi.

Alikunja ndita akikodoa macho ndani ya miwani yake. Aliikwapua simu na kuitazama. Nade!

Akasonya na kuiweka simu pembeni kisha akaendelea na kazi zake kama kawaida.

Simu ikaendelea kuita na kuita. Aliipuzia akaendelea na kazi zake kama kawaida.

Siku hiyo alikuwa ametingwa na kazi na tangu asubuhi na hakuwa na muda wa kupumzika. Alikuwa na kazi kama tatu hivi, kama si za kuzimaliza basi za kuzifikisha mahala fulani.
Kazi hizo zilikuwa ni za michoro ya kawaida, michoro ambayo anaweza kuifanya, kama ingelikuwa ni ya tingatinga basi Jumanne angelimsaidia.

Sasa ilikuwa ni majira ya saa sita mchana na ni kazi moja tu ndiyo alikuwa ameshaichorea ramani.

Siku yake ilikuwa imebanwa kiasi kwamba hata simu hakushika, wala hakutaka kuishika.

Jumbe kadhaa zilikuwa zimeingia, za kawaida na za mtandao wa Facebook ila hakupata wasaa wa kuzisoma.

Ilipofika majira ya saa nane mchana, akiwa hata hajala, mgeni akaingia ndani ya fremu yake. Ila haraka akadakwa na Jumanne.
Alikuwa ni mwanamke. Jona alijua hilo kwa sauti kwani hakuwa na muda wa kutazama.

Ila punde akiendelea kusikia sauti hiyo ikiendelea kuongea na Jumanne, akaing'amua si ngeni.

Akatazama, akamuona Nade. Alistaajabu amepajuaje hapo. Aliacha shughuli yake akamtazama mwanamke huyo aliyekuwa amevalia taiti ya zambarau na tisheti nyeusi.

Miguuni alikuwa amevalia raba nyeusi na kama kawaida alikuwa amevalia miwani yenye fremu kubwa nyeusi, nywele zake ndefu zikiwa zimelala.
.
.
.
"Habari, Jona!" Akasalimu. Jona akashusha kwanza pumzi ndefu. .
.
"Njema, karibu,"
.
.
"Ni mgeni wako?" Jumanne akauliza.
.
.
"Ndio, wa kwangu," Jona akajibu upesi.
.
.
"Duh! Haya bana. Acha mie mtazamaji nikae kando." Jumanne akatania, Jona akatabasamu. Alienda zake banda lingine na kumwacha Nade na Jona peke yao.
.
.
"Karibu."
.
.
"Ahsante, samahani kwa usumbufu Jona."
.
.
"Pasipo samahani."
"Nilijaribu sana kukutafuta kwa simu lakini haukuwa unapokea, ndiyo maana nikaja hapa."
.
.
"Umepajuaje hapa?"
.
.
Nade akatabasamu. .
.
"Ni mtafuta cha uvunguni tu," akajibu akiminya macho yake kana kwamba anakonyeza.
.
.
"Enhe, kuna kipya?"Jona akauliza. Uso wake haukuwa na tembe ya masikhara. Hakutaka kupoteza muda kwa kazi alizonazo.

Nade akaguna.
.
.
"Sina. Nimekuja kutafuta hilo jipya kwako." Jona akatikisa kichwa. Akiwa ameshika brashi yake ya rangi akaendelea kuchora kwa sekunde ishirini kana kwamba hana mgeni.

Alikuwa anafikiria jambo kichwani. Japokuwa macho yake yalikuwa juu ya ubao, akili yake ilikuwa inahangaika.
.
.
Akaita:
.
.
"Nade!" pasipo kung'oa macho yake kwenye kibao.
.
.
"Abee!" Nade akaitika.
.
.
"Kuna kitu wewe na Mheshimiwa mnanificha."
.
.
Nade akanyamaza kwanza asiwahi kujibu.
.
.
"Kitu gani, Jona?"
.
.
"Mnajua wewe na mheshimiwa. Ni kipi hicho?"
.
.
"Mbona hamna!"
.
.
"Una uhakika na usemalo?"
.
.
"Ndio. Nina uhakika."
.
.
"Ni nini kinawasumbua hivi? Ni kitu gani hamtaki nijue?"
.
.
"Hamna kitu, Jona. Kwanini unawaza hivyo?"
.
.
"Kwanini unanifuatilia hivyo?"
.
.
"Nakuf ... kivipi?"
.
.
"Nade, embu tuache kufanyana watoto. Kuna jambo kati yako na mheshimiwa." Jona akaacha kuchora, akamtazama Nade machoni.
.
.
"Kuna jambo mnanificha. Kuna jambo mnaepuka nisilijue. Ni bora mkaniambia mapema. "

Nade akawa kimya akimtazama Jona. Mara akanyanyuka.
.
.
"Naona leo haupo kwenye mood. Naomba niende." Jona akatikisa kichwa kisha akaendelea na kazi yake ya kuchora.
"Nitakapokigundua mtakuwa mmechelewa."
.
.
Nade asiseme jambo, akatoka ndani. Akaenda kwenye gari, Toyota Harrier, nyeusi alipojiweka na kufunga mlango.

Ndani ya gari alikuwa mwenyewe. Alijilaza kwenye kiti kabla hajatoa simu yake mfukoni na kupiga.

Punde ikapokelewa.
.
.
"Mkuu, tunapoelekea kitumbua hiki kitaingia mchanga."
.
.
.
***
***
.
.
.
.
- *NINI NADE ANATAKA SEMA?*
.
.
- *NINI KIMEBEGUBIKA SAKATA LA MHESHIMIWA NA KAZI YAKE YA KUMTAFUTA MKE WAKE?*
.
.
- *NINI MIRANDA NA KINOO WANADHAMIRIA KUFANYA?*
 
Back
Top Bottom