Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Aisee nimekurupuka asubuhi yote hii kumbe washenzi hakuna? [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Screenshot_2017-07-31-21-45-27-1.png


Aliitwa Mamba ... ama simba! Akiwapo ndani ya mbuga hata kama hautakutana naye, basi lazima utauhisi uwepo wake.


Silaha yake ilikuwa inamwaga damu. Mikono yake ilikuwa mepesi na miguu mizito ya kukuacha hoi kwa mateke yenye nidhamu!
.
.
.
Leo saa tatu usiku. ANGA LA WASHENZI!
 
View attachment 631406

Aliitwa Mamba ... ama simba! Akiwapo ndani ya mbuga hata kama hautakutana naye, basi lazima utauhisi uwepo wake.


Silaha yake ilikuwa inamwaga damu. Mikono yake ilikuwa mepesi na miguu mizito ya kukuacha hoi kwa mateke yenye nidhamu!
.
.
.
Leo saa tatu usiku. ANGA LA WASHENZI!
[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji7]
Unajua vile tunakupenda Steve
 
*ANGA LA WASHENZI -- 22*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Nina wazo," akasema Nigaa. "Kwanini tusiende kumuuliza mkuu juu ya yule mshkaji ambaye alitakiwa kuuawa na Bigo?"

"Ili?" Devi akauliza.

"Ili tumfuatilie mshkaji wetu. Kama jamaa huyo aliyetakiwa kuuawa bado yupo hai, maana yake Bigo ndiyo atakuwa ameuawa.

Kukawa kimya kidogo watu wakimeza wazo hilo.

"Naunga mkono hoja," Lee akasema akitikisa kichwa. "Kama kweli tunataka kujua hatma ya Bigo, hiyo ndiyo njia pekee."

Basi wakakubaliana wote kufanya vivyo.

ENDELEA...

"Vipi kama Bigo atakuwa ameuawa?" Akauliza Mombo.

"Sasa kutakuwa na kingine zaidi ya kummaliza huyo aliyemuua?" Akatahamaki Nigaa. "Ni kumuua tu na yeye, moja kulipiza kisasi cha msh'kaji wetu. Na mbili kumaliza kazi ambayo Bigo atakuwa ameishindwa."

Wakaendelea kunywa. Na baadae wakawaita wanawake kwa mujibu wa idadi yao waendelee kufurahia.

Wakadumu hapo mpaka kwenye majira ya saa tisa usiku, kisha kila mmoja akaelekea upande wake.

Lee akiwa ameongozana na mwanamke mrefu mwembamba mwenye nywele ndefu za bandia wao wakaenda hotelini.

Hoteli kubwa yenye jina la TUMID, hapo wakachukua vyumba na kujiweka ndani.

Wakaenda kuoga kisha wakarejea ndani.

"Naomba pesa yangu kwanza," akasema mwanamke akisugulisha vidole vyake.

"Shilingi ngapi?"

"Laki moja!"

"Mbona kubwa?"

"Ndiyo bei ya kulala na mimi usiku mzima."

"Usiku mzima na saa hizi ni saa tisa?"

"Kwani si usiku? Na si nitaondoka asubuhi?"

Lee asibishane, akakubali. Ila akilini mwake alikuwa ameshapanga kumdhulumu mwanamke huyo kwa kumpatia pesa ile anayoona anastahili.

Unajua hawa wanawake wakiona ngozi nyeupe huwa wanawehuka na kudhani wana pesa, aliwaza Lee. Ila nitamkomesha, akaweka nadhiri.

Wakapeana penzi kabla Lee hajachukuliwa na usingizi mzito uliompeleka mpaka asubuhi ya saa moja.

Alifungua jicho moja akaangaza, hakukuwa na mtu kitandani. Haraka akakurupuka na kukagua chumba kizima. Hamna mtu.

Akaenda na bafuni napo, hakuona mtu pia.

Akili yake ikamtaka atizame suruali yake upesi. Akatazama na kukagua mifukoni, mifuko yote ilikuwa meupe!

Hakubakiziwa hata mchanga.

Akalaumu sana. Badala ya kukasirika akajikuta anatabasamu, na mwishowe akacheka. Alijiona fala kabisa, tena yule mtepetevu.

Aliketi juu ya kitanda akashika kichwa akiuchambua usiku mzima namna ulivyokuwa. Akahisi tumbo limekuwa la baridi punde alipokumbuka kuwa ndani ya suruali aliweka pochi.

Macho yakamtoka, mdomo ukamkauka.

Pochi ile ilikuwa na vitu vya msingi na maana sana. Ilikuwa na nyaraka zake za siri! Ni bora mwanamke yule angekomba pesa akamwachia vinginevyo.

Akanyanyuka na kushika kiuno. Tumbo lilinguruma. Alihisi miguu inapoteza nguvu.

Alikuwa amefanya uzembe mkubwa sana ambao hata kuwaeleza marafiki zake ilikuwa ni aibu. Ni kwa namna gani hilo liliwezekana wakati yeye huwa mwangalifu?

Akahisi ametiliwa madawa. Hilo ndilo jibu pekee ambalo lilionekana kusuuza nafsi yake japo hakujuwa ametiliwaje madawa hayo.

Sasa alipata kibarua ambacho hakukitarajia- kibarua cha dharura. Cha kumtafuta mwanamke huyo ampatie pochi yake kulinda nyaraka zilizomo ndani.

Hakuwaza pesa. Lah! Aliwaza nyaraka. Alijikuta anamiminika kijasho chembamba akipepesa pepesa macho chumba kizima kana kwamba kaambiwa na mshenga pochi ipo ndani.

Alihofia endapo pochi hiyo ikikamatwa na mikono isiyo salama. Itakuaje?

Kwani ni nyaraka zipi hizo zi ndani ya pochi?

---

"Huwezi amini, leo nimeangukiwa na embe chini ya mwarobaini!" Alisema mwanamke ambaye ndiye yule aliyemzidi kete bwana Lee.

Hapa alikuwa na mwenzake mfupi mnene ndani ya chumba kimoja kikubwa kipana kilichotandikwa godoro chini.

Chumba hichi kilikuwa kimejazwa vitu lukuki chini mathalan chupa ya chai na beseni dogo jekundu lililokuwa limesheheni vyombo.

Hakukuwa na vitu vingi humo. Na hata vilivyokuwepo havikuwa vya thamani kubwa, wala havikuwa vimepangiliwa vizuri.

Ila ukiwatazama wanawake hawa walivyokuwa wameupara. Loh! Waweza sema makazi yao ni Abu dhabi. Nywele feki za bei, na nguo ambazo si haba.

"Enhe! Nipe mchapo!" Akadakia mwanamke mwingine kwa mdomo wake mpana.

"Bwana wee si nimekutana na mchina si mchina, mjapani si mjapani, sijui mkorea yule jana kule golini."

"Nilikuona mwenzangu. Nikasema la haulaa! Ushaula shoga maana mie mwenzako nilitoka kapa."

"Yaani nimeula nimeula! Ila mama mchina mwenyewe anatwanga Kiswahili kama kazaliwa Kigogo!"

Wakaangua kicheko.

"Kwahiyo hakuwa na pesa?"

"Nawe wapenda kuwahi mbele, tuliaa."

"Haya nafunga bakuli."

"Pesa alikuwa nazo ila akajifanya anabania. Nikasema hunijui wewe. Chap! Nikafanya mambo yangu yale. Kaingia kichwa kichwa chali! Nikajibebea vyangu."

"Shing'ngapi?"

"Najua basii? Nimefungua pochi hivi, naona madola dola tu."

"Weee!"

"Oooh! Nakwambia hivyo."

Mwanamke yule mwivi akatoa pochi ya Lee toka kwenye mkoba wake akamkabidhi mwenziwe ambaye aliidaka na kuifungua haraka.

Hakukuta kitu!

"Mbona sioni kitu?" Akauliza akiendelea kukagua.

"Nimekuonyesha ushahidi tu, pesa nishazitoa."

"Na wewe bana! Na hivi je?"

"Hivyo vitambulisho vitambulisho vyake. Mie sijahangaika navyo!"

"Sasa si bora ungemwachia tu. Umevibeba vya nini?"

"Hivi we unadhani nilipata muda wa kukagua kagua pochi? Mie nilifunua nikaona pesa, basi nikaitupia tu mkobani."

Yule mwanamke aliyebebelea pochi akatazama na kukagua vitambulisho na karatasi zingine alizokumbana nazo huko.

Alitazama kwa muda kabla hajaamua kuachana nazo kwa maana hakuwa anaelewa.
"Naona yameandikwa kwa kichina china na Kiingereza tu."

Akatupia pochi kando na kuanza kujadili namna watakavyotumbua pesa iliyopatikana.

Laiti kama wangelikuwa wanalijua namna Lee anavyotoka jasho kuitafuta hiyo pochi, wangemrudishia hata kwa kumtuma wakala.

---

"Can I see you?"(Naweza kukuona?) Jona aliuchapa ujumbe huo kwenye simu yake kisha akautuma. Alikuwa ndani ya mtandao wa Facebook akichati na mke wake Eliakimu.

Ni majira ya jioni haya na siku hiyo Jona hakwenda popote pale zaidi ya kuhama toka chumbani kwenda sebuleni, sebuleni chumbani siku nzima.

Alichokifanya punde tu alipoamka ni kumtaarifu Jumanne kwamba hatakuja kazini kisha akalala kwa muda kidogo kabla hajaja kuamka jua likiwa tayari limeshanawiri.

Alipika akala, akateka tarakilishi yake na kuanza kurandaranda mtandaoni. Alianzia huko Facebook ambapo hakupata anachokitaka. Akatoka na kwenda kwenye mambo mengine.

Muda huu sasa ndiyo anarejea baada ya kuona mtu anayemtaka yupo hewani.

"See me? Serious?" (Kuniona? Kweli?) Uliuliza ujumbe wa Miriam, mke wa Eliakimu.

"Yes for sure!" (Ndio kabisa!) Akachapa Jona na kutuma.

"How can you see me while you are so far?" (Unawezaje kuniona ingali upo mbali?)

"I am in Nairobi now for a fashion show." (Nipo Nairobi sasa kwa ajili ya onyesho la mitindo.)

"Nairobi???"

"Yes. You don't believe? - I am in Nairobi and I expect to be in Dar es salaam soon." (Ndio. Huamini? - nipo Nairobi na nategemea kuwa Dar es salaam karibuni.)

"Sure, I would love to see you." (Kweli, ningependa kukuona.)

"Me as well. Hope to you see soon. Bye!" (Mimi pia. Natumai kukuona karibuni. Kwaheri!)

Jona akaaga na tabasamu. Mbinu yake ilikuwa inaendelea kutimia. Hakutaka kujirahisisha kwa 'mteja' wake huyo ili kutompatia doa la shaka.

Alitaka Miriam apate picha kwamba yeye ni mtu ambaye yupo bize, ametingwa na kazi. Ana muda mchache sana wa kuteta na watu mitandaoni.

Alipotoka kwenye mtandao huo wa Facebook, akazima kabisa tarakilishi yake alafu akajiandaa kwa muda mfupi kabla hajatoka ndani akibebelea tarakilishi.

Akaenda internet café, sehemu wanapofanya biashara ya mtandao, akakutana na mhudumu: mwanamke mmoja mweupe, akamuulizia kuhusu huduma ya scanning.

"Ipo," akajibu mhudumu pasipo kumtazama Jona. Alikuwa yupo bize kutazama tarakilishi yake akichezesha vidole kwenye keyboard.

Jona akatafuta mahali pa kukaa. Punde akaja mhudumu kumsikiliza. Akampatia kibahasha cheupe.

"Humo kuna picha, naomba uziskani na kuzituma kwenye hii kompyuta."

Mhudumu akatikisa kichwa kisha akaenda. Jona akawasha tarakilishi na baada ya mfupi akaona picha zile zikiwa zimetumwa.

Mhudumu akaja kuulizia muda wa mteja na pesa yake. Jona akalipia kisha akaendelea na shughuli zake.

Akafungua injini ya kusaka majibu alafu akaanza kuchukua picha moja baada ya nyingine na kuanza kuzisakia majibu yake mtandaoni.

Alifanya hivyo kwa picha zote hizo kasoro ya Fakiri. Akajikuta amepata majibu ya picha mbili tu zingine zikiwa hazina mrejesho wowote wa maana.

Picha ya kwanza ilikuwa ni ya mwanaume mwalimu wa shule ya sekondari ya Lamu, Thadeus Malima, na ya pili ni ya aliyekuwa mbunge wa jimbo la Nyamagana, Mwanza, kwa jina Ditto Jigeleka.

Wote hawa walikuwa wameuawa kwa risasi. Na muuaji akiwa bado anaitwa 'asiyejulikana'. Mauaji ya watu hawa yalitenganishwa na masaa matano tu.

Hapo Jona akapata shaka kidogo juu ya mtendaji wa mauaji haya. Huyu mwalimu alikuwa ni wa shule iliyopo Dar es salaam, wakati mbunge akiwa ni wa Mwanza.

Muuaji alitekelezaje mauaji haya kwa tofauti ya masaa matano tu?

Hata kama alipanda ndege, bado ikamuwia vigumu kuamini kwani mauaji haya yalihitaji mipango thabiti.

Kwahiyo kuna muuaji zaidi ya mmoja? Na wote wanakuwa na hizi picha?

Kabla hajasumbuka sana na hayo maswali akaendelea kuperuzi juu ya marehemu mbunge maana yeye ndiye ambaye taarifa zake zilikuwa zinapatikana kwa wingi ukilinganisha na bwana Thadeus ambaye mtandao ulimtambua kwa taarifa za kifo tu na akaunti ya Facebook.

Akiwa anapekua pekua kuhusu taarifa hizo, akagundua kwamba mauaji ya Jigeleka yalikuwa yalikuwa yanahusishwa na sababu za kisiasa kwakuwa alikuwa chama pinzani akianzisha hoja iliyoonekana kuibana serikali huko bungeni.

Lakini Jona alikuwa mwerevu kung'amua jambo. Muuaji alikuwa ana mipango na malengo fulani. Ukitazama kwa Fakiri na kwa huyu mbunge, utapata kugundua muuaji alikuwa anacheza na matukio na hivyo basi kuacha watu njia panda kwa kusingizia jambo fulani.

Haswa serikali.


NINI JONA ATAENDELEA GUNDUA?

LEE ATAPATA NYARAKA ZAKE MIKONONI MWA WALE WANAWAKE?

USIKOSE IJAYO.
 
*ANGA LA WASHENZI --- 23*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Lakini Jona alikuwa mwerevu kung’amua jambo. Muuaji alikuwa ana mipango na malengo fulani. Ukitazama kwa Fakiri na kwa huyu mbunge, utapata kugundua muuaji alikuwa anacheza na matukio na hivyo basi kuacha watu njia panda kwa kusingizia jambo fulani.

Haswa serikali.

ENDELEA

Alimaliza muda wake wa kuperuzi akajirudisha nyumbani. Lakini hakuwa amepoteza muda wala pesa kwani kuna kitu alikuwa amepata. Ila basi alitokea kujiuliza sana kuhusu picha ya yule mtu mmoja ambaye hakuwa amepata taarifa zake miongoni mwa zile picha.

Ina maana yeye hajauawa au taarifa zake hazijulikani? Alitamani kujua ili kama basi hajauawa aweze kumwokoa, ila akajikuta hana cha kufanya. Hana pa kuanzia kupata hizo taarifa.

Akiwa anawaza waza na kujiuliza, akakumbuka kuna kitu alitakiwa kupitia kwenye tarakilishi yake. Mojawapo ya faili moja ambalo alilikomba toka kwenye simu ya marehemu Bigo.

Basi haraka akavuta mashine hiyo na kwenda kwenye faili alilolitunza kwa jina la ‘Bigo docs’ akafungua na kwendea faili moja kando ya kioo likiitwa ‘gallery’. Humo akakuta picha nyingi sana.

Hakuona hasara kupitia picha moja baada ya nyingine.

Miongoni mwa picha hizo nyingi zilikuwa zikimwonyesha Bigo akiwa sehemu mbalimbali na watu mbalimbali.

Jona alivutiwa na picha kama tano hivi ambazo alipata kuzitenga kadiri alivyokuwa anazitazama. Picha tatu zilikuwa zinamwonyesha Bigo akiwa na marafiki zake: Lee na wenza. Na mbili zingine akiwa na mwanamke fulani hivi na watoto ambao Jona alihisi wanaweza kuwa familia ya Bigo.

Akazitazama picha hizo kwa umakini. Mojawapo akagundua mandhari yake kutokana na uwenyeji wake ndani ya jiji. Picha hii ilikuwa imepigwa Mango garden, Bigo akiwa na marafiki zake.

Hizo zingine kidogo ikawa ngumu kutambua wapi zilipigwa. Akaziweka kapuni.

Lilikuwa ni swala la muda tu. alijua atapata kujua kadiri hatua zitakavyosonga mbele. Acha apumzike kwanza.


***


Usiku wa saa tatu, ndani ya nyumba ya BC.

Miranda akiwa amevalia suruali ya jeans rangi bluu, na tisheti nyeupe. BC alikuwa amevalia suti ya udongo pasipo kuweka kikolombwezo kingine chochote zaidi ya saa kwenye mkono uliokuwa umebebelea sigara kubwa.

Mezani kuna chupa kubwa ya champagne na glasi mbili.

“The guy might sense something fishy,” (Jamaa huenda akahisi jambo mrama.) alisema Miranda akimtazama BC. “You know he’s in this dirty game for long. He has that nose to smell when things turn awkward.” (Unajua yupo kwenye huu mchezo kwa muda mrefu. Ana pua ya kumfanya anuse pale mambo yanapoenda kombo.)

Miranda alikuwa anahofia. Kwa namna ambavyo Eliakimu alikuwa anamtazama mara yake ya mwisho wakiongea naye, kulimfanya ahisi jambo fulani halipo sawa.

Hakuwa anamchukulia Eliakimu kiwepesi hata kidogo.

“Have you told him about his price being high?” (Umemwambia kuhusu bei yake kuwa juu?) BC akauliza.

“That’s of you to tell him.” (Hilo ni lako kumwambia.) Akajibu Rhoda kabla hajanywa kinywaji chake. Jibu hilo likaonekana ni kali kwa mkuu. BC alisafisha koo lake lake asitie neno. Akanyanyua glasi ya kinywaji na kunywa.

Walikuwa njia panda haswa. Walihitaji muda zaidi wa kumsubirisha Eliakimu, ila hilo jambo likaonekana ni gumu kutokea.

Miranda aliona hamna njia nyingine bali kukubali tu kuhusu Eliakimu kwani kuhusu upande huu mwingine wa Boka na mkewe, wanaofuatilia hauwezi kuzaa matunda kwa wepesi hivyo.

Kidogo hilo likawa gumu kwa BC kulipokea. Alijaribu kulisindikiza na kinywaji lishuke ila bado likang’ang’ania koo.

“Wait, I shall talk to him seriously this time and address him about our offer. It’s up for him to decide either to dig in or out. I don’t mind waiting but loss.” (Ngoja, nitaongea naye kuhusu hili swala kwa umakini muda huu na kumwambia kuhusu ofa yetu. Ni juu yake sasa kukubali aidha kuwa ndani ama nje. Sijali kungojea bali hasara.)

Ungeona sura ya Miranda, haikuwa sawa. Alipuuza akanywa glasi mbili za kinywaji kwa pupa kabla hajanyanyuka na kuaga, kuna kazi inamngojea nyumbani.

Alitoka akaenda kwenye makazi ya Kinoo, wakateta kwa kama dakika tatu kabla hawajaachana.

---

Asubuhi ya saa kumi na moja, Miranda akadamka akajitia kwenye gari lake kuanza safari mpaka maeneo ya Makumbusho, si mbali sana na kituo cha mabasi. Hapo akapaki mahali anapostahili na kutulia ndani ya gari akiangaza.

Punde akawaona watu kadhaa wakiingia ndani ya jengo. Akangojea mpaka majira ya saa mbili ndipo akashuka na kuzama ndani ya jengo.

Jengo hilo lilikuwa limebebelea bango kubwa likisomeka: ROADAR SOLAR COMPANY. Pembeni ya bango hilo kulikuwa kuna mabango mengine ya ofisi zingine zilizokuwa zinapatikana ndani ya jengo hilo.

Miranda aliekea kwenye ofisi hii ya solar – umeme wa jua, akaomba kuonana na mkurugenzi wa kampuni. Pasipo kuzungushwa, akapewa nafasi hiyo. Aliingia ndani ya ofisi akamkuta mwanaume mmoja mnene mweusi mwenye kiwaraza.

Alikaribishwa kwa ukarimu akaketi na kueleza shida yake ni kuunganishiwa umeme wa jua kwenye jengo lake zima, jengo kubwa la biashara.

“Huduma hiyo inatolewa,” akajibu mkurugenzi. “Kwani haujapewa maelekezo huko ulipotoka?”

“Nimepewa, sema nikaona ni uwekezaji mkubwa na hivyo natakiwa kuongea nawe. Nahitaji mradi huo utekelezeke sio tu kwenye ofisi zangu hapa bali pia na huko mikoani.”

Wakaongea kwa muda wa dakika kumi na tano kisha wakaagana.

Lengo la Miranda halikuwa biashara bali upelelezi. Macho yake yalikuwa yanatambaa tambaa huku na huko kukagua na kuchambua. Mpaka anaondoka alikuwa ameshapata anachokitaka.

Aliwasiliana na Kinoo wakakutana na kumpasha habari.

“Ile kampuni ya umeme wa jua, ni ya wale wachina.”

“Umejuaje?”

“Nimeona mojawapo ya picha ya mkuu wao ukutani.”

“Kweli?”

“Ndio, ni kampuni mtoto ya wale wachina.”

Kinoo akatikisa kichwa. Sasa alikuwa ameshaunganisha dots za uthibitisho, ya kwamba aliyemuua Bite ni wachina, mahasimu wao. Ndiyo hao wanaoitafuta ile picha. Picha ambayo na wao wanaitaka.

Picha ambayo wanaamini wakiipata itakuwa ndiyo mwanzo wa wao kuwamaliza mahasimu hao. Walitokea kuamini picha hiyo ina ujumbe. Ina neno ambalo Bite alitaka kulisema.

Bite hakuwepo katika upande wowote ule: aidha wa wachina ama wakina Miranda. Daraja hili lilikuwa muhimu. Haswa kwa wakina Miranda ambao wanaamini kwa kiasi kidogo ambacho Bite alikuwa na wale wachina, basi kuna kitu alivuna.

Wakakubalia na Miranda kwamba inabidi baadae wakaonane na Jona. Tena wote kwa pamoja.

“Inabidi ajue kwamba yupo hatarini,” alisema Miranda. “Kama alifanikiwa kumkamata moja wa memba wao, basi inabidi ajue yupo kwenye orodha na hawataacha kumfuata.”


***


Saa mbili usiku, Lorenzo Night club.


Lee alitoka kwenye gari, Noah ya kijivu yenye vioo vyeusi, akanyookea moja kwa moja ndani. Bado muda haukuwa umeanza kuiva ndani ya eneo hili hivyo hakukuwa na watu wengi. Hata hao aliowakuta ni kwasababu tu ilikuwa ni mwisho wa wiki.

Klabu hii ni ya usiku, si usiku wa saa mbili kama huu, bali usiku mzito.

Lee alitembea klabu nzima akipekua mazingira kwa macho yake madogo. Mashaka yalikuwa yameshika uso wake kana kwamba mpangaji aliyepoteza ufunguo pekee uliobakia.

Aliongea na mlinzi wa eneo hilo akijaribu kumfafanulia umbo la mwanamke yule aliyemkwapulia vitu na kumuuliza kama amemwona eneoni hapo. Mlinzi akatikisa kichwa. Hakumwona.

“Tafadhali ukimwona, naomba umshikilie na unipashe habari,” alisema Lee akimkabidhi mlinzi namba yake ya simu na shilingi elfu kumi. “Ukifanya hivyo n’takupatia zaidi.”

Alifanya hivyo kwa watu watatu kabla hajatoka ndani ya klabu na kurudi ndani ya gari. Ndani alikuwepo Nigaa akiwa amekaa pembeni ya kiti cha dereva ambacho ndicho Lee alikalia.

“Umempata?” Nigaa akauliza.

“Hapana,” Lee akajibu akitikisa kichwa.

“Nilikwambia, ila ukashindwa kuelewa. Huu siyo muda wao. Tatizo lako una haraka mno.”

“Siwezi nikangoja zaidi,” Lee akajibu. Alikuwa amechanganyikiwa.

“Brother, huna haja ya kuhofia. Yule malaya atakuja tu hapa na tutampata kiurahisi. Ulikuwa huna hata haja ya kupoteza pesa yako.”

Wakangoja na masaa yakazidi kwenda mpaka saa saba usiku, mwanamke yule hakuonekana. Saa nane … saa tisa, kimya.

“Imekula kwetu,” Nigaa akasema.

“Sasa nafanyaje?” Lee akauliza.

“Inaonekana hili zoezi litatuchukua zaidi ya leo hii.”


***

USIKOSE SEHEMU IJAYO.
 
*ANGA LA WASHENZI –24*


*Simulizi za series*




ILIPOISHIA



Wakangoja na masaa yakazidi kwenda mpaka saa saba usiku, mwanamke yule hakuonekana. Saa nane … saa tisa, kimya.


“Imekula kwetu,” Nigaa akasema.
“Sasa nafanyaje?” Lee akauliza.
“Inaonekana hili zoezi litatuchukua zaidi ya leo hii.”


ENDELEA


Walikaa hapo mpaka kwenye mishale ya kukaribia asubuhi pasipo kumwona mtu wanayemngoja. Waliamua kutia moto chombo na kwenda zao. Lee akiwa na mawazo na majuto.


Akitafakari na kudadavua kichwani. Akitanabahi ni njia gani ya kuenenda pasipo kupata majibu yoyote yale. Aliwaza endapo mkuu wake akipata habari hizi, nini kitatokea.
Hakuna kingine zaidi ya kifo.


“Nigaa, naomba ushike usukani,” alisema Lee akiegesha gari pembeni. “Sijisikii vema.”


“Usiwaze sana, Lee. Huyo malaya tutampata tu,” Nigaa alimpa Lee moyo.
“Shida si kumpata, Nigaa. Bali yale yaliyomo mule kwenye pochi kama yatakuwepo salama. Sijawahi kufanya uzembe wa aina hii.”


Nigaa alichukua usukani wakaendelea na safari mpaka kwenye makazi yao ambapo waliamua kupumzika kwanza kabla ya baadae kuendelea na kazi zingine. Haswa ya kwenda kuonana na mkuu wao awaeleze kumhusu mtu yule ambaye Bigo alitumwa akammalize.


Kwenye majira ya saa nane mchana wakawa tayari wameshaamka na kujumuika na mwenzao aitwaye Mombo wakaenda kuonana na mkuu wao.


Wakamweleza haja ya mioyo yao. Mkuu akawataka watulie kwani tayari hilo jambo ashalichukulia hatua.



“Wŏ yĭjīng fāle lìng yīgè rén,” (Tayari nimeshamtuma mtu mwingine,) alisema mkuu akikuna kidevu chake chongofu. “Ràng wŏmen kàn kàn hui fāshēng shènme.” (Acha tuone nini kitatokea.)
Kwahiyo hapo wakawa hawana tena kauli mpaka pale yule aliyetumwa arejeshe taarifa ama naye atokomee ndipo mkuu achukue hatua nzito.


Kwasababu Jona ni mchoraji tu, hamna haja ya kuhofia sana mpaka kutuma kikosi kamili.


Mwanaume aliyetumwa alijulikana kwa jina la Panky. Mwanaume fulani mwembamba urefu saizi ya kati. Kichwani mwake alikuwa ana nywele zilizochongwa kama mtaro zikiwa zimesimama kama moja.


Kwa shingo upande Lee na wenzake wakaridhia. Ila kabla hawajaondoka, mkuu akauliza:


“Lee, nĭ hái hăo ma?” (Lee, upo sawa?) Akimtazama Lee machoni. upesi Lee akatazama chini na kutikisa kichwa chake kuridhia ya kwamba alikuwa sawa. Wakatoka nje.




***



Saa nane mchana …



“Vipi upo poa now?”
“Ndiyo, nadhani nina muda sasa. Tunaweza tukaenda.”
“Saa hii?”
“Ndio. Au wewe ulikuwa unataka twenda muda gani?”
“Usiku. Bila shaka ndiyo muda atakaokuwa nyumbani.”
“Unajua usiku nina miadi na Boka. Siwezi kwenda, kama unavyojua kuna ishu nataka nichonge naye.”
“Lakini sidhani kama muda huu atakuwepo nyumbani. Mchana huu.”
“Basi fanya hivi, si upo town, pitia pale ofisini kwake umcheki.”
“Nipe kama robo saa.”
“Iwe kweli.
Baada ya robo saa …
“Hayupo!”
“Pamefungwa?”
“Hapana. Yupo yupo mshkaji mwingine.”
“Muulize basi.”


Punde, Kinoo anashuka kwenye gari na kufuata ofisi ya Jona. Alimkuta Jumanne pekee ambaye alimsalimu na kumuulizia Jona.


“Atakuwa yupo kwake, jana na leo hajafika job. Ila naweza nikakusaidia.”
“Usijali,” akajibu Kinoo. “Nilikuwa namhitaji yeye mwenyewe.”


Akarudi kwenye gari na kumtumia Miranda ujumbe:


“Tuelekee nyumbani.”
“Poa, nipitie nipo tayari,” ujumbe ukajibu.


____



Saa nane na dakika hamsini na tano …



Jona alikuwa amevalia bukta na kaushi nyeupe. Kuna baadhi ya michoro alikuwa anaiweka sawa kwenye ubao wake wa karatasi, michoro ambayo kwa kuitazama upesi huwezi jua alikuwa anachora nini hasa.


Alisikia hodi getini, akaacha shughuli yake na kuangaza dirishani. Akaona Range Rover sport nyeupe. Akashtuka kidogo. Alijua usafiri huo ni wakina nani. Basi akaenda chumbani na kukwapua bunduki yake aliyofichia nyuma ya kiuno akiijaladia na shati jeusi.


Kwa kujiamini akalifuata geti na kuwaruhusu wageni waingie ndani.
“Hatujaja kwa shari, bali maongezi,” alisema Miranda. Mwanamke ndani ya sketi fupi nyeusi na topu ya pinki. Akiongozana na Kinoo mwenye nguo zijulikanazo kila uchwao.


Jona akawakaribisha sebuleni akiketi kwenye kiti cha kando kilichoruhusu kila mmoja kumtazama mwenzake.


“Karibuni japo ujio wenu haukuwa na taarifa. Natumai mlikuwa mnajua kama nipo nyumbani.”

“Ndio, tulipitia kazini kwako.”
Pasipo kupoteza muda Miranda akaeleza kilichowaleta. Ya kwamba ni picha na baadhi ya taarifa ambazo wanataka kumfikishia Jona.


Wakamwambia kuhusu msako ule wa picha, haswa wakiuhusisha na kundi la kihalifu la kichina ambalo lipo nyuma yake. Ya kwamba picha ile ni mali yao, wanaitafuta na kwa gharama yoyote ile wataipata.


“Uhai wako upo hatarini. Watu hawa hawatakoma kutuma watu wao mpaka pale watakapohakikisha wameitia hiyo picha mkononi. Japokuwa hatujawahi kuiona hiyo picha, tunaamini itakuwa na nyaraka muhimu sana kwao. Na ndiyo maana nasi twaisaka.”


Huu ukawa muda muafaka kwa Jona kuuganisha tarifa zake kichwani na kupata mantiki. Ina maana wageni wake hawa wanawafahamu hawa wachina ambao alikuwa anahangaika kufumbua fumbo?


Hawa wachina ambao wamefanya mauaji ya watu kadhaa!


Kabla hajaongelea picha, akawauliza wakina Miranda kama wanafahamu lolote juu ya kifo cha bwana Fakiri na Jigeleka. Wakasema hawafahamu. Jona akawaambia ni kwa namna gani amepata taarifa za hao marehemu.


“Nilikuta picha zao kwenye hifadhi ya mtumishi wao.”

“Bila shaka walikuwa kwenye pumzi zao za mwisho,” akasema Miranda. Jona akakumbuka neno hilo ‘pumzi ya mwisho’. Ni neno la kichina lililoandikwa kwenye picha za watu wale aliowaona kwenye paspot.


“Unajua lolote kuhusu pumzi ya mwisho?” Akauliza.

“Ndio, najua. Ni kikosi cha mauaji kinachohusika na mauaji ya wale wote wanaoleta kizingiti mbele ya kazi yao. Kikosi hichi kinaundwa na watu stadi wa kazi. Wenye uwezo wa kuua pasipo kubakiza ushahidi wala kielelezo.”

“Na unajua kilichomuua bwana Jigeleka?”

“Hapana, sijajua. Wanaua watu wengi, siwezi nikajua haswa kwanini kila mmoja huuawa.”


Baada ya Jona kuuliza maswali ya kutosha, akataka kujua kwa undani juu ya wakina Miranda, wao ni wa kina nani haswa na wanajishughulisha na nini. Miranda akajibu kwa ufupi kwamba wao ni wafanyabiashara, wakihusika na biashara za kuingiza madawa nchini, madawa ya afya wakiwa na ubia na MSD.
“Makajuanaje na hawa wachina?” Jona akauliza.


“Kwasababu walikuwa ndiyo wapinzani wetu kibiasara. Siku zote rafiki huwa karibu, ila adui karibu zaidi.”

“Sasa picha itawasaidia nini?”

“Kama tulivyosema ni adui zetu. Tunataka kujua kila nyendo yao.”

“Basi?”

“Basi. Hicho pekee ndicho kinatuhusu.”


Jona akakereketwa rohoni. Kwanini watu hawa wanafanya uhalifu nab ado wanadunda mtaani? Kwanini wanaua watu nab ado hawachukuliwi hatua? Alijaribu kuwauliza wakina Miranda, akajibiwa kwa ufupi.


“Mikono na miguu yao ina mafunzo. Akili zao zina ujuzi. Mifuko yao ina pesa.”


Wakateta kwa ufupi kabla Jona hajaenda kuwaletea picha ambayo aliwakabidhi na kuwaambia:

“Mnaweza mkanishrikisha kama kuna jambo mtaling’amua kwenye picha hiyo. samahani sitawapa mwende nayo.”
Miranda na Kinoo wakaridhia.

Wakaitazama picha kwa umakini sana wakila dakika kama kumi na tano. Lakini wakatoka patupu!


“Una uhakika picha yenyewe ni hii?” akauliza Kinoo.

“Ndiyo yenyewe. Sina zaidi.”


Mbona ni picha ya kawaida tu? visiwa na ndege! Wakatahamaki. Hawakujua nini haswa dhamira ya picha ile. Waliona ni kama urembo.


Ila kama isingelikuwa na maana kwanini itafutwe? Kwanini Jona alengwe kuuawa?


“Hamna chochote ulichokipata pichani?” Miranda akamuuliza Jona. Jona akatikisa kichwa.


“Hapana. Nikadhani pengine nyie mwajua.”


Wote walitota. Hakuna aliyeona cha maana. Ila Jona akasisitizia lazima picha hiyo itakuwa na maana, hawana budi kufuatilia.


“Nakumbuka wakati Bite ananiambia nimchoree hii picha alinipa maelezo very simple, ila alitaka niyafuate na kuyazingatia haswa. Nilirudia kuchora picha hii mara tatu, tena kwasababu ndogo ndogo sana, mara ndege wamekaa mbali, niwasogeze, ama visiwa ni virefu sana na kadhalika. Bila shaka alikuwa na maana yake.”


Mwishowe Jona akawakabidhi wakina Miranda picha nyingine, kopi ya ile orijino ambayo aliichora kwa penseli na karatasi, wakakubaliana yeye abakie na ile orijino.


“Jona,” Miranda akaita. “Wewe ni nani?” Akauliza. Jona akatabasamu kwanza kabla ya kujibu kwa kuuliza:
“Kwanini wauliza?”
“Kwasababu wewe si mchoraji pekee. Wewe ni nani?”
Jona hakutaka kusema mambo mengi, akawaambia hayo mengine yatakuja kadiri na muda.
“Kuwa makini sana,” Miranda akamsisitizia Jona.
“Usijali,” Jona akamjibu. “Naweza kujitazama vema.”



_____



Robo saa mbele...



"Mkuu, kuna jambo lipo katikati ya Jona na na wakina Miranda,"Nade akatoa taarifa. Wakati huo alikuwa amejiweka kando kidogo ya nyumba ya Jona macho yake ndani ya miwani yakiwa yanaangaza kutazama gari, Range Rover sport nyeupe, ikiishilia.


"Ndio, nimewaona wakiingia ndani ya nyumba ya Jona," akasema Nade sasa akianza kuchukua hatua kusonga mbali na nyumba ya Joana.


"Wametoka muda si mrefu. Wamedumu kwa muda wa kasoro lisaa."


Akasikilizia kidogo, kisha akasema:
"Sawa, mkuu. Ila inakuwa ngumu kujua wanachokiongelea. Nahofu isije ikawa ni kuhusu Miriam."


Kimya kidogo akisikilizia. Kisha akasema:
"Sawa, mkuu. Jicho halitafunga."
Akakata simu. Ila mara akasikia mkono wa mtu begani. Haraka akageuka.
Kutazama alikuwa ni Jona!
.
.
.
***
 
Back
Top Bottom