Anna Makinda: Kuna Mawaziri walikuwa wanapinga Serikali kuhamia Dodoma, bila Hayati Magufuli isingewezekana

Anna Makinda: Kuna Mawaziri walikuwa wanapinga Serikali kuhamia Dodoma, bila Hayati Magufuli isingewezekana

Mahakama ilimkuta na kesi ya kujibu

Kesi ya kujibu ni procedure tu kwamba mahakama isikilize upande mwingine unavyojitetea. Sasa mahakama kumruhusu mtuhumiwa kujitetea imekuwa nongwa. Mlitaka asijitetee?.

Halafu Ni lini ugaidi ulifanyika Tanzania?. Yani Tanzania hakujafanyika ugaidi ila mnakamata watu kwa ugaidi.
 
Mawaziri wenyewe na serikali bado wamejazana Dar es Salaam sana tu. Ni kweli hafahamu gharama serikali inayoingia kuendesha ikulu mbili kubwa katika nchi kama hii
 
Kesi ya kujibu ni procedure tu kwamba mahakama isikilize upande mwingine unavyojitetea. Sasa mahakama kumruhusu mtuhumiwa kujitetea imekuwa nongwa. Mlitaka asijitetee?.

Halafu Ni lini ugaidi ulifanyika Tanzania?. Yani Tanzania hakujafanyika ugaidi ila mnakamata watu kwa ugaidi.
Alijitetea akashinda kesi ya ugaidi?
 
Spika wa bunge msitaafu Mh Anna Makinda ambaye pia amehudumu serikalini Kwa zaidi ya miaka 40, akiwa kwenye Misa ya kumbukizi ya hayati Magufuli ametoa sifa nyingi kuhusu Rais huyo wa awamu ya tano, na akatoa Siri kwamba Kuna viongozi wengi walikuwa hawataki serikali kuhamia Dodoma na walikuwa wanaona ni upuuzi tu

Lakini alipoingia Rais Magufuli serikali ilihamia na ikajengwa Ikulu bora kabisa na kubwa kwenye ukanda wote wa Afrika mashariki na ya kati.

Anne Makinda ameonya kuwa mwanasiasa yoyote anayepotosha kwamba Magufuli hakuwa chochote Tanzania atashindwa tu.


Makinda aache majukwaa tangu sijazaliwa namsikia, apumzike sasa.
 
1. Yeye anaishi Dar na kwa pesa ya kodi amejenga jumba la kifahari sana Dar! Kwa nini yeye hajahamia Dodoma? Kimsingi kulikuwa hakuna uharaka wa Taifa kuhama Dar wakati kwa miaka 20 hivi serikali na balozi zimewekeza pesa ndefu sana katika miundombinu Dar!
2. Kuhamia Dodoma kwa haraka ni matumizi mabovu katika raslimali za Taifa hili!
3. Hata leo hii kazi nyingi za serikali zinafanyika Dar! Raisi, mawaziri, maafisa bado wanpenda Dar kuliko Dodoma na huo ni ukweli!
4. Mbaya sana kuweka mayai yote katika kapu moja! yaani Dodoma! why? Angalia kwa mfano Afrika ya Kusini Serikali iko Pretoria, Bunge Cape Town na Mahahaka Pietzmarisburg! Sisi tz tunasema kila kitu kiwe Dodoma!
5. Mambo kama ya kuhamia Dodoma kama nchi tulihitaji utafiti, na upembuzi makini, na pia kura ya maoni kwa wananchi wote na sii mtu mmoja kuamka tu na kutumia raslimali za taifa hili changa na maskini kuahamia Dodoma
 
1. Yeye anaishi Dar na kwa pesa ya kodi amejenga jumba la kifahari sana Dar! Kwa nini yeye hajahamia Dodoma? Kimsingi kulikuwa hakuna uharaka wa Taifa kuhama Dar wakati kwa miaka 20 hivi serikali na balozi zimewekeza pesa ndefu sana katika miundombinu Dar!
2. Kuhamia Dodoma kwa haraka ni matumizi mabovu katika raslimali za Taifa hili!
3. Hata leo hii kazi nyingi za serikali zinafanyika Dar! Raisi, mawaziri, maafisa bado wanpenda Dar kuliko Dodoma na huo ni ukweli!
4. Mbaya sana kuweka mayai yote katika kapu moja! yaani Dodoma! why? Angalia kwa mfano Afrika ya Kusini Serikali iko Pretoria, Bunge Cape Town na Mahahaka Pietzmarisburg! Sisi tz tunasema kila kitu kiwe Dodoma!
5. Mambo kama ya kuhamia Dodoma kama nchi tulihitaji utafiti, na upembuzi makini, na pia kura ya maoni kwa wananchi wote na sii mtu mmoja kuamka tu na kutumia raslimali za taifa hili changa na maskini kuahamia Dodoma
Ilishahamia Sasa ,kama hutaki jinyonge
 
..fedha zilizotumika kujenga ikulu na maofisi ya serikali Dodoma zingesaidia zaidi kama zingetumika kwenye ujenzi wa industrial parks, au miradi ya uzalishaji kama yakilimo, uvuvi, na ufugaji.
 
..fedha zilizotumika kujenga ikulu na maofisi ya serikali Dodoma zingesaidia zaidi kama zingetumika kwenye ujenzi wa industrial parks, au miradi ya uzalishaji kama yakilimo, uvuvi, na ufugaji.
Jinyonge sasa
 
Back
Top Bottom