Ansbert Ngurumo na Dkt. Minja mubashara kwenye Al Jazeera

Ansbert Ngurumo na Dkt. Minja mubashara kwenye Al Jazeera

Blaming the victim ni kuchukulia kuwa kuchukua tahadhari na kujikinga ni jukumu lao wenyewe hao senior citizens - ni jukumu la wote, dola inayombwelambwela na ninyi madogo mnaojirusha kidimbwi kisha mnarudi na uviko-19 aina ya sauzi nyumbani kuwaambukiza wazee wetu.
Hakuna aliyesema kuwa kuchukua tahadhari na kujikinga ni jukumu lao peke yao.

Lakini pia, tahadhari na kujikinga kunaanzia na wewe mwenyewe.

Dhibiti kile na yale yaliyo ndani ya uwezo wako maana ya wengine hutoweza.
 
Hakuna aliyesema kuwa kuchukua tahadhari na kujikinga ni jukumu lao peke yao.

Lakini pia, tahadhari na kujikinga kunaanzia na wewe mwenyewe.

Dhibiti kile na yale yaliyo ndani ya uwezo wako maana ya wengine hutoweza.

Naam, wazee wanajikinga sana wanaangushwa na vijana mlioenda kuhesabiwa kwenye North Migration, mnaoshiriki marathon na kujirusha kwenye mabonanza bila kuisahau dola ndumilakuwili.
 
Naam, wazee wanajikinga sana wanaangushwa na vijana mlioenda kuhesabiwa kwenye North Migration, mnaoshiriki marathon na kujirusha kwenye mabonanza bila kuisahau dola ndumilakuwili.
Kwenye hao ‘vijana’ nawe umo?
 
Dr Minja kiufupi anasema kwamba kule US ambako yeye anafanya kazi, ni njia tatu hasa, kabla ya chanjo, ambazo wameona zikifanya kazi vizuri - uvaaji wa barakoa, kuzuia mikusanyiko na kunawa mikono. Ukifanya mambo haya matatu, ndani ya wiki 3 unaona mabadiliko.

Minja pia ameeleza kuwa kimojawapo ambacho kimechangia wimbi kubwa la maambukizi na vifo, ni mikutano ya kampeni ambayo ilikuwa ikikusanya maelfu ya watu. Tangu mwezi ule wa 10, kilifuata kipondi cha incubation. Matokeo yameanza kuonekana kuanzia December 2020.

Ansbert anaeleza kuwa Rais amekuwa mzito kukiri tatizo kutokana na kauli zake za mwanzo kuwa Tanzania hakuna corona. Sasa hivi anakubali taratibu, lakini kwa kuzunguka. Wananchi tuongeze pressure kwa Rais ili serikali itimize wajibu wake haraka na siyo kuzidi kuchelewa.

Dr Minja anasema, kwa Tanzania, maamuzi hayafanywi na Serikali, ni Rais Magufuli pekee yake. Akisema kuwa kesho watu wote wahakikishe wamevaa barakoa, watu si chini ya milioni 6, watavaa. Na hilo likitokea, tutakuwa tumeokoa maisha ya watanzania wengi.

Jamani haya kweli yanatushinda? Na kwenye barakoa kasema haijalishi Ni barakoa za kitabibu au kutengenezwa Hilo mitaani.

Tuzidi kupaza sauti haya matatu angalao yafanyike. Serikali iyasimamie, isiendelee kuwapotosha watu.
 
Ngurumo ni anti-government usitarajie mchango chanya au ushauri wowote productive kutoka kwake
Ni captain wa kundi la kulaumu/kulalamika
Sasa mkuu hayo ya ugomvi wenu wa anti-government mimi hayanihusu ujue, nataka kujua walichoongea maana hakuwa mwenyewe kwenye kipindi.
 
Hakuna aliyesema kuwa kuchukua tahadhari na kujikinga ni jukumu lao peke yao.

Lakini pia, tahadhari na kujikinga kunaanzia na wewe mwenyewe.

Dhibiti kile na yale yaliyo ndani ya uwezo wako maana ya wengine hutoweza.
Nyani Ngadu, japo jina lako silipendi Sana maana haliendani Ni michango yako ya kujenga lakini naheshimu Uhuru wako wa kuchagua jina.

Ni kweli, sisi wananchi, kila mmoja ana wajibu wake Kama raia wa kujilinda na kuwalinda wengine. Lakini unapozunhumzia wajibu, so wote watakapokuwa tayari kuutimiza wajibu huo, na hapo ndipo umuhimu wa serikali unapokuja.

Katika mapambano haya, kuna wajibu wa mtu mmoja mmoja, wajibu wa familia, wajibu wa taasisi mbalimbali, na wajibu wa Serikali.

Kwa ujumla Rais Magufuli anaogopwa sana na wasaidizi wake na watendaji wote wa serikali na hata wasio na Serikali. Hali hiyo kama akiitumia kwa nia ya kuyaokoa maisha ya watu, atafanikiwa kiurahisi Sana. Rais Magufuli akitamka leo hii kuwa kesho kila ofisi, kila kwenye mikusanyiko wa watu lazima kuwe na maji tiririka, hakuna mahali patakapokosekana maji tiririka.
 
Nyani Ngadu, japo jina lako silipendi Sana maana haliendani Ni michango yako ya kujenga lakini naheshimu Uhuru wako wa kuchagua jina.
Yawezekana hulipendi sana kwa sababu unalikosea!
Ni kweli, sisi wananchi, kila mmoja ana wajibu wake Kama raia wa kujilinda na kuwalinda wengine. Lakini unapozunhumzia wajibu, so wote watakapokuwa tayari kuutimiza wajibu huo, na hapo ndipo umuhimu wa serikali unapokuja.

Katika mapambano haya, kuna wajibu wa mtu mmoja mmoja, wajibu wa familia, wajibu wa taasisi mbalimbali, na wajibu wa Serikali.

Kwa ujumla Rais Magufuli anaogopwa sana na wasaidizi wake na watendaji wote wa serikali na hata wasio na Serikali. Hali hiyo kama akiitumia kwa nia ya kuyaokoa maisha ya watu, atafanikiwa kiurahisi Sana. Rais Magufuli akitamka leo hii kuwa kesho kila ofisi, kila kwenye mikusanyiko wa watu lazima kuwe na maji tiririka, hakuna mahali patakapokosekana maji tiririka.
Mimi siikwepeshi lawama serikali pamoja na Rais Magufuli. Wanabeba lawama karibu zote.

Lakini pia, mimi kama raia huru mwenye akili timamu, sihitaji Rais Magufuli aniambie eti nivae barakoa au sijui ninawe mikono na maji tiririka au kuepuka misongamano.
 
Rais Magufuli kakosea sana kwenye suala la PR kwa kudai COVID-19 haipo nchini.

Huwezi kudai kitu hakipo, hususan ugonjwa unaosababishwa na ki/virusi [ambavyo havionekani], bila ushahidi.

Rais Magufuli ni mwanasayansi wa wapi yeye?

Mimi bado naamini C-19 si kali wala hatari kama inavyotangazwa, lakini hiyo haina maana watu wasichukue tahadhari, hususan wale walio medically fragile.
Si alipima, akaona vipimo ni 'feki', kwa vile mapapai, mafuta ya oil navyo vilikuwa na corona. Akaachana na upimaji. Lakini kabla ya hapo, kuna picha za wafu walioanguka kwa ugonjwa zikionyesha maziko ya usiku..., hiyo ikiwa ni juhudi ya kuonyesha kaugonjwa hakapo, na kama kapo ni kadhaifu mno!

Halafu akaweka "maombi maalum" kwa mungu wake. Hata kama corona ilikuwa imeanza kuonekana kuwa ilikuwepo nchini, 'mungu wake' akaifutilia mbali na akatangaza "Tanzania isiyo na corona.

Baada ya "maombi maalum" kusikilizwa na 'mungu' hatua zote na juhudi muhimu zilizokuwa zimeanza kutumika (ambazo huenda ndizo zilizofifisha maenezi yale ya mwanzo zikatupiliwa mbali. Haya makorokoro ya kujikinga ya nini tena kama 'mungu' amekwishatuondolea corona.
Kampeni zote zikabuma.

Hili wimbi la pili, sio corona yetu hapa. Hii ililetwa na watu kutoka nje na wa hapa kwetu waliokwenda matembezi huko nje. Sisi hapa hatukuwa tumewahi kupata corona.
Hata hivyo, wananchi walishaambiwa waache woga/hofu; kwani woga/hofu ni hatari zaidi ya corona. Uoga hofu itawaua.
Na raia walimwelewa vyema kiongozi wao juu ya woga/hofu hiyo. Wakajiachia kwenye madaladala, mabaa, kule kwa akina machinga na kwenye sehemu zote za mikusanyiko.
Wananchi hawaiogopi corona tena, badala yake woha/hofu yao kubwa ipo kwa kiongozi wao. Kati ya corona na kiongozi, mwananchi ni bora aidharau corona kuliko kukabiliana na kiongozi na mashine zake.

Pamoja na corona "kutokuwepo kabisa, kuwepo kidogo sana...", wananchi wanahimizwa kulima mazao ya chakula kwa wingi, ili tuwauzie walioshambuliwa na corona na kushindwa kufanaya kazi. Lakini kama njaa ikiingia hapa, wananchi wanaambiwa wataachwa wafe kwa njaa!

Sasa tumefika hatua ambayo corona ni mipango ya mabeberu. Ni mbinu za kutushambulia katika vita vya kiuchumi. Hatutaki ma-barakoa yao. Chanjo zao ni njia ya kutuua ili waje kirahisi kubeba mali zetu. Wakati huo huo, juhudi kubwa zinafanyika kufufua dawa zetu za jadi kupambana na corona, ugonjwa ambao ni mafua tu kama mafua mengine.

Hata hivyo, kwani nani kauliwa na corona. Wanaokufa sasa hivi matatizo yao yanafahamika. Siyo corona ni changamoto tu za kupumua.

Tanzania Corona haipo! Kuvaa barakoa na kutumia njia nyingine za kujikinga ni alama ya kutokuwa na IMANI kwa 'mungu'.
 
Lakini pia, mimi kama raia huru mwenye akili timamu, sihitaji Rais Magufuli aniambie eti nivae barakoa au sijui ninawe mikono na maji tiririka au kuepuka misongamano.
Inawezekana sana, pia kwamba utaonekana kutokuwa na "akili timamu" kama unahimizwa na kiongozi wako, tena uliyemwamini sana na kumchagua, anapokwambia ugonjwa huo haupo. Unavaa barakoa, wewe hata 'mungu' huna imani naye?
 
Rais Magufuli kakosea sana kwenye suala la PR kwa kudai COVID-19 haipo nchini.

Huwezi kudai kitu hakipo, hususan ugonjwa unaosababishwa na ki/virusi [ambavyo havionekani], bila ushahidi.

Rais Magufuli ni mwanasayansi wa wapi yeye?

Mimi bado naamini C-19 si kali wala hatari kama inavyotangazwa, lakini hiyo haina maana watu wasichukue tahadhari, hususan wale walio medically fragile.
Naona nawewe umeamua kumpuuza, Jamaa nilimshtukia kitambo hafai
 
Back
Top Bottom