App Mpya ya JamiiForums: Fuata hatua hizi
Naam wakuu,

Kwa mara nyingine tumeona tuboreshe huduma ya JF ili izidi kuwa rahisi kutumia.

Kwa sasa unaweza ku-Install JF App kwa PC au Tablet (iPad zikiwemo) na Simu za Mkononi (Android na iPhones).

FAIDA:

1) Ni rahisi kutumia na haina tofauti yoyote na main site, hakutakuwa na malalamiko tena kuwa kuna kukosa notifications au kushindwa kufanya actions kadhaa

2) Ni rahisi kufunguka kuliko unavyodhania. Installation yake inachukua sekunde moja au pungufu. Haichukui space kwenye simu yako au kifaa chako

3) Ukiwa offline, bado kuna content utakuwa na access nayo kwa urahisi zaidi. Hulazimiki kuwa mtandaoni

4) na mengine mengi

Hatua za kufuata:

Kwa wanaotumia PC:

Tembelea JF kwa kutumia Google Chrome Browser, kisha utaona sehemu kama hii kwenye browser yako:

View attachment 1791283

View attachment 1791292

Kisha bonyeza Install kama inavyoonekana hapa chini:

View attachment 1791284

Utaona tayari unayo App kwenye PC yako. Kuanzia hapo hutokuwa ukilazimika kutembelea tovuti kwa njia ya browsing ya kawaida.

Mfano, mwenye Macbkook ataona icon ya App ya JF ikiwa hivi:

View attachment 1791290

Kwa wanaotumia Android Devices:

Tumia Google Chrome (au native browser ya simu yako):

Bonyeza mistari mitatu iliyo kushoto mwa LOGO ya JamiiForums, utaona kitu kama hiki chini:

View attachment 1791285

View attachment 1791286

Bonyeza INSTALL kisha utaona hivi (itachukua sekunde 1 ku-Install)

View attachment 1791287

Kwa wanaotumia iPhone au iOS devices:

Tumia Safari Browser, bonyeza sehemu hizi zilizozungushiwa na fuata maelekezo kwenye simu... Just add to your device's home screen.

View attachment 1791288
View attachment 1791289

Ukikwama usisite kuuliza, tupo kwa ajili yako.

TAKE NOTE: Siku zijazo tutaondoa App zilizopo kwenye Google na Apple stores!

Karibuni
Weuweeee[emoji7][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847]
Melo katika ubora wako[emoji122][emoji122][emoji122]

Karma jf kumenoga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeiona ila bado sijaiweka ndani.
Natumia hacked internet (siweki bando) na iko fasta
Screenshot_20210520-075027.png
 
Si lazima Chrome maana nadhani umeona kuna wadau hapa wanakiri hata Brave iko njema kabisa
Mkuu hongera kwa maboresho.

Kwa upande wa notifications ni hadi uifungue App ndio uzione, hazionekani kama notifications za App zinavyoonekanaga juu(nyuma) screen.

Hii App mpya ya desktop naifananisha na ile ya forum ya kinaijeria, lakini ile ya kinaija inatoa notifications kama kawaida kama App zingine.

Naomba ulifanyie kazi hili ili tupate notifications hata kama hatujafungua App ila tu tukiwa tumewasha data.
 
Maxence Melo
Hongera kwa hatus hii

Nilikimbia app miaka mingi nyuma.. na sikucheki tena.. sababu ya permissions mlizotaka za lazima.. kwa hii ni zipi?
 
Asante kwa maelekezo. Nimeijaribu na ina work vizuri tu.
Japo sijajua kwanini mna mpango wa kuondoa App zilizopo kwenye Google na Apple stores?
Ila all in all, it works fine kabisa.
 
Back
Top Bottom