"Nilivyomuoa mke wangu, Hiba Abouk mwaka 2020 hadi 2023, baada ya miezi miwili, niligundua amekuja kuchukua pesa zangu, hivyo nikaamua kuhamisha kila kitu kwa jina la mama
yangu na nikawa nasubiri ajaze fomu ya talaka.
Kamwe sitokuja kumuamini mwanamke yeyote tena isipokuwa mama yangu. Mimi na mama yangu tulicheza muziki baada ya kuona talaka.
Nilisajili mali zangu zote kwa jina la mama baada ya kuhisi kuna kitu kibaya anapanga.
Baada ya mwaka mmoja wa ndoa, kabla ya talaka, tuligombana kidogo tu asubuhi ile, alisema natakiwa kujua anaweza kutaka talaka muda wowote na tutagawana mali zote sawa sawa.
Baada ya kusikia hivyo, nilitambua mke wangu ni malaya (gold digger) kisha sikupuuzia kauli yake na kuanza kufikiria nini cha kufanya.
Wazo la kumpatia mali zangu mtu ninayemuamini, jina la mama yangu likanijinia kichwani.
Tumepambana sana kufika ulipo, hivyo hakuna mwanamke aliyetoka huko aje kukuangusha, Basi haraka tulihamisha kila ninachomiliki hadi nguo mpaka jezi ninazochezea, zimehamia kwa mama.
Baada ya mke wangu kudai talaka na kutaka nusu ya mali zangu, sikuumia akili, Alikuwa ananiambia nitaenda kuwa kapuku, mganga njaa baada ya talaka, nilibaki nacheka moyoni.
Ukifeli kupanga basi jipange kufeli... Alifeli kupanga, nilifanikiwa kupanga alishtuka baada ya kugundua sina kitu.
Alikuwa analia sana mahakamani sio uchungu wa talaka ila kwa sababu aliondoka kama alivyokuja.
Wanaume wenzangu, marafiki watakusaliti, wanawake watakusaliti ila upendo wa mama
hauelezeki;
Achraf Hakimi.
UMEJIFUNZA NINI?
NB: MWANETU MKATILI