Arusha: Aliyekuwa Mgombea wa Ujumbe katika Serikali ya Mtaa akutwa kwake akiwa amefariki huku akiwa na alama kukatwa shingoni

Arusha: Aliyekuwa Mgombea wa Ujumbe katika Serikali ya Mtaa akutwa kwake akiwa amefariki huku akiwa na alama kukatwa shingoni

"inawezekana pia amejidhuru mwenyewe kutokana na labda msongo wa mawazo” amesema Shana.

kamanda anapiga ramli kama mganga wa kienyeji
Kwajibu hilo la Kamanda ujue hakuna uchunguzi utakaofanyika hapo, zuga na gheresha mpaka watu wasahau. Ndio basi tena. Poleni sana kwa waliofikwa na Msiba.
 
Aliyekuwa Mgombea katika nafasi ya Ujumbe wa Serikali ya Mtaa ya eneo la Mnara wa Voda, kupitia CHADEMA kabla ya Chama hicho hakijajitoa kushiriki, Sirili Homary amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake huku akidaiwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni


Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kifo hicho kina muda wa siku tatu tangu kimetokea.

Amesema Marehemu Homary amekutwa ndani ya nyumbani kwake katika eneo la Mnara wa Voda, huku funguo ikiwa ndani akiwa amefariki Dunia.

“Bado tunachunguza na tutatoa taarifa maana mtu amekutwa ndani na funguo ikiwa ndani inawezekana pia amejidhuru mwenyewe kutokana na labda msongo wa mawazo” amesema Shana.

Aidha amesema wako wanasiasa wanaleta uchochezi juu la kifo hicho na ameahidi wakiendelea atawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

“Naomba watupe muda vyombo rasmi vya uchunguzi vifanye kazi yake, jambo kama hilo lina taratibu linapotokea tunachunguza kwa kuhusisha vyombo vinavyoaminiwa na wananchi na tutatoa taarifa kupitia Vyombo vya Habari”amesema Shana.

Naye Mbunge wa Arusha, Godibless Lema akihojiwa na Nipashe, amesema jambo hilo ni la kikatili na la kuhuzunisha na kwamba amezungumza na Kamanda wa Polisi mkoani humo ambaye amemuambia watu kadhaa wanashikiliwa kuhojiwa juu ya tukio hilo.

Amesema CHADEMA mkoani Arusha wameunda Kamati Maalum kufuatilia Mauaji hayo maana yana utata kwani Homary ni Kada Maarufu na mwaminifu wa Chama hicho.

“Sio kawaida kwa polisi kukaa kimya hapa kuna utata, RPC alipaswa aite kikao na wanahabari na waulize majibu na ajibu sasa ukimya huu unatushangaza maana jamii itapata picha gani?”amehoji Lema.
Tunalazimishwa kuelekea tusipohitaji kufika. Inna lillah wa inna ilahi rajiun
 
Lisu hayupo hajaenda kufungua kesi kwa hiyo polisi haiwezi kufanya uchunguzi na huyo marehemu hayupo hawezi kufungua kesi kwa hiyo uchunguzi haupo vile vile. Polisi wataanzia wapi wakati marehemu hajafungua kesi kama Tundu Lisu?
 
vijana wadogo mnatafuta umaarufu kupitia siasa kama vile hamjui kua siasa ni.mchezo mchafu! hivi hakuna issue nyingine za kufanya??
Nyerere alianza siasa akiwa kijana mdogo kabisa na akafanya makubwa. Usiwakatishe tamaa vijana, cha msingi siasa ya nchi hii irudi kwenye misingi ya ustaarabu kuliko hii ya kuchinjana.
Rais wa nchi asiposimama kinyume na mauaji haya ya watanzania wasio na hatia nchi itapata laana na kuingia kwenye machafuko. JPM tafadhali kemea haya mauaji ya kisiasa hadharani nchi iweze kupona.
Rais Magufuli yafaa nini kupokea gawio kutoka katika mashirika ya umma ili hali walipa kodi na nguvu kazi ya taifa ndo hawa wanauawa? Kodi itakayoleta gawio mwakani itapakanaje kama walipa kodi wanapunguzwa kwa mapenzi ya wanadamu wachache?
 
Haya majibu ya RPC ni ya kijinga sana sana! Eti huenda MTU amejidhuru kutokana na msongo.....pumbavu kweli
 
vijana wadogo mnatafuta umaarufu kupitia siasa kama vile hamjui kua siasa ni.mchezo mchafu! hivi hakuna issue nyingine za kufanya??
Kwani wakina Salim a. Salim, kikwete etc walingia kwenye siasa wakiwa wazee

Ova
 
Aliyekuwa Mgombea katika nafasi ya Ujumbe wa Serikali ya Mtaa ya eneo la Mnara wa Voda, kupitia CHADEMA kabla ya Chama hicho hakijajitoa kushiriki, Sirili Homary amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake huku akidaiwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni


Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kifo hicho kina muda wa siku tatu tangu kimetokea.

Amesema Marehemu Homary amekutwa ndani ya nyumbani kwake katika eneo la Mnara wa Voda, huku funguo ikiwa ndani akiwa amefariki Dunia.

“Bado tunachunguza na tutatoa taarifa maana mtu amekutwa ndani na funguo ikiwa ndani inawezekana pia amejidhuru mwenyewe kutokana na labda msongo wa mawazo” amesema Shana.

Aidha amesema wako wanasiasa wanaleta uchochezi juu la kifo hicho na ameahidi wakiendelea atawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

“Naomba watupe muda vyombo rasmi vya uchunguzi vifanye kazi yake, jambo kama hilo lina taratibu linapotokea tunachunguza kwa kuhusisha vyombo vinavyoaminiwa na wananchi na tutatoa taarifa kupitia Vyombo vya Habari”amesema Shana.

Naye Mbunge wa Arusha, Godibless Lema akihojiwa na Nipashe, amesema jambo hilo ni la kikatili na la kuhuzunisha na kwamba amezungumza na Kamanda wa Polisi mkoani humo ambaye amemuambia watu kadhaa wanashikiliwa kuhojiwa juu ya tukio hilo.

Amesema CHADEMA mkoani Arusha wameunda Kamati Maalum kufuatilia Mauaji hayo maana yana utata kwani Homary ni Kada Maarufu na mwaminifu wa Chama hicho.

“Sio kawaida kwa polisi kukaa kimya hapa kuna utata, RPC alipaswa aite kikao na wanahabari na waulize majibu na ajibu sasa ukimya huu unatushangaza maana jamii itapata picha gani?”amehoji Lema.
ACP aache visingizio na vitisho, kuwepo funguo ndani si hoja ya msingi. Yeye mwenyewe anadhani inawezekana amejidhuru mwenyewe labda kutokana na msongo wa mawazo. Sasa ikitokea mtu mwingine akadhani kuna walio mdhuru kwa sababu za kisiasa ama nyinginezo, uchochezi unatokea wapi hapo?
 
Back
Top Bottom