*KUKAMATWA VIONGOZI CHADEMA ARUSHA*
*Na Felix Mushi,Arusha*
Niko hapa eneo la tukio Shule ya Msingi Lucky Vicent iliyopo Olasit Jijini Arusha, Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha, na Viongozi wengine wa Chadema wamekamatwa wakiwa kwenye mkutano na wazazi wa watoto waliofariki kwenye ajali hiyo.
Katika kikao hicho Meya wa Jiji alianza kwa kutoa pole kwa wafiwa na kuwaeleza kuwa ametumwa na Mbunge ili kuwapa pole za kipekee kwa msiba huu na zaidi ameelekezwa kuja kuwajengea ujasiri wazazi ili waendelee kudai fedha zilizoliwa na wajanja.
Akawaeleza kuwa wao kama Chama makini wako pamoja na wafiwa kwa hali zote na kwamba lazima haki itashinda. Pia aliwafafanulia kuwa ni jambo la aibu kuona wadau mbalimbali wametoa fedha lakini watu wachache wanakula michango hiyo lakini wanaachwa.
Kabla hajaendelea na maelezo hayo, alisimama mzazi aliyejulikana kwa jina moja la mama Ivo ambaye alimuuliza Meya juu ya fedha milioni 10 ambazo Mbunge na uongozi wa CHADEMA waaliahidi walipokuja kuwapa pole siku ya msiba kwamba ni vyema wangezitoa ziwasaidie kuliko kuendelea kuwaeleza juu ya wizi wa rambirambi ambazo hata hawana uchungu nazo. Aidha alumina Meya Alasdair kurejeshewa fedha za ada ambazo walilipa shuleni siku moja kabla ya ajali kwani ni haki yao.
Swali hilo liliamsha shangwe na vigelegele kutoka kwa baadhi ya wazazi huku wengine wakiguna kichinichini. Hata hivyo Meya aliwaeleza kuwa fedha ambazo wao kama CHADEMA waliziahidi wasiwe na hofu watazipata lakini hiyo siyo agenda iliyowaleta leo! Akawaomba wamvumilie kwani yeye na viongozi wenzake watatafuta siku muafaaka ambayo Mbunge atakuwepo ili awakabidhi mwenyewe. Alitumia nafasi hiyo pia kuwasihi wafiwa wapuuze maneno ya mtaani kwamba CHADEMA hawajachangia chochote zaidi ya kufanya siasa Kwenye mitandao. Akawahakikishia kuwa fedha hizo watazipata kabla ya tarehe 21 Mei.
Hata hivyo maelezo haya yalionekana kutojitosheleza kwa baadhi ya wazazi ambao waliendelea kuguna na wengine wakizomea huku wengine wakionyesha kufurahishwa na majibu hayo na wakizomea kwa nguvu. Fujo za kutosikilizana zilipoendelea iliymlazimu mzazi mmoja kuwapigia simu polisi kuja kudhibiti sintofahamu iliyojitokeza. Naamini watakuwa wanaendelea kutoa maelezo huko!
Hasira za Baadhi ya wazazi hao pamoja na walimu ni kuchoshwa na kile walichokiona ni usanii wa baadhi ya viongozi kuendelea kutumia msiba huo kama ngao ya siasa huku wakiwa hawatoi michango waliyoahidi zaidi ya kupiga danadana.
____
Nitaendelea kuwajuza kinachoendelea juu ya Muvi hii nzuri!