Arusha na Moshi ndio moyo wa Dar es Salaam, pasipo mapato kutoka hizi sehemu mbili Dar maendeleo yake yangekuwa taabani sana

We bwana mdogo hebu acha kelele.. Angalia mikoa inayochangia pato la Taifa hapo.. Mikoa yako ni namba 7 na 8 huko.. Mwanza na Shinyanga unaowadharau ni namba 2 na 3.. Acha bangi..

SOURCE: NATIONAL BUREAU OF STATISTICS..
View attachment 2415556
Population inachangia sana.
Halafu hiyo mikoa inafeed bidhaa mikoa mingine.
Mwanza inafeed, kagera, Geita, kigoma, Tabora, Simiyu, Mara na Shinyanga lazima uchangie pato kubwa.
 
Wasukuma hawana R kwenye lugha yao.

Hayo ni matokeo ya elimu hohehahe tu kwa mtoa mada.
 
Chanzo kikubwa cha Mapato ya nchi kiko Dar es salaam kuanzia kodi

Pili Dar es salaam ina chanzi kikubwa cha mapato namba nchini ambacho ni bandari ya Dar es salaam

Mapati ya babdari ya Dar es salaam ni makubwa kuliko yote ya utalii wa Arusha na kilimanjaro
 
Ww ni zezeta kweli, mbona haujasema utalii unaingiza sh ngap kwenye Pato la taifa, na vp kuhusu madini na maliasili nyingine unafikiri hizo fedha hazitumiki kujenga miundombinu ndani ya nchi?
 
Kwanza tambua 3/4 ya mapato ya utalii yanatokana na Mbuga 2
1.Serengeti-3/4 ipo Mkoa wa Mara
2.Ngorongoro-ipo Manyara
Serikali kuiweka Arusha kama Kitovu cha Utalii kulelenga katika kuupa thamani mlima wetu wa Kilimanjaro na ukaribu wa kuzifikia hizo Mbuga 2 za Serengeti na Ngorongoro.

Anayekupa anaweza pia kukunyanganya,Leo hii inaweza ikaja Serikali nyingine ikaamua Mkoa wa Mara ndio uwe kitovu maana bado napo papo jirani ya hivyo vivutio 3,Je Watu wa Mkoa wa Mara nao wanaweza kutokana na kusema ndio wanailisha Dar kwa kuwe wamewekwa kuwa kitovu??
 
Kakanjifunze kuandika zingatia nukta,koma na paragraph acha kuandika kama mtoto wa standard 4,Unatuchosha wasomaji.
 
Kakanjifunze kuandika zingatia nukta,koma na paragraph acha kuandika kama mtoto wa standard 4,Unatuchosha wasomaji.
Huo uwozo wako ulio andika hapa kwanini usingejibu hoja iliyopo badala yake uaanza kuandika mipasho mpuuzi mmoja wee katafute MASHOGA wenzio mpashane hapa cyo mahala pake pumbafuu na nusu wewe mwehu mmoja ww
 
Nadhani huyu jamaa ameruka step
Alitakiwa aanzie Facebook
Halafu Instagram
Then kule Twitter
Aende Qoura

Halafu aje home of great thinkers
N.B jamii forum imevamiwa
Msiweweseke mwamba anapiga penyewe tulieni dawa ipenye
 
Msiweweseke mwamba anapiga penyewe tulieni dawa ipenye
We jamaa hata unaelewa takwimu ni kwamba dar mapato ya bandari tu iyo Sijui kanda ya kaskazini yote haifiki kwa pesa zao..

Technically kama we ni msomi dar inakusanya 90% ya mapato yote ya Tz, 10% iliyobaki ndo mikoa yote iyo ilibaki wanashare izo 10% ,..weka bangi pembeni then fikiria
 
SOMA HIYO TAARIFA YA SERIKALI UIONE ARUSHA IMESIMAMA WAPI.
Kwa mara ya kwanza Nchini Halmashauri zote 185 zimefanikiwa kukusanya sh. bilioni 661.4 ambayo ni sawa na asilimia 91 ya malengo ya mwaka wa Fedha 2018/19 ya kukusanya sh bilioni 723.

Matokeo haya ni ongezeko la asilimia 9 kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ukilinganisha na makusanyo ya asilimia 81 ya Mwaka wa Fedha 2017/18 huku Halmashauri ya Jiji la Dodoma sambamba na Mkoa wa Dar es salaam zikiongoza kwa mapato ghafi.

Hayo yabamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa alipokuwa akitoa taarifa ya mapato na matumizi ya fedha za vyanzo vya ndani vya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/19. Mapato haya ya ndani hayijumuishi vyanzo vinavyokusanywa na Serikali kuu.

Akifafanua zaidi Mhe. Jafo alisema halmashauri za Wilaya tano zilizoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi(asilimia 171), Wanging’ombe(asilimia 165), Kilolo (asilimia 150), Misenyi (asilimia 142) huku Mbeya Dc ikishika nafasi ya tano kwa kukusanya asilimia 141.

Halmashauri za Wilaya zilizofanya vibaya kiasilimia ni Tandahimba Dc (asilimia 19), Msalala (asilimia 19), Masasi Dc (asilimia 26) Newala (asilimia 27) pamoja na Nanyumbu (asilimia 36).

Kwa kigezo cha pato ghafi, Mhe. Jafo alisema halmashauri zilizoongoza kwa wingi wa mapato kuwa ni Halmashauri ya Jiji la Dodoma (Sh bilioni 71.7), Ilala (Sh bilioni 58.1), Kinondoni(Sh bilioni 34) Temeke Sh bilioni 33.3), Ubungo Mc (bilioni 18.6) na Jiji la Arusha (Sh bilioni 16.4) wakati halmashauri tano zilizofanya vibaya katika kundi hili ni Nanyamba (sh milioni 258), Gairo Dc(Sh milioni 396), Kigoma Dc (Sh milioni 397.1) Buhigwe (Sh milioni 403.8) na Kakonko Dc (Sh milioni 403.8).

Aidha, katika kundi la mikoa kwa kigezo cha asilimia, Jafo alisema mikoa inayoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani ni Mkoa wa Geita (asilimia 119), Iringa (asilimia 117),Songwe (asilimia 112), Kagera (asilimia 105) na Njombe (asilimia 104), wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Mtwara (asilimia 42), Simiyu (asilimia 459), Shinyinga (asilimia 62), Kigoma (asilimia 74) Mara na Morogoro (asilimia 80).

Kwa upande wa mikoa kwa kigezo cha pato ghafi, Mhe. Jafo alitaja Mikoa inayoongoza kuwa ni Dar es Salaam (Sh bilioni1 163.5) Dodoma (Sh bilioni 82.6), Mwanza (Sh bilioni 32.6) Arusha (Sh bilioni 31.9) na Mbeya (Sh bilioni 31.4) wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Katavi (Sh bilioni 7.3), Kigoma (Sh bilioni 7.7), Rukwa (Sh bilioni 8.2) Simiyu (Sh bilioni 8.8) na Njombe (Sh bilioni 11.4).

Aidha, Jafo alisema Jiji la Arusha limeongoza katika kundi la halmashauri za majiji kwa asilimia kwa kukusanya asilimia 105 ya makisio huku jiji la Mbeya likiwa la mwisho katikakundi hilo baada ya kukusanya asilimia 89 ya makisio.

Alisema Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaongeza kwa kigezo cha pato ghafi ambapo imekusanya Sh bilioni 71.7 na halmashauri ya jiji la Mbeya imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya Sh bilioni 11.4.

Aidha, Jafo alisema halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga imeongoza kundi la halmashauri za Manispaa kwa kukusanya asilimia 138 ya makisio huku Lindi ikishika nafasi ya mwisho kwa kukusanya asilimia 54 ya makisio.

Jafo alisema kwa upande wa halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeoongoza katika kundi la halmashauri za Manispaa kwa kigezo cha mapato ghafi baada ya kukusanyw Sh bilioni 58 huku Lindi ikiwa ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 1.0.

Aidha, JAfo alisema halmashauri ya Mji wa Geita imeongoeza kundi la halmashauri za miji kwa kigezo cha asilimia ambapo wamekusanya kwa asilimia 157 ya makisio huku halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya asilimi 11 ya makisio.

“ Katika kigezo ya pato ghafi kwa halmashauri za mji, Geita inaongeza baada ya kukusanya Sh bilioni 8.02 na halmashauri ya mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho ikiwa imekusanya Shilingi milioni 257.6.

Kwa upande wa halmashauri za wilaya, Jafo alisema Mbozi inaongoza kwa kukusanya kwa asilimia 171 ya makisio na ya mwisho ni Tandahimba iliyokusanya asilimia 19 ya makisio wakati kwa upande wa pato ghafi, Chalinze inaoongoza kwa kukusanya Sh bilioni 7.6 na ya mwisho katika kundi hili ni Gairo iliyokusanya Sh milioni 396.1.

Aidha, Jafo aliwataka wakurugenzi ambao Halmashauri zao zimefanya vibaya katika ukusanyaji wa mapato kujitathimini na kuweka mikakati ya ya kuongeza vyanzo vya mapato na mapato ya halmashauri zao kwa ujumla.

Pia Waziri Jafo aliwaagiza Wakurugenzi ambao Halmashauri zao zimetoa mikopo ya wanawake, vijana na walemavu chini ya asilimia 50 kuandika barua za maelezo kwanini wasichukuliwe hatua kwa kuvunja sheria na barua hizo ziwasilishwe ndani ya muda wa wiki mbili.

Aliongeza kuwa Wakurugenzi wote wahakikishe ukusanyaji wa mapato hayo ya ndani unaenda sambamba na upelekeji wa fedha kwenye miradi ya maendeleo na mikopo kwa wanawake, vijana na walemavu.

Aidha, Mhe. Jafo ameendelea kusisitiza matumizi ya mifumo ya kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuzuia upotevu wa mapato hayo.
 
Utapoteza mda na kuonekana kichaa..Achana nae hao madogo wanamezeshana sumu kama kujiona ila washamba tu yaani hizo halmashauri za dar karibia tatu ziko fire yeye na hako kamkoa lake ka wavuta bangi ,hata izo hotels ni kwa ajili ya watalii wao wapo wpao tu kuvaa manguo oversize.
 
Nisaidie hiyo pichani ni hoteli gani niitembelee
 
Kuhusu stendi na barabara pambaneni na viongozi wenu wa jiji
 
Hivi serious mleta maada unataka serikali iache kupajenga Dar alafu wakajenge kwenye mapori ya Kaskazini[emoji38][emoji38] Unaumwa wewe sio bure....
 
Vyote ulivyotaja vimejengwa kwa mikopo tu
 
Sekta ya Utalii inachangia 17.5% ya pato la taifa na kulipatia taifa 25% ya fedha za kigeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…