Arusha: Ukikutwa umevaa Suruali ya kubana, Sketi fupi Faini Tsh. 50,000

Hawataweza.

Hawataweza ng'oo

Huo muda Kwanza wametoa wapi wa kujadili mavazi ya mtu hizi ni dalili za kukosa Kazi za kufanya.

Maisha yakikaza hata muda wa kuvaa hovyo hawawez kuwaza
Ukienda kwa wameru hizi sheria zipo mda sana na unachapwa viboko kweli kweli hawana masihara
 
Ukianza kuingia kwenye mipaka ya Meru kuwa makin ukileta uduanzi unachapwa 70 chap wadada wa kimeru wanajua likizo hawaendi na vimini meru

Hiyo elf 50 ni kiini macho tu hapo lazima uchezee fimbo hawana shida na hiyo 50
Tumefanana mawazo hiyo faini au kupelekwa mahakamani ni geresha ili wapitishe ila ukikutwa hzo fimbo utakazochezea hutakaa uamini kama upo Tz🤣🤣, kipindi flan wadada walikua wakiwa town wanavaaa vbya kinyama ila mda wa kurudi wakifika maeneo ya jiran wanafunga vitenge siku Moja akijichanganya aisee alitandikwa mpaka akajikojolea
 
Nimesikia Aibu mimi kwa niaba ya Waziri Dorothy Gwajima, Yani Waziri Mzima ana endorse hii taka taka kweli? Sheria za ovyo sana izo tunarudi nyuma aisee
Kwaio kuvua nguo hadharan ndio kwenda mbele
 
Nimesikia Aibu mimi kwa niaba ya Waziri Dorothy Gwajima, Yani Waziri Mzima ana endorse hii taka taka kweli? Sheria za ovyo sana izo tunarudi nyuma aisee
Ukivaa katakundu huko meru umeusha!! Ni taarifa nimekupa
 
Tatizo lako huna akili, we na mbuzi hamna utofauti.... nguruwe pori
Hamna tatizo Mimi kuwa mbuzi au nguruwe pori,maana kama kukosa akili alianza bibi na babu Yako walioshindwa kugundua nguo walikaa uchiiiii mpaka mzungu alipoleta nguo,Sasa hivi usijifanye unazijua sana nguo....
 
Tena nyie wakutokea "daslama" habari iwafikie vizuri msije kusema hamkuambiwa, nyie ndio mnaongoza kwa kutembea uchi hadharani, ole wenu sasa sheeeenzi kabisa 😡
 
Mnakubaliana wachache ili muwakamate na muwaadhibu walio wengi
 
Lazima mdhibitiwe tu hakuna namna. Mmezidi kuvaa na kunyoa minyoo ya kihuni. Dawa yenu ishachemka; kaa tayari kuinywa!
😂😂Hii dunia imebadilika Mzee Acha mawazo ya kizee kudeal na watu ni saikolojia sio nguvu
 
Punguani hao wa huko Longido Vijijini wanamtishia nani?

Serikali ingilia kati ujinga huu kabla ya kuleta Madhara.
 
Sombetin tu watu wanachezea 70
Sombetini ipi wewe, kuanzia soko mjinga, kwa mjapan, sawmill, kwa mama nairo, kanisani, duka la cement, madukani , kwa shemeji yake mkapa, imani, kwa diwani, shuleni, shuka mpaka ngusero huko hakuna huo upumbavu

Au ulijua unaishi sombetini pekeyako
 
Nimesikia Aibu mimi kwa niaba ya Waziri Dorothy Gwajima, Yani Waziri Mzima ana endorse hii taka taka kweli? Sheria za ovyo sana izo tunarudi nyuma aisee
Hbr za jioni ndugu.

Awali kabisa naomba niwapongeze wote kwa ufuatiliaji wa mijadala ya jamii.

Aidha, niseme kuwa, mimi binafsi sitaona aibu kusema kuwa nimewapongeza jamii hiyo kwanza kwa uthubutu tu wa kubaini kuna changamoto na kuketi pamoja kama jamii ya rika zote kujadili na kukubaliana wao.

Hii kwangu ni ishara kwamba, sasa kumbe jamii yetu imeanza kubaini changamoto na kuzimiliki na kuzijadili na Sasa kinachofuata ni msaada wa kitaalamu Ili mijadala yao isikinzane na sheria mama za nchi na uhuru wa haki za binadamu. Mm nimelitazama hivyo.

Sasa kwa kuwa nyie mmelitazama tofauti, haki yenu kujadili katika jicho lenu. Ila sisi huu ni mwanzo mwema wa jamii Sasa kuanza safari ya mabadiliko ya fikra kwamba wao ndiyo injini ya kujadili changamoto zao na sisi ni wa kupeleka msaada wa kitaalamu Ili wafike salama safari yao pasipo kuathiri sheria kuu zote.

Ruksa kuniona mm siko sawa ila niwaombe tu pia kuwa, ziko Mila au sheria za kijamii huko kwenye maeneo yetu ambazo zina athari kiafya, zinaua na kuleta ulemavu, ningependa pia zianzishiwe mjadala kwani ni dharura.

Ahsanteni sana, tupo pamoja na mawazo tunapokea. Mbarikiwe.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…