Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Mimi sio bodaboda Ila nawaheshimu sana maana wapo watu wazima wenye familia na wanasomesha Watoto kwa kazi hiyo
Huwaonei huruma hao wanapoteza maisha au kupata vilema kila kukicha kutokana na kuendesha bodaboda au bajaji kiholela tena bila leseni wala kuzingatia sheria za usalama barabarani?!
 
Enzi za Julias nchi ilikuwa na viwanda e.g Tanganyika Packers, UFI, Kiuta,print pack etc kulikuwa hamna kijana anaendesha Bodaboda,sasa tuna laana kweli
Technology enzi hizo ya kuweza kuunda Bodaboda nyingi kwa muda mfupi and cheap ilikuwa hamna! Tusingepata bodabodanyingi kama leo. Watu walikuwa wachache sana hivyo ungetumia Bodaboda kuhudumia nani? Pia barabara zilikuwa ni chache na mbovu sana. Na pia uwezo kiuchumi wa mtu mmoja mmoja ulikuwa mdogo sana kuweza kumudu Bodaboda. Je! Ulipo andika, haya uliyafikilia au Ulitaka kumuunga mkono Lema ambaye Hakujifunza maisha alipokuwa Canada!
 
Maisha sio Lelemama. Inawezekana Lema amelemaa na misaada iliyokuwa inamuwezesha kuishi bila kufanya kazi huko Kanada...
 
Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Kenani Kihongosi amesikitishwa na kauli ya Mwanasiasa wa Upinzani Godbless Lema kunanga Vijana na Watanzania waliojiajiri kupitia Bodaboda.
MBONA WAKATI WA MAGUFULI NYIE VIONGOZI MLIDHARAU SANA WANANCHI MPAKA MKAWAITA WANYONGE NDANI YA NCHI YAO?
 
Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Kenani Kihongosi amesikitishwa na kauli ya Mwanasiasa wa Upinzani Godbless Lema kunanga Vijana na Watanzania waliojiajiri kupitia Bodaboda.

Kihongosi hana uhalali wa kutoa tamko hilo,au amesahau alitishia kuua wapinzani,sera mbovu za ccm ndio zimetengeneza hao madereva boda boda.
 
Godbless Lema amewatukana vijana Waliojiajiri kwa kuwaambia wanafanya kazi za laana, hii suala limeacha simanzi kwa vijana wengi sana.

Jana nilikua Arusha nimezunguka sehemu mbalimbali kuona wamepokeaje kauli hii yenye dharau kubwa sana. Hakika walio wengi wanajuta kwa Nini walienda Kumpokea Lema.

Serikali inapambana usiku na mchana ili vijana wapate ajira na wajiajiri alafu leo lema anakuja kuwatukana?

Lema anapaswa kuomba radhi kwa kauli hii. Yeye kwa kuwa anakula na kulala bure kule canada basi anataka watu wote waishi hivyo kitu ambacho hakiwezekani. Imeandikwa kwenye vitabu takatifu kuwa mwanaume atakula kwa jasho, wewe inakuaje unakula bure alafu unaleta dharau kwa wanaokula kwa jasho?

Lema anapaswa kuomba radhi mara moja kwa kauli hii.
Haya si matusi, ni lugha ya Kocha. Kwani ni nani anapenda awe bodaboda huku ni graduate wa SUA au wa Muhimbili kakosa ajira tu kwa bile maccm wamekataa tumehuru? Anachosema Mr Lema ni kuwa vijana msichague kazi, changamkeni kesho tutapara tumehuru na Rais tundulissu asiye na madaraka makubwa, ili serkali ya Majimbo ilete ajira kutegemea na kabila lako - at least kwa kina Mhe. Lema hawana shida ndogondogo kama Airport au Hospitali ya Rufaa au lami: ziko hadi Migombani, kwa kina Nape na Jiwe shauri yao walizubaa wakaachwa nyuma majimbo yao watakoma ubishi, walie tu, watajiju. Mr Lema hajakosea kitu, waulize bodaboda watakujibu.
 
Godbless Lema amewatukana vijana Waliojiajiri kwa kuwaambia wanafanya kazi za laana, hii suala limeacha simanzi kwa vijana wengi sana.

Jana nilikua Arusha nimezunguka sehemu mbalimbali kuona wamepokeaje kauli hii yenye dharau kubwa sana. Hakika walio wengi wanajuta kwa Nini walienda Kumpokea Lema.

Serikali inapambana usiku na mchana ili vijana wapate ajira na wajiajiri alafu leo lema anakuja kuwatukana?

Lema anapaswa kuomba radhi kwa kauli hii. Yeye kwa kuwa anakula na kulala bure kule canada basi anataka watu wote waishi hivyo kitu ambacho hakiwezekani. Imeandikwa kwenye vitabu takatifu kuwa mwanaume atakula kwa jasho, wewe inakuaje unakula bure alafu unaleta dharau kwa wanaokula kwa jasho?

Lema anapaswa kuomba radhi mara moja kwa kauli hii.
Hajui kwamba mtu mzima na familia yake kulishwa na wanaume wenzake ndo LAANA kubwa
 
Yule baba Prophet katoa pesa zake milioni 100 kusaidia wananchi ambapo si mbunge wala kiongozi yoyote wa serikali, inatokea tu kajamaa ambako kalikuwa kakilipwa mamilioni ya fedha na posho kibao, na hakakuchangia chochote kwa wananchi, halafu kanatoa kashifa mbele ya haohao wananchi ambao kaliwafanya mgongo wa kupandia eti mmelaaniwa kwa sababu ya biashara zenu za kufukuza upepo?

Siasa zingine za kijinga tu!

Tamko la Lema kuwahusu bodaboda, ni msimamo wa Chadema? Na kama siyo, Lema akemewe mara moja!

Mtu amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, bodaboda alizikuta na akaziacha, lakini hakufanya lolote ili tu kuwatoa hao bodaboda kwenye biashara hiyo ya laana kama anavyodai, isitoshe, bodaboda zimekuwa zikitumika sana kwenye mikutano ya Chadema na zimekuwa zikikiheshimisha chama na Viongozi wake

Sisi tukuiteje?

Ni ujingaa au Canada anataka kuihamishia Tanzania kwa maneno tupu?

Bodaboda zimesomesha watoto na wengine wapo vyuoni wazazi wao wakiwasomesha kwa hizo boda, halafu mtu mmoja tu kutoka Kanada tena kwa ukimbizi wa kuhongwa ili tu aitwe mkimbizi aje kutukana kazi zetu?

Lema, ulilpaswa kuwasimanga boda baada ya kuainisha ulichowafanyia wana Arusha miaka 15 ukiwa mbunge na au ungeshuka na mbadala wa kazi hiyo kutokea huko Canada

Lema, Licha ya kukaa ughaibuni miaka zaidi ya miwili bado haikutosha kuondoa upuuzi wa kufikiri?
 
Mimi sio bodaboda Ila nawaheshimu sana maana wapo watu wazima wenye familia na wanasomesha Watoto kwa kazi hiyo
Hata makahaba na machangudoa wanasomesha watoto na kutunza familia zao. Jee kazi hiyo ni ya baraka? Mtu akiisema kuwa haifai nyie CCM mtamlaumu kuwa ana discourage watu waliojiajiri?
Acheni kuwafanya vijana wa Bodaboda ni wajinga, hawafanyi kazi hiyo Kwa kupenda Bali ni Kwa vile hamjawapa fursa nzuri zaidi
 
Heshimu kazi ya mwenzako mkuu!

Ukiona ni kazi ya laana na ni kiongozi, fanya njia na sio ututukane kwa maneno ya shombo!

Miaka 15 Lema amekuwa mbunge, amefanya nini cha maana ili kuwatoa vijana kwenye biashara hii ya laana?
Lema aligombea ubunge 2005 akakosa sasa miaka 15 inafikaje acha siasa Mkuu

Bodaboda Kama nzuri mbona watoto wao hawaendeshi.
 
Heshimu kazi ya mwenzako mkuu!

Ukiona ni kazi ya laana na ni kiongozi, fanya njia na sio ututukane kwa maneno ya shombo!

Miaka 15 Lema amekuwa mbunge, amefanya nini cha maana ili kuwatoa vijana kwenye biashara hii ya laana?
Lema anakusanya kodi? wajinga wakubwa nyie, mbona watoto wenu hawapo kwenye ajira ya bodaboda? kuna mtoto wa Waziri, RC, KM, RAS, DAS, DC, DED, Mbunge ni bodaboda? ukimtaja mmoja najinyea siku nzima
 
Siasa zingine za kijinga tu!

Tamko la Lema kuwahusu bodaboda, ni msimamo wa Chadema? Na kama siyo, Lema akemewe mara moja!

Mtu amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, bodaboda alizikuta na akaziacha, lakini hakufanya lolote ili tu kuwatoa hao bodaboda kwenye biashara hiyo ya laana kama anavyodai, isitoshe, bodaboda zimekuwa zikitumika sana kwenye mikutano ya Chadema na zimekuwa zikikiheshimisha chama na Viongozi wake

Sisi tukuiteje?

Ni ujingaa au Canada anataka kuihamishia Tanzania kwa maneno tupu?

Bodaboda zimesomesha watoto na wengine wapo vyuoni wazazi wao wakiwasomesha kwa hizo boda, halafu mtu mmoja tu kutoka Kanada tena kwa ukimbizi wa kuhongwa ili tu aitwe mkimbizi aje kutukana kazi zetu?

Lema, ulilpaswa kuwasimanga boda baada ya kuainisha ulichowafanyia wana Arusha miaka 15 ukiwa mbunge na au ungeshuka na mbadala wa kazi hiyo kutokea huko Canada

Lema, Licha ya kukaa ughaibuni miaka zaidi ya miwili bado haikutosha kuondoa upuuzi wa kufikiri?
Hiki ulichokiandika ndio Ujinga hasa! Lema Kwa hiyo miaka 15 uliyoisema, alikuwa mbunge tu. Mbunge ni mwakilishi wa wananchi wa Jimbo lake. Kazi ya mbunge ni kuwasemea wananchi. Ambaye anatakiwa kutenda ni serikali na Wadau wengine. Mbunge hakusanyi Kodi. Mbunge hana dola. Mbunge ni mtu wa kawaida kabisa kama ulivyo wewe na mimi. Tofauti yetu na mbunge ni kuwa yeye ana platform rasmi ya kuongelea (Bunge).

So kusema Lema hakufanya kitu, ni ujinga wa hali ya juu. Someni jamani ili mjue majukumu ya mbunge ni yepi?
 
Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Kenani Kihongosi amesikitishwa na kauli ya Mwanasiasa wa Upinzani Godbless Lema kunanga Vijana na Watanzania waliojiajiri kupitia Bodaboda.
Kama Katibu mkuu wa UVCCM anatoka hadharani na kueleza kuwa Bodaboda ni ajira basi ujue vijana wa chama Cha Mapinduzi hawana viongozi kabisa.
Ajira Gani hizo za kiongozi wa juu kuziweka hadharani?
 
Hiki ulichokiandika ndio Ujinga hasa! Lema Kwa hiyo miaka 15 uliyoisema, alikuwa mbunge tu. Mbunge ni mwakilishi wa wananchi wa Jimbo lake. Kazi ya mbunge ni kuwasemea wananchi. Ambaye anatakiwa kutenda ni serikali na Wadau wengine. Mbunge hakusanyi Kodi. Mbunge hana dola. Mbunge ni mtu wa kawaida kabisa kama ulivyo wewe na mimi. Tofauti yetu na mbunge ni kuwa yeye ana platform rasmi ya kuongelea (Bunge).

So kusema Lema hakufanya kitu, ni ujinga wa hali ya juu. Someni jamani ili mjue majukumu ya mbunge ni yepi?
Unafikiri sawasawa wewe?

Ni mjinga tu ambaye anaweza kukubaliana na huo ujinga uliousema wewe!

Mbali na kuwasemea wananchi I kuhakikisha huduma zimewafikia sawasawa, Mbunge pia ni mtu ambaye anauhuru wa kuingia ofis yoyote au Taasisi yoyote akiwa na agenda ya wananchi na akasikilizwa!

Ila inawahusu watu simarti tu na sio kila mtu anaweza kutatua changamoto ya wananchi nje ya mfumo alioaminishwa eti serikali peke yake ndo itashughurikia kero za wananchi

Kuwa mbunge haitoshi tu kusema kero za jimbo lako

unadhani mkuu Tunachagua wabunge wa nini sasa hata hawana uwezo wowote binafsi wa kushughurikia kero zetu?
 
Lema anakusanya kodi? wajinga wakubwa nyie, mbona watoto wenu hawapo kwenye ajira ya bodaboda? kuna mtoto wa Waziri, RC, KM, RAS, DAS, DC, DED, Mbunge ni bodaboda? ukimtaja mmoja najinyea siku nzima
Ndiyo maana Nchi hii haiwezi kuendelea! Wananchi wenyewe wanamawazo haya mgando na ya kipumbavu wataendeleaje?

Jifunze namna ya uongozi na kutatua kero za watu pasina hata kutegemea kodi za serikali
 
Siasa zingine za kijinga tu!

Tamko la Lema kuwahusu bodaboda, ni msimamo wa Chadema? Na kama siyo, Lema akemewe mara moja!

Mtu amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, bodaboda alizikuta na akaziacha, lakini hakufanya lolote ili tu kuwatoa hao bodaboda kwenye biashara hiyo ya laana kama anavyodai, isitoshe, bodaboda zimekuwa zikitumika sana kwenye mikutano ya Chadema na zimekuwa zikikiheshimisha chama na Viongozi wake

Sisi tukuiteje?

Ni ujingaa au Canada anataka kuihamishia Tanzania kwa maneno tupu?

Bodaboda zimesomesha watoto na wengine wapo vyuoni wazazi wao wakiwasomesha kwa hizo boda, halafu mtu mmoja tu kutoka Kanada tena kwa ukimbizi wa kuhongwa ili tu aitwe mkimbizi aje kutukana kazi zetu?

Lema, ulilpaswa kuwasimanga boda baada ya kuainisha ulichowafanyia wana Arusha miaka 15 ukiwa mbunge na au ungeshuka na mbadala wa kazi hiyo kutokea huko Canada

Lema, Licha ya kukaa ughaibuni miaka zaidi ya miwili bado haikutosha kuondoa upuuzi wa kufikiri?
Rejea kauli ya shujaa wenu... Sipeleki maendeleo mlipochagua upinzani!! Bila kutumia tu akili kua hao unaowanyima maendeleo ni walipa kodi. Sipati picha dunian ingekua mwanadam anatoa riziki ingekuaje!!
 
Back
Top Bottom