Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Kenani Kihongosi amesikitishwa na kauli ya Mwanasiasa wa Upinzani Godbless Lema kunanga Vijana na Watanzania waliojiajiri kupitia Bodaboda.
Rev. Phd. Muta aliwahi kuhoji kuwa inakuaje mtu, tena kijana wa CCM, kuhamasisha wenzao wafanye fujo ya kuwakata mapanga wale wote walio kuwa wapingaji wakuu wa utawala wa Awamu ya Tano?

Kihongosi ni mmoja wa vijana walio kuwa mstari wa mbele kusema na kuhamasisha kufanya fujo dhidi ya wapinzani. Nakumbuka wakati alipokuwa mwenyekiti wetu hapa Iringa, aliwahi kutembelea wanachuo hapa RUCO na kutoa kauli kuwa yeye akimuona mtu kama Zitto, yupo tayari kumkata mapanga.
 
Kazi za kuingiza kipato zipo nyingi lakini sio zote zakujivunia. Bodaboda sio kazi ya kujivunia hata kidogo.
Kunawakati watu waliaminishwa kwamba unyonge nijambo la kujisifia. Watu walijiita viongozi wa wanyonge. Nakumbuka Mbowe alisema kuambiwa wanyonge nikudharauliwa. Nilikubaliana na hoja yake.
Hao wanaoshabikia vijana wajiajiri kwenye bodaboda mbona wao wameomba ubunge?
Mbona watoto na jamaa zao sio mabodaboda?
Ndio hiyo nikazi lakini sio yakujivunia. Kubangaiza sio neema bado
Shule na vyuoni wanamaliza wanafunzi laki tano kwa mwaka mmoja wenye uhakika wa kuendelea na elimu za juu hawafiki elfu hamsini.

Piga hesabu hao karibu laki nne na nusu wataishi vipi. Nadharia hizo za mbona mtoto wake sio bodaboda ni nyepesi kuzitumia lakini hazifanani na uhalisia tunaouishi.
 
1. Ajali
bodaboda wanahusika katika kusababisha ajali nyingi barabarani, tofauti na magari sio rahisi sana kudhibiti bodaboda. Ni bodaboda pekee ambayo utaikuta inaendesha kulia sehemu inatakiwa kuendesha kushoto.

2. Afya
katika bodaboda dereva na abiria wake ndio bodi za chombo, ajali ndogo tu inaweza kusababisha kifo, madhara makubwa kichwani, kukatwa miguu, mikono n.k. Hii inamaanisha kwamba inaleta mzigo mkubwa katika mfumo wa afya ambao umezidiwa kwa uchache wa madaktari.

3. Usalama wa raia na mali zao
Bodaboda zinahusika sana katika matukio ya uhalifu wa silaha na ukwapuaji barabarani kwa sababu ya uwezo mkubwa wa kupenya.

4. Athari kwa sekta muhimu kiuchumi
Kama vile mitumba na nguo za wachina zinavyoendelea kuua na kuzuia kushamiri sekta ya viwanda, Bodaboda ambayo imekuwa kimbilio kwa vijana ni changamoto sana katika kuleta mageuzi ya kiuchumi. Tanzania ina ardhi kubwa ya kulima na kufanya shughuli nyingine ila vijana wanakimbilia kwenye bodaboda tu kwa sababu ni kazi rahisi kuanza nayo.

5. Kutumika vibaya kisiasa
Waendesha magari au ndege huwezi kuwashawishi wakukubali kwa masuala ya hisia tu kwamba umenunua ndege nyingi au umefanya uingizaji wa magari kuwa rahisi. Wao huwa wanaangalia mambo mengine mengi zaidi ya hayo tofauti na bodaboda.

Hata hivyo ukosefu wa fursa na ugumu wa maisha hufanya binadamu wakati mwingine kutokuwa na chaguo zaidi ya kufanya kazi za laana ambazo hajivunii kabisa.
Jamii haijayaona ila Lema ndio kaona? Pumbavu
 
Unafikiri sawasawa wewe?

Ni mjinga tu ambaye anaweza kukubaliana na huo ujinga uliousema wewe!

Mbali na kuwasemea wananchi I kuhakikisha huduma zimewafikia sawasawa, Mbunge pia ni mtu ambaye anauhuru wa kuingia ofis yoyote au Taasisi yoyote akiwa na agenda ya wananchi na akasikilizwa!

Ila inawahusu watu simarti tu na sio kila mtu anaweza kutatua changamoto ya wananchi nje ya mfumo alioaminishwa eti serikali peke yake ndo itashughurikia kero za wananchi

Kuwa mbunge haitoshi tu kusema kero za jimbo lako

unadhani mkuu Tunachagua wabunge wa nini sasa hata hawana uwezo wowote binafsi wa kushughurikia kero zetu?
Ungefika ata kidato Cha nne ungeelewa majukumu ya mbunge
Hakuna mmbunge anaweza tatua kero zako ,jukumu lake ni kuongea kukuwakilisha , anafikisha kero zako kwa serekali, serekali ndio inauwezo wa kutatua au kutotatua
 
Hotuba ndefu inaharibu! Ina maana walokupokea na kujaza mkutano wamelaaniwa?
Waombe, radhi upesi

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
Lema amechemka vibaya ameropoka kwa kutumia vipaza sauti hivyo dunia nzima imemsikia.

Rais SSH ni mjanja sana katika hizi siasa za vyama vingi, anajua kuwa akiwapa uhuru lazima wataropoka na wasikilizaji watawapima na kugundua kuwa hawana mantiki katika maongezi yao.

Uhuru ukizidi sana ni mtego kwa yule anayepewa.
 
Hata siasa ni kazi ya laana ..basi Tu..
Definition ya kazi za laana ni kubwa..
Ku bet je?
Viwanda vya pombe?
Ma bar je?...

Bottom line shughuli yeyote inayo muingizia mwingine kipato tusiwe na haraka ya kuilaani huku hatuwezi kuwalisha..wala hawajaja kuomba msaada kwetu
 
Siasa zingine za kijinga tu!

Tamko la Lema kuwahusu bodaboda, ni msimamo wa Chadema? Na kama siyo, Lema akemewe mara moja!

Mtu amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, bodaboda alizikuta na akaziacha, lakini hakufanya lolote ili tu kuwatoa hao bodaboda kwenye biashara hiyo ya laana kama anavyodai, isitoshe, bodaboda zimekuwa zikitumika sana kwenye mikutano ya Chadema na zimekuwa zikikiheshimisha chama na Viongozi wake

Sisi tukuiteje?

Ni ujingaa au Canada anataka kuihamishia Tanzania kwa maneno tupu?

Bodaboda zimesomesha watoto na wengine wapo vyuoni wazazi wao wakiwasomesha kwa hizo boda, halafu mtu mmoja tu kutoka Kanada tena kwa ukimbizi wa kuhongwa ili tu aitwe mkimbizi aje kutukana kazi zetu?

Lema, ulilpaswa kuwasimanga boda baada ya kuainisha ulichowafanyia wana Arusha miaka 15 ukiwa mbunge na au ungeshuka na mbadala wa kazi hiyo kutokea huko Canada

Lema, Licha ya kukaa ughaibuni miaka zaidi ya miwili bado haikutosha kuondoa upuuzi wa kufikiri?
Boda boda wenyewe wanasema ni laana!
 
Siasa zingine za kijinga tu!

Tamko la Lema kuwahusu bodaboda, ni msimamo wa Chadema? Na kama siyo, Lema akemewe mara moja!

Mtu amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, bodaboda alizikuta na akaziacha, lakini hakufanya lolote ili tu kuwatoa hao bodaboda kwenye biashara hiyo ya laana kama anavyodai, isitoshe, bodaboda zimekuwa zikitumika sana kwenye mikutano ya Chadema na zimekuwa zikikiheshimisha chama na Viongozi wake

Sisi tukuiteje?

Ni ujingaa au Canada anataka kuihamishia Tanzania kwa maneno tupu?

Bodaboda zimesomesha watoto na wengine wapo vyuoni wazazi wao wakiwasomesha kwa hizo boda, halafu mtu mmoja tu kutoka Kanada tena kwa ukimbizi wa kuhongwa ili tu aitwe mkimbizi aje kutukana kazi zetu?

Lema, ulilpaswa kuwasimanga boda baada ya kuainisha ulichowafanyia wana Arusha miaka 15 ukiwa mbunge na au ungeshuka na mbadala wa kazi hiyo kutokea huko Canada

Lema, Licha ya kukaa ughaibuni miaka zaidi ya miwili bado haikutosha kuondoa upuuzi wa kufikiri?
Pia atuambie kisa cha kumtukana Nabii wa Mungu!

Alietoa milioni mia moja kuchangia wafanyabiashara wa soko la Samunge.
 
Kazi/ajira: ni shughuli yoyote halali inayomsaidia mtu kupata mahitaji yake ya muhimu (chakula, malazi na mavazi).

Kwani bodaboda anaenda kinyume na maana hii ya kazi/ajira kwa mujibu wa somo la Uraia kidato cha kwanza?

Laana inatoka wapi hapo?
 
Back
Top Bottom