Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Hapa ndipo mmekuja na majibu sahihi itabidi watafute mbinu za kupunguZa pikipiki au ziuzwe bei ghali ambapo mtu atasota kuipata sio m2 tena
 
Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Ndugu Kenani Kihongosi amesikitishwa na kauli ya Mwanasiasa wa Upinzani Godbless Lema kunanga Vijana na Watanzania waliojiajiri kupitia Bodaboda.
Rev. Phd. Muta aliwahi kuhoji kuwa inakuaje mtu, tena kijana wa CCM, kuhamasisha wenzao wafanye fujo ya kuwakata mapanga wale wote walio kuwa wapingaji wakuu wa utawala wa Awamu ya Tano?

Kihongosi ni mmoja wa vijana walio kuwa mstari wa mbele kusema na kuhamasisha kufanya fujo dhidi ya wapinzani. Nakumbuka wakati alipokuwa mwenyekiti wetu hapa Iringa, aliwahi kutembelea wanachuo hapa RUCO na kutoa kauli kuwa yeye akimuona mtu kama Zitto, yupo tayari kumkata mapanga.
 
Shule na vyuoni wanamaliza wanafunzi laki tano kwa mwaka mmoja wenye uhakika wa kuendelea na elimu za juu hawafiki elfu hamsini.

Piga hesabu hao karibu laki nne na nusu wataishi vipi. Nadharia hizo za mbona mtoto wake sio bodaboda ni nyepesi kuzitumia lakini hazifanani na uhalisia tunaouishi.
 
Jamii haijayaona ila Lema ndio kaona? Pumbavu
 
Ungefika ata kidato Cha nne ungeelewa majukumu ya mbunge
Hakuna mmbunge anaweza tatua kero zako ,jukumu lake ni kuongea kukuwakilisha , anafikisha kero zako kwa serekali, serekali ndio inauwezo wa kutatua au kutotatua
 
Hotuba ndefu inaharibu! Ina maana walokupokea na kujaza mkutano wamelaaniwa?
Waombe, radhi upesi

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
Lema amechemka vibaya ameropoka kwa kutumia vipaza sauti hivyo dunia nzima imemsikia.

Rais SSH ni mjanja sana katika hizi siasa za vyama vingi, anajua kuwa akiwapa uhuru lazima wataropoka na wasikilizaji watawapima na kugundua kuwa hawana mantiki katika maongezi yao.

Uhuru ukizidi sana ni mtego kwa yule anayepewa.
 
Hata siasa ni kazi ya laana ..basi Tu..
Definition ya kazi za laana ni kubwa..
Ku bet je?
Viwanda vya pombe?
Ma bar je?...

Bottom line shughuli yeyote inayo muingizia mwingine kipato tusiwe na haraka ya kuilaani huku hatuwezi kuwalisha..wala hawajaja kuomba msaada kwetu
 
Boda boda wenyewe wanasema ni laana!
 
Pia atuambie kisa cha kumtukana Nabii wa Mungu!

Alietoa milioni mia moja kuchangia wafanyabiashara wa soko la Samunge.
 
Kazi/ajira: ni shughuli yoyote halali inayomsaidia mtu kupata mahitaji yake ya muhimu (chakula, malazi na mavazi).

Kwani bodaboda anaenda kinyume na maana hii ya kazi/ajira kwa mujibu wa somo la Uraia kidato cha kwanza?

Laana inatoka wapi hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…